Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Siku ya leo Rais Magufuli aliitumia kwa kulihutubia Bunge la 11 na kulivunja rasmi, huku wabunge hao akiwaaga wakielekea majimboni mwao, kwenda kwenye mchakato wa kujaribu bahati yao, ili kama watarejea tena kwenye Bunge lijalo la 12 mwakani baada ya uchaguzi Mkuu.
Kama tunavyokumbuka kuwa katika siku chache zilizopita aliibuka Mbunge wa Mwibara kwa tiketi ya CCM Kangi Lugola "akimmwagia" sifa nyingi, Rais Magufuli na kumfananisha na Yesu Kristo katika utendaji wa kazi zake!
Kutokana na kauli hiyo ya Kangi Lugola, walijitokeza viongozi mbalimbali wa dini ya kikristo na wananchi wengine waliokemea vikali kauli yake hiyo na kuiita ni ya kufuru, kwa kuwa hakuna binadamu yeyote wa kumfanamisha na Yesu Kristo na hivyo kumuomba huyo Kangi Lugola aombe radhi na kuifuta kauli yake hiyo.
Ninavyomjua Rais wetu ikiwa kuna jambo lililosemwa au kutendwa siku za karibuni na halikumfurahisha, basi angelikemea vikali sana
Nimeisikiliza kwa makini hotuba yake yote aliyoitoa na sikusikia sehemu yoyote aliyomkemea Kangi Lugola kwa kitendo chake cha kumfananisha yeye Rais na Yesu Kristo.
Kitendo chake cha kulinyamazia kabisa jambo hilo, inaonyesha kuwa "amefurahishwa" na sifa hizo alizopewa za kufananishwa na Yesu Kristo!
Kama tujuavyo ni kuwa katika imani ya dini ya kikristo tunaamini katika utatu mtakatifu, ambao ni Mungu Baba, Mungu mwana na Roho mtakatifu, kuwa ni kitu kimoja ambacho ni Mungu mwenyewe.
Hebu twende kwenye maandiko, kwenye kitabu cha Biblia takatifu, kwenye kitabu cha Kutoka 20:4-6 inasema hivi "Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini, chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia, kwa kuwa mimi BWANA Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu kwa maelfu wanipendao na kuzishika amri zangu" mwisho wa kunukuu maandiko hayo ya Mungu
Hebu tuangalie mistari mingine kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume 12:20-23 inasema hivi "Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni, wakamwendea kwa nia moja na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha Mfalme cha kulalia, wakataka amani, kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya Mfalme.
Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi kwenye kiti cha enzi, akasema mbele yao. Watu wakapiga kelele wakisema, hii ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akaja na kumpiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu anaostahili. Akaliwa na chango akafa" mwisho wa kunukuu.
Kwa hiyo kitendo cha kutokemea au kulitolea ufafanuzi suala hilo, maana yake amelibariki na kulikubali na pia ameona kitendo kilichofanywa na Kangi Lugola ni sahihi kabisa.
Kwa hali hiyo tutegemee Mungu wetu atajibu kwa ghadhabu kubwa kwa wakati muafaka kitendo hiki alichofanya Kangi Lugola na Rais Magufuli kuonekana amekifurahia kitendo hicho.
Kama tunavyokumbuka kuwa katika siku chache zilizopita aliibuka Mbunge wa Mwibara kwa tiketi ya CCM Kangi Lugola "akimmwagia" sifa nyingi, Rais Magufuli na kumfananisha na Yesu Kristo katika utendaji wa kazi zake!
Kutokana na kauli hiyo ya Kangi Lugola, walijitokeza viongozi mbalimbali wa dini ya kikristo na wananchi wengine waliokemea vikali kauli yake hiyo na kuiita ni ya kufuru, kwa kuwa hakuna binadamu yeyote wa kumfanamisha na Yesu Kristo na hivyo kumuomba huyo Kangi Lugola aombe radhi na kuifuta kauli yake hiyo.
Ninavyomjua Rais wetu ikiwa kuna jambo lililosemwa au kutendwa siku za karibuni na halikumfurahisha, basi angelikemea vikali sana
Nimeisikiliza kwa makini hotuba yake yote aliyoitoa na sikusikia sehemu yoyote aliyomkemea Kangi Lugola kwa kitendo chake cha kumfananisha yeye Rais na Yesu Kristo.
Kitendo chake cha kulinyamazia kabisa jambo hilo, inaonyesha kuwa "amefurahishwa" na sifa hizo alizopewa za kufananishwa na Yesu Kristo!
Kama tujuavyo ni kuwa katika imani ya dini ya kikristo tunaamini katika utatu mtakatifu, ambao ni Mungu Baba, Mungu mwana na Roho mtakatifu, kuwa ni kitu kimoja ambacho ni Mungu mwenyewe.
Hebu twende kwenye maandiko, kwenye kitabu cha Biblia takatifu, kwenye kitabu cha Kutoka 20:4-6 inasema hivi "Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini, chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia, kwa kuwa mimi BWANA Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu kwa maelfu wanipendao na kuzishika amri zangu" mwisho wa kunukuu maandiko hayo ya Mungu
Hebu tuangalie mistari mingine kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume 12:20-23 inasema hivi "Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni, wakamwendea kwa nia moja na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha Mfalme cha kulalia, wakataka amani, kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya Mfalme.
Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi kwenye kiti cha enzi, akasema mbele yao. Watu wakapiga kelele wakisema, hii ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akaja na kumpiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu anaostahili. Akaliwa na chango akafa" mwisho wa kunukuu.
Kwa hiyo kitendo cha kutokemea au kulitolea ufafanuzi suala hilo, maana yake amelibariki na kulikubali na pia ameona kitendo kilichofanywa na Kangi Lugola ni sahihi kabisa.
Kwa hali hiyo tutegemee Mungu wetu atajibu kwa ghadhabu kubwa kwa wakati muafaka kitendo hiki alichofanya Kangi Lugola na Rais Magufuli kuonekana amekifurahia kitendo hicho.