econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 15,804
- 21,777
Nimefuatilia hicho kinachoitwa ziara za rais huko mkoani mtwara. Kuanzia Jana mkutano wa Mtwara mjini na Leo Tandahimba. Nilichogundua, hizi sio ziara za kazi Bali ni kampeni za uchaguzi.
Sababu zangu ni zifuatazo:
1. Sababu ya kwanza, Kila anayesimama anampigia debe Rais kana kwamba ni mkutano wa kampeni. Mara Rais kaleta maji , umeme, kajenga barabara, mara royal tour nk. Kama Leo kwenye mkutano wa Tandahimba Kuna kiongozi mmoja kadai kuwa Rais Samiah ndio Rais wa kwanza tangu uhuru kuleta maendeleo Mkoa wa Mtwara. Nadhani haya yalitakiwa yasemwe 2025 wakati wa kampeni. Kuelezea Yale mafanikio ya Rais na kwanini achaguliwe Tena.
2. Jambo la pili, Wasemaji kugusia uchaguzi wa 2025. Nimeshangaa Viongozi waliopewa nafasi kudai 2025 kwenye uchaguzi mkuu Dr Samiah Hana mpinzani. Kwa mfano kwenye mkutano wa Leo hapo Tandahimba mbunge kadai, ya kwamba uchaguzi wa 2025 watamshindilia kura nyingi za urais Mh Samiah.
3. Jambo la tatu, Mikutano kujaa sare za CCM. Nadhani sio sahihi kufanya mkutano wa ziara ya Rais kuonekana katika mrengo wa kichama. Yani walioenda pale ni wanachama wa mapinduzi na hivyo kuujenga picha ya mkutano wa CCM. Kwa mfano alipoongea yule mbunge Tunza Malapa, wengi walidhani ni CCM, wakawa wanampigia makofi, ila alipomaliza kuongea na yule MC kumtaja Kama mbunge wa vitu maalum CHADEMA, umati karibia wote ulipigwa na butwaa maana hawakutegemea mbunge wa chama kingine awe pale. Kisaikilojia walijua ni mkutano wa CCM pekee yao.
4. Jambo la nne, wasanii wanaotumbuiza wote ni Kama wanamuimba Mh Samiah. Yani kila msanii akiimba lazima apayuke Samiah oyeeh!. Hii inaleta picha ya kampeni na kumjenga Mh Samiah kuliko kuwa ziara ya kazi.
5. Jambo la mwisho, mabango, t-shirt nk Zina picha ya Samiah na maneno ya kuashiria kampeni. Hii siyo sahihi kabisa.
Kwa ushauri hizi ziara ziwe za kikazi, Rais aondokane na haya makampeni. Afike kwa wananchi aulize shida zao na Kama wahusika wapo wajibu tuhuma zao.
Sababu zangu ni zifuatazo:
1. Sababu ya kwanza, Kila anayesimama anampigia debe Rais kana kwamba ni mkutano wa kampeni. Mara Rais kaleta maji , umeme, kajenga barabara, mara royal tour nk. Kama Leo kwenye mkutano wa Tandahimba Kuna kiongozi mmoja kadai kuwa Rais Samiah ndio Rais wa kwanza tangu uhuru kuleta maendeleo Mkoa wa Mtwara. Nadhani haya yalitakiwa yasemwe 2025 wakati wa kampeni. Kuelezea Yale mafanikio ya Rais na kwanini achaguliwe Tena.
2. Jambo la pili, Wasemaji kugusia uchaguzi wa 2025. Nimeshangaa Viongozi waliopewa nafasi kudai 2025 kwenye uchaguzi mkuu Dr Samiah Hana mpinzani. Kwa mfano kwenye mkutano wa Leo hapo Tandahimba mbunge kadai, ya kwamba uchaguzi wa 2025 watamshindilia kura nyingi za urais Mh Samiah.
3. Jambo la tatu, Mikutano kujaa sare za CCM. Nadhani sio sahihi kufanya mkutano wa ziara ya Rais kuonekana katika mrengo wa kichama. Yani walioenda pale ni wanachama wa mapinduzi na hivyo kuujenga picha ya mkutano wa CCM. Kwa mfano alipoongea yule mbunge Tunza Malapa, wengi walidhani ni CCM, wakawa wanampigia makofi, ila alipomaliza kuongea na yule MC kumtaja Kama mbunge wa vitu maalum CHADEMA, umati karibia wote ulipigwa na butwaa maana hawakutegemea mbunge wa chama kingine awe pale. Kisaikilojia walijua ni mkutano wa CCM pekee yao.
4. Jambo la nne, wasanii wanaotumbuiza wote ni Kama wanamuimba Mh Samiah. Yani kila msanii akiimba lazima apayuke Samiah oyeeh!. Hii inaleta picha ya kampeni na kumjenga Mh Samiah kuliko kuwa ziara ya kazi.
5. Jambo la mwisho, mabango, t-shirt nk Zina picha ya Samiah na maneno ya kuashiria kampeni. Hii siyo sahihi kabisa.
Kwa ushauri hizi ziara ziwe za kikazi, Rais aondokane na haya makampeni. Afike kwa wananchi aulize shida zao na Kama wahusika wapo wajibu tuhuma zao.