Rais Samia, ni sawa kutaka tuanze upya lakini lazima tuwe na pa kuanzia

Chadema wakati inapigania hoja ya ufisadi ilikua on fire leo hii wapo kupiginia madudu yasioeleweka eti tuzo za BET na kuonyesha mavazi kila jumamosi na kutunisha mfuko wa mwenyekiti kwa kadi za kikoba aibu yao!

Mada hii ni kubwa na ya kufikirisha kuliko huu utoto ulioandika hapa. Ni vyema shule zifunguliwe mapema urudi shule kuliko kuingiza utoto kwenye mada za wakubwa.
 
Anza kuomba msamaha wewe kwanza humu kwenye jukwaa la mficho kisha nenda hadharani ufanye hivyo hivyo ili kutia nguvu hoja yako bila hivyo hizo ni siasa tu ambazo zinashamiri kwa kuendekeza unafiki, uzandiki na majungu

Hii mada imebeba ukweli unaoumiza, na kwakuwa dhamira yako inakusuta, namna pekee ni kuupindisha ili wangalau makali ya ukweli huu yapungue. Hakuna mjadala kuwa Magu alikuwa kiongozi muovu, na aliachwa atakeleze uovu wake kutokana na katiba mbovu. Tunamshukuru Mungu kwa kuamua kumuondoa dunia maana imesababisha nchi hii kutokuendelea kumwaga damu
 
Kwa wale waumini, tunafundishwa kuwa ili upate msamaha ni lazima utubu, na utaratibu wa toba unaeleweka - kamwombe msamaha kwanza uliyemkosea kabla ya kuomba msamaha kwa Mungu.

Kwa mantiki hiyo, Taifa haliwezi kupokea neema ya Mungu kama kwanza hakutakuwa na msamaha miongoni mwa wananchi wenyewe..
Pia utaratibu wa toba lazima utaje makosa yako yote hata uliyofanya gizani.
 
Magufuli alikuwa ni rais muuaji na hilo halina ubishi, kuna watu hadi leo haijulikani waliko na hakutaka kabisa mtu aongelee kutoweka kwao.

Thank God for his timely and a well deserved intervention to end the life of the ruthless butcher.
 
Malezi bora utoa familia bora familia bora utoa viongozi bora, watawala wa kiafrica ni zao la ukosefu wa malezi bora kwenye familia.
Mtoto aliyezoea kupigwa viboko ndio atii huyu lazima atakuwa dikteta akipewa leseni ya kuongozea watu.
 
Waliokomalia sheria ya kutoza faini ya shs 30,000 kwa bodaboda bado wamo bungeni, hao hao wanashangilia faini kushushwa; utadhani wakati ule ubongo ulikuwa umefunikwa kwa kitambaa, sasa umefunuliwa Tazama na hii

Ili uishi bungeni ni lzm uendane na mdundo
 
Kuna kitu kikubwa sana kwenye mamlaka na utakijua tu ukisha kuwa nayo. Ni utamu ambao ukionja kuachia ni kazi kubwa sana yataka moyo na neema ya Mungu.
Zao rahisi la mamlaka ni kiburi na dhulma. Wanaotambua hili hutawala kwa haki!
 
Shinda kubwa katika taifa letu ni unafiki na watu kuwa wazalendo kwa viongozi na sio taifa haya mambo yataendelea Mpaka siku wananchi watambue haki zao
 
Rais Samia mara baada ya kuapishwa alisema, tuanze upya. Sentensi ile ilibeba maana nzito iliyofichika kwa wasiotaka kutafakari.

Unaanza upya pale ambapo unaamini ulikosea, na ili uanze upya ni lazima ufahamu ulipokuwa, ulipokosea na namna ulivyokosea, ili unapoanza upya usiingie kwenye makosa ya mwanzo. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unajenga mifumo itakayozuia kabisa kuangukia kwenye makosa ya mwanzo.

Sote, tunafahamu utawala wa awamu ya 5 ulivyoleta madhira mengi kwa watu wengi. Na wengi wao hawatausahau utawala wa awamu ya 5 kwa mabaya. Na wengine hawana nafasi hata ya kuukumbuka maana hawapo katika Ulimwengu huu. Bila shaka hao wameyafikisha masikitiko yao kwa mkuu wa Mbingu/ahera na Ulimwengu.

Fikiria ndugu, wanafamilia, marafiki wa waliopotezwa au kuuawa:

Ben Saanane
Azory Gwanda
Kanguye
Yule diwani wa Dar
Yule diwani Kilosa
Akwilina

Wafikirie waliojeruhiwa na familia zao:

Tundu Lisu
Na wengine wengi ambao majina yao siyo makubwa

Wafikirie walioporwa pesa kupitia TRA na wasiojulikana.

Wafikirie waliowekwa ndani kwa kesi za kubambikiwa, n.k.

Wafikirie akina Mbowe, Halima Mdee, Msigwa, n.k. waliowekwa ndani kwa tuhuma za kutengenezwa za kumwua Akwilina, huku wote tukijua kuwa Akwilina aliuawa na Polisi.

Watu wamepoteza wapendwa wao, watu wamefanywa kuwa vilema, watu wamepoteza fedha zao walizozipata kwa taabu na mateso, watu wameteseka mahabusu kwa kesi za kutengenezwa, watu wamedhalilishwa kwa kuvuliwa nguo mpaka kupekuliwa kwenye njia za siri, watu wamewekwa mahabusu kwa kesi za kihayawani, watu wamepoteza ajira baada ya waajiri wengi kufunga makampuni yao kutokana na mazingira mabaya ya uwekezaji, n.k, hivi hawa unaweza tu kuwaambia kuwa TUANZE UPYA, na kweli tukaanza upya?

Yaani tuanze upya, tusahau yote, huku:
Waliomteka na kumpoteza Ben Saanane wakifahamika na kuranda mitaani,
Huku waliomchukua na kumpoteza Azory Gwanda mbele ya familia yake, wakiwa wanafahamika, na wanaranda mitaani,

Huku waliomwua Akwilina wakiwa wanafahamika wazi, na wanaendelea kukalia viti vya ofisi za umma,

Huku waliomfyatulia risasi Tundu Lisu wakiwa wanafahamika na wanarandarandaranda mitaani,

Huku waliowabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi, wakibadilishiwa ofisi,

Huku waliowabambikizia watu kesi za madawa ya kulevya, wakiwa wanaranda mitaani,

Huku waliowadhulumu watu pesa zao halali kupitia madai ya uwongo ya uhujumu uchumi wakiwa wamejaa tele maofisini?

Wenzetu kule Afrika Kusini, walipoamua kuanza upya, waliunda Tume ya maridhiano iliyoongozwa na Askofu Desmond Tutu. Tume hii ilizungumza na waathirika wote, watenda maovu, watunga sheria na sera, na kisha kuweka kila kitu wazi ikiwa ni pamoja na watenda maovu waliokuwa hai, kuomba msamaha. Hiyo ilileta faraja ya moyo japo haikufuta machozi ya walioumizwa.

Kama hatutafanya hivyo, hakika hii kuamza upya itabakia kuwa midomoni lakini mioyo ya watu bado ni mizito dhidi ya watenda maovu wote, maana wengi wao wanafahamika.

Utawala wa Mama Samia una nafuu kubwa lakini hauwezi kuwa na utakatifu kwa sababu ndani yake wale wauaji wamo, wale watesaji wamo, waliokuwa wanabambikizia watu kesi bado wamo, waliokuwa wanawaweka mahabusu wanasiasa wa upinzani kwa uonevu bado wamo.

Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5.

Mama Samia tunakuomba uliunganishe Taifa. Kwanza tupate taarifa kamili za walioiawa na kupotezwa, tuomboleze na waliowapoteza wanafamilia wao, tuwaombe msamaha maana kama jamii tulishindwa kutetea uhai wa hawa Watanzania wenzetu. Lililo kubwa zaidi, kama Taifa turudi kwenye kutengeneza Katiba mpya na kubadilisha baadhi ya sheria, ili mfumo wetu usiruhusu kuwapata viongozi/watawala dhulumati katika ngazi yoyote ile kama ilivyotokea wakati wa awamu ya 5. Leo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu, DC anashtakiwa kwa kosa la kuwa kiongozi wa genge la majambazi! Laana kubwa hii.
well
 
Hivi huwa hamna la maana kufanya?
Kujua ni lipi la maana na lipi siyo la maana inahitaji angalao kiwango fulani cha chini cha ufahamu. Kama hujakifikia, unaweza kuona kila ambacho watu wanajadili hakina maana, ila wakiongelea ubwabwa, biriani, hapo utaona wameongea cha maana, kwa sababu hata aliyepungukiwa akili, angalao anajua lazima ale.
 
Anza kuomba msamaha wewe kwanza humu kwenye jukwaa la mficho kisha nenda hadharani ufanye hivyo hivyo ili kutia nguvu hoja yako bila hivyo hizo ni siasa tu ambazo zinashamiri kwa kuendekeza unafiki, uzandiki na majungu
Ungewaacha kwanza wenye uelewa wajadili.
 
Km hukushangilia wewe wengine walishangilia...dunia hii ina mambo ndugu yangu..it is what it is...kwahio songa mbele..kesho unaeza chomwa chanjo ukapotea vilevile, who cares...utakuwa sio wa kwanza kufa...at the end of the day we will all die...
Hakuna asiyejua kuwa kifo kipo na ndiyo mwisho wa maisha ya kila mwanadamu aishiye hapa Duniani. Suala siyo kuishi au kufa, cha muhimu uliishi vipi ukiwa hai, uliwasaidiaje Dunia na Taifa lako kuwa mahali pema pa kuishi wanadamu wa leo na kesho? Ulikuja kuitengeneza au kuiharibu Dunia? Kama huwezi kuiboresha Dunia, kama huwezi kuchangia ustawi wa wanadamu na Dunia kwa ujumla, ni aheri usingelizaliwa.

Mwanadamu mwenye hekima, kwa muda mfupi aliopewa kuishi Duniani, hujenga kumbukumbu yake ya kukumbukwa kwa mema, na siyo kwa kuteka, kuua na kutesa wanadamu wenzake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom