Rais Samia achana na siasa za watemi na machifu, ni hatari, hazikusaidii na hazilisaidii taifa

Mungu ni dhana na shetani ni dhana. Usifungwe na utamaduni wa kimagharibi. Hata sisi tunaweza kuwa na mungu wetu siyo lazima huyo mungu aliyeletwa na wazungu na wewe ukakalilishwa bila kujua
Tunaambiwa kila mtu ana uhuru wa kuabudu hivyo wewe amini tu huyo mungu wako haina shida na mimi nitamwamini ninayemwamini. Upo hapo..?
 
Mimi ninavyoelewa Mungu ni moja na ndiye aliyeumba vyote vilivyomo katika dunia hii, mimi siamini kama kuna Mungu wa wazungu na Mungu wa waafrika, kwa kifupi siamini ktk uwepo wa hao miungu unaosema.
Kabla ya wazungu kuja wazazi wako walikuwa wanaabudu mungu yupi
 
Acheni kumtukana Magufuli nchi itatulia, vinginevyo tunaelekea kuwa sawa na watu wa Babiloni
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Jamani muacheni ajaribu anacho jaribu majibu atayapata baadae...
Hili taifa sasa hivi kila mtu anajaribu kitu chake hata walivyo ambiwa wasijaribu wanajaribu... Wacha wajaribu
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Wakulaumiwa ni washauri wake. Hii ni ku balcanise
Chief Marialle huwa analetewa fedha kutoka kwa Malkia Elizabeth wa Uingireza.
Hivyo kitendo cha samia kuungana naye kuna upigaji mkubwa wa fedha kutoka UK. Na picha zitatumwa UK nyingi sana Leo
Hii Balkanisation/Kutugawa Kikabila ni hatari sana. Ila wa kulaumiwa ni WASHAURI wake maana wanampotosha.
 
Machifu walikuwa kwa sehemu kubwa vibaraka wa ukoloni. Wengi pia walitawala kwa mifumo ya kitapeli, kiwiziwizi, unyanyasaji, udikteta, uporaji nk.
Kuuza wanajamii yao kwa wakoloni.

Museve, suala la Machief lilitaka kumuweka matatani! Huko west Uganda watu wakawa hawaogopi risasi za polisi kisa Chief kaagiza. Ili mlazimu Museveni kumuamisha chifu huyo nankumuweka kwenye kind of house arrest!!!

Machief....tuna wapenda lakini wana taabu zao.
 
Ulipotaja Magufuli ndo ulipoharibu, kwa dunia ya wasitaarabu na yenye usitawi haiwezi kulilia kuongozwa na sadist Kama JPM. Taja mwingine plz, Kama Taifa tulikosea sana awamu ya tano, na Mungu akaamua kutuponya, usiturejeshe huko.
Umeona eh watu wengine badala ya kumshukuru Mungu tena wanakumbushia machungu,hii ni ajabu kabisa.
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Anataka aweke legacy ya kurudisha uchifu, pia tunamuomba kule Zenj arudishe usultan.
 
Chief Marialle huwa analetewa fedha kutoka kwa Malkia Elizabeth wa Uingireza.
Hivyo kitendo cha samia kuungana naye kuna upigaji mkubwa wa fedha kutoka UK. Na picha zitatumwa UK nyingi sana Leo
Dah kumbe bibi anatuma mzigo kwenye koloni lake? Hapo sawa
 
Nimewahi kuishi Moshi miaka mingi sana. Nawafahamu kwa kiasi fulani wachaga. Wakiwa mikoa mengine tofauti na kwao wachaga ni kama wamoja hivi lakini ukiwa kwao Kilimanjaro aisee hawa jamaa kila moja na kwao utasikia tu mimi mmarangu, mkibosho, mrombo, mmachame, mnarumu, muoldmoshi, muuru, msiha, mkiruwa n.k. Na kwa kiasi kikubwa hayo maeneo yote yana machifu/mangi/viongozi wao japo siku hizi hawana nguvu sana nje ya maeneo yao toka serikali ilipofuta hayo mambo ya machifu.

Maswali ya msingi hapa
1. Je hao mamangi/viongozi wa kila eneo walikaa lini na wapi wakakubaliana kuwa Mareale ndio mkuu wao?
2. Kuna kipindi si muda mrefu sana huyo Mareale alikuwa na kesi mahakamani na ndugu yake ya kugombea uchifu, je ilishaiisha na maamuzi
yalikuwaje
3. Na kama machifu wote wa Moshi walikubaliana kumualika mgeni rasmi mbona kwenye tangazo anatajwa tu Marealle kwa nini isiwe "chifu
mkuu Marealle kwa pamoja na machifu wenzake fulani na fulani wa Kilimnjaro wanamwalika mgeni rasmi ........... kwenye tamasha?
4. Shughuli nyingi za machifu huwa zinaambatana na shughuli za kishirikina na uganga wa jadi kwa kiasi fulani hili kila mtu anajua, je kwa mtu
ambaye ana imani na hofu ya Mungu kushiriki shughuli za hawa watu si kuchanganya mambo kweli?

Ni mtizamo tu.
Wakati mwingine ifike mahali wasaidizi wa SSH wasimhusishe na watu wa ajabu..
Huyu anayejiita Mangi Mkuu wa Wachaga si ndiye aliyeupora umangi kutoka kwa ndugu yake?
Si ndiye aliyenunua mahoteli kibao kwa mgongo wa uwekezaji kisha akayafunga? Embassy Hotel - Dar etc..
 
Hizi siasa za kukumbatia viongozi wa kimila hazina tija kwa nchi yetu zama hizi.....kuna sehemu tunafeli tunapoendekeza hui usanii
Wanaoandaa events za Rais wajitahidi sana ili isionekane kuwa Rais anatafuta support ya wadau.

Kwasababu inaonekana kabisa kuwa haya ni maandalizi ya 2025.

Anyways. Namtakia kila la heri Madam President.
 
Huyu mama anafikiri anajijenga kiasiasa kwa kukumbatia mambo ya kishirikina yaliyopitwa na wakati, zaidi ya kufanya uganga na matambiko machifu wana jambo gani la maana kwenye jamii ya watu waliostaarabika katika karne hii ya 21..........hivi leo tunaweza kuwatumia machifu kubuni chombo cha kwenda kufanya utafiti anga za juu, au watachekecha manyanga na matunguli yao na kurusha ungo kwenda sayari ya Mars........bwahahahaaa...........chifu hangaya bhana..​
 
Tangu Rais Samia ashike madaraka amekuwa busy sana kuzing'ang'ania na kuzipigia debe siasa za kuwaenzi na kuuenzi utamaduni wa machifu na watemi hapa Tanzania. Hapa nitaweka kweli kadhaa kuhusu ubaya wa siasa hizo kwa nchi yetu na vizazi vijavyo.

1. Utamaduni wa watemi na machifu ni utamaduni wa kikabila na kikoo kwa 100%. Hawa hawafanani, hawakubaliani na hawakai chungu kimoja. Unalenga kuwagawa watanzania kuliko kuwaunganisha.

2. Utamaduni wa watemi na machifu umezungukwa na mfumo dume kwa karibu 100%. Kadri unavyopaliliwa ndivyo ambavyo mfumo dume unakuzwa na kuota mizizi kwenye jamii.

3. Kwa sehemu kubwa sana tamaduni za watemi na machifu zimejikita kwenye ubagani, matambiko, ushirikina na mambo ya kale. Sioni mantiki yoyote kwa serikali kuukumbatia sasa kwenye karne ya 21.

4. Kwa sehemu kubwa utamaduni wa tawala za machifu unakinzana na mifumo ya tawala rasmi za kiserikali na kisheria. Huwa ni vitu visivyoweza kwenda sambamba. Kuimarika kwa tawala rasmi za kiserikali automatically kuliua tawala za machifu na watemi, kuzifufua upya hizo tawala za machifu sasa ni kuhatarisha uwepo wa tawala rasmi za kisheria na kiserikali.

5. Utamaduni wa tawala za watemi na machifu kwa sehemu kubwa umedhoofika, kufifia, kuparaganyika au ulishakufa kwa jamii nyingi sana hapa Tanzania. Wengi watakaoibuka sasa na kuitwa watemi au machifu huenda watakuwa waganga wa kienyeji, wazee wa kikoo, matapeli (wazee wa fursa), wajumbe wa CCM wa nyumba kumi kumi (wazee wazee). Kiuhalisia utakuta sio watu halisi wa kuwakilisha watemi na machifu wa zama zile. Kuwakumbatia watu wa namna hiyo ni kupoteza muda na rasimali.
Divide and rule; katika karne ya ishirini tupande basi la ukabila !
 
Chief Marialle huwa analetewa fedha kutoka kwa Malkia Elizabeth wa Uingireza.
Hivyo kitendo cha samia kuungana naye kuna upigaji mkubwa wa fedha kutoka UK. Na picha zitatumwa UK nyingi sana Leo
Justification ya kipuuzi sana. Sijui kuwa kuna watu hapa JF wanaweza kuandika vitu vya kipuuzi namna hii.
 
Back
Top Bottom