Edson
JF-Expert Member
- Mar 7, 2009
- 10,016
- 5,824
Ukweli husemwa:
Mkuu, hayo maneno kwenye red yana maana gani au ulikuwa una maana ya cartography na stenography.
jaribu kuya google hayo ya kwangu kama yalivyo...kisha ya kwako......usichanganye
Ukweli husemwa:
Mkuu, hayo maneno kwenye red yana maana gani au ulikuwa una maana ya cartography na stenography.
jaribu kuya google hayo ya kwangu kama yalivyo...kisha ya kwako......usichanganye
Wakuu, binafsi nilikuwa shabiki wa huyu mkongwe wa JF. Nikagundua kwamba MMK amechanganya fani mbili tofauti na hivyo kujichanganya na kuchanganya wasomaji wa posts/makalazake. Nikaacha kufuatilia na kusoma anachokiandika.
MMK amechanganya SIASA na UANDISHI wa habari.........
sidhani kama nimesema kuna umimi; CDM ndicho chama pekee sasa hivi kinachoweza kujipanga na kuchukua madaraka ya nchi. Kumbuka kina mtaji mkubwa sana wa mapenzi ya watu wengi. Wapo watu wengi ambao wamejitolea na wanaendelea kujitolea hali na mali kukijenga. Lakini hili peke yake la kupendwa halitoshi kufanya wawe wanastahili. Fikiria hapa ninachokisema vizuri.
Umesema kipimo cha kushindwa kwa mwenyekiti wa chadema ni 2010.Kukweli mwaka huo,chadema walikuwa na matumaini makubwa,na hata waliamini kwamba uchaguzi ulichakachuliwa.Mzee Mwanakijiji said:Kilichobadilika zaidi ni kuwa ninaelewa zaidi kuwa wanasiasa wanataka mabadaraka zaidi kwa ajili ya madaraka. Ni kama Kikwete alivyoutaka Urais kwa ajili ya Urais. Mbowe bado hajaonesha uongozi na kipimo cha kushindwa kwake kilionekana 2010; viongozi wengine ndani ya CDM nao wanapata shida ya kuonesha uongozi na badala yake kuelekea 2015 CDM inaweza kwenda ikiwa imegawanyika kuliko CCM!
Wanaofikiri kuwa ati itakuja kujipanga baadaye wanajidanganya. CDM ilitakiwa iwe imeshajipanga sasa hivi kuelekea uchaguzi wa 2014 na ule wa 2015. Badala yake mwaka huu tumeshuhudia malumbano ya ajabu sana na visa vya ajabu vikitokea. Utagundua kuwa sijawahi kwa mwaka huu kutoa maoni yangu kuhusu hili kabisa na labda nitalitolea maoni lakini naendelea kukata tamaa na inakatisha tamaa! Nilisema wakati wa uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki ningekuwa na uwezo ningewatia bakora viongozi wa CDM na nilimaanisha! Na nilisema wangepoteza Arumeru Mashariki Mbowe na uongozi wote wa juu wangetakiwa kujiuzulu; na hata sasa labda kesi inaweza kujengwa ya kwanini wajiuzulu mapema zaidi (bado sijamaliza kuijenga hii hoja, inshallah).
Bado siamini kuwa CDM ilivyo sasa iko tayari kushika hatamu za uongozi wa taifa letu. Ndio maana utaona kuwa mimi pia siyo muumini wa "tuiondoe kwanza CCM halafu tutajua mbele ya safari". Siamini katika kuiondoa CCM ili tuingize chama kingine alimradi turidhike kuwa tumeiondoa CCM. Ninaamini yatupasa tuiondoe CCM kwa sababu kuna chama kingine kina sera na dira nzuri kwa taifa; kina viongozi wenye busara, na kinasimamia kanuni za msingi zilizojenga taifa letu.
Wanaofikiri kuwa ati itakuja kujipanga baadaye wanajidanganya. CDM ilitakiwa iwe imeshajipanga sasa hivi kuelekea uchaguzi wa 2014 na ule wa 2015.
Unaposema "vision concerning key areas ya utawala" una maana gani?Unaweza kufafanua zaidi ili tukuelewe specifically kile unachomaanisha?Vision ya chama haiwezi kua kuondoa chama tawala madarakani. That is merely a consequence of the take over. What is the vision of CDM concerning key areas ya utawala? I believe that is what Mzee Mwanakijiji meant: Sio CDM ishinde ili [tu] CCM itoke madarakani.
Mkuu MMM,
Hoja yako kuu ni kuwa CDM haijajipanga, hujaelezea kuhusu M4C inayoendelea kama sehemu ya kujipanga! Pia unalalamikia migawanyko iliyopo CDM huku ukisahau kuwa CCM ni chanzo kikuu cha migawanyiko kwenye vyama vya upinzani! Nakuona kama mtu wa kukata tamaa haraka sana japokuwa unataka kujiaminisha kuwa "hushabikii matukio" bali fikra! Ukisoma between the lines kwenye hoja zako zimejaa matukio zaidi kuliko kile unachokiita fikra, ndio maana umeanza na kabla ya uchaguzi na baada ya hapo, huku ukionesha kuchanganyikiwa kuwa ubaki CCM au CDM! Sijui kama wewe ni mtu wa msimamo kama ulivyofanikiwa kuwaaminisha wengi! Mada yako kwa ufupi imenishangza sana, unatumiwa na CCM kama ilivyo kwa akina Zitto Kabwe, usitudanganye, huwezi kuwatumikia mabwana wawili (CCM vs CDM)!
Lakini tena kipimo chako wakati wa JK kilikuwa hicho hapo chini...Mzee Mwanakijiji said:Sivutwi na hotuba hewa, au na mivuto ya umaarufu wa watu. Sipimi watu kwa kuangalia nani anaungwa mkono zaidi au nani haungwi mkono. Ninapima watu kwa fikra zao na mambo wanayoyasimamia lakini kwa jinsi gani wanaongozwa na kanuni (principle oriented) kuliko wanaoongozwa na matukio (events-oriented). Watu wanaoongozwa na matukio huitikia matukio yanapotokea; wanaoongozwa na fikra huitikia hata wakati kuko kimya!
Na. M. M. Mwanakijiji
Mzee Mwanakijiji said:"Kikwete alipopitishwa na kuwa mgombea wa Urais mimi nilikuwa miongoni mwa watu ambao tulimuunga mkono kwa sababu mbalimbali. Ya kwangu ilikuwa ni sababu ya kisiasa zaidi. Kwamba, alionekana kupendwa na kukubaliwa na wananchi wengi sana."
sidhani kama nimesema kuna umimi; CDM ndicho chama pekee sasa hivi kinachoweza kujipanga na kuchukua madaraka ya nchi. Kumbuka kina mtaji mkubwa sana wa mapenzi ya watu wengi. Wapo watu wengi ambao wamejitolea na wanaendelea kujitolea hali na mali kukijenga. Lakini hili peke yake la kupendwa halitoshi kufanya wawe wanastahili. Fikiria hapa ninachokisema vizuri.
CDM haiwezi uliza watu wenye loosing spirit chochote.kama wote hapa hamkuweza ona ilipoanzia CDM na vikwazo vilivyorukwa, ni vipi mnaweza elewa vision ya waanzilishi wa chama?Ni kama mazaramo anayefikiria kwenda mcheza ngoma binti yake akitaka mshauri mchaga kuhusu shule na biashara.Vision ya chama haiwezi kua kuondoa chama tawala madarakani. That is merely a consequence of the take over. What is the vision of CDM concerning key areas ya utawala? I believe that is what Mzee Mwanakijiji meant: Sio CDM ishinde ili [tu] CCM itoke madarakani.
Watu wengi sana wamebadilika baada ya kuifahamu "kweli" na "kweli" imewaweka huru. MMM ni mmoja wapo!