Rais Samia, ni sawa kutaka tuanze upya lakini lazima tuwe na pa kuanzia

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,526
41,040
Rais Samia mara baada ya kuapishwa alisema, tuanze upya. Sentensi ile ilibeba maana nzito iliyofichika kwa wasiotaka kutafakari.

Unaanza upya pale ambapo unaamini ulikosea, na ili uanze upya ni lazima ufahamu ulipokuwa, ulipokosea na namna ulivyokosea, ili unapoanza upya usiingie kwenye makosa ya mwanzo. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unajenga mifumo itakayozuia kabisa kuangukia kwenye makosa ya mwanzo.

Sote, tunafahamu utawala wa awamu ya 5 ulivyoleta madhira mengi kwa watu wengi. Na wengi wao hawatausahau utawala wa awamu ya 5 kwa mabaya. Na wengine hawana nafasi hata ya kuukumbuka maana hawapo katika Ulimwengu huu. Bila shaka hao wameyafikisha masikitiko yao kwa mkuu wa Mbingu/ahera na Ulimwengu.

Fikiria ndugu, wanafamilia, marafiki wa waliopotezwa au kuuawa:

Ben Saanane
Azory Gwanda
Kanguye
Yule diwani wa Dar
Yule diwani Kilosa
Akwilina

Wafikirie waliojeruhiwa na familia zao:

Tundu Lisu
Na wengine wengi ambao majina yao siyo makubwa

Wafikirie walioporwa pesa kupitia TRA na wasiojulikana.

Wafikirie waliowekwa ndani kwa kesi za kubambikiwa, n.k.

Wafikirie akina Mbowe, Halima Mdee, Msigwa, n.k. waliowekwa ndani kwa tuhuma za kutengenezwa za kumwua Akwilina, huku wote tukijua kuwa Akwilina aliuawa na Polisi.

Watu wamepoteza wapendwa wao, watu wamefanywa kuwa vilema, watu wamepoteza fedha zao walizozipata kwa taabu na mateso, watu wameteseka mahabusu kwa kesi za kutengenezwa, watu wamedhalilishwa kwa kuvuliwa nguo mpaka kupekuliwa kwenye njia za siri, watu wamewekwa mahabusu kwa kesi za kihayawani, watu wamepoteza ajira baada ya waajiri wengi kufunga makampuni yao kutokana na mazingira mabaya ya uwekezaji, n.k, hivi hawa unaweza tu kuwaambia kuwa TUANZE UPYA, na kweli tukaanza upya?

Yaani tuanze upya, tusahau yote, huku:
Waliomteka na kumpoteza Ben Saanane wakifahamika na kuranda mitaani,
Huku waliomchukua na kumpoteza Azory Gwanda mbele ya familia yake, wakiwa wanafahamika, na wanaranda mitaani,

Huku waliomwua Akwilina wakiwa wanafahamika wazi, na wanaendelea kukalia viti vya ofisi za umma,

Huku waliomfyatulia risasi Tundu Lisu wakiwa wanafahamika na wanarandarandaranda mitaani,

Huku waliowabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi, wakibadilishiwa ofisi,

Huku waliowabambikizia watu kesi za madawa ya kulevya, wakiwa wanaranda mitaani,

Huku waliowadhulumu watu pesa zao halali kupitia madai ya uwongo ya uhujumu uchumi wakiwa wamejaa tele maofisini?

Wenzetu kule Afrika Kusini, walipoamua kuanza upya, waliunda Tume ya maridhiano iliyoongozwa na Askofu Desmond Tutu. Tume hii ilizungumza na waathirika wote, watenda maovu, watunga sheria na sera, na kisha kuweka kila kitu wazi ikiwa ni pamoja na watenda maovu waliokuwa hai, kuomba msamaha. Hiyo ilileta faraja ya moyo japo haikufuta machozi ya walioumizwa.

Kama hatutafanya hivyo, hakika hii kuamza upya itabakia kuwa midomoni lakini mioyo ya watu bado ni mizito dhidi ya watenda maovu wote, maana wengi wao wanafahamika.

Utawala wa Mama Samia una nafuu kubwa lakini hauwezi kuwa na utakatifu kwa sababu ndani yake wale wauaji wamo, wale watesaji wamo, waliokuwa wanabambikizia watu kesi bado wamo, waliokuwa wanawaweka mahabusu wanasiasa wa upinzani kwa uonevu bado wamo.

Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5.

Mama Samia tunakuomba uliunganishe Taifa. Kwanza tupate taarifa kamili za walioiawa na kupotezwa, tuomboleze na waliowapoteza wanafamilia wao, tuwaombe msamaha maana kama jamii tulishindwa kutetea uhai wa hawa Watanzania wenzetu. Lililo kubwa zaidi, kama Taifa turudi kwenye kutengeneza Katiba mpya na kubadilisha baadhi ya sheria, ili mfumo wetu usiruhusu kuwapata viongozi/watawala dhulumati katika ngazi yoyote ile kama ilivyotokea wakati wa awamu ya 5. Leo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu, DC anashtakiwa kwa kosa la kuwa kiongozi wa genge la majambazi! Laana kubwa hii.
 
Endelea kumchochea ili azidi kuharibu zaidi.

"..Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5...."

Kwa ufupi ni kwamba hana uwezo wa kuwaondoa wote uliowataja kwa kuwa aliyewawekwa bahati mbaya aliondoka na funguo zake, labda abomoe mlango kuingia ndani au apitie dirishani yaani aandae uchaguzi upya kisha watakaopatikana ndio watakuwa watiifu kwake kwa asilimia kubwa ijapokuwa ni za unafiki. Kila mmoja anatetea tumbo binafsi na familia yake sio kwa manufaa ya taifa.

Maelezo mengi uliyotoa yamejaa visasi moyoni, kwa mtazamo huo tiba haiwezekani kupatikana kamwe.

Amani na mshikamano wa taifa la Tanzania utategemea Majaliwa ya Mwenyezi Mungu sio Suluhu za kibinadamu ambazo ni ubatili na kujilisha upepo
 
Chadema wakati inapigania hoja ya ufisadi ilikua on fire leo hii wapo kupiginia madudu yasioeleweka eti tuzo za BET na kuonyesha mavazi kila jumamosi na kutunisha mfuko wa mwenyekiti kwa kadi za kikoba aibu yao!
 
Endelea kumchochea ili azidi kuharibu zaidi.

"..Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5...."

Kwa ufupi ni kwamba hana uwezo wa kuwaondoa wote uliowataja kwa kuwa aliyewawekwa bahati mbaya aliondoka na funguo zake, labda abomoe mlango kuingia ndani au apitie dirishani yaani aandae uchaguzi upya kisha watakaopatikana ndio watakuwa watiifu kwake kwa asilimia kubwa ijapokuwa ni za unafiki. Kila mmoja anatetea tumbo binafsi na familia yake sio kwa manufaa ya taifa.

Maelezo mengi uliyotoa yamejaa visasi moyoni, kwa mtazamo huo tiba haiwezekani kupatikana kamwe.

Amani na mshikamano wa taifa la Tanzania utategemea Majaliwa ya Mwenyezi Mungu sio Suluhu za kibinadamu ambazo ni ubatili na kujilisha upepo
Kwa wale waumini, tunafundishwa kuwa ili upate msamaha ni lazima utubu, na utaratibu wa toba unaeleweka - kamwombe msamaha kwanza uliyemkosea kabla ya kuomba msamaha kwa Mungu.

Kwa mantiki hiyo, Taifa haliwezi kupokea neema ya Mungu kama kwanza hakutakuwa na msamaha miongoni mwa wananchi wenyewe..
 
Bora umeandika ili yakutoke tu rohoni. Majibu yake sahau hadi kiama.
Sisi wanananchi jukumu letu la kwanza kwa Taifa letu ni kunena - yaweza kuwa ni kushauri, kuonya, kukosoa, kupongeza au kulaani.

Waliopo katika uongozi, jukumu lao mojawapo ni kufanyia kazi kauli au kupuuza. Lakini mwisho wa yote kauli za umma, zenye lengo jema, zikipuuzwa wakati wote, kuna siku umma utachukua hatua, tena yaweza kuwa sio waliokuwa wakitoa kauli.
 
Rais Samia mara baada ya kuapishwa alisema, tuanze upya. Sentensi ile ilibeba maana nzito iliyofichika kwa wasiotaka kutafakari.

Unaanza upya pale ambapo unaamini ulikosea, na ili uanze upya ni lazima ufahamu ulipokuwa, ulipokosea na namna ulivyokosea, ili unapoanza upya usiingie kwenye makosa ya mwanzo. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba unajenga mifumo itakayozuia kabisa kuangukia kwenye makosa ya mwanzo.

Sote, tunafahamu utawala wa awamu ya 5 ulivyoleta madhira mengi kwa watu wengi. Na wengi wao hawatausahau utawala wa awamu ya 5 kwa mabaya. Na wengine hawana nafasi hata ya kuukumbuka maana hawapo katika Ulimwengu huu. Bila shaka hao wameyafikisha masikitiko yao kwa mkuu wa Mbingu/ahera na Ulimwengu.

Fikiria ndugu, wanafamilia, marafiki wa waliopotezwa au kuuawa:

Ben Saanane
Azory Gwanda
Kanguye
Yule diwani wa Dar
Yule diwani Kilosa
Akwilina

Wafikirie waliojeruhiwa na familia zao:

Tundu Lisu
Na wengine wengi ambao majina yao siyo makubwa

Wafikirie walioporwa pesa kupitia TRA na wasiojulikana.

Wafikirie waliowekwa ndani kwa kesi za kubambikiwa, n.k.

Wafikirie akina Mbowe, Halima Mdee, Msigwa, n.k. waliowekwa ndani kwa tuhuma za kutengenezwa za kumwua Akwilina, huku wote tukijua kuwa Akwilina aliuawa na Polisi.

Watu wamepoteza wapendwa wao, watu wamefanywa kuwa vilema, watu wamepoteza fedha zao walizozipata kwa taabu na mateso, watu wameteseka mahabusu kwa kesi za kutengenezwa, watu wamedhalilishwa kwa kuvuliwa nguo mpaka kupekuliwa kwenye njia za siri, watu wamewekwa mahabusu kwa kesi za kihayawani, watu wamepoteza ajira baada ya waajiri wengi kufunga makampuni yao kutokana na mazingira mabaya ya uwekezaji, n.k, hivi hawa unaweza tu kuwaambia kuwa TUANZE UPYA, na kweli tukaanza upya?

Yaani tuanze upya, tusahau yote, huku:
Waliomteka na kumpoteza Ben Saanane wakifahamika na kuranda mitaani,
Huku waliomchukua na kumpoteza Azory Gwanda mbele ya familia yake, wakiwa wanafahamika, na wanaranda mitaani,

Huku waliomwua Akwilina wakiwa wanafahamika wazi, na wanaendelea kukalia viti vya ofisi za umma,

Huku waliomfyatulia risasi Tundu Lisu wakiwa wanafahamika na wanarandarandaranda mitaani,

Huku waliowabambikizia watu kesi za uhujumu uchumi, wakibadilishiwa ofisi,

Huku waliowabambikizia watu kesi za madawa ya kulevya, wakiwa wanaranda mitaani,

Huku waliowadhulumu watu pesa zao halali kupitia madai ya uwongo ya uhujumu uchumi wakiwa wamejaa tele maofisini?

Wenzetu kule Afrika Kusini, walipoamua kuanza upya, waliunda Tume ya maridhiano iliyoongozwa na Askofu Desmond Tutu. Tume hii ilizungumza na waathirika wote, watenda maovu, watunga sheria na sera, na kisha kuweka kila kitu wazi ikiwa ni pamoja na watenda maovu waliokuwa hai, kuomba msamaha. Hiyo ilileta faraja ya moyo japo haikufuta machozi ya walioumizwa.

Kama hatutafanya hivyo, hakika hii kuamza upya itabakia kuwa midomoni lakini mioyo ya watu bado ni mizito dhidi ya watenda maovu wote, maana wengi wao wanafahamika.

Utawala wa Mama Samia una nafuu kubwa lakini hauwezi kuwa na utakatifu kwa sababu ndani yake wale wauaji wamo, wale watesaji wamo, waliokuwa wanabambikizia watu kesi bado wamo, waliokuwa wanawaweka mahabusu wanasiasa wa upinzani kwa uonevu bado wamo.

Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5.

Mama Samia tunakuomba uliunganishe Taifa. Kwanza tupate taarifa kamili za walioiawa na kupotezwa, tuomboleze na waliowapoteza wanafamilia wao, tuwaombe msamaha maana kama jamii tulishindwa kutetea uhai wa hawa Watanzania wenzetu. Lililo kubwa zaidi, kama Taifa turudi kwenye kutengeneza Katiba mpya na kubadilisha baadhi ya sheria, ili mfumo wetu usiruhusu kuwapata viongozi/watawala dhulumati katika ngazi yoyote ile kama ilivyotokea wakati wa awamu ya 5. Leo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Taifa letu, DC anashtakiwa kwa kosa la kuwa kiongozi wa genge la majambazi! Laana kubwa hii.
Hivi huwa hamna la maana kufanya?
 
Kwa wale waumini, tunafundishwa kuwa ili upate msamaha ni lazima utubu, na utaratibu wa toba unaeleweka - kamwombe msamaha kwanza uliyemkosea kabla ya kuomba msamaha kwa Mungu.

Kwa mantiki hiyo, Taifa haliwezi kupokea neema ya Mungu kama kwanza hakutakuwa na msamaha miongoni mwa wananchi wenyewe..
What are you talking about?!...Fanya kazi ulishe familia yako na wewe usubirie kudondoka..hakuna mtu ataishi milele hapa duniani..

Waliokufa wakipigania uhuru/mapinduzi sio watu, waliokufa kwenye uchaguzi sio watu, watu wameenza kupotea awamu ya tano tu?!...hata wewe sasa hv jitoe fahamu uone km hutopotezwa...

Tulia....tii mamlaka...
 
Endelea kumchochea ili azidi kuharibu zaidi.

"..Hawa wasipoondolewa, wasipotubu, utawala wa Mama Samia bado utaendelea kutembea na laana ya utawala wa awamu ya 5...."

Kwa ufupi ni kwamba hana uwezo wa kuwaondoa wote uliowataja kwa kuwa aliyewawekwa bahati mbaya aliondoka na funguo zake, labda abomoe mlango kuingia ndani au apitie dirishani yaani aandae uchaguzi upya kisha watakaopatikana ndio watakuwa watiifu kwake kwa asilimia kubwa ijapokuwa ni za unafiki. Kila mmoja anatetea tumbo binafsi na familia yake sio kwa manufaa ya taifa.

Maelezo mengi uliyotoa yamejaa visasi moyoni, kwa mtazamo huo tiba haiwezekani kupatikana kamwe.

Amani na mshikamano wa taifa la Tanzania utategemea Majaliwa ya Mwenyezi Mungu sio Suluhu za kibinadamu ambazo ni ubatili na kujilisha upepo
Naunga mkono

Jamaa amesahau Dr Ulimboka, Sengondo Mvungi, Kibanda, Kubenea, Mwangosi, Profesa Juan
 
What are you talking about?!...Fanya kazi ulishe familia yako na wewe usubirie kudondoka..hakuna mtu ataishi milele hapa duniani..

Waliokufa wakipigania uhuru/mapinduzi sio watu, waliokufa kwenye uchaguzi sio watu, watu wameenza kupotea awamu ya tano tu?!...hata wewe sasa hv jitoe fahamu uone km hutopotezwa...

Tulia....tii mamlaka...
Pumbavu.
 
Pia katika kuanza upya tusiwasahau viongozi wote wa serikali ngazi za mtaa na vitongoji waliouwawa kwa kupigwa risasi na makundi ya watu waliokuwa na nia ya kutaka eneo lote Mkuranga, Kisiju na Rufiji lisitawalike. Wakitaka iwepo serikali ndani ya serikali halali.

Ulihitajika uimara wa JWTZ kuweza kuwavurumisha bila ya huruma, wengi wao wakakimbilia ndani ya nyumba za ibada wakidhani itakuwa salama yao, humo humo ndani wakapewa adhabu nzito. Wachache ndio hawa wapo huko Msumbiji.

Yamefanyika mengi mabaya na damu zimemwagika, zisizo na hatia yoyote. Ipo haja ya kuendelea kuliweka taifa hili mikononi mwa Mungu.
 
Mama Samia ahakikishe wananchi tunapata maendeleo. Hizi siasa zenu hazituletei mlo nyuumbani. Ombeni audiance naye mkamwambie.
Sisi tunataka biashara zetu zifunguliwe. Miradi ya serikali ya maendeleo ikamilike. Bygones are bygones
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Waliokomalia sheria ya kutoza faini ya shs 30,000 kwa bodaboda bado wamo bungeni, hao hao wanashangilia faini kushushwa; utadhani wakati ule ubongo ulikuwa umefunikwa kwa kitambaa, sasa umefunuliwa Tazama na hii
 
What are you talking about?!...Fanya kazi ulishe familia yako na wewe usubirie kudondoka..hakuna mtu ataishi milele hapa duniani..

Waliokufa wakipigania uhuru/mapinduzi sio watu, waliokufa kwenye uchaguzi sio watu, watu wameenza kupotea awamu ya tano tu?!...hata wewe sasa hv jitoe fahamu uone km hutopotezwa...

Tulia....tii mamlaka...
Punguza bangi basi. Kwa hiyo ni halali kuua watu kisa tu walikuwa wakiuliwa hata zamani au hao waliokufa wakipigania uhuru kuna walioshangilia vifo vyao.

Please come to your senses and be informed accordingly.
 
What are you talking about?!...Fanya kazi ulishe familia yako na wewe usubirie kudondoka..hakuna mtu ataishi milele hapa duniani..

Waliokufa wakipigania uhuru/mapinduzi sio watu, waliokufa kwenye uchaguzi sio watu, watu wameenza kupotea awamu ya tano tu?!...hata wewe sasa hv jitoe fahamu uone km hutopotezwa...

Tulia....tii mamlaka...
Acha kutisha watu. Mamlaka sahihi inatoka kwa Mungu,si akina Magufuli wenu hao.
 
Punguza bangi basi. Kwa hiyo ni halali kuua watu kisa tu walikuwa wakiuliwa hata zamani au hao waliokufa wakipigania uhuru kuna walioshangilia vifo vyao.

Please come to your senses and be informed accordingly.
Km hukushangilia wewe wengine walishangilia...dunia hii ina mambo ndugu yangu..it is what it is...kwahio songa mbele..kesho unaeza chomwa chanjo ukapotea vilevile, who cares...utakuwa sio wa kwanza kufa...at the end of the day we will all die...
 
Kwa wale waumini, tunafundishwa kuwa ili upate msamaha ni lazima utubu, na utaratibu wa toba unaeleweka - kamwombe msamaha kwanza uliyemkosea kabla ya kuomba msamaha kwa Mungu.

Kwa mantiki hiyo, Taifa haliwezi kupokea neema ya Mungu kama kwanza hakutakuwa na msamaha miongoni mwa wananchi wenyewe..
Anza kuomba msamaha wewe kwanza humu kwenye jukwaa la mficho kisha nenda hadharani ufanye hivyo hivyo ili kutia nguvu hoja yako bila hivyo hizo ni siasa tu ambazo zinashamiri kwa kuendekeza unafiki, uzandiki na majungu
 
  • Thanks
Reactions: Ame

Similar Discussions

Back
Top Bottom