Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Rais Kikwete kuhutubia Ijumaa

Kumekuwepo na utaratibu wa hovyo ambao umeanza kumea kwa kasi siku baada ya siku wa watu kutunga na kusambaza taarifa za uzushi na uongo kwa maslahi yao binafsi, na hili limefanywa kuwa jambo rahisi kwa kuwepo mitandao ya kijamii na vyombo vya habari ambavyo havina weledi katika kazi zao.

NAOMBA NIJIBIWE NI LINI IKULU ILITANGAZA KUWA LEO IJUMAA, TAREHE 19, DEC 2014 MHE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ATAZUNGUMZA NA WAZEE WA JIJI LA DAR ES SALAAM..?

Utaratibu na tabia ya baadhi ya watu kupata taarifa zisizo authenticated na kuanza kuzisambaza ni tabia ya KIMBEA na haina budi iachwe na itokomezwe mara moja.
 
kamuulize rweyemamu alienda clouds kutangaza kuahirishwa hadi jumatatu alikuwa ana maana gani?
 
kwani ile siku amerudi toka USA pale airport alitoa wapi taarifa kuwa ataongea?
 
JK%2BMWISHO%2BMWEZI.JPG


Rais Kikwete ameahirisha kulihutubia bunge na 'Wazee wa Dar'; ambapo sasa ataongea nao Jumatatu wiki ijayo(Disemba 22, 2014),Ikulu imethibitisha kuwa na kusema muda utatangazwa.


Rais kikwete leo alitarajiwa kulihutubia taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es salaam katika mkutano wake ambao ulikuwa ufanyike katika ukumbi wa Hotel ya Blue Pearl,ubungo jijini Dar es salaam.

Katika mkutano wake huo Rais Kikwete alitazamia kuzungumzia mustakabali wa nchini sambamba na kuweka wazi juu ya sakata la utekelezaji wa maazimio nane likiwamo la bunge la kuwawajibisha viongozi waliotajwa katika sakata la uchotwaji wa fedha bilioni 360 katika akaunti ya Tegeta Escrow Pamoja na mambo mengine.

Katika maazimio nane ya bunge yaliyopendekezwa yalitaka viongozi waliotajwa katika ripoti hiyo kwa tuhuma za uchotwaji wa fedha kuchukuliwa hatua za kinidhamu na hata wanapo bainika kufilisiwa mali zao na kushitakiwa katika viombo husika kwa kuonekana kulihujumu taifa katika sakata hilo la uchotwaji wa fedha akaunti ya Escrow.

Rais pia alipanga kuzungumzia juu ya Sekta ya Elimu pamoja na agizo lake la ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari nchini,Upigaji kura za maoni kuhusu katiba Mpya utakao fanyika Aprili 30 pamoja na daftari la wapiga kura.

Hata hivyo Katika Hotuba hiyo Rais aliazimia kuelezea uchaguzi wa serikali za Mitaa ulivyo fanyika ambao ulionekana kukumba na dosari kadhaa katika vituo vya kupigia kura katika sehemu mbali mbali za nchi ulipo kuwa ukifanyika uchaguzi huo ambao uliweza kugharimu maisha ya watu kwa kupoteza maisha.
 
Atahutubia taifa kupitia wazee wa dar es salaam Ijumaa wiki hii alasiri.
chanzo: ikulu

He may as well save his breath!! hana jipya sana sana anataka kupotosha umma kuhusu sakata la Escrow kama alivyofanya kwenye bunge la katiba
 
Hivi huyu Shonza si nasikia ameolewa jamani?? Saa ngapi huwa anahudumia ndoa yake?? Naona hapa amejipa mamlaka ya usemaji kutoka magogoni.....
 
Kumekuwepo na utaratibu wa hovyo ambao umeanza kumea kwa kasi siku baada ya siku wa watu kutunga na kusambaza taarifa za uzushi na uongo kwa maslahi yao binafsi, na hili limefanywa kuwa jambo rahisi kwa kuwepo mitandao ya kijamii na vyombo vya habari ambavyo havina weledi katika kazi zao.

NAOMBA NIJIBIWE NI LINI IKULU ILITANGAZA KUWA LEO IJUMAA, TAREHE 19, DEC 2014 MHE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ATAZUNGUMZA NA WAZEE WA JIJI LA DAR ES SALAAM..?

Utaratibu na tabia ya baadhi ya watu kupata taarifa zisizo authenticated na kuanza kuzisambaza ni tabia ya KIMBEA na haina budi iachwe na itokomezwe mara moja.

Sawa mama mdogo tumekusikia..... Naona unatafuta kiki......
 
Back
Top Bottom