Fukua
JF-Expert Member
- Jun 1, 2022
- 546
- 479
Watanzania wengi sana wapo magerezani kwa kesi za kusingiziwa.
Na wengi sana wapo vifungoni kwa makosa ya kusameheka kabisa.
Ukweli ni kwamba wengi ni maskini sana hawana watu wa kusimamia hata haki zao kama kukata rufaa au kuweka mawakili hivyo waliishia kufungwa bila huruma kabisa.
Mama Samia watoto wa maskini ndio wanaoozea jela, wewe ni mama na uzuri ni kwamba unaijua vyema mifumo yetu ya mahakama na mapungufu yake.
Kwa moyo mkunjufu kabisa ninakuomba sana litazame jambo hili.
Una mamlaka yote, kama itakufaa agiza vyombo vyako vya uchunguzi Ili angalau wale waliofikishwa hapo kwa kusingiziwa, kuonewa na kwa fitna tu za kitanzania uwasaidie wapate uhuru wao.
Wanaoiba na kulifilisi taifa hili wako uraiani lakini wezi wa unga wa kula au kuku wanaozea jela hii ni laana kwa nchi.
Ripoti ya CAG Kila mwaka inabainisha wizi wa kutisha wa mabilioni lkn wahusika hatua wanazochukuliwa ni vichekesho kabisa
Ulisema tushauri kistaarabu na Mimi nimetumia haki yangu ya kutoa maoni
Mungu akulinde na kukupa maisha marefu pia nguvu na maarifa ya kulitumikia taifa lake
Na wengi sana wapo vifungoni kwa makosa ya kusameheka kabisa.
Ukweli ni kwamba wengi ni maskini sana hawana watu wa kusimamia hata haki zao kama kukata rufaa au kuweka mawakili hivyo waliishia kufungwa bila huruma kabisa.
Mama Samia watoto wa maskini ndio wanaoozea jela, wewe ni mama na uzuri ni kwamba unaijua vyema mifumo yetu ya mahakama na mapungufu yake.
Kwa moyo mkunjufu kabisa ninakuomba sana litazame jambo hili.
Una mamlaka yote, kama itakufaa agiza vyombo vyako vya uchunguzi Ili angalau wale waliofikishwa hapo kwa kusingiziwa, kuonewa na kwa fitna tu za kitanzania uwasaidie wapate uhuru wao.
Wanaoiba na kulifilisi taifa hili wako uraiani lakini wezi wa unga wa kula au kuku wanaozea jela hii ni laana kwa nchi.
Ripoti ya CAG Kila mwaka inabainisha wizi wa kutisha wa mabilioni lkn wahusika hatua wanazochukuliwa ni vichekesho kabisa
Ulisema tushauri kistaarabu na Mimi nimetumia haki yangu ya kutoa maoni
Mungu akulinde na kukupa maisha marefu pia nguvu na maarifa ya kulitumikia taifa lake