mbona Nyerere hawajawahi kumkosea wala Mkapa wala MugufuliUmeandika upuuzi wa ajabu sana, tatizo la inferiority complex linawatesa sana, Magufuli atafanywa na nani kuwa mtakatifu? hivi mkiwa mnaandika huu upuuzi wenu huwa mnajipa muda kidogo wa kufikiri au mnakurupuka tu? unadhani mtu kuitwa mtakatifu ni suala la kuamka asubuhi na kumpachika hilo jina? huo ni mchakato ambao hata hivyo kwa Magufuli sijawahi kusikia kama upo zaidi ya kelele za mtaani tu ulizoandika hapa.
TEC hawajawahi kusema wanaanzisha huo mchakato, kama una ushahidi weka hapa, kwa haya mawazo yako hutaki Rais akosolewe hata akikosea, kwani wakifanya hivyo utasema wanamu-attack kwasababu ya dini yake, mambo ya imani unayachanganya na siasa kwa maneno ya kuokoteza mtaani, very small mind, halafu wanakuita great thinker!