Rais Samia, unapoteua zingatia watumishi wa muda mrefu na wenye uzoefu serikalini badala ya kuwatoa mtaani

Tatizo ni kwamba hata hao wenye maadili mema hufanya vituko vitupu. Kuna wale waliosaini mikataba wakiwa Ulaya kwa masharti ya wazungu, ukizitazama CV zao ni waheshimiwa wakubwa wenye muonekano wa hali ya juu.

Cha muhimu kwa hivi vyeo ni uzalendo wa mtu, kujituma kwa mtu, ubunifu wa mtu. Hizo personalities zimeikwaza sana Tanzania kuanzia awamu ya tatu kuja hizi za sasa. Tusipende kuyakariri haya maisha.
 
Mimi nafikiri watu wateuliwe kulingana na weledi wao kiutendaji na sio kuangalia watumishi wa umma tu. Watumishi wengi wa umma hufanya kazi kimazoea na wamejaa viburi hatari. Mtu ofisi anaifanya kama yake na kufanya vile atakavyo.
 
Hilo la Kalist kupewa cheo ninalipinga kwa 100%. Kwanini? Kalist anapewa cheo sasa kama fadhila za kuunga mkono juhudi na sio kwa sababu ya utendaji wake kama meya wa Arusha. Kile kitendo kiliharibu mwenendo mzima wa utendaji wake, hapaswi kupewa cheo. Tukiendelea na hizi tabia tutaishia kuwa na nchi ya kinafiki sana.
ACHA JAZIBA!.
Although nilisema "mfano" ila umekuja kama simba aliyejeruhiwa!.

Ila ndiyo kesha pewa hivyo anakwenda "sasa unaingia mkoa wa Mara"
 
Ninashauri ni wakati wa serikali kufikiria namna nzuri kufanya teuzi mbalimbali katika nafasi za serikali kwa kuzingatia uzoefu wa Kazi serikalini, uadilifu ili kutengeneza uzalendo.

Kwa mfano haileti taswira nzuri kumuacha katibu wa tarafa au maafisa wameoshika nyadhifa mbalimbali ktk Idara zao wilayani au mikoani aliekaa kazini miaka 15 na zaidi serikalini mwenye elimu ya kutosha wengine wanawazidi hata elimu Ma DC ma Das na Ma RC lkn ukapuuza utumishi wao ukatoa watu mtaani kuja kuwa Ma DC, DAS, RC’s, RAS etc.

Zamani Kila mfanyakazi alijua iwapo atahudumu kwa mda mrefu na uadilifu angefika katika nafasi ya juu kwa bidii yake ya Kazi uadilifu na kujituma, na hiyo ndio kulikozaa uzalendo hapo zamani ma Afisa utumishi, makatibu tarafa, maafisa maendeleo, kilimo, Afya, Walimu, walipanda nafasi za juu za kiselikali na hiyo ilijenga kuwa na viongozi wengi wenye uadilifu uzalendo na kupenda nchi sbb walipanda nafasi kwa mafaili yao na si kwa majina yao.

Maafisa wakuu wa idara mbalimbali kutoka sekta tofauti mfano elimu, Afya, kilimo, maendelo, utawala iwe wilayani au mkoani wenye miaka 20 ktk kazi, uzoefu na weledi serikalini ndoto zao nao ni kushika nafasi za juu ktk wilaya au mkoa unapowaletea mtu ambae hajawahi kuwa mtumishi huwaongezei tija ila unawavunja moyo na hiyo inashusha uzalendo wa nchi na tija kwenye Kazi zao, Hawa walitegemea miongoni mwao ndio atakaepanda na huo ndio utaratibu wa huko nyuma.

Mfumo huu uangaliwe upya kwa nini mfano makatibu tarafa na maafisa wengine wa wilaya wasipande kuwa Ma DAS na ma DC na wakurugenzi wa halmashauri halafu hao wapya nao wakaanzia chini kupata uzoefu na kupimwa huko chini na kujifunza kujua mifumo ya serikali inafanyaje Kazi kuanzia chini. Huko nyuma hatukuwahi kuona Ma DC ma Ma RC wakivunja maadili sbb walitokana na mfumo mzuri vyeo havikuwapa ukichaa kwani walipanda navyo polepole, hivyo waliheshimu sana utu na maadili ya Kazi na miiko ya kazi zao.

Zamani watu waioshika nafasi hizo Walionekana ni watu wenye heshima iliotukuka na wazalendo kweli kweli na Jamii ziliwaheshimu sana ila leo jamii inaziona nafasi hizo kama ni zakupewa kwa wateule fulani waliokosa fursa mahali pengine.

Na shauri serikali ianze marekebisho kwa Kurekebisha hili kwenye mkeka wa MA DAS iwapo kutakuwa na mabadiliko kwenye nafasi hizo.
Mama anajaribu kufuta Mwendazake mentality. Hao unaoita wenye uzoefu ndio wametufikisha hapa tulipo
 
Mataqo yako, Mungu akusaidie wewe uache kuliwa na ndizi,

Rais hakuna ,si uhamie nchi yenye rahisi

20210505_040610.jpg
 
Hapana..! Kuchanganya ndio njia bora. Hao watendaji wa serikali unaowasema wawepo, na hao wa mtaani pia wawepo, wa private sector wawepo, wa vyama pinzani wawepo, wa jumuiya na asasi za kiraia pia wawepo, nk. Hapo ndipo tutajenga taifa lenye umoja na mshikamano..
Kuchanganya kama ulivyosema ni sawa,lakini kumchukua PHD holder unaweka kwenye rank mmoja na muigizaji wa bongo movie kwa maoni yangu sio sahihi.
 
Ninashauri ni wakati wa serikali kufikiria namna nzuri kufanya teuzi mbalimbali katika nafasi za serikali kwa kuzingatia uzoefu wa Kazi serikalini, uadilifu ili kutengeneza uzalendo.

Kwa mfano haileti taswira nzuri kumuacha katibu wa tarafa au maafisa wameoshika nyadhifa mbalimbali ktk Idara zao wilayani au mikoani aliekaa kazini miaka 15 na zaidi serikalini mwenye elimu ya kutosha wengine wanawazidi hata elimu Ma DC ma Das na Ma RC lkn ukapuuza utumishi wao ukatoa watu mtaani kuja kuwa Ma DC, DAS, RC’s, RAS etc.

Zamani Kila mfanyakazi alijua iwapo atahudumu kwa mda mrefu na uadilifu angefika katika nafasi ya juu kwa bidii yake ya Kazi uadilifu na kujituma, na hiyo ndio kulikozaa uzalendo hapo zamani ma Afisa utumishi, makatibu tarafa, maafisa maendeleo, kilimo, Afya, Walimu, walipanda nafasi za juu za kiselikali na hiyo ilijenga kuwa na viongozi wengi wenye uadilifu uzalendo na kupenda nchi sbb walipanda nafasi kwa mafaili yao na si kwa majina yao.

Maafisa wakuu wa idara mbalimbali kutoka sekta tofauti mfano elimu, Afya, kilimo, maendelo, utawala iwe wilayani au mkoani wenye miaka 20 ktk kazi, uzoefu na weledi serikalini ndoto zao nao ni kushika nafasi za juu ktk wilaya au mkoa unapowaletea mtu ambae hajawahi kuwa mtumishi huwaongezei tija ila unawavunja moyo na hiyo inashusha uzalendo wa nchi na tija kwenye Kazi zao, Hawa walitegemea miongoni mwao ndio atakaepanda na huo ndio utaratibu wa huko nyuma.

Mfumo huu uangaliwe upya kwa nini mfano makatibu tarafa na maafisa wengine wa wilaya wasipande kuwa Ma DAS na ma DC na wakurugenzi wa halmashauri halafu hao wapya nao wakaanzia chini kupata uzoefu na kupimwa huko chini na kujifunza kujua mifumo ya serikali inafanyaje Kazi kuanzia chini. Huko nyuma hatukuwahi kuona Ma DC ma Ma RC wakivunja maadili sbb walitokana na mfumo mzuri vyeo havikuwapa ukichaa kwani walipanda navyo polepole, hivyo waliheshimu sana utu na maadili ya Kazi na miiko ya kazi zao.

Zamani watu waioshika nafasi hizo Walionekana ni watu wenye heshima iliotukuka na wazalendo kweli kweli na Jamii ziliwaheshimu sana ila leo jamii inaziona nafasi hizo kama ni zakupewa kwa wateule fulani waliokosa fursa mahali pengine.

Na shauri serikali ianze marekebisho kwa Kurekebisha hili kwenye mkeka wa MA DAS iwapo kutakuwa na mabadiliko kwenye nafasi hizo.
Ushauri mzuri sana. Miaka yamwisho ya utawala wa Nyerere, nadhani zaidi ya nusu ya maDC ni watu waliowahi kuwa makatibu watendaji wa Tarafa (kuna kipindi wakiitwa Division Executive Secretary) ; na walitumia madaraka yao vizuri sana na kwa weledi wa juu sana.
 
Kwa nini wanaofanya private sector wanataka kuhamia serikalini? Kwa nini hao wanaotoka private sekta wasianzie kuwa watendaji wa kata au watumishi wa ngazi za chini huko wilayani?
Kila mtanzania ana Uhuru wa kuteuliwa na kufanya serikalini au private, Tena wa serikalini ubunifu huwa ni zero maana wanajua ukipata kazi mpaka uzeeke nayo
 
acha ubinafsi wewe kwani walioko serikalini ndo wana uwezo zaidi ya walio kwenye private sector na NGOs? wakati walipo serikalini hata ukimwambia andika riport ya kiingereza anashindwa kabisa....
 
Kufanya kazi serikalini Ni utumwa wa Aina fulani hivi .

Thamani yako haionekani hata kidogo .

Ukifa kesho wengine watajaza hio nafasi sio wanao Wala ndugu yako ataiziba nafasi yako.

Kuna watu wanafanya kazi Wana masters ,post graduate Ila wapi wanapokea mishahara ya laki laki Hadi Leo hawana marupurupu yeyote .

Mi naona kufanya kazi serikalini iwe Target tu uki hit target unatoka unafanya harakati zingine
 
Sikubaliani na ushaur wako aisee ulisema wawe watumishi wa serikali vipi wanaofanya private sector na wako vizuri hafu unasema achukue waliokaa serikalini 20 years hao hata utendaji huwa wa mazoea Tena hawana exposure yoyote, Bora kuteua hata wa binafsi wenye exposure ili kuleta mabadiliko
Sawa la exposure Ni niambie mtu Kama chopa mchopanga ana exposure gani kwenye Mambo ya serikali .

Kwenye taratibu za uendeshaji wa kazi za kiserikali anajua Nini ?

Exposure unayoiongelea hapa Ni ipi !? Ile kusafiri nje ya nchi au ipi?

Kumchagua DC,RC,auDED kutoka Kita Ni sawa na kuwapeleke wanajeshi general ambaye hajui hata kufanya usafi wa silaha kwa kuzingatia Sheria za usalama wa silaha .

Otherwise utakuwa una faidika na hizi teuzi
 
Sawa la exposure Ni niambie mtu Kama chopa mchopanga ana exposure gani kwenye Mambo ya serikali .

Kwenye taratibu za uendeshaji wa kazi za kiserikali anajua Nini ?

Exposure unayoiongelea hapa Ni ipi !? Ile kusafiri nje ya nchi au ipi?

Kumchagua DC,RC,auDED kutoka Kita Ni sawa na kuwapeleke wanajeshi general ambaye hajui hata kufanya usafi wa silaha kwa kuzingatia Sheria za usalama wa silaha .

Otherwise utakuwa una faidika na hizi teuzi
Sasa huyo mchopanga namjua kwenye bongo movie tu ila Kuna watu wengi wazuri wazoefu na wenye exposure hawako serikalini huko na hawajaingia siasani na ni watendaji wazuri kuliko huko serikalini na wenye maono na hawajapata nafasi. So nafasi zikianza kutolewa kwa utendaji mbona wapo wengi.
 
Ushauri huu ni mzuri mno pia utapunguza wanasiasa uchwara hasa wa chama tawala wanaoishi kwa kuvizia teuzi kila kukicha
 
Back
Top Bottom