Wana JF,
Ndugu zangu nimeshuhudia watu wakizima TV na radio zao baada ya kuona JK anaanza kuhutubia. Wengine wanasema kumsikiliza huyu jamaa ni kujiumiza kichwa bure.Maana TV stations na redio mbalimbali zimeweka hicho kipindi, watu wanaona ni bora kuzima vyote na baada ya yeye kuhutubia ndo wawashe TV na radio zao.Hii inadhihirisha jinsi gani watu walivyomchoka rais Kikwete.
Nyerere alipokuwa anahutubia kila mtu alikuwa na hamu ya kusikiliza anasema nini, JK hasemi la maana hivyo naturally watu hawawezi kumsikiliza. Hata UN ukiwa na pumba kama JK wakati unahutubia ndio watu wanatoka kuvuta sigara
Anatupa takwimu za shule na despensary na idadi ya wanafunzi,huyu raisi ni kituko!!
bonge la hutuba tupo hapa watu wanashangilia ile mbaya mheshimiwa ni rais wa karne
Dah mkuu 0Tatizo vijana wa sasa hatujui Mambo muhimu na pili watanzania hatuna uzalendo kabisaa. Mie si mfuasi wa vyama vya siasa ila ninajua kumsikiliza kiongozi wa taifa langu ni muhimu sana. Tuwapende na kuheshimu viongozi wetu tusijechekwa na mataifa mengine
Kwahiyo?Nilikuwa naangalia Channel Ten, na walipojiunga kwenye hotuba jamaa nikaona wamejiunga kupitia TBC1 nikazima tv na kwenda jogging!!!!