Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,526
- 41,040
Rais Samia mara baada ya kuapishwa alisema, tuanze upya. Sentensi ile ilibeba maana nzito iliyofichika kwa wasiotaka kutafakari.
Unaanza upya pale ambapo unaamini ulikosea, na ili uanze upya ni lazima ufahamu ulipokuwa, ulipokosea na namna ulivyokosea, ili unapoanza upya usiingie kwenye makosa ya mwanzo. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unajenga mifumo itakayozuia kabisa kuangukia kwenye makosa ya mwanzo.
Sote, tunafahamu utawala wa awamu ya 5 ulivyoleta madhira mengi kwa watu wengi. Na wengi wao hawatausahau utawala wa awamu ya 5 kwa mabaya. Na wengine hawana nafasi hata ya kuukumbuka maana hawapo katika Ulimwengu huu. Bila shaka hao wameyafikisha masikitiko yao kwa mkuu wa Mbingu/ahera na Ulimwengu.
Fikiria ndugu, wanafamilia, marafiki wa waliopotezwa au kuuawa:
Ben Saanane
Azory Gwanda
Kanguye
Yule diwani wa Dar
Yule diwani Kilosa
Akwilina
Wafikirie waliojeruhiwa na familia zao:
Tundu Lisu
Na wengine wengi ambao majina yao siyo makubwa
Wafikirie walioporwa pesa kupitia TRA na wasiojulikana.
Wafikirie waliowekwa ndani kwa kesi za kubambikiwa, n.k.
Wafikirie akina Mbowe, Halima Mdee, Msigwa, n.k. waliowekwa ndani kwa tuhuma za kutengenezwa za kumwua Akwilina, huku wote tukijua kuwa Akwilina aliuawa na Polisi.
Watu wamepoteza wapendwa wao, watu wamefanywa kuwa vilema, watu wamepoteza fedha zao walizozipata kwa taabu na mateso, watu wameteseka mahabusu kwa kesi za kutengenezwa, watu wamedhalilishwa kwa kuvuliwa nguo mpaka kupekuliwa kwenye njia za siri, watu wamewekwa mahabusu kwa kesi za kihayawani, watu wamepoteza ajira baada ya waajiri wengi kufunga makampuni yao kutokana na mazingira mabaya ya uwekezaji, n.k, hivi hawa unaweza tu kuwaambia kuwa TUANZE UPYA, na kweli tukaanza upya?
Yaani tuanze upya, tusahau yote, huku:
Waliomteka na kumpoteza Ben Saanane wakifahamika na kuranda mitaani,
Huku waliomchukua na kumpoteza Azory Gwanda mbele ya familia yake, wakiwa wanafahamika, na wanaranda mitaani,
Huku waliomwua Akwilina wakiwa wanafahamika wazi, na wanaendelea kukalia viti vya ofisi za umma,
Huku waliomfyatulia risasi Tundu Lisu wakiwa wanafahamika na wanarandarandaranda mitaani,
Huku waliowabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi, wakibadilishiwa ofisi,
Huku waliowabambikizia watu kesi za madawa ya kulevya, wakiwa wanaranda mitaani,
Huku waliowadhulumu watu pesa zao halali kupitia madai ya uwongo ya uhujumu uchumi wakiwa wamejaa tele maofisini?
Wenzetu kule Afrika Kusini, walipoamua kuanza upya, waliunda Tume ya maridhiano iliyoongozwa na Askofu Desmond Tutu. Tume hii ilizungumza na waathirika wote, watenda maovu, watunga sheria na sera, na kisha kuweka kila kitu wazi ikiwa ni pamoja na watenda maovu waliokuwa hai, kuomba msamaha. Hiyo ilileta faraja ya moyo japo haikufuta machozi ya walioumizwa.
Kama hatutafanya hivyo, hakika hii kuamza upya itabakia kuwa midomoni lakini mioyo ya watu bado ni mizito dhidi ya watenda maovu wote, maana wengi wao wanafahamika.
Utawala wa Mama Samia una nafuu kubwa lakini hauwezi kuwa na utakatifu kwa sababu ndani yake wale wauaji wamo, wale watesaji wamo, waliokuwa wanabambikizia watu kesi bado wamo, waliokuwa wanawaweka mahabusu wanasiasa wa upinzani kwa uonevu bado wamo.
Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5.
Mama Samia tunakuomba uliunganishe Taifa. Kwanza tupate taarifa kamili za walioiawa na kupotezwa, tuomboleze na waliowapoteza wanafamilia wao, tuwaombe msamaha maana kama jamii tulishindwa kutetea uhai wa hawa Watanzania wenzetu. Lililo kubwa zaidi, kama Taifa turudi kwenye kutengeneza Katiba mpya na kubadilisha baadhi ya sheria, ili mfumo wetu usiruhusu kuwapata viongozi/watawala dhulumati katika ngazi yoyote ile kama ilivyotokea wakati wa awamu ya 5. Leo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu, DC anashtakiwa kwa kosa la kuwa kiongozi wa genge la majambazi! Laana kubwa hii.
Unaanza upya pale ambapo unaamini ulikosea, na ili uanze upya ni lazima ufahamu ulipokuwa, ulipokosea na namna ulivyokosea, ili unapoanza upya usiingie kwenye makosa ya mwanzo. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unajenga mifumo itakayozuia kabisa kuangukia kwenye makosa ya mwanzo.
Sote, tunafahamu utawala wa awamu ya 5 ulivyoleta madhira mengi kwa watu wengi. Na wengi wao hawatausahau utawala wa awamu ya 5 kwa mabaya. Na wengine hawana nafasi hata ya kuukumbuka maana hawapo katika Ulimwengu huu. Bila shaka hao wameyafikisha masikitiko yao kwa mkuu wa Mbingu/ahera na Ulimwengu.
Fikiria ndugu, wanafamilia, marafiki wa waliopotezwa au kuuawa:
Ben Saanane
Azory Gwanda
Kanguye
Yule diwani wa Dar
Yule diwani Kilosa
Akwilina
Wafikirie waliojeruhiwa na familia zao:
Tundu Lisu
Na wengine wengi ambao majina yao siyo makubwa
Wafikirie walioporwa pesa kupitia TRA na wasiojulikana.
Wafikirie waliowekwa ndani kwa kesi za kubambikiwa, n.k.
Wafikirie akina Mbowe, Halima Mdee, Msigwa, n.k. waliowekwa ndani kwa tuhuma za kutengenezwa za kumwua Akwilina, huku wote tukijua kuwa Akwilina aliuawa na Polisi.
Watu wamepoteza wapendwa wao, watu wamefanywa kuwa vilema, watu wamepoteza fedha zao walizozipata kwa taabu na mateso, watu wameteseka mahabusu kwa kesi za kutengenezwa, watu wamedhalilishwa kwa kuvuliwa nguo mpaka kupekuliwa kwenye njia za siri, watu wamewekwa mahabusu kwa kesi za kihayawani, watu wamepoteza ajira baada ya waajiri wengi kufunga makampuni yao kutokana na mazingira mabaya ya uwekezaji, n.k, hivi hawa unaweza tu kuwaambia kuwa TUANZE UPYA, na kweli tukaanza upya?
Yaani tuanze upya, tusahau yote, huku:
Waliomteka na kumpoteza Ben Saanane wakifahamika na kuranda mitaani,
Huku waliomchukua na kumpoteza Azory Gwanda mbele ya familia yake, wakiwa wanafahamika, na wanaranda mitaani,
Huku waliomwua Akwilina wakiwa wanafahamika wazi, na wanaendelea kukalia viti vya ofisi za umma,
Huku waliomfyatulia risasi Tundu Lisu wakiwa wanafahamika na wanarandarandaranda mitaani,
Huku waliowabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi, wakibadilishiwa ofisi,
Huku waliowabambikizia watu kesi za madawa ya kulevya, wakiwa wanaranda mitaani,
Huku waliowadhulumu watu pesa zao halali kupitia madai ya uwongo ya uhujumu uchumi wakiwa wamejaa tele maofisini?
Wenzetu kule Afrika Kusini, walipoamua kuanza upya, waliunda Tume ya maridhiano iliyoongozwa na Askofu Desmond Tutu. Tume hii ilizungumza na waathirika wote, watenda maovu, watunga sheria na sera, na kisha kuweka kila kitu wazi ikiwa ni pamoja na watenda maovu waliokuwa hai, kuomba msamaha. Hiyo ilileta faraja ya moyo japo haikufuta machozi ya walioumizwa.
Kama hatutafanya hivyo, hakika hii kuamza upya itabakia kuwa midomoni lakini mioyo ya watu bado ni mizito dhidi ya watenda maovu wote, maana wengi wao wanafahamika.
Utawala wa Mama Samia una nafuu kubwa lakini hauwezi kuwa na utakatifu kwa sababu ndani yake wale wauaji wamo, wale watesaji wamo, waliokuwa wanabambikizia watu kesi bado wamo, waliokuwa wanawaweka mahabusu wanasiasa wa upinzani kwa uonevu bado wamo.
Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5.
Mama Samia tunakuomba uliunganishe Taifa. Kwanza tupate taarifa kamili za walioiawa na kupotezwa, tuomboleze na waliowapoteza wanafamilia wao, tuwaombe msamaha maana kama jamii tulishindwa kutetea uhai wa hawa Watanzania wenzetu. Lililo kubwa zaidi, kama Taifa turudi kwenye kutengeneza Katiba mpya na kubadilisha baadhi ya sheria, ili mfumo wetu usiruhusu kuwapata viongozi/watawala dhulumati katika ngazi yoyote ile kama ilivyotokea wakati wa awamu ya 5. Leo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu, DC anashtakiwa kwa kosa la kuwa kiongozi wa genge la majambazi! Laana kubwa hii.