MPIGA ZEZE
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 2,539
- 2,297
Ninashangaa wanaJF - washabiki na wakosaiaji wa JPM - mnatokwa povu kuhusu habari ya mtukufu kuahirisha safari ya kuhudhuria UN! Kuna ushahidi gani kwamba hiyo safari ilikuwa imepangwa kuwepo? Tumesikia nchi nyingine za Afrika wakitoa taarifa mapema kuhusu ushiriki wa wakuu wa nchi zao na ajenda waliyokuwa wameishadhamiria kuiwasilisha. Angalao ile safari ya kwenda Zambia kushiriki katika uapishashi wa Rais wao ilikuwa imeishatolewa taarifa rasmi kutoka Kurugenzi ya mawasiliano na baada ya masaa macahche ndio ikatoka nyingine rasmi ikifuta ile ya awali. Hapa tunaweza kujadili kuhusu hilo bila wasiwasi. Lakini hili la UN sijui kama kunataarifa rasmi ilikuwa imeishatoka kuhusu uwepo wa safari. Kwa hivyo tunajadili safari HEWA iliyoahirishwa - ama kwa kujipatia umaarufu wa kisiasa au vinginevyo.
