Simuelewi kabisa huyu jamaa
IFIKE MAHALI WATANZANIA TUACHE HUU UPAMBAVU PAMOJA NA UNAFIKI! Inafika mahali unashindwa kuelewa kama kuna watu wamepata ajira ya kutumia JF kwa kuwakilisha mawazo potofu ya vikundi fulani. Ni aibu KUBWA kwa sisi Watanzania ambao huu UJINGA NA UHUNI hatukuwa nao wala haukuwa katika malezi YETU kama watanzania.
Inakauwaje mtu anaanza kumuandama MHS Rais hapa JF na sababu za kijinga kama hizi? Hebu tujiulize haya:
1. Kwani ni lazima Mhs Rais aende kwenye ule mkutano? Jibu ni kuwa si lazima! Sasa wewe au nyie mnawashwa NINI? Tatizo deal zenu za kisanii zimekosa milango ndo maana mnatoa mawazo ya kijinga kama haya.
2. Mhs Rais tumemchagua sisi, na wala si nyie tu hicho kikundi cha KIJINGA. Koma kabisa kutumia JF kama sehemu ya kutoa mawazo HASI kwa watu ambao wamechaguliwa na asilimia kubwa ya watanzania na si nyie hicho kikundi kidogo.
3. Kumbuka kuwa hata mfanye NINI he is here to STAY na ataendelea kusafisha site ili nyumba itakayojengwa iwe imara kwa vizazi vingi vijavyo.
4. Kwa wale ambao wana itikadi zingine mbali na za Mhs Rais, tueleze mnataka kufanya NINI? Kulea UOZO ili deal na missions zenu ziendelee? Hizo ndizo agenda za kuleta maendeleo ENDELEVU? Au tueleze kama mngekuwa serikalini mngelifanya NINI kwanza? Fanya hata the so called political dev simulation tuone mngelifanya nini pamoja na predictions zenu? Acha kabisa mawazo ya kijinga jaribu kuongea vitu vyenye tija kwa watu wetu na taifa lao.
5. IKUMBUKWE nchi ilikuwa IMEOZA na MHS Rais anafanya vizuri. Na hata nyie mkiendeleza mbinu zenu za kutaka kumkatisha TAMAA na kutuchanganya sisi tulio mchagua basi MNAJIDANGANYA kabisa. Tuko na yeye na matundu yanukuja ingawa si leo lkn yatakuja.
Hongera Mhs Rais wetu kipenzi na usikatishwe tamaa na hiki kikundi kidogo cha kIHUNI tu. TOGETHER AHEAD. MUNGU ibariki Tanzania na watu wake.