Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Mama Samia, kama kweli umedhamiria kurudisha umoja wa kitaifa na kutibu majeraha yaliyotokana na uongozi uliopita, moja ya jambo linalostahili kufanyika ni kwa serikali yako kumlipa Tundu Lissu haki zake zote zikiwemo fedha za matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi.
Japo mini si kiongozi ndani ya CHADEMA, ila ni imani yangu utapokutana na viongozi wa upinzani( viongozi wa CHADEMA), hili ni moja ya jambo wataloliwasilisha kwako lakini itakuwa ni uungwana kwako iwapo utalifanyia kazi kabla ya kusubiri kuombwa kufanya hivyo na viongozi wa CHADEMA.
Hivyo, Mama hii ni fursa kwako kuonyesha kuwa wewe ni Mama na zaidi uko serious katika kurekebisha makosa yaliyofanyika chini ya utawala wa Hayati Magufuli.
Katika hili, usisikilize ushauri wa watu waliokuwepo katika serikali iliyopita hata kama umewapa nafasi katika serikali yako kwani naamini baadhi hawapendi kuona unafanya kinyume na mtangulizi wako hivyo wanaweza kukushauri vibaya.
Actions speak louder than words.
Nawasilisha.
Japo mini si kiongozi ndani ya CHADEMA, ila ni imani yangu utapokutana na viongozi wa upinzani( viongozi wa CHADEMA), hili ni moja ya jambo wataloliwasilisha kwako lakini itakuwa ni uungwana kwako iwapo utalifanyia kazi kabla ya kusubiri kuombwa kufanya hivyo na viongozi wa CHADEMA.
Hivyo, Mama hii ni fursa kwako kuonyesha kuwa wewe ni Mama na zaidi uko serious katika kurekebisha makosa yaliyofanyika chini ya utawala wa Hayati Magufuli.
Katika hili, usisikilize ushauri wa watu waliokuwepo katika serikali iliyopita hata kama umewapa nafasi katika serikali yako kwani naamini baadhi hawapendi kuona unafanya kinyume na mtangulizi wako hivyo wanaweza kukushauri vibaya.
Actions speak louder than words.
Nawasilisha.