Rais hajui kuzungumza na wananchi, ziara za njiani zisitishwe

wewe ulishaacha kula rushwa toka lini?
Rais wenu naye ni mla rushwa, maana rafiki zake wote ni wala rushwa na Mafisadi,tokea ashike madaraka hajawai kukemea wala rushwa, uzembe na ufasadi.Ndio maana rushwa, uzembe na ufisadi vimerudi kwa mwendo wa 5g
 
Una roho mbaya sana na hii inaonesha uafrika ni ushetani. We unafurahia mtu kutumbuliwa. Yaani jpm alivyokuwa sheitwani basi riho ile aliwaambukiza na wewe na smai unataka aige ushetani huo, never!!

Umepaniki sana utafikiri uyo mama ni ndugu yako, kama kiongozi hafanyi kazi yake atumbuliwe apewe mwingine anayeweza sio wanakula kodi za wananchi bure
 
Naongea ukweli kutoka moyoni CCM mtanisamehe, Rais wetu hajui kuzungumza na raia barabarani, ni vyema ziara ya njiani zikanseliwe.

Rais hatatui changamoto unasimama njiani unaanza kuwaambia kurekodi filamu na tozo hiyo haisadii, wala sisi hatukusimamishi ili utwambie mambo ya filamu, sisi tunakusimamisha kukueleza kero na shida zetu tulizonazo eneo husika.

Ukisimama njiani tafadhali uliza wananchi wa pale wana shida gani, muite mkuu wa mkoa aeleze ataitatua lini au kwanini kashindwa kuitatua hilo ndio lengo la wananchi kusimama njiani,

Wananchi wanachangamoto sugu ambazo wakuu wa mikoa hawajawai kufanyia ziara, masoko yana shida, ushuru usio na tija, Rais simama omba hata Raia mmoja aelezee matatizo ya pale, muite mkuu wa mkoa umuhoji, Mweshmiwa Rais labda kwa taarifa tu ni kwamba hao wakuu wa mikoa hawafanyagi ziara wananchi hawajui wapate wapi msaada.

Nimeona leo hata pale Kwenye maonyesho wamekuomba ujenzi wa lami ya kilomita moja toka uwanjani hadi makumbusho ya bujora lakini hukuwajibu kitu.

siku nyingine tutakua hatuji maana kero zetu wakuu wa wilaya zimewashinda, mkuu wa mkoa kashindwa hata wewe Rais tunayekutegemea husemi chochote si bora vyavziara uviache tu tujikalie majumbani kwetu,

Naomba ziara za njiani zife ni kupotezea muda wananchi tu

Kama haiwezekani kusikiliza kero za wananchi eneo husika usiwe unasimama barabarani, kuumishana njaa tu
Hahahaha mwamba kweli imekugusa hii mpaka umeandikia uzi
 
Huwa naona aibu, hana mvuto kabisa wala ushawishi...JPM kamzidi kwa mbali kabisa
 
Naongea ukweli kutoka moyoni CCM mtanisamehe, Rais wetu hajui kuzungumza na raia barabarani, ni vyema ziara ya njiani zikanseliwe.

Rais hatatui changamoto unasimama njiani unaanza kuwaambia kurekodi filamu na tozo hiyo haisadii, wala sisi hatukusimamishi ili utwambie mambo ya filamu, sisi tunakusimamisha kukueleza kero na shida zetu tulizonazo eneo husika.

Ukisimama njiani tafadhali uliza wananchi wa pale wana shida gani, muite mkuu wa mkoa aeleze ataitatua lini au kwanini kashindwa kuitatua hilo ndio lengo la wananchi kusimama njiani,

Wananchi wanachangamoto sugu ambazo wakuu wa mikoa hawajawai kufanyia ziara, masoko yana shida, ushuru usio na tija, Rais simama omba hata Raia mmoja aelezee matatizo ya pale, muite mkuu wa mkoa umuhoji, Mweshmiwa Rais labda kwa taarifa tu ni kwamba hao wakuu wa mikoa hawafanyagi ziara wananchi hawajui wapate wapi msaada.

Nimeona leo hata pale Kwenye maonyesho wamekuomba ujenzi wa lami ya kilomita moja toka uwanjani hadi makumbusho ya bujora lakini hukuwajibu kitu.

siku nyingine tutakua hatuji maana kero zetu wakuu wa wilaya zimewashinda, mkuu wa mkoa kashindwa hata wewe Rais tunayekutegemea husemi chochote si bora vyavziara uviache tu tujikalie majumbani kwetu,

Naomba ziara za njiani zife ni kupotezea muda wananchi tu

Kama haiwezekani kusikiliza kero za wananchi eneo husika usiwe unasimama barabarani, kuumishana njaa tu
Unamkandia FaizaFoxy wewe? Huna adabu.
 
Kero za wananchi hazitakiwi kufika kwa rais moja kwa moja kuna utaratibu wake , ndio maanabkuna madiwani na wabunge, wakuu wa wilaya na mikoa nk. na hii ni ili kuepusha maamuzi ya ukandamizaji na unyanyasaji yasiyo na utu, maana maamuzi na kauli ya rais kwa mtu yeyote yule sio jambo la mchezo ,

wananchi wengi wamejawa na majungu na chuki dhidi ya watumishi wa umma na hilo halina pingamizi hicho ndicho alicho kuwa anakifanya magufuli na wafuasi wake, hatutaki mfumo ule ujirudie! Kero za wananchi zitatatuliwa kwa utaratibu unao takiwa na sio majukwaani kutukana wasaidizi na watendani wa chini mbele ya jamii inayo shangilia na kupiga miluzi ya furaha na kutaka sifa , watu wameumizwa sana wakati wa magufuli tena wengine bila hatia,watu wamedhalilishwa na kutwezwa utu wao, watu wamevunjiwa heshima mbele ya wanao waongoza na familia zao eti kisa tu mwananchi tabulalasa asiye jua utaratibu kalalamika jambo ambalo ni la kitaalamu na sio nguvu au siasa.

Rudini kwenye mifumo ya uongozi na sio mifumo ya utawala na mzilazimishe akili na fahamu zenu zitambue kwamba mnatakiwa kuongozwa na sio kutawaliwa
Wewe hata huelewi mambo huko maofisini saizi ni hovyo hovyo! Hujasikia mpaka daktari amnafumua nyuzi za mgonjwa kisa kakosa pesa! Uliza watu wa bandari pia fatilia kama kuna mfanya biashara anatoa risiti kwa ukamirifu! Umebaki kubweka tu! Hakuna nchi inaendeshwa kishikaji huu ujinga upo nchi zetu weusi tu!
 
We kweli kilaza, mkishaongea changamoto zenu huwa zinaandikwa na wasaidizi wa Rais, then zitafanyiwa kazi, tatizo mshazoea yule mwendazake aliekuwa anagawa maburungutu ya hela njiani, mama mtoto wa mjini sio limbukeni wakugawa fedha ovyohovyo
Kisa ni msukuma ndo sio wa mjini utoto wa mjini ndo nini? Mara nyingi watoto wa mjini ndo watu wapumbavu na wasiojielewa kazi kutafuta mteremko na ujuaji mwingi! Hata hapa Dar angali watu wengi wenye mafanikio ni watu wakuja wao wa mjini wengi wao ujinga ujinga tu!
 
Rais Kuzungumza na wananchi Mara kwa Mara kunaongeza uwajibikaji kwa watendaji wa chini
Hamasa ya watendaji wa chini maDC, maRC havikuja kwa bahati mbaya
Rais ukipoa na watendaji wako wanapoa
Hakujiandaa kuwa Ràis hivyo msimlaumu vumilieni tu
 
Waziri Mkuu ndiyo mtendaji mkuu wa Serikali, na yeye akifika sehemu fulani huwa tayari analo jambo lake. Hii ni tafauti na Raisi kusimama njiani tu na kuanza kutoa hukumu. Matukio kama haya mara nyingi yanaleta kudanganywa.
sawa ila mama simuelewi kabisa, bora aendelee kushoot movie yake tu, awaache watu waparuane mtaani mwisho atakuta ikulu wamemsaidia kukaa
 
Una roho mbaya sana na hii inaonesha uafrika ni ushetani. We unafurahia mtu kutumbuliwa. Yaani jpm alivyokuwa sheitwani basi riho ile aliwaambukiza na wewe na smai unataka aige ushetani huo, never!!
Mtu kama hawajibiki ni sahihi kabisa kutumbuliwa, there is no other way out, wala hakuna usheitwani hapo, kama huwezi kufanya kazi ni bora uwaachie wanaoweza kuifanya hiyo kazi,
 
Back
Top Bottom