kalacha mateo
Senior Member
- Sep 27, 2021
- 122
- 241
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka majaji kuwasaidia wananchi waweze kupata haki zao kwa kuwa wengi hawana uelewa wa nini wafanye. Lakini katika kuhakikisha wanapata haki zao kwa wakati ametoa wito wa mapitio ya sheria ili kupunguza michakato inayosababisha maamuzi ya kesi hizo kuchelewa.
"Natoa wito kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Fedha, pamoja na mwanasheria mkuu na wote wanaohusika kushirikiana na kuzifanyia marekebisho sheria zote zenye mizunguko inayochelewesha kesi na upatikanaji wa haki mapema" - Rais Samia Suluhu
Aidha amesisitiza juu ya hatari ya taifa kupoteza amani ikiwa wananchi watakosa haki zao kwani haki ikipotezwa na amani inakua amna.
"Uwepo wa amani nchini ni chachu ya maendeleo ya kijamii, kisiasa. Mara nyinyi panatokea uvunjifu wa amani, ni kwamba haki imepotezwa, na haki ikopotezwa na amani inakuwa haipo" Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Natoa wito kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Fedha, pamoja na mwanasheria mkuu na wote wanaohusika kushirikiana na kuzifanyia marekebisho sheria zote zenye mizunguko inayochelewesha kesi na upatikanaji wa haki mapema" - Rais Samia Suluhu
Aidha amesisitiza juu ya hatari ya taifa kupoteza amani ikiwa wananchi watakosa haki zao kwani haki ikipotezwa na amani inakua amna.
"Uwepo wa amani nchini ni chachu ya maendeleo ya kijamii, kisiasa. Mara nyinyi panatokea uvunjifu wa amani, ni kwamba haki imepotezwa, na haki ikopotezwa na amani inakuwa haipo" Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.