Rais Samia amerejea kuomboleza msiba wa Hanang au amekuja kutuhamishia Burundi?

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,859
18,282
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

1701796652753.png

Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
 
Toa mbadala wafsnye nini angalau twende sawa? Usituachee hewani .....tafadhalii seriakali sikivuu itafuatisha tu maoni yakoooo
 
Toa mbadala wafsnye nini angalau twende sawa? Usituachee hewani .....tafadhalii seriakali sikivuu itafuatisha tu maoni yakoooo
Nashauri wabunge, mawaziri, rais, makamu wa rais na waziri mkuu wapunguziwe mishahara, posho na marupurupu na kiasi cha fedha kitakachopatikana kitumike kuwatibia masikini wasiokuwana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Pili, nashauri watu hawa nao waanze kukatwa kodi. Hawa jamaa hawana sababu ya kutolipa kodi. Haiwezekani masikini walipe kodi ya kizalendo wakati watu wenye mishahara minene hawalipi kodi yoyote.

Je, wewe Lambardi unashauri nini kifanyike?
 
Nashauri wabunge, mawaziri, rais, makamu wa rais na waziri mkuu wapunguziwe mishahara, posho na marupurupu na kiasi cha fedha kitakachopatikana kitumike kuwatibia masikini wasiokuwana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

Pili, nashauri watu hawa nao waanze kukatwa kodi. Hawa jamaa hawana sababu ya kutolipa kodi. Haiwezekani masikini walipe kodi ya kizalendo wakati watu wenye mishahara minene hawalipi kodi yoyote.

Je, wewe Lambardi unashauri nini kifanyike?
Mtanzania mzalendo mwenye uelewa na uwezo wa kutekeleza dhana ya utawala bora ajitokeze 2025 tumfanyie kampeni ya kufa mtu pamoja na kuhakikisha hakuna wizi wa kura kupitia vyombo vya dola ambavyo vinatakiwa kutetea maslahi ya wananchi!
 
Mtanzania mzalendo mwenye uelewa na uwezo wa kutekeleza dhana ya utawala bora ajitokeze 2025 tumfanyie kampeni ya kufa mtu pamoja na kuhakikisha hakuna wizi wa kura kupitia vyombo vya dola ambavyo vinatakiwa kutetea maslahi ya wananchi!
Kama nani? Pendekeza nitawaomba wasi mkolimbe.
 
Sisi ni wapole Hadi raha kama huyo ng'ombe.
Sijui ni macho yangu,pale chini ni miiba sijui!.
Wenye akili kubwa,wakisema tunahitaji KATIBA mpya,maskini anasema hata iliyopo haijui na hajawahi kuisoma Wala kuishika mkononi😠😠.
So,hakuna namna.
Wasomi wanapiga kelele juu ya katiba mpya,mtu WA chini anakwambia acha wapararuane wao kwa wao yeye hayamhusu.
Mada hii inatakiwa uilete kipindi Cha Kampeni,hapo ndo utatathimini,je uwaelezee au ujikaushie tu.
🇹🇿🤔.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

View attachment 2834133
Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
Mkuu Nina maswali kidogo kwako:
1. Hivi mkuu unategemea ni nan alipe kodi na ni nan asilipe kodi? Hao unaowatetea kwenye tozo za simu je hawatumii hizi barabara zilizojengwa kwa lami? Je hawalindwi na jeshi la police? Je watoto wao hawaendi shule hizi za serikali? Nk nk nk!
Kama huko pote wanapata Huduma je unategemea hizo huduma nani anaziwezesha? Au waona ni haki wao wahudumiwe bure wakati wengine wanarundikiwa mikodi?
2. Je unafahamu idadi ya watu wazima ilivo kubwa (wenye miaka zaidi ya 18) ambao wamekaa bure tu hawazalishi wala kulisaidia taifa kwa chochote zaidi ya kulalamika tu kushoto na kulia? Na tafadhali tusiambiane hakuna ajira kwasababu hili limekuwa kimbilio (sababu ya kila anayetaka hata kufanya uvivu tuu). Wakati mwingine huwa natamani kodi ya kichwa irudishwe ili kupambana na kundi hili. (Tuliokuwepo wakati wa kodi ya kichwa inakusanywa mtakubaliana nami jinsi ilivolazimisha watu kufanya kazi)

Ningeelewa iwapo ungependekeza maboresho katika baadhi ya mambo yalivo sasa na sio kuongelea watu wasilipe kodi.

Nitasema machache nayoona ni ya kuboresha ili twende mbele kwa kasi.

1. Futa seating allowance zote za watumishi wa uma (hichi ni kichaka cha wizi na ufisadi)
2. Ubadhirifu wote unaotajwa kila mwaka kwenye report za ÇAĞ ushughulikiwe kikamilifu na watu wafungwe na mali zao zitaifishwe kweli.
3. Taasisi huru na zenye weledi zifanye majukumu yao kikamilifu.
4. Kurekebisha sheria za kodi zinazotoa upendeleo kwa viongozi ili kufuta dhana nzima ya sisi na wao.

Hayo ni baadhi tu ya mapendekezo ya kuboresha na nina amini yapo mengi ya kuboresha kuliko kutetea watu kutokulipa kodi.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

View attachment 2834133
Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
Nadhani unakumbuka ile kauli ya hayati JPM kule Bukoba baada ya tetemeko kuharibu miundo mbinu, alisema kwamba tetemeko hakulileta yeye.

Rais SSH, ni muungwana na hajaja na kauli ya kifedhuli kama ile ya kule Bukoba, wenye akili timamu na kumbukumbu nzuri vichwani wataendelea kupima kwa haki kila kinachofanyika.
 
Tukiacha uongo,
Wanaotumia pesa nyingi kwenye hizo electronic money, ni hao hao matajiri, masikini wataolipiwa bure bima utakuta wanafanya transfer zisizozidi laki kwa mwezi ambazo tozo ya serikali ni chini ya 2000/-,

Lakin wale wenye uwezo ndio utakuta kwa mwezi kafanya miamala ya electronic zaidi ya 5M makato ya tozo 30K na bado anaenda kulipa bima ya Afya kwa pesa nyingine,

Bima hii ni msaada kwa hao masikini, usiseme watakatwa tozo, ukweli hata hizo tozo zao kwa mwezi hazifiki 5k
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja sitaki kuwachosha. Mnakumbuka vizuri madhila yaliyotupata watanzania mwaka jana wakati serikali ilipoongezeka tozo za miamala maradufu hivyo kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu maradufu. Kana kwamba hiyo haitoshi waziri wa fedha msomi, Mwigulu Nchemba aliwakejeli watanzania kwa kusema kuwa kodi lazima zikatwe haijalishi watanzania wanaumia kiasi gani na kwamba asiyetaka kukamuliwa tozo ahamie Burundi.

Suala hili liliwauma sana watanzania lakini kwa kuwa hawana pa kukimbilia wameendelea kubakia hapa nchini na wanakamuliwa ‘kodi ya kizalendo’ kweli kweli. Kinachoudhi zaidi ni kwamba wabunge wa CCM wanaofanya haya maamuzi, hawalipi kodi, hivyo hawahusiki na kodi hizi za kizalendo kwa kuwa wao sio wazalendo bali wananchi masikini ndio wazalendo kindakindaki.

Wakati vumbi la kodi ya uzalendo halijatua, Rais Samia amerejea nchini kwa dharula kuja kusaini muswada wa bima ya afya. Baadhi ya watanzania mbumbumbu wasiojua kitu na wasiokuwa na chembe ya ufahamu wa mambo, hasa chawa wa mama, wamesikika wakishangilia kitendo hiki alichofanya Rais kama mazuzu. Wasichokifahamu ni kwamba fedha zitakazotumika kugharamia matibabu ya bima ya afya kwa wote zitatokana na ongezeko la tozo litakaloingizwa tena kwenye miamala ya kieletroniki.

Wakati muswada ulipopitishwa bungeni kwa 100% na wabunge wa CCM, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, alisema moja ya vya mapato ya kugharamia matibabu haya kwa watanzania masikini ni ongezeko jipya la tozo za miamala. Sote tunafahamu kuwa miamala haibagui. Haimjui tajiri wala masikini. Inakata kotekote. Haohao masikini ambao serikali ya CCM inajidai kuwahurumia ndio hao hao watakaobebeshwa mzigo wa tozo ili kugharamia matibabu yao wenyewe. Sasa hapa unafuu upo wapi? Ikiwa wanajinasibu kuwa wanawajali masikini mbona wanawakamua tena masikini kupata fedha za kuwahudumia masikini ‘bila malipo’?

Ni mwendawzimu pekee atakayefurahia ujio wa sheria ya bima ya afya kwa wote. Tukumbuke bima ya afya ya sasa haikamui watu wasiohusika. Naomba tuelewane vizuri hapa. Mfuko wa NHIF unatunishwa kutokana na michango ya wanachama tu. Hauwagusi wasiokuwa wanachama. Lakini bima ya afya kwa wote itawagusa wote……waliomo na wasiokuwamo. Huu ni zaidi uzezeta.

Na tukumbuke kwamba sio watanzania wote wanaotegemea bima ya NHIF. Wengine wamo kwenye bima nyingine kama vile AAR, Strategies, Momentum, nk. Sasa kitakachotokea ni kwamba hata kama mtu unatibiwa kwa bima ya AAR ambako michango yako inaingia, utalazimika tena kukatwa pesa zaidi ili ziende kuhudumia wanachama wa NHIF. Maana yake ni kwamba utalazimika kujilipia bima yako ya AAR huku ukijiandaa kukamuliwa fedha zaidi ziende zikawalipie watu wengine kwenye bima nyingine ya afya isiyokuhusu ndewe wala sikio.

View attachment 2834133
Watanzania tunakamuliwa mno!

Viongozi wa nchi hii wamekosa ubunifu. Wanajiendea tu kama vipepeo wasiokuwa na dira wala muelekeo. Nchi ingekuwa na watu wanaofikiri sawasawa, wasingekuja na hoja ya kutaka kuwakamua wananchi zaidi wakati wananchi hao hao wanaendelea kukamuliwa kodi ya kizalendo isiyokuwa na kichwa wala miguu. Haya ndiyo matokeo ya kutawaliwa na watu wasiokuwa na dira wala muelekeo. Wanapuyanga tu bora liende.

Nawasilisha.
Utaambiwa wewe ni mchochezi,
Unatumika kisiasa!
Unatumika na "mabeberu."
 
Mkuu Nina maswali kidogo kwako:
1. Hivi mkuu unategemea ni nan alipe kodi na ni nan asilipe kodi? Hao unaowatetea kwenye tozo za simu je hawatumii hizi barabara zilizojengwa kwa lami? Je hawalindwi na jeshi la police? Je watoto wao hawaendi shule hizi za serikali? Nk nk nk!
Kama huko pote wanapata Huduma je unategemea hizo huduma nani anaziwezesha? Au waona ni haki wao wahudumiwe bure wakati wengine wanarundikiwa mikodi?
2. Je unafahamu idadi ya watu wazima ilivo kubwa (wenye miaka zaidi ya 18) ambao wamekaa bure tu hawazalishi wala kulisaidia taifa kwa chochote zaidi ya kulalamika tu kushoto na kulia? Na tafadhali tusiambiane hakuna ajira kwasababu hili limekuwa kimbilio (sababu ya kila anayetaka hata kufanya uvivu tuu). Wakati mwingine huwa natamani kodi ya kichwa irudishwe ili kupambana na kundi hili. (Tuliokuwepo wakati wa kodi ya kichwa inakusanywa mtakubaliana nami jinsi ilivolazimisha watu kufanya kazi)

Ningeelewa iwapo ungependekeza maboresho katika baadhi ya mambo yalivo sasa na sio kuongelea watu wasilipe kodi.

Nitasema machache nayoona ni ya kuboresha ili twende mbele kwa kasi.

1. Futa seating allowance zote za watumishi wa uma (hichi ni kichaka cha wizi na ufisadi)
2. Ubadhirifu wote unaotajwa kila mwaka kwenye report za ÇAĞ ushughulikiwe kikamilifu na watu wafungwe na mali zao zitaifishwe kweli.
3. Taasisi huru na zenye weledi zifanye majukumu yao kikamilifu.
4. Kurekebisha sheria za kodi zinazotoa upendeleo kwa viongozi ili kufuta dhana nzima ya sisi na wao.

Hayo ni baadhi tu ya mapendekezo ya kuboresha na nina amini yapo mengi ya kuboresha kuliko kutetea watu kutokulipa kodi.
1. Serikali siku zote wanajinasibu kuwa wanawasaidia kupata matibabu BURE lakini pesa inayotumika kugharamia matibabu inakamuliwa kutoka kwa wanyonge hao hao. Kwa hiyo wanakuwa hawajawapa unafuu wowote. Hii ndio pointi yangu.

2. Idadi ya watu wazima (hasa waliohitimu vyuoni) kutokuwa na kazi hili ni tatizo la serikali. Ndiyo inayopaswa kuboresha mitaala itakayowawezesha wahitimu kujiajiri na pia serikali ndio inapaswa kutengeneza nafasi za ajira ili wananchi wapate kuajiriwa.

Kuhusu mapendekezo yako umemsahau Mwigulu Nchemba aliyechota zaidi ya trilionii 3 za ufisadi kupitia mkataba wa ujenzi wa SGR. Hili utekelezaji wake ni mgumu. Kinachoweza kumaliza kansa hii kabisa ni kuwaondoa CCM madarakani kwani CCM ni kama ukoo wa panya......kila panya akizaliwa anakuwa mwizi.
 
Sisi ni wapole Hadi raha kama huyo ng'ombe.
Sijui ni macho yangu,pale chini ni miiba sijui!.
Wenye akili kubwa,wakisema tunahitaji KATIBA mpya,maskini anasema hata iliyopo haijui na hajawahi kuisoma Wala kuishika mkononi😠😠.
So,hakuna namna.
Wasomi wanapiga kelele juu ya katiba mpya,mtu WA chini anakwambia acha wapararuane wao kwa wao yeye hayamhusu.
Mada hii inatakiwa uilete kipindi Cha Kampeni,hapo ndo utatathimini,je uwaelezee au ujikaushie tu.
🇹🇿🤔.
Watu wa chini wanapaswa kuelimishwa namna serikali ya CCM inavyowafanya punda kupitia katiba mbovu. Kidogo kidogo wataelewa somo na kujanjaruka.
 
Tukiacha uongo,
Wanaotumia pesa nyingi kwenye hizo electronic money, ni hao hao matajiri, masikini wataolipiwa bure bima utakuta wanafanya transfer zisizozidi laki kwa mwezi ambazo tozo ya serikali ni chini ya 2000/-,

Lakin wale wenye uwezo ndio utakuta kwa mwezi kafanya miamala ya electronic zaidi ya 5M makato ya tozo 30K na bado anaenda kulipa bima ya Afya kwa pesa nyingine,

Bima hii ni msaada kwa hao masikini, usiseme watakatwa tozo, ukweli hata hizo tozo zao kwa mwezi hazifiki 5k
Mkuu ukichukua 2,000 ya masikini inauma zaidi kuliko kuchukua 2,000,000 ya tajiri. Ukirudia kusoma uzi kwa makini utaelwa hoja yangu.
 
Back
Top Bottom