sidhani kama nimesema kuna umimi; CDM ndicho chama pekee sasa hivi kinachoweza kujipanga na kuchukua madaraka ya nchi. Kumbuka kina mtaji mkubwa sana wa mapenzi ya watu wengi. Wapo watu wengi ambao wamejitolea na wanaendelea kujitolea hali na mali kukijenga. Lakini hili peke yake la kupendwa halitoshi kufanya wawe wanastahili. Fikiria hapa ninachokisema vizuri.
Mzee Mwanakijiji, unasomeka kama hutaki kueleweka, umetuambia kuwa ulimkubali jk kwa kuwa alikuwa anakubalika miongoni mwa watanzania wengi isipokuwa mimi, nakugundua kuwa hukuwa unajua kwa makusudi kuwa huyo uliyemkubali alikuwa anapewa ridhaa kuongoza nchi kupitia genge lenye sura mbili, sura ya kwanza ya genge hili ccm imejifutika kiupole sana kwenye "ridhaa" ya wananchi kanakwamba inakubalika, na sura ya pili ipo kwenye mali,
inasomeka wazi kuwa tafsiri ya ccm, kupewa "ridhaa" ni kumilikishwa mali za tanzania, na afikiriye kinyume ni mkosefu anastahili kulipuliwa kwa bomu, Tukatae hili.
Imefaa kuwakubali cdm angalau kwa sasa kwa kuwa wanajipambanua na kutuhimiza kukataa kuonewa, kukataa kunyonywa na mnyonyaji yeyote, kukataa kudharauliwa na mtu yeyote, kukataa kupuuzwa na mpuuzi yeyote, kukataa kuibiwa na mwizi yeyote.
tuikate ccm kwa sababu inatuhimiza kuwapuuza wengine isipokuwa yenyewe inayotupuuza, ukitengeneza kanuni kuuhusu upuuzi, unakuta cdm ni wazuri kuzidi ya ccm kwani inatuhimiza kumkataa yeyote miongoni mwa wapuuzi, kwa sasa ccm ndiyo wapuuzi, na ikitokea cdm nao wakawa wapuuzi tuwakatae!
Tunahitaji kuwa wamoja zaidi kuliko wakati mwingine wowote wa historia ya nchi yetu kwani adui yetu wa sasa yupo miongoni mwetu.