Rais Samia amesema anarejesha mahusiano na nchi za Ulaya. Je, kukopa ndio njia bora ya kufanya hivyo?

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,675
40,928
Rais Samia wakati akirejea toka France na Belgium wakati akitoa salamu zake na asante kwa mapokezi pale uwanja wa Mwalimu Nyerere alisema kwamba wakati wa awamu ya tano mahusiano yetu na nchi za Ulaya yalilega sana ila kwa sasa amejitahidi kuyarejesha.

Observation yangu ndogo ya matendo yatokanayo na jitihada hizo za kurejesha mahusiano na nchi za ulaya yanaonesha kwamba kasi ya ukopaji na misaada toka nchi za Ulaya na taasisi za kifedha imeongezeka.

Rais mwenyewe anakiri kwamba kuna fedha zilikuwa withheld ila kuna possibility kubwa sasa zikaachiwa.

Kauli ya Rais Magufuli mara kwa mara ilikua kukataa mikopo na misaada yenye masharti magumu kwa Taifa.

Ushahidi wa kauli za Magufuli za kukataa kwa mikopo awamu ya tano ni kwa kauli ya Rais hivi majuzi kuwa kuna fedha zilizuiwa.

Kwakua sasa misaada na mikopo imeanza kumiminika kwa wingi ni wazi kwamba uongozi wa awamu hii unakubaliana na masharti ya mikopo hiyo.

Swala hapa la kujiuliza ni je masharti hayo yana madhara gani kwa Taifa letu.

Na kama yana faida basi tuambiwe faida hizo ni zipi?

Ninachoomba tu kwa Serikali ni kuwa makini wakati inapokubaliana na masharti hayo ya mikopo na misaada isiwe tunafanya tu kwa lengo la kuwafurahisha nchi za ulaya wakati kwa uhalisia tunaoumia ni sisi na vizazi vyetu huku wao na vizazi vyao wakinufaika.

Pia ningependa kujua, je ni lazima tukope na kupokea misaada toka nchi za Ulaya ili mahusiano yetu na wao yawe mazuri.

Kwani hatuwezi kuwa na mahusiano nao mazuri bila kukopa na kupewa misaada.

Nasema hivi kwani inaonekana kwamba kukopa na kuomba misaada ndio njia pekee ya kuwa na mahusiano mazuri na nchi za Ulaya.

Nachelea kusema kwamba Nchi za Ulaya zinanufaika mno na mikopo na misaada wanayotupa maana wasingepata hasira kwa sisi kukataa mikopo na misaada yao.

Tuwe makini.
 
Walikuwa wanashangilia magu kutokopa bado wapo chamani wanapiga shangilio
Kama tunarejesha mahusiano na nchi za Ulaya,

Hatuwezi kuyarejesha kwa kufanya mambo mengine zaidi ya kukimbilia mikopo na misaada yao?

Yaani Ulaya wanapenda tuwakope tu??

Marafiki gani hao ambao wanapenda kutuona tukiwa tegemezi kwao kila siku?
 
Mh. Rais Samia wakati akirejea toka France na Belgium wakati akitoa salamu zake na asante kwa mapokezi pale uwanja wa Mwalimu Nyerere alisema kwamba wakati wa awamu ya tano mahusiano yetu na nchi za Ulaya yalilega sana ila kwa sasa amejitahidi kuyarejesha...
Kauli za JPM zilikuwa hazifanani na matendo yake mbali na majukwaa ya siasa. Aliwajaza watu kiburi cha kujitegemea wakati kiuhalisia tupo mbali sana na uwezo wa kushindana kiuchumi na mataifa ya Ulaya.

Mzungu anayo know how (maarifa) na ndio kitu ambacho kinampa umaarufu mchina kwa sasa, utundu na ubunifu wa hali ya juu.

Huwezi kushinda na mzungu mwenye taasisi zote za pesa, utakuwa unajisumbua bure tu. Nyerere aliwawekea kiburi na haikumsaidia chochote ndio akaingia Mwinyi madarakani akawapigia magoti wazungu.

Huu ni utamaduni wa kidunia, huwezi kuwavimbia waliotutawala halafu ukawa na uchumi endelevu
 
Kama tunarejesha mahusiano na nchi za Ulaya,

Hatuwezi kuyarejesha kwa kufanya mambo mengine zaidi ya kukimbilia mikopo na misaada yao?

Yaani Ulaya wanapenda tuwakope tu??

Marafiki gani hao ambao wanapenda kutuona tukiwa tegemezi kwao kila siku??
Hawajatukataza kuwa wabunifu kama wachina. Mtu kuwa mbunifu siku zote ni bure kabisa. Tunakosea mahali fulani.
 
Kauli za JPM zilikuwa hazifanani na matendo yake mbali na majukwaa ya siasa. Aliwajaza watu kiburi cha kujitegemea wakati kiuhalisia tupo mbali sana na uwezo wa kushindana kiuchumi na mataifa ya Ulaya...
Wewe ulikuwa miongoni mwa waliomsupport Magufuli na falsafa zake hivyo huna moral authority kumkosoa sasa.
 
Jambo zuri ni kwamba wote nyie ni CCM.kwa hivyo hakuna wa kumsimanga mwenzake.hata hivyo bora huyu anasema ukweli na kuweka wazi kwamba kuna msaada na Kuna mkopo kuliko yule marehemu amabae alijifanya hako pi na kumbe anakopa kimya kimya.

Wewe labda unaumia na Mama kwa sababu bado una Magufuli ideology..jaribuni kukubali kwamba huyo mtu wenu alishakufa na hatofufuka tena na hamtoonana tena milele na milele.

Karibuni huku tuidai katiba mpya ambayo itaweka mipaka ya viongozi kukopa na kuweka uwazi
 
Jambo zuri ni kwamba wote nyie ni CCM.kwa hivyo hakuna wa kumsimanga mwenzake.hata hivyo bora huyu anasema ukweli na kuweka wazi kwamba kuna msaada na Kuna mkopo kuliko yule marehemu amabae alijifanya hako pi na kumbe anakopa kimya kimya .wewe labda unaumia na Mama kwa sababu bado una Magufuli ideology..jaribuni kukubali kwamba huyo mtu wenu alishakufa na hatofufuka tena na hamtoonana tena milele na milele…karibuni huku tuidai katiba mpya ambayo itaweka mipaka ya viongozi kukopa na kuweka uwazi
Hoja hapa ni rahisi tu.

Je kukopa ndio njia inayosemekana ya kurejesha mahusiano na nchi za Ulaya??

Je hakuna njia nyingine ya kufanya hivyo??

Majibu yake tafadhali.
 
Hoja hapa ni rahisi tu.

Je kukopa ndio njia inayosemekana ya kurejesha mahusiano na nchi za Ulaya??

Je hakuna njia nyingine ya kufanya hivyo??

Majibu yake tafadhali.
Kumbuka kuwa SSH amerithi miradi mikubwa kutoka kwa JPM. Ni lazima imalizike kwa udi na uvumba, hivyo anachokopa ni kukwepa matusi wakati wa kampeni za 2025.

Sisi tunaomsema vibaya kwanini anakopa ndio tutakaomcheka wakati tutakapomuuliza mbona miradi uliyoachiwa haijamalizika?.
 
Kama tunarejesha mahusiano na nchi za Ulaya,

Hatuwezi kuyarejesha kwa kufanya mambo mengine zaidi ya kukimbilia mikopo na misaada yao?

Yaani Ulaya wanapenda tuwakope tu??

Marafiki gani hao ambao wanapenda kutuona tukiwa tegemezi kwao kila siku??
Ulaya bila kukopesha inapotea mazima! Kukopesha ni moja ya shamba lao kubwa la kuna. Hata kama hutaki watakubembeleza wee ama watakusulubu wuu mpaka uingine kwenye shamba lao "uvunwe".
===
Tukiwa wajanja tunaweza kuingia kwenye shamba lao lakini tukagoma kuvunwa.
 
Kumbuka kuwa SSH amerithi miradi mikubwa kutoka kwa JPM. Ni lazima imalizike kwa udi na uvumba, hivyo anachokopa ni kukwepa matusi wakati wa kampeni za 2025.

Sisi tunaomsema vibaya kwanini anakopa ndio tutakaomcheka wakati tutakapomuuliza mbona miradi uliyoachiwa haijamalizika?.
Sio kweli kwamba fedha zote zinazokopwa ni kwa ajili ya miradi iliyoachwa Magufuli.

Fedha za Uviko zilikwenda kwenye madarasa na vyoo hazikwenda SGR wala Stiglers.

Fedha toka world bank - usalama wa Ardhi.

Fedha za Ufaransa - Miradi Tanga na Pemba.

Hivyo ukiangalia kwa haraka utaona kwamba mikopo imechukua sehemu kubwa sana ya mahusiano yetu na Ulaya jambo ambalo linashitua.
 
Back
Top Bottom