Rais huyu kiboko. Mweeeeeh

Msharika

JF-Expert Member
May 15, 2009
947
69



Rais Jakaya Kikwete akijiandaa kumzawadia fedha, mtoto Liano Adamu (7) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ruaha Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro baada ya kuvutiwa na uchezaji wake wa ngoma ya Lizombe ya kabila la Wangoni. Rais yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu. Nyuma ya Rais ni Mkuu wa Mkoa, Joel Bendera. (Picha na John Nditi).

RAIS AKITOA MSHIKO BAADA YA MTOTO KUKATA MAUNO KWENYE NGOMA. SWALI LANGU, HUYU MTOTO KWA UMRI WAKE ANAHITAJI FEDHA AU ELIMU BORA?
 
Anahitaji kila kitu, fedha na elimu bora. Kwahiyo sioni tatizo lolote kwa JK kumpa zawadi ila nina wasiwasi na uwezo wako wa kufikiri
 
Hahahahah JK bwana kwa nini asiseme nakupeleka Bagamoyo ukasome chuo cha ngoma lakini pia next to that nitakulipia Elimu y msingi ?
 

Ingependeza kumwachia mkuu wa mkoa taarifa kuwa akiludi ikulu Dar amuone mtoto huyo ikulu,na yeye Presidar akifika ikulu pia awaite mkuu wa chuo cha utamaduni na tajiri mmoja muadilifu awakabidhi mtoto huyo kuwa asomeshe na kuendelezwa kipaji chake hicho cha ngoma za jadi anawakabidhi watu hao jukumu la mtoto huyo kufikishwa kwenye ndoto ya kuwa mwendeleza jadi ya Tanzania lakini mwenye elimu tena elimu kwa nguvu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Anakuwa akiwa na bonge la uzalendo kuwa alitayarishwa kuwa Mwananchi mwenye uzalendo kulinda utamaduni wa Taifa kwa lungu la matakwa ya Rais.
 

mi chichemi, kwetu ntwara bha ngoma na chamak nchanga tunapenda kwel!
 
hapana tatizo hapo JK ana mmotivate mtoto ili apende zaidi utamaduni wa Kitanzania siyo kama wanao iga tamaduni /ngoma za nje na kudharau za kwao
 

Hicho ndicho alichoweza kufikiri haraka haraka.
 
Wahehe huwa tunasema "uluhala kumtwe" yaani akili kichwani tu, sasa jamaa yetu kichwani kweupe ndo maana anapenda sana degree za kupewa, ndo maana hata yeye anajitahidi kugawa hela akidhani ndo anatatua matatizo ya wananchi baadala ya kuwapa miundo mbinu ya kuwapeleka kwenye upeo wa mbali zaidi.
 
Leo kapiga picha na Njohole yule alokuwa mchezaji wa simba, kule mbingu
 

Hilo lilikuwa tukio ambalo hakupanga halikuwa k wenye ratiba zake ghafla akajipapaa musofe.
We acha tu rais wetu akili zinafanya kaz fasta hata akistukizwa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…