Rais Magufuli anavyozungumzwa maofisini

Rais Magufuli anavyozungumzwa maofisini

Hili jamaa litoa mada jana lilijitanabaisha kwenye uzi mmoja una husu 9% kwamba limejiyolea kukandia kila kitu anachofanya Magu..

Lakini tusishangae sana maana hiki ndicho walichobaki nacho UKAWA ....
 
Inawezekana mleta mada hajafanya utafiti wowowte ila ameleta hisia zake, lakini hisia hizi zinaweza kuwa kiwakilishi cha uhalisia wa malalamiko ya wafanyakazi wengi Serikalini na washirika wao katika sekta binafsi na jamii za Kiraia.

[Null hypothesis] Kwa vyovyote vile kipindi cha uongozi butu cha Mwinyi, Mkapa na Kikiwete kilizalishia taifa la mediocre and incompetent personnel, mitandao ya rushwa na inept leadership. Hali hii iliathiri nyanja na sekta zote; Sekta Binafsi, Serikalini na hata Jamii ya Kiraia. Licha ya kuelimishwa kwa gharama kubwa, wafanyakazi serikalini na washirika wao katika sekta binafsi na Jamii ya Kiraia waliishi bila kujali umuhimu wa kutumia ujuzi na maarifa waliyopewa kwa gharama kubwa.

Utawala wa JPM unawataka wafanyakazi wa serikali na washirika wao katika sekta binafsi na Jamii ya Kiraia kuwa waadilifu, competitive na competent. Lakini wahusika wananshindwa, kwa kuwa hawakuzoea (mzoea vya kunyonga). Kwa hiyo, na kwa yovyote vile, inategemewa kuwa kada hii ya watumishi wa umma na washirika wao katika sekta tofauti, italalamikia sera na mwelekeo mpya wa sera za serikali ya JPM.

Hayo ndio MABADILIKO! huko ndiko taifa kuelekea KUJITEGEMEA. Lakini sera ya umma yoyote ikilalamikiwa na watu wa kada zote (longitudinally na latitudinally) ni kipimo cha kutosha kuwa sera husika imefanikiwa malengo yake, kwa maana imefikia na kugusa kila mtu bila kubagua.

Katika mazingira ya kisiasa ya namna hii, na tofauti na tawala za Mwinyi, Mkapa na Kikwete, utawala wa Magufuli hautatembelea nyota ya Mwl. Nyerere kama watangulizi wake.
Mkuu unapoteza mda wako bure kumjibu huyu nyumbu
 
Hizi akili butu za watanzania zitatutoka lini?

Hv nani kasema rais lazima apendwe na wote? Au kila anachokifanya kiungwe mkono na watu wote?

Likubwa ni kuwa anafanya kwa maslahi mapana ya wananchi na nchi kwa ujumla.
 
Hoja za wapuuzi huleta upuuzi.Mimi nipo Ofisini,tena Ofisi ya serikali hakuna upuuzi huo ila kwa waliozibiwa njia zao za kipuuzi. Mtoa mada sema JPM kapunguza nini cha halali yako kilichokuwepo wakati wa JK?
 
Hizo ofisi ni majipu...siku zake zinahesabika! Kama wanataka comedian wangemchagua mr.Bean...
 
Sasa kama yeye anajutia ninyi mliomchagua mtaendelea kumsifia?
 
maneno mazito kama haya si vizuri kuyatoa bila ushahidi, pili si vyema hata kidogo kusema wafanyakazi waserikali (nadhani ulimaanisha wote) wanawaza na kuzungumza hivyo. Kwa kifupi hizi ni kauli kutoka kwa majipu. ..!
 
Acha atunyooshe tu, bata zilizidi, kuna ofisi za umma walikua wanajiona kama wanafanya kazi international organisation, pesa ya wavuja jasho ilikua inatafunwa na wachache. Magu anachofanya ni kuturudisha katika misingi.
 
"Hakuna kitu kwa huyu jamaa,bora hata li-Kikwete,linachekacheka lakini uhakika wa maisha unakuwepo"...."Bora mimi sikumchagua...nilitaka Lowassa apite"....

"Aah bora mimi nilibaki na mke wangu nyumbani,mtu OC toka Novemba hazijaja,za Maji zilikuja kulipa madeni ya wakandarasi".

Haya maneno yanazungumzwa sana maofisini,ni ofisi zote za umma na binafsi,ni kada zote,kuanzia mabosi mpaka wafagizi.Kauli za kujutia jutia tu.Yaani wakikutana wawili watatu hawawezi kuachana bila kuzungumzia hali ngumu ya sasa.

Wafanyakazi wenzangu nawatia moyo tuendelee kuvuta subira,labda bajeti ijayo
Wewe punguani kweli unajifungia ndani na mke wako unaandika porojo unaleta JF hizo ofisi gani ulizopita.
 
Hayo unayazungumza mwenyewe udimezeshe watu maneno yako. Huyo tupe unafuu wa aliyepita kwa mchanganuo maana hayo ni maneno yako
Huku napo ndio wanaongea hivyo mkuu hii inanifanya nimuamini huyu jamaa aliyeleta huu uzi
 
Wewe punguani kweli unajifungia ndani na mke wako unaandika porojo unaleta JF hizo ofisi gani ulizopita.
Inawezekana sio porojo mkuu kuna ofisi mbili tatu katika shughuli yangu nayofanya inayonifanya nizungukie ofisi mbalimbali nimesikia mzungumzo kama hayo
 
Sema Rais apewe muda lakini kwa maoni yangu afanye kazi za uraisi hizi nyingine awaachie mawaziri
 
Inawezekana sio porojo mkuu kuna ofisi mbili tatu katika shughuli yangu nayofanya inayonifanya nizungukie ofisi mbalimbali nimesikia mzungumzo kama hayo
Tutaamini vipi weka ushahidi wa audio.
 
Tutaamini vipi weka ushahidi wa audio.
Nitakua mchawi kama nitaenda mahalimna kuanza kurekodi maongezi ya watu,by the way zipo ambazo zinamuongelea kwa mazuri.sasa msitake kujidanganya kila mtu atakua na mtazamo chanya juu ya uongozi huu wapo wengi tu wanaoona mambo hayaendi na wapo wanaojaribu kuupa muda zaidi
 
Back
Top Bottom