Rais Samia amteua Mavere Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD)

Raymond Mndolwa aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Operesheni za Mikoa pale NHC. Kumbukumbu zinaonyesha alisimamishwa kazi kwa tuhuma za ufisadi na aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Mhe Lukuvi.

Sasa leo tunaona amepata uteuzi wa Rais. Je zile tuhuma zilikuwa ni malicious!?
Kusimamishwa sio shida inawezekana uchunguzi umefanyika ikabainika hakuhusika ,hongera sana Raymond Mungu akubariki
 
CAG naye awe anaimulika serikali je ilipeleka msd pesa ya kununua dawa Kama ilivyopitishwa bajeti ya dawa bungeni? Sio unampima ili umdhalilishe ikiwa unaelewa serikali imepeleka pesa 40% na madeni ya nyuma kibao hujalipa alafu unataka matokeo yawe 100 kwa 100.
CAG nao huwa vilaza msiwashabikie muda wote Kuna baadhi ya maeneo hawasaidii nchi zaidi ya sifa za kijinga na mbwembwe kwenye ripoti zao
CAG hatafuti sifa za kijinga kama unavyodai,bali anafanya kazi professionally kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya ukaguzi(International Standards of Auditing) hivyo kazi yake ni ku-Audit,Kutoa Taarifa na kutoa Reccomendation.Kwenye Report husika CAG karipoti kuwa Deni la MSD limefikia 382 Bln na akashauri lilipwe ili kulinda Mtaji wa MSD,hapo CAG kishafanya kazi yake,Utekelezaji(Implimentantion) inabaki kuwa Taasisi Husika Chini ya Serikali.Hsta hivyo,Kuidai serikali siyo Justification ya MSD kuvunja taratibu xa manunuzi ya Umma(Public Ptocutement) kama kulipa suppliers bila contracts, kununua madawa bila ku-involve PMU wala TenderBoard ya MSD,kununua dawa overseas za 17Bln kwa Mikataba ambayo haikufanyiwa vetting na AG?,n.k,ambavyo vimechangia kula kichwa cha Mjeshi Maj.General Mhidze

IMG-20220414-WA0000.jpg
 
CAG hatafuti sifa za kijinga kama unavyodai,bali anafanya kazi professionally kwa mujibu wa viwango vya kimataifa vya ukaguzi(International Standards of Auditing) hivyo kazi yake ni ku-Audit,Kutoa Taarifa na kutoa Reccomendation.Kwenye Report husika CAG karipoti kuwa Deni la MSD limefikia 382 Bln na akashauri lilipwe ili kulinda Mtaji wa MSD,hapo CAG kishafanya kazi yake,Utekelezaji(Implimentantion) inabaki kuwa Taasisi Husika Chini ya Serikali.Hsta hivyo,Kuidai serikali siyo Justification ya MSD kuvunja taratibu xa manunuzi ya Umma(Public Ptocutement) kama kulipa suppliers bila contracts, kununua madawa bila ku-involve PMU wala TenderBoard ya MSD,kununua dawa overseas za 17Bln kwa Mikataba ambayo haikufanyiwa vetting na AG?,n.k,ambavyo vimechangia kula kichwa cha Mjeshi Maj.General Mhidze

View attachment 2188312
Nimekuelewa baadhi ya categories, nililenga lile kasambaza dawa 34% hii iko proportion na approved budget, je zilipelekwa fedha hizo za kununua dawa. Note: Kama una madeni kwa washitiri huwa nao ni wajanja ukimpa tenda nyingine anachukua anafanya partial delivery hadi ulipe lile . Hivyo mbinu jinsi ya kupata dawa zitumike. Maana ukitenda wanajitokeza hao hao wanakudai. Hivyo kuwe na ustaarabu wa serikali kulipa deni la msd na kutekeleza bajeti ya dawa Kama ilivyopitishwa bungeni na msd ilipe washitiri iliowakopa
 
Hizi nafasi ilipaswa ziwe za ushindani na kuwe kuna open platorm hadi tupate shortlisted candidates kwa uwazi ila kwa katiba hii kila siku itakua okota okota tu na panga pangua..
 
Amemteua Rosemary William Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD), Bi. Slaa ni Afisa Mwandamizi katika Kampuni ya Picenaterhouse Coopers PWC.

Amemteua Mavere Ali Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Tukai ni Kiongozi Mkuu wa Mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance.

Amemteua Raymond William Mndolwa kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Mndolwa ni Mtaalam wa Operesheni, Kampuni ya STC Construction, Dar es Salaam
Ipo kila sababu hizi nafasi za juu wawe wanaomba badala ya teuzi zenye malengo ya maslahi binafsi
 
View attachment 2187838

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi jioni ya Aprili 14, 2022 kama ifuatavyo:

Amemteua Rosemary William Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD), Bi. Slaa ni Afisa Mwandamizi katika Kampuni ya Picenaterhouse Coopers PWC.

Amemteua Mavere Ali Tukai kuwa Mtendaji Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Tukai ni Kiongozi Mkuu wa Mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance.

Amemteua Raymond William Mndolwa kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Mndolwa ni Mtaalam wa Operesheni, Kampuni ya STC Construction, Dar es Salaam.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus ni kuwa uteuzi huo unaanza mara moja.
View attachment 2187787


Chaguo zuri my schoolmate Ilboru Sec School. Tatizo kubwa pale ni siasa
 
Hongera Le super chief Hangaya. Teuzi hizi mbili za MSD ni nzuri sema funding iwe kwa wakati na wanachokihitaji.

Alipelekwa Mgaya pale jamaa katoka marekani lakini hakuweza kuperform wakati wa kikwete.

Siasa naona kidogo wakati huu zinaweza kupungua juu ya menejimenti. Kupewa amri za wanasiasa.
 
MSD wizi haujaanza leo na wala hautoisha leo. Wizi wa MSD ni mnyororo mrefu sana unaoanzia huko MSD kuja kwenye Halmashauri mpaka kwa Waganga wakuu wa Hospitali na Maafisa Ugavi wao... Manunuzi mengi yanayofanyika MSD yana wizi ndani yake.

Kitambo kile kabla ya hela kuingizwa kwenye mfumo wa manunuzi kidijitali ilikuwa Hospitali inaenda kufanya manunuzi MSD wa dawa mfano za Milioni 100, lakini dawa zinazoletwa ni za Milioni 50 halafu hiyo Milioni 50 watu wanagawana,,, Zinaletwa mashine ambazo ni za bei za chini na zingine unaziona kabisa hizi hazitokaa hata miezi 6 halafu Waganga Wakuu na viongozi wenzake, Afisa Ugavi, Makatibu na huko Halmashauri wanapandisha bei hata mara 10 ya uhalisia na nyiye watumiaji mnalazimishwa msaini madokezo.
 
Siku hizi barua za uteuzi zinasainiwa hotelini. Haya mama endelea kuupiga mwingi.
Zama zimebadilika sana , hizi ni enzi za E government, , mtu anaweza kufanya mkutano na wakirugenzi kadhaa akiwa mbali kabisa na ofisi alimradi tu kuna internet.
 
Huyu ndugu Mavere Tukai ni "kichwa" haswaa.....

Ni "pharmaceutical management specialist"....

Jamaa yuko FOCUSED na DETERMINED sana.....

Alikuwa pale USAID....wamarekani wanamfahamu kwa uwezo mkubwa alionao....watammiss sana.....

Imefika muda atutumikie katika MSD.....

Kila la heri kwake kamarada Mavere Tukai ,amen🙏

#Siempre JMT🙏
#YetzerHatov🙏
Akitaka kufanikiwa wale wakurugenzi wote wa idara aombe kibali wapangiwe Kazi nyingne... Otherwise Bado atanyoshwa tu Kama mwenzake na watu wanaojiita wazoefu wa kaz
 
Back
Top Bottom