Mie sidhani kama kabadilika sana. nakumbuka katikakati mwaka 2010 wakati suala la CCJ linapamba moto humu JF alionekana kuiponda sana CDM na kuiunga mkono CCJ na kuna thread moja kama atakumbuka, niliweka post kwa kusema something like "There is more in MMK and CCJ than what meets the eye' -- yaani "Kuna zaidi ndani ya MMK na CCJ kuliko inavyoonekana kwa macho."
Mnajua alivyonijibu? Aliandika something like "You appear to be smart person in this issue." Yaani "Unaonekana kuwa mjanja sana katika ishu hii."
Nina hakika nilimgusa mahala fulani -- hasa kuhusika kwake katika mradi wa CCJ, ambao wengi tunaamini ulikuwa ni mradi wa CCM kuidhoofisha CDM, hasa pale awali.
Lakini nachompendea MMK ni kwamba huwa hafichi sana undani wape hasa unapom-corner kwa hoja madhubuti.
Nawasilisha.