RAIS KUHUTUBIA TAIFA IJUMAA TAREHE 19/12/2014!
MDAU HUYU👇👇, KAAMUA KUITUNGIA SHAIRI KABISAAA SIKU HIYO MAALUMU!
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
NA IFIKE-IJUMAA!
(1) Na ifike ijumaa, twaisubiri kwa hamu,Hatutaki kuzubaa, siku ya mashamushamu,Kusuka ama kunyoa, kwao wezi wa kalamu,Na ifike ijumaa, tuone hatima yao
(2.)Mmoja kakata kamba, kakimbia machinjio,
Imekuwa ni kasumba, wakikosa kimbilio,
Wengine wayumbayumba, kama siku ya gulio,
Na ifike ijumaa, tuone hatima yao.
(3)Ijumaa sio mbali, twangojea uamuzi,
Naona moshi kwa mbali,wafuka bila ajizi,
Walishaonja asali, mzinga hawauwezi,
Na ifike ijumaa, tuone hatima yao!
(4)Shoka limo shinani, kukata lipo tayari,Limeanza mitaani, kutanguliza habari,Laendelea mwakani, wakizidisha jeuri,Na ifike ijumaa, tuone hatima yao!
(5)Majizi yote pembeni, twaja mbio tupisheni,
Utani weka pembeni, ofisi zetu pisheni,
Fedha zetu rudisheni, vifungo ni haki yenu,
Na ifike ijumaa, tuone hatima yao!