Rais Samia fanya hili ili ukali wa gharama za maisha uwe historia Tanzania

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Tanzania tuna hifadhi ya gesi iliyofikia ujazo wa Trilion 57 cubic f.

Kwa mujibu wa hotuba ya Rais wakati wa kusaini mkataba wa kwanza wa uwekezaji wa Gesi baina ya Serikali na wawekezaji kuna vitalu takribani 28 vya gesi bado havijafanyiwa utafiti jambo ambalo endapo litafanyika linaweza kuifanya Tanzania kuwa na Lita za ujazo zaidi ya Trilioni hata 200 huko mbeleni.

Kwa sasa kuna Gesi inatolewa Songosongo na inasemekana ipo nyingi sana na matumizi yake madogo sana. Hali halisi inaonesha gesi inayouzwa na TPDC inauzwa kwa gharama ndogo sana kulinganisha na mafuta

Mapendekezo yangu
1. Serikali ije na mpango wa kubadilisha matumizi ya vyombo vya moto kutoka kutumia Mafuta tu hadi Gesi na Mafuta. Hii itawapa ahueni wananchi kuchagua kutumia Gesi au mafuta

2. Vianzishwe vituo vya Gesi nchi nzima kwa ushirikiano wa Serikali na Sekta binafsi

Haina ubishi kuwa gharama kubwa za nishati duniani ikiwemo Tanzania zinachangia sana kupanda gharama za maisha na bidhaa nyingine . Ni vizuri tukaenda kweli kwenye uchumi wa Gesi kwa kubadili chanzo cheti cha Nishati. Hili litaenda vizuri sana

Tumeanza kwenye nishati ya kupikia. Nina uhakika litaokoa sana miti yetu na mazingira yetu miaka ijayo, sasa twende kwenye vyombo vya moto ili tuokoe kuongezeka kwa gharama za maisha
 
Hilo wazi lako Raisi hawezi kulifanyia kazi.
Gas sio rahisi kama unavyosema, pia TPDC sio kwamba anauza gas bali ni mtu wa Kati sipendi kutumia neno dalali
Nchi haiwezekani kuhamia kutumia nishati hiyo tu ikiwa hatuzalishi bali tunainunua kutoka kwa wawekezaji ambao wanaweza kupandisha bei wakati wowote kufidiaa gharama zao.
 
Hilo wazi lako Raisi hawezi kulifanyia kazi.
Gas sio rahisi kama unavyosema, pia TPDC sio kwamba anauza gas bali ni mtu wa Kati sipendi kutumia neno dalali
Nchi haiwezekani kuhamia kutumia nishati hiyo tu ikiwa hatuzalishi bali tunainunua kutoka kwa wawekezaji ambao wanaweza kupandisha bei wakati wowote kufidiaa gharama zao.
Nani kasema Gas sio rahisi? Mtu gani wati unamsema? Mtaje na tupe uthibitisho?
 
Hivi vitu vinahitaji maandalizi, na vingine naona maandalizi yake yanaweza kuwa ya muda mrefu hivyo kushindwa kutatua hili tatizo la mfumuko wa bei tunalokabiliana nalo kwa wakati.

Mfano hilo la kubadilisha mfumo wa matumizi yetu ya vyombo vya moto, kutoka kwenye mafuta kwenda kwenye gas.

Hapo naona lazima ufanyike utaratibu utakaozuia kuagiza vyombo vya moto vinavyotumia mafuta then tuanze kuagiza vinavyotumia gas, hili litachukua muda.

Hata ukiangalia hili la nishati ya kupikia lililoanzishwa sasa na Waziri Makamba, bado utaona uwezo wa watanzania wengi kumudu gharama za gas bado ni mdogo.

Hasa wakati huu hali ya kiuchumi ilivyokuwa ngumu miongoni mwa watumianji wengi wa gas, hivyo hata hili naona mafanikio yake mpaka kuja kupatikana yatachukua muda mrefu ukizingatia bei ya gas bado haishikiki.
 
Hivi vitu vinahitaji maandalizi, na vingine naona maandalizi yake yanaweza kuwa ya muda mrefu hivyo kushindwa kutatua hili tatizo la mfumuko wa bei tunalokabiliana nalo kwa wakati.

Mfano hilo la kubadilisha mfumo wa matumizi yetu ya vyombo vya moto, kutoka kwenye mafuta kwenda kwenye gas.

Hapo naona lazima ufanyike utaratibu utakaozuia kuagiza vyombo vya moto vinavyotumia mafuta then tuanze kuagiza vinavyotumia gas, hili litachukua muda.
Lifanyike tu! Hata kama litachukua muda
 
Hivi vitu vinahitaji maandalizi, na vingine naona maandalizi yake yanaweza kuwa ya muda mrefu hivyo kushindwa kutatua hili tatizo la mfumuko wa bei tunalokabiliana nalo kwa wakati.

Mfano hilo la kubadilisha mfumo wa matumizi yetu ya vyombo vya moto, kutoka kwenye mafuta kwenda kwenye gas.

Hapo naona lazima ufanyike utaratibu utakaozuia kuagiza vyombo vya moto vinavyotumia mafuta then tuanze kuagiza vinavyotumia gas, hili litachukua muda.

Hata ukiangalia hili la nishati ya kupikia lililoanzishwa sasa na Waziri Makamba, bado utaona uwezo wa watanzania wengi kumudu gharama za gas bado ni mdogo.

Hasa wakati huu hali ya kiuchumi ilivyokuwa ngumu miongoni mwa watumianji wengi wa gas, hivyo hata hili naona mafanikio yake mpaka kuja kupatikana yatachukua muda mrefu ukizingatia bei ya gas bado haishikiki.
Haya ndiyo matatizo yaliyoko kichwani mwa watanzania wengi..yaani kila analotaka kufanya lazima yeye awe mnufaika..high level of selfishness! Wote wanaobuni na kufanya mambo ya maendeleo wangefikiri MUDA tungekuwa hapa?
 
Haya ndiyo matatizo yaliyoko kichwani mwa watanzania wengi..yaani kila analotaka kufanya lazima yeye awe mnufaika..high level of selfishness! Wote wanaobuni na kufanya mambo ya maendeleo wangefikiri MUDA tungekuwa hapa?
Naona hutaki ukweli usemwe.

Ok, kaanzishe hivyo vituo vya gas uone utamuuzia nani kama matumizi ya magari bado yanahitaji mafuta, na uwezo wa watanzania kumudu hizo gharama za gas bado upo chini.
 
Lifanyike tu! Hata kama litachukua muda
Hiki ndio kipindi hasa kupima kama nchi tuna viongozi au bobishi..ni litmus test ya baraza la mawaziri na serikali yote kama kweli wanastahili hicho tunachowalipa kupitia kodi na kama maarifa waliyo nayo yana thamani kwa nchi..this time tutajua kwa vielelezo, hata maana ya kuwa na wastaafu, isijekuwa umuhimu wao uliobaki ni kuhudhuria sherehe tu..
 
Tanzania tuna hifadhi ya gesi iliyofikia ujazo wa Trilion 57 cubic f.

Kwa mujibu wa hotuba ya Rais wakati wa kusaini mkataba wa kwanza wa uwekezaji wa Gesi baina ya Serikali na wawekezaji kuna vitalu takribani 28 vya gesi bado havijafanyiwa utafiti jambo ambalo endapo litafanyika linaweza kuifanya Tanzania kuwa na Lita za ujazo zaidi ya Trilioni hata 200 huko mbeleni.

Kwa sasa kuna Gesi inatolewa Songosongo na inasemekana ipo nyingi sana na matumizi yake madogo sana. Hali halisi inaonesha gesi inayouzwa na TPDC inauzwa kwa gharama ndogo sana kulinganisha na mafuta

Mapendekezo yangu
1. Serikali ije na mpango wa kubadilisha matumizi ya vyombo vya moto kutoka kutumia Mafuta tu hadi Gesi na Mafuta. Hii itawapa ahueni wananchi kuchagua kutumia Gesi au mafuta

2. Vianzishwe vituo vya Gesi nchi nzima kwa ushirikiano wa Serikali na Sekta binafsi

Haina ubishi kuwa gharama kubwa za nishati duniani ikiwemo Tanzania zinachangia sana kupanda gharama za maisha na bidhaa nyingine . Ni vizuri tukaenda kweli kwenye uchumi wa Gesi kwa kubadili chanzo cheti cha Nishati. Hili litaenda vizuri sana

Tumeanza kwenye nishati ya kupikia. Nina uhakika litaokoa sana miti yetu na mazingira yetu miaka ijayo, sasa twende kwenye vyombo vya moto ili tuokoe kuongezeka kwa gharama za maisha
Tuanze kutumia mitungi ya CNG kwa matumizi ya nyumbani badala ya LPG
 
Naona hutaki ukweli usemwe.

Ok, kaanzishe hivyo vituo vya gas uone utamuuzia nani kama matumizi ya magari bado yanahitaji mafuta, na uwezo wa watanzania kumudu hizo gharama za gas bado upo chini.
Unapimaje uwezo wa kutumia gesi ni mdogo lakini wa kutumia mafuta ni mkubwa? Mungu aliweka hiyo gesi hapa ili tuuze kwa wengine au lini hasa itatumika..
 
Hii hali ya ukali wa maisha ni faida kwake na mabepari wanaomzunguka. Pambana utakavyoweza kuyakabili maisha, watawala hawana huruma mtu.
 
Unapimaje uwezo wa kutumia gesi ni mdogo lakini wa kutumia mafuta ni mkubwa? Mungu aliweka hiyo gesi hapa ili tuuze kwa wengine au lini hasa itatumika..
Nchi za Norway na Urusi pamoja na nchi nyingine zenye hazina ya Gesi wanatumia hazina hii katika kuboresha uchumi wao na kufanya gharama za maisha kuwa chini kwa wananchi wao.

Ni wakati sasa kwa Tanzania kufanya hili kivitendo zaidi
 
Unapimaje uwezo wa kutumia gesi ni mdogo lakini wa kutumia mafuta ni mkubwa? Mungu aliweka hiyo gesi hapa ili tuuze kwa wengine au lini hasa itatumika..
Kama unataka kuitumia huo uwezo wa kuichimba unao? au mpaka umuite mwekezaji atakayekuja kuchimba kwa gharama zake matokeo yake ajipangie bei yake ili arudishe pesa zake?

Suala sio Mungu kuweka, issue ni uwezo wa kukitumia kile alichokupa Mungu effectively kwa manufaa ya watu wako, tunaweza? think man.

Mfano hiyo gas huko Songas toka ianze kuchimbwa umewahi kuona bei yake ikishuka? think aisee..
 
Kama unataka kuitumia huo uwezo wa kuichimba unao? au mpaka umuite mwekezaji atakayekuja kuchimba kwa gharama zake matokeo yake ajipangie bei yake ili arudishe pesa zake?

Suala sio Mungu kuweka, issue ni uwezo wa kukitumia kile alichokupa Mungu effectively kwa manufaa ya watu wako, tunaweza? think man.

Mfano hiyo gas huko Songas toka ianze kuchimbwa umewahi kuona bei yake ikishuka? think aisee..
sio kwamba hatuna Gesi ya kutumia kwenye vyombo vyetu vya moto! Hapana

Nishati tunayo tena nyingi sana! Visima vya Songosongo na Mnazi Bay vinatoa Gesi nyingi sana ambayo kiukweli hadi sasa hatuitumii vizuri! Matumizi ya Gesi kwetu Tanzania ni madogo sana kulinganisha na hifadhi tuliyokuwa nayo ambayo imeshaanza kuchimbwa

Suala linalotakiwa sasa ni kuhimiza uwekezaji massively kwenye hii sekta, serikali na wawekezaji wakarinishwe kujenga miundombinu na pipelines mikoa yote Tanzania ili hii rasilimali ianze kutumika kama inavyopaswa na kushusha gharama za maisha
 
Tanzania tuna hifadhi ya gesi iliyofikia ujazo wa Trilion 57 cubic f.

Kwa mujibu wa hotuba ya Rais wakati wa kusaini mkataba wa kwanza wa uwekezaji wa Gesi baina ya Serikali na wawekezaji kuna vitalu takribani 28 vya gesi bado havijafanyiwa utafiti jambo ambalo endapo litafanyika linaweza kuifanya Tanzania kuwa na Lita za ujazo zaidi ya Trilioni hata 200 huko mbeleni.

Kwa sasa kuna Gesi inatolewa Songosongo na inasemekana ipo nyingi sana na matumizi yake madogo sana. Hali halisi inaonesha gesi inayouzwa na TPDC inauzwa kwa gharama ndogo sana kulinganisha na mafuta

Mapendekezo yangu
1. Serikali ije na mpango wa kubadilisha matumizi ya vyombo vya moto kutoka kutumia Mafuta tu hadi Gesi na Mafuta. Hii itawapa ahueni wananchi kuchagua kutumia Gesi au mafuta

2. Vianzishwe vituo vya Gesi nchi nzima kwa ushirikiano wa Serikali na Sekta binafsi

Haina ubishi kuwa gharama kubwa za nishati duniani ikiwemo Tanzania zinachangia sana kupanda gharama za maisha na bidhaa nyingine . Ni vizuri tukaenda kweli kwenye uchumi wa Gesi kwa kubadili chanzo cheti cha Nishati. Hili litaenda vizuri sana

Tumeanza kwenye nishati ya kupikia. Nina uhakika litaokoa sana miti yetu na mazingira yetu miaka ijayo, sasa twende kwenye vyombo vya moto ili tuokoe kuongezeka kwa gharama za maisha
Nkujuze?

Nikwambie tu gas hio sio yetu hata najua utashangaa..kupatikana na kuchimbwa kwenu haimaanishi ni yenu..sisi wenyewe tunanunua hio gas

Na mkataba ni miaka na miaka ...ukiambiwa ni miaka 50 plus kisha ndo mtaachiwa ..imagine mtoto ambae hajazaliwa hadi anakuja kuitwa babu😁
 
Zinatafutwa fedha za makarani wa sensa. Baada ya sensa mafuta yatapungua gharama.
 
Back
Top Bottom