Rais Kikwete kweli watu wamekuchoka

Rais Kikwete kweli watu wamekuchoka

Kila neno huyu jamaa analotamka, linazidi kuigawa nchi vipande vingi zaidi. Sijui mwisho wa siku, atatawala kipande kipi kati ya vipande hivyo anavyovitengeneza, kwa midomo yake mwenyewe!!!!????? Mbona hajifunzi kwa makosa?? Labda aliyemroga, amekwisha kufa!!!!!! Laiti angejua kwamba kupigiwa makofi na vigelegele, na hao mburula wa kukodi, ni sawa na kujipigia yeye mwenyewe makofi na vigelegele!!!!!!! Aliulilia Urais, lakini hakujua Urais ni nini!!!!!!!
 
Sina hamu jinsi alivyomsaliti Warioba na kuwa mtu wa kwanza kuikana nchi yetu Tanganyika isiyo na mwenyewe mpaka sasa.
 
Tatizo vijana wa sasa hatujui Mambo muhimu na pili watanzania hatuna uzalendo kabisaa. Mie si mfuasi wa vyama vya siasa ila ninajua kumsikiliza kiongozi wa taifa langu ni muhimu sana. Tuwapende na kuheshimu viongozi wetu tusijechekwa na mataifa mengine
 
Tatizo vijana wa sasa hatujui Mambo muhimu na pili watanzania hatuna uzalendo kabisaa. Mie si mfuasi wa vyama vya siasa ila ninajua kumsikiliza kiongozi wa taifa langu ni muhimu sana. Tuwapende na kuheshimu viongozi wetu tusijechekwa na mataifa mengine
Vijana? ba nso, wewe una umri gani?
 
Last edited by a moderator:
Tatizo vijana wa sasa hatujui Mambo muhimu na pili watanzania hatuna uzalendo kabisaa. Mie si mfuasi wa vyama vya siasa ila ninajua kumsikiliza kiongozi wa taifa langu ni muhimu sana. Tuwapende na kuheshimu viongozi wetu tusijechekwa na mataifa mengine
Nyerere alipokuwa anahutubia kila mtu alikuwa na hamu ya kusikiliza anasema nini, JK hasemi la maana hivyo naturally watu hawawezi kumsikiliza. Hata UN ukiwa na pumba kama JK wakati unahutubia ndio watu wanatoka kuvuta sigara
 
Tatizo vijana wa sasa hatujui Mambo muhimu na pili watanzania hatuna uzalendo kabisaa. Mie si mfuasi wa vyama vya siasa ila ninajua kumsikiliza kiongozi wa taifa langu ni muhimu sana. Tuwapende na kuheshimu viongozi wetu tusijechekwa na mataifa mengine

Kiongozi yoyote utapenda kumsikiliza kama yuko neutral na anachohutubia kweli kinaakisi anachofikiria ,lakini yule leo anasema hiki akiwa ughaibuni anaongea kingine,akiwa Dodoma anahutubia kingine, akirudi bonga anahutubia tofauti na cha juzi,hotuba za kiongozi huyo zinakuwa hazina ladha ya kuzisikiliza.

Tofauti na Nyerere pamoja na mambo yake yote lakini hotuba zake hadi hii leo zinamfanya mtu akimbilie kuziangalia tena na tena hazichoshi japo za miaka mingi,sababu anaamini anachokiongea na anafanana na anachokiongea.
 
Mie ikabidi tv nniwaachie watoto waangalie carton, nani ana muda wa kumsikiliza Dhaifu?

Na asivyozua kufupisha hotuba, hivi ulimwengu huu wa sasa nani ana muda wa kusikiliza hotuba ya masaa 2? hajui ata kusoma mazingira? toa hutuba na unaowahutubia wawe live huku ukifahamu binadamu hawezi kukusikiliza kwa makini kwa muda mrefu hivyo labda tu uwe kweli umebarikiwa kwa hotuba za kusisimua, sasa uwezo mdogo wa hotuba wa Kikwete na hotuba ya masaa 2 si nikuwatesa tu wasaka tonge waliokuwa ukumbini?
 
Nyerere alipokuwa anahutubia kila mtu alikuwa na hamu ya kusikiliza anasema nini, JK hasemi la maana hivyo naturally watu hawawezi kumsikiliza. Hata UN ukiwa na pumba kama JK wakati unahutubia ndio watu wanatoka kuvuta sigara[/QUOTE


Yaweza kua kweli ila sisi kama raia wenye uzalendo na heshima kwa taifa hatuna budi kumsikiliza kiongozi wetu tuliempa kazi ya kutuongoza.
 
Duh! rais wao hapendwi au interahamwe ndo hapendwi?
 
Back
Top Bottom