"Mkeka" wa Rais Samia wamuondoa Mkurugenzi wa Bukoba

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Hamid Njovu.jpg

Rais Samia Hassan Suluhu amemteua Jacob Simon Nkwera kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba.

Kabla ya uteuzi huu, Nkwera alikuwa Afisa Mwandamizi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Kutokana na uteuzi huo inamaanisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Hamid Njovu ameondolewa katika nafasi yake.

Mkeka wote wa Uteuzi na uhamisho uko hapa - Uteuzi na Uhamisho: Rais Samia amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali

Uamuzi huo umefanyika ikiwa ni siku chache tangu Member wa Jamii Forums aripoti kuhusu kutolipwa kwa posho za Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHWs) Wilaya ya Bukoba ambao waliingia makubaliano na Ofisi ya Makurugenzi wa Manispaa kusaidia Jamii wakati wa mlipuko wa Ugonjwa wa Marburg.

Wahudumu hao ambao walidai kuwa walishiriki uhamasishaji kwa Jamii jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Marburg kwa kuzunguka kata mbalimbali kw muwa wa miezi mitatu (Machi – Juni 2023) hawajalipwa posho zao ambazo waliahidiwa, walidai kuwa waliandika barua kwa Mkurugenzi huyo Januari 2024 wakikumbushia malipo lakini hawakujibiwa.

Andiko la Member hili hapa: Malalamiko ya posho ya CHWs ya uhamasishaji wa kujikinga na ugonjwa wa mlipuko wa Marburg Bukoba
 
Uzuri wa Rais Comrade Dr SSH, kiongozi mwandamizi akituhumiwa kwa jambo lolote nae akatuma timu ya kumchunguza na ikabainika na kudhihirika kiongozi huyo hakuwajibika ipasavyo, Rais comrade Dr SSH hachelei kumuwajibisha kwa wakati muafaka kabisa bila kuchelewa 🐒

Wito wangu mimi nisie stahili kwa viongozi waandamizi wa umma, tafadhali sana, wajibikeni kwa haki na usawa kwa wananchi. Msipofanya hivyo wanainchi are watching you, serikali is watching you. Mtawajibishwa kwa kutowajibika kwenu 🐒
 
Teua tengua kila siku, huku kukiwa hakuna tija wala mabadiliko yoyote yale ya kiutendaji ni wastage tu of time and resources.
 
View attachment 2932469
Rais Samia Hassan Suluhu amemteua Jacob Simon Nkwera kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba.

Kabla ya uteuzi huu, Nkwera alikuwa Afisa Mwandamizi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Kutokana na uteuzi huo inamaanisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Hamid Njovu ameondolewa katika nafasi yake.

Mkeka wote wa Uteuzi na uhamisho uko hapa - Uteuzi na Uhamisho: Rais Samia amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali

Uamuzi huo umefanyika ikiwa ni siku chache tangu Member wa Jamii Forums aripoti kuhusu kutolipwa kwa posho za Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHWs) Wilaya ya Bukoba ambao waliingia makubaliano na Ofisi ya Makurugenzi wa Manispaa kusaidia Jamii wakati wa mlipuko wa Ugonjwa wa Marburg.

Wahudumu hao ambao walidai kuwa walishiriki uhamasishaji kwa Jamii jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Marburg kwa kuzunguka kata mbalimbali kw muwa wa miezi mitatu (Machi – Juni 2023) hawajalipwa posho zao ambazo waliahidiwa, walidai kuwa waliandika barua kwa Mkurugenzi huyo Januari 2024 wakikumbushia malipo lakini hawakujibiwa.

Andiko la Member hili hapa: Malalamiko ya posho ya CHWs ya uhamasishaji wa kujikinga na ugonjwa wa mlipuko wa Marburg Bukoba
Tatizo ni kuteua makada wa chama kwenye nafasi za Utumishi wa Umma badala ya kuongalia sifa na vigezo. Tatizo hili lilianzia hasa kwenye uongozi wa jiwe
 
Teua tengua kila siku, huku kukiwa hakuna tija wala mabadiliko yoyote yale ya kiutendaji ni wastage tu of time and resources.
Tija kamwe haitaweza kuwepo, kwa sababu tatizo kubwa kabisa sugu ililopo ni Ubovu wa Gari lenyewe. Gari ni bovu sana halifai tena kwa Safari salama, hata akibadilisha madereva mara bilioni mia moja wala haitasaidia kitu.

Ni lazima Kwanza tuunde (tutengeneze) gari jipya na ndipo tufikirie kubadilisha madereva wapya ili tupate Tija(Productivity)
 
Wawe wanapelekwa mahakamani ili wawe na akili
Kupelekwa Mahakamani itakuwa vigumu hadi aliyewateua aridhie.

Nimesikia muendelezo wa ile kesi ya aliyekuwa DED Arusha Jiji, Mahakama ilimwachia huru Kwa kuwa Mhe. Rais alikuwa hajatoa kibali kwenye ile kesi, hivyo DPP akaondoa nia ya kumshtaki yule DED hivyo aliachiwa huru.
 
View attachment 2932469
Rais Samia Hassan Suluhu amemteua Jacob Simon Nkwera kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba.

Kabla ya uteuzi huu, Nkwera alikuwa Afisa Mwandamizi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.

Kutokana na uteuzi huo inamaanisha aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Hamid Njovu ameondolewa katika nafasi yake.

Mkeka wote wa Uteuzi na uhamisho uko hapa - Uteuzi na Uhamisho: Rais Samia amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi mbalimbali

Uamuzi huo umefanyika ikiwa ni siku chache tangu Member wa Jamii Forums aripoti kuhusu kutolipwa kwa posho za Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii (CHWs) Wilaya ya Bukoba ambao waliingia makubaliano na Ofisi ya Makurugenzi wa Manispaa kusaidia Jamii wakati wa mlipuko wa Ugonjwa wa Marburg.

Wahudumu hao ambao walidai kuwa walishiriki uhamasishaji kwa Jamii jinsi ya kujikinga na maambukizi ya Marburg kwa kuzunguka kata mbalimbali kw muwa wa miezi mitatu (Machi – Juni 2023) hawajalipwa posho zao ambazo waliahidiwa, walidai kuwa waliandika barua kwa Mkurugenzi huyo Januari 2024 wakikumbushia malipo lakini hawakujibiwa.

Andiko la Member hili hapa: Malalamiko ya posho ya CHWs ya uhamasishaji wa kujikinga na ugonjwa wa mlipuko wa Marburg Bukoba
Huyo Mwamba kutoka TAKUKURU anaenda kufanya kazi Maalumu!
 
Mhe Rais alisema kuwa anasoma sana mitandao, na nadhani hata hapa JF ni member mwenzetu katika fake IDs 🤗
 
Back
Top Bottom