Rais Kikwete anaipenda CHADEMA!

Rais Kikwete anaipenda CHADEMA!

Kikwete anakili na busara sio akina mwigulu anajua maana ya demokrasia na maana ya mfumo wa vyama vingi
 
Nimekuwa kwenye msafara wa ziara ya mh.rais kanda ya ziwa,ziara ambaya imemalizika jana na leo rais anarejea jijini dar.
Katika ziara hiyo tumeshuhudia mambo mengi yaliyofanywa na rais lkn mimi nimeibuka na moja kuwa RAIS WETU KIKWETE anaipenda Chadema.Dalili zipo nyingi nitataja chache🙁1) Mkuu wa mkoa Ndikiro alimnyima Wenje(CDM) nafasi ya kuwasalimia wananchi wake wa nyamagana lkn JK alimsimamisha naye Wenje akiwa jukwaa kuu alisalimia waliokuwepo kwa salaam ya makamanda nao wakajb(na jk akiwemo)poweeeeer...(2)JK alitumia muda mwingi kuwasifu HIGHNESS na WENJE (wote wa CDM)kwa jitihada zao kuwaletea maendeleo wapiga kura wao.Kwa sbb hizo na nyinginezo nyingi nashawishika kuamini JK YUPO CCM KIMWILI lkn ROHO YAKE IPO CHADEMA.Wapi Ritz,Zemacopolo,Lizaboni na buk 7 wote? njoo huku haraka nafasi zimebaki chache.
Jk ni pragmatic; anajua wanacdm wana agenda ya maendeleo ya wananchi na wanaccm wana agenda ya maendeleo yao binafsi. kama rais mzuri yuko tayari kufanya kazi na cdm kwa roho nyeupe.
 
kikwete ni mchapakazi sana, sema uungwana wake ndio unaotafsiriwa na baadhi ya watu kama ni udhaifu
 
JK ni rais wa tanzania na alifanya ziara mwanza akiwa rais na sio mwenyekiti wa CCM. Hivyo basi akiwa rais, yeye ni wa wote hivyo alichokifanya Mwanza sio kuwa anaipenda Chadema bali anaikubali siasa ya vyama vingi na kuwa hata kule ambako inatawala chadema pia ni kwake kama Rais.
 
Pia ieleweke kuwa Rais alimruhusu Wenje asalimie wananchi ili kupembua ukweli wa yale aliyokuwa ameambiwa na viongozi wa chama na serikali akiwemo mkuu wa mkoa wa mwanza kuwa CCM watanyakuwa majimbo yote ya mwanza katika uchaguzi ujao wa 2015. Hivyo basi kama Wenje angezomewa hoja yao ingepokelewa lakini kwa kuwa alishangiliwa, tayari ni meseji sent kwa rais kuwa CCM haina chake mwanza na viongozi wa chama na serikali wa Mwanza tayari wameumbuka na nina imani Rais atakuwa amewahoji ni kwa nini wamemdanganya?????????? inasemekana mwenyekiti wa CCM mkweli kanda ya ziwa ni mheshimiwa MSUKUMA tu.
 
Kweli bora kufilisika mali maana ipo siku utapata kuliko kufilisika mawazo na mtazamo xaxa we ndugu yangu umefilisika mawazo na mtazamo pole xana
 
Hilo halina ubishi. Mimi siyo shabiki wa JK wala CCM lakini kwenye uungwana,nakubali kwa 100%. Na siyo uungwana tu bali hata hekima pia, na ndiyo maana atamaliza kipindi chake bila rabsha kubwa. Anapigana vita ngumu, anapigwa vita na madikteta ndani ya CCM, na huku nje anasakamwa na wapinzani na baadhi ya wananchi pia. Muda mwingi badala ya kuwaza juu ya maendeleo ya nchi kwanza inabidi utumie muda wake kuvishinda vita vya ndani ya chama.

Nafarijika kuona vijana mkiwa wakweli.
 
Thubutu, Huyo hakutaka embarrassment, hivyo alikifanya wanachokitaka wananchi ili na yeye apate temporary acceptance.
 
Nimekuwa kwenye msafara wa ziara ya mh.rais kanda ya ziwa,ziara ambaya imemalizika jana na leo rais anarejea jijini dar.
Katika ziara hiyo tumeshuhudia mambo mengi yaliyofanywa na rais lkn mimi nimeibuka na moja kuwa RAIS WETU KIKWETE anaipenda Chadema.Dalili zipo nyingi nitataja chache🙁1) Mkuu wa mkoa Ndikiro alimnyima Wenje(CDM) nafasi ya kuwasalimia wananchi wake wa nyamagana lkn JK alimsimamisha naye Wenje akiwa jukwaa kuu alisalimia waliokuwepo kwa salaam ya makamanda nao wakajb(na jk akiwemo)poweeeeer...(2)JK alitumia muda mwingi kuwasifu HIGHNESS na WENJE (wote wa CDM)kwa jitihada zao kuwaletea maendeleo wapiga kura wao.Kwa sbb hizo na nyinginezo nyingi nashawishika kuamini JK YUPO CCM KIMWILI lkn ROHO YAKE IPO CHADEMA.Wapi Ritz,Zemacopolo,Lizaboni na buk 7 wote? njoo huku haraka nafasi zimebaki chache.
Ikiwa hivyo basi Chadema itakosa mvuto. Jamani anatafuta pa kudondokea huyo baada ya kuona CCM mambo si shwari tena. CDM haiwezi kuwa na watu wa design ya Kikwete
 
Watanzania tukiwa wakweli nchi yetu tutaipeleka mbele. Vijana tufanye siasa safi japo tunavyama vyetu. Kwenye maslahi ya taifa tuonyeshe utanzania wetu. Kikwete ni rais wa mfano katika historia ya taifa letu.
 
Ulishasikia Dr Slaa kazomewa?????
Khaa!! hakuna atakaye mzomea kwa sababu hajafanya kitu kwao na hawamdai kitu. WanaCDM tu ndiyo wenye haki ya kumzomea kwa sababu ana mamlaka juu yao :whistle:
 
JK ni rais wa tanzania na alifanya ziara mwanza akiwa rais na sio mwenyekiti wa CCM. Hivyo basi akiwa rais, yeye ni wa wote hivyo alichokifanya Mwanza sio kuwa anaipenda Chadema bali anaikubali siasa ya vyama vingi na kuwa hata kule ambako inatawala chadema pia ni kwake kama Rais.

Jakaya ni Kama Nyerere, wote hawajawahi kupenda siasa za vyama vingi, Jakaya angekuwa anaushawishi kama wa nyerere nisingeshangaa kama asingevifutilia mbali.
 
Khaa!! hakuna atakaye mzomea kwa sababu hajafanya kitu kwao na hawamdai kitu. WanaCDM tu ndiyo wenye haki ya kumzomea kwa sababu ana mamlaka juu yao :whistle:

na wale wanaomzomea Kinana anamamlaka gani juu yao?
 
kikwete ni mchapakazi sana, sema uungwana wake ndio unaotafsiriwa na baadhi ya watu kama ni udhaifu

Hana uungwana wowote, angekuwa muungwana angeachia Matokeo ya Uchaguzi 2010 yatangazwe kama yalivyokuwa kwenye vituo cha uchaguzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom