Wanabodi.
7. Umasikini uliotopea, ambao pia pia unakwenda sambamba na ujinga. Mtu masikini wa kipato, chakula cha shida, mlo mmoja kwa siku, anaishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, akili yake pia inadumaa. Mtu kama huyu shida yake ni mlo, na mavazi, sasa akiletewa ile Tshirt na kofia, na pilau ya siku moja, inatosha kabisa kukichagua chama kilichokulisha na kukuvisha, anakuwa hana uwezo kusikiliza sera na kufanya informed decisions, angalieni maeneo yenye umasikini uliotopea na elimu duni ndio strong holds za CCM. Mikoa yenye ehueni kiuchumi kama Arusha, Kilimanjaro, Bukoba, Iringa, Mbeya. Tanga na maeneo ya mijini, watu walioelimika, kidogo wanaweza kuchagua upinzani, lakini mikoa yenye umasikini wa kutupa kama Dodoma, etc, usitegemee upinzani unaweza kushinda!, shida ya masikini ni njaa tuu, CCM ndicho chama kinachoongoza kwa kugawa rushwa, ushahidi wa kazi nzuri iliyofanywa na fedha za Kagoda upo!. Hivyo CCM kuutumia umasikini wa Watanzania na Ujinga wa Watanzania kama mtaji wake wa Ushindi.
Wasalaam
Paskali