Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Ni bora angeenda kutoa hotuba ya Ijumaa kabisa. :confused2:
 
Atahutubia taifa kupitia wazee wa dar es salaam Ijumaa wiki hii alasiri.
chanzo: ikulu

Acheni kudhalilisha wazee wengine wasiohusika.Ninyi kama waandishi wa habari wekeni ukweli sawa.

Atahutubia wa Wazee Wanachama wa CCM wa Mkoa wa Dar Es Salaam.
 
"Tumempoteza mwanasheria mahiri kwa sababu zisizo na msingi alikuwa hodari sana kajiuzulu mzee wa watu----------------"
 
Muhongo kakomaa naye, akimwaga ugali lenyewe linamwaga mboga, athubutu kulitoa uwaziri aone!

Haya ndio madhara ya kufanyabiashara Ikulu; amekula 50% ya Simba Trust, sasa makina Muhongo na Maswi yamekomaa naye!! Inabidi apige domo na wazee ili upepo upite... lakini ndo anaua chama, CCM haitakaa imsahau huyu jamaa!
 
Hii idea ya kuongea na wazee wa CCM nani alileta? Sijawahi kusikia raisi yoyote duaniani anaongea na wazee.
Only in Tanzania
 
Muhongo kakomaa naye, akimwaga ugali lenyewe linamwaga mboga, athubutu kulitoa uwaziri aone!

Haya ndio madhara ya kufanyabiashara Ikulu; amekula 50% ya Simba Trust, sasa makina Muhongo na Maswi yamekomaa naye!! Inabidi apige domo na wazee ili upepo upite... lakini ndo anaua chama, CCM haitakaa imsahau huyu jamaa!

ni kweli kabisa mkuu. anakwenda kuongea na "WAZEE WA DAR" na kupindua maazimio ya bunge na hatimaye kuizika CCM kabisa. huyu bwana akili zake anazijua mwenyewe.
 
hakuna la maana hapo,ni mipasho kwenda mbele na hayo maccm ya daslam....muhongo kuendelea kupeta na bunge limedharauliwa..
 
Atahutubia taifa kupitia wazee wa dar es salaam Ijumaa wiki hii alasiri.
chanzo: ikulu

Ndugu Manyerer, siyo kupitia wazee wa Dar es Salaam bali vizee vya Chama cha Mafisadi (CCM) ambavyo vitakusanywa kwa mafuso na kugawiwa shs. elfu mbili mbili za ugoro. Kazi ya vizee hivyo itakuwa kushangilia hata akivitukana. Kwa nini asihutubie kupitia wahariri wa vyombo vya habari na akajibu maswali. Hana lolote la maana na vizee vingi vitakuwa vimelala kutokana na uchovu wa kubebwa na fuso (lorry)
 
Hivi anaongea na wazee ili iweje
Kwani wazee ndio Escrow
Kwani uozo wa uchaguzi wa serikali za mitaa umehusisha wazee
Nchi kwenda mzobe mzobe ni tatizo la wazee
Rweyemam kuhonga waandishi wa habari ni tatizo la Wazee
Kwani wazee ndio wameleta upungufu wa dawa
Wazee ndio wamezuia wafadhali
Wazee ndio wamepokea mgao wa tupa tupa kwa viroba kule stanbic
Wazee wameandika barua aliyoandika Mbena katibu wa Rais


Huko miaka ya nyuma, ukimsikia Rais anaongea na wazee, alikuwa anatoa ufafanunuzi wa mambo mhuimu ya kitaifa
Leo JK anakwenda kutafuta huruma za wazee ambao wengi umri hauwaruhusu kuelewa nini kinaendelea.

Anachokifanya ni kwenda kutafuta huruma, badala ya kukaa chini na kutoa suluhu.

Huruma anaitafuta baada ya kuona uchaguzi walioharibu haukuleta matokeo mazuri kwa propaganda.

Zamani ningesikiliza, siku hizi nasubiri kusimuliwa!
 
Atahutubia taifa kupitia wazee wa dar es salaam Ijumaa wiki hii alasiri.
chanzo: ikulu

wazee wa dar.jpg
"WAZEE WA DAR" wakiwa wamevaa sare za "UZEE WA DAR" wakifuatilia moja ya hotuba ya Mtukufu Profesa JK kwa umakini mkubwa sana. Ngoja wamsikilize kisha waje watuambie wameambiwa nini. Chezea "Wazee wa Dar" wewe!!!!
 
Back
Top Bottom