Rais Samia serikali yako imwachie Mbowe. Siyo gaidi

Damu ya Mbowe inakulilia kwasabb wewe ndiye kiongozi mkuu wa chama tawala na serikali.

Wafuasi wa Mbowe kucha kutwa wanajenga chuki dhidi yako mpk hapo utakapomwachia kiongozi wao.

Familia ya Mbowe inakulilia usiku na mchana, inapoamka, inapokula na inapolala.

Mliopo karibu na Samia mwambieni amwachie Mbowe. Siyo gaidi.

Mkuu ukishafika huko ni sheria tu inayotakiwa kuamua. Subiri tu mbowe atatoka kama hana hatia
 
Damu ya Mbowe inakulilia kwasabb wewe ndiye kiongozi mkuu wa chama tawala na serikali.

Wafuasi wa Mbowe kucha kutwa wanajenga chuki dhidi yako mpk hapo utakapomwachia kiongozi wao.

Familia ya Mbowe inakulilia usiku na mchana, inapoamka, inapokula na inapolala.

Mliopo karibu na Samia mwambieni amwachie Mbowe. Siyo gaidi.
Kama unaeza kushuka kutoka kwenye bed yako na sides zote wewe ni tajiri
 
Aibu Sana viongozi oh amani ,umoja wa taifa. Bora mchawi kuliko mnafiki
 
Hii kesi ni kesi bandia iliyotengenezwa na Serikali. Anachotakiwa Samia ni kufanya toba kwa uovu huu walioutenda dhidi ya Mbowe na wale vijana. Kisha kuwaachia.

Huko siyo kuingilia uhuru wa mahakama. Ni sawa na wewe, kwa hila na uwongo, uende kumshtaki jirani yako mwema kuwa ni jambazi, akakamatwa akawekwa ndani, ukatafuta mashahidi wa uwongo. Kabla ya kesi kwisha, ukaujutia uovu ulioutenda, ukaenda polisi kuomba kesi ifutwe, hiyo haiwezi kutafsiriwa kuwa umeingilia uhuru wa mahakama.

Kuingilia uhuru wa mahakama, ni kama endapo Rais ataiambia mahakama itoe hukumu anayoitaka yeye.

Kwani Katiba ni ishu ya mtu binafsi!?? Kwamba ni Mbowe pekee nchi hii ndie anataka Katiba Mpya

Kama Katiba Mpya ni ishu ya wananchi walio wengi (kama msemavyo Chadema) kwann uhisi Mbowe kakamatwa kisa agenda ya katiba mpya ilhali Chadema yote ilihamasika kwenye hio movements!??
Mbona kina Mnyika, Kigaila, Heche na wengne walihamasisha hii movement lakn hawajashikiliwa kwa makosa ya ugaidi????

Na je agenda ya Katiba Mpya imekufa kisa Mbowe kashikiliwa mahabusu!??

Nijibu haya maswali
 
Kwaiyo wakilia ndo afutiwe tuhuma? Kwani watuhumiwa wengine ambao kesi zao zipo mahakamani hawana ndugu wala jamaa ambao wanawalilia?

Walioko karibu na raisi wanapita humu pia, kwavile unafahamu vyema ili jambo Ebu acha kulialia shusha vielelezo hapa kwann afutiwe izo tuhuma, kwanini hapaswi kutuhumiwa kwa ugaidi ili wampelekee mama amwachie.

Kama huna basi nakushauri kama umeshakula kalale ili jambo limekuzidi uwezo wa kufikiri
 
Msipoteze muda, hao ni wamoja, hapo kuna ajenda wanaitimiza tu, mtaona akitoka rumande haraka sana atalilia kwenda kunywa chai ikulu na kuomba maridhiano.
Wananchi tumieni muda wenu kufanya kazi ili kujenga taifa na familia zenu.
Mwenzenu ana vuta mshiko wake kila siku yaani (per day payments of unconducive environment)

Ushauri wa bure kabisa
 
Ithibitishie jf kwamba kwenye harakati za kupigania katiba mpya, mbowe alikua peke yake!

kama hakua peke yake! na wenzake hawajashitakiwa kwa makosa kama ya mbowe, iambie jf ni kwanini mbowe na si hao wenzake?

lakini vipi kuhusu washitakiwa wa kwanza hadi wa tatu katika kesi hii hii inayomuhusu mbowe, nao walikua kwenye harakati za katiba mpya?
Marehemu alitaka CHADEMA ifutwe. Kazi hiyo alipewa mtungi akishirikiana na ziro, diwani na simba.

Ukasukwa mpango Mbowe upatikane na hatia ya ugaidi, na hivyo Chadema kifutwa kwa grounds za kuwa ni chama cha kigaidi.

Kabla ya hilo kukamilika, roho ya mtawala ikachukuliwa. Mpango mzima ukasitishwa.

Mbowe alivyoanza harakati za kudai katiba mpya, na mama kuonekana amekereka sana na hilo, ziro akapata mwanya wa kuufufua mpango wa awali.

Kule Mza walikamatwa wengi pamoja na Mbowe. Wakiwa ndani, wengine waliachiwa, wengine walibambikiwa kesi mbalimbali. Mbowe wakakubaliana, waendeleze pale walipoachia. Lakini hawakutegemea mambo yaende kama yalivyoenda, ndiyo maana wanahaha sana, na hakuna mwenye uhakika wa kesho yake.
 
Marehemu alitaka CHADEMA ifutwe. Kazi hiyo alipewa mtungi akishirikiana na ziro, diwani na simba.

Ukasukwa mpango Mbowe upatikane na hatia ya ugaidi, na hivyo Chadema kifutwa kwa grounds za kuwa ni chama cha kigaidi.

Kabla ya hilo kukamilika, roho ya mtawala ikachukuliwa. Mpango mzima ukasitishwa.
thibitisha hii ndio tuendelee.
 
Damu ya Mbowe inakulilia kwasabb wewe ndiye kiongozi mkuu wa chama tawala na serikali.

Wafuasi wa Mbowe kucha kutwa wanajenga chuki dhidi yako mpk hapo utakapomwachia kiongozi wao.

Familia ya Mbowe inakulilia usiku na mchana, inapoamka, inapokula na inapolala.

Mliopo karibu na Samia mwambieni amwachie Mbowe. Siyo gaidi.
Samia kashauziwa mbuzi kwenye gunia
 
Marehemu alitaka CHADEMA ifutwe. Kazi hiyo alipewa mtungi akishirikiana na ziro, diwani na simba.

Ukasukwa mpango Mbowe upatikane na hatia ya ugaidi, na hivyo Chadema kifutwa kwa grounds za kuwa ni chama cha kigaidi.

Kabla ya hilo kukamilika, roho ya mtawala ikachukuliwa. Mpango mzima ukasitishwa.

Mbowe alivyoanza harakati za kudai katiba mpya, na mama kuonekana amekereka sana na hilo, ziro akapata mwanya wa kuufufua mpango wa awali.

Kule Mza walikamatwa wengi pamoja na Mbowe. Wakiwa ndani, wengine waliachiwa, wengine walibambikiwa kesi mbalimbali. Mbowe wakakubaliana, waendeleze pale walipoachia. Lakini hawakutegemea mambo yaende kama yalivyoenda, ndiyo maana wanahaha sana, na hakuna mwenye uhakika wa kesho yake.
Kesi imegauka juu chini
 
swala la gaidi mbowe liko kwenye vyombo vya dola,subili mahakama itatoa hukumu,usiwehuke kuhusu mbowe kushitakiwa kwa ugaidi,wewe sio roho yake!!acha kuwehuka subili mahakama itaamua !!
 
Back
Top Bottom