Profile la kijana mkataa ndoa

Profile la kijana mkataa ndoa

Naomba profile ya wanawake wanaokataa ndoa....

Screenshot_20230221-161557.jpg
 
Kumtuhumu mwanaume ambaye ni rijali kuwa ni shoga kwa sababu ya view zake kuhusu chqngamoto za ndoa ni kujilisha upepo tu.

Mimi naona vijana wana hoja na jamii inayokubali hoja haitaki kuwssikiliza ili kuzikabili hizo changamoto badala yake jamii inalazimisha ndoa hata kama mfumo wake ni mbovu.

Hizi ndoa za siku hizi ni tofauti na mpango wa Mungu. Ndoa hamilikowi na kanisa au msikiti. Ndoa ni taasisi inayojitegemea..... inapaswa kujafiliana badala ya kutishana na kudhalilishana

Ndoa ya Mungu Mwanamke alikuwa msaidizi WA mwanaume, ndoa za kishetani zinazoendelea humu Duniani, Mwanamke anakuwa mnyonyaji WA wanaume. Lihudumiwe kila kitu kama maiti.
Na hapo hapo lifanye umalaya ulisamehe.
Hiyo ndoa au upuuzi
 
furaha ya kunyonyana?
Vijana waendelee kukataa makupe kama ninyi, mnaingia ndoani kutafuta Ajira ya kulishwa na kuvishwa kama mifugo.

Wanawake wenye Akili hawahudumiwi, Ila wanafanya Maisha pamoja na waume zao. Ni wasaidizi wa waume zao sio wanyonyaji. Kwa kisingizio cha MKE SIJUI UPUUZI GANI.

Ukahaba ndio unaita Ndoa,
Yaani bila Pesa hakuna ndoa, bila Mahari hakuna Ndoa. Huoni hiyo ni biashara?
Wewe tafuta hiyo misukule mliozoea kuitumikisha iwahudumie.

Sisi tunaoa Wake Bora, wenye ubepari. Ili ule lazima ufanye kazi
W

Eti wanyonyaji kwa hio kumuhudumia mkeo ni unyonyaji??,Kumsaidia mume ndio asikuhudumie????hakuna mwanamke asiyependa kuhudumiwa Fact number moja,unless mkeo ni pretender,mmekutana mume ana views za ajabu ajabu mke anapretend hapendi kuhudumiwa,

Ningependa kujua huyo mkeo mlibebana hukutoa mahari au na wazazi wake nao ni mabepari???????
 
1. Ni vijana wadogo hawajafikisha 35 years old, infact majority wako 30's and under...

2.Financially insecured,ama washawahi kuwa na experience iliyowafanya wafeel vulnerable financially..

3.Wachoyo hata kwa mambo madogo kama sukari, LOL.

4. Most ni introverts wanao struggle ku form relationships,

5. Most ni wana ishu na mama zao, hii imewapelekea kutokuwa na healthy relationships hivyo kupelekea kuchukia zaidi wanawake.


Mnaopinga ndoa simply kuweni na faken life!...acheni upuuzi wa kuinfluence wengine negatively.
Pole una stress za kutokuolewa


Afu watu wamesema hawataki kuoa Sasa wewe unaumia nn😂😂

Nuna afu fanya Kama unajioa vile
 
Ndoa ya Mungu Mwanamke alikuwa msaidizi WA mwanaume, ndoa za kishetani zinazoendelea humu Duniani, Mwanamke anakuwa mnyonyaji WA wanaume. Lihudumiwe kila kitu kama maiti.
Na hapo hapo lifanye umalaya ulisamehe.
Hiyo ndoa au upuuzi
Kwa hio msaidizi mke alikua hauhudumiwi?????Shida yako ni kuhudumia??? kaazi kweli kweli...nilisema pale juu most mko financially insecured sijui kama ulinielewa???? mwanaume financially yuko njema sidhani kama ataona shida kumhudumia mke wake...
 
Eti wanyonyaji kwa hio kumuhudumia mkeo ni unyonyaji??,Kumsaidia mume ndio asikuhudumie????hakuna mwanamke asiyependa kuhudumiwa Fact number moja,unless mkeo ni pretender,mmekutana mume ana views za ajabu ajabu mke anapretend hapendi kuhudumiwa,

Ningependa kujua huyo mkeo mlibebana hukutoa mahari au na wazazi wake nao ni mabepari???????

Ndio maana nikakuambia ukishakuwa Kupe unafikiri kila MTU ni Kupe kama wewe.

Kama anapretend atajua mwenyewe, Ila hiyo ndio formation,
Wanawake wanaopenda kuhudumiwa tuu kama maiti au midoli huzaa jamii ya Watu Maskini na wajinga WAJINGA,

Elimu ndogo ya Ndoa hamna, ukahaba ndio mnaita Ndoa,
Ndoa inajengwa na mume na MKE. Wote lazima mzalishe Mali.
Hata amri za Mungu zinaeleza kuwa MTU la,ima afanye kazi, haijataja Mwanaume pekee ndio afanye kazi.

Kuoa Wanawake mwenye mawazo Kama yako ni kupoteza muelekeo wa Maisha. Ndio maana Vijana wakishaoa wengi wanakufa mapema Kwa ujingaujinga.

Soma Sifa ya MKE Mwema, sio hao makupe unaowazungumzia(ikiwemo wewe mwenye mtazamo,
Anza na hii
Mithali 31:
27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake;
Wala hali chakula cha uvivu.

Kisha maliza Hii yote
Mithali 31:

10Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?
Maana thamani yake yapita thamani ya marijani.
11Moyo wa mumewe humwamini,
Wala hatakosa kupata mapato.
12Humtendea mema wala si mabaya,
Siku zote za maisha yake.
13Hutafuta sufu na kitani;
Hufanya kazi yake kwa moyo wote.
14Afanana na merikebu za biashara;
Huleta chakula chake kutoka mbali.
15 Tena huamka, kabla usiku haujaisha;
Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;
Na wajakazi wake sehemu zao.
16Huangalia shamba, akalinunua;
Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
17Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;
Hutia mikono yake nguvu.
18Huona kama bidhaa yake ina faida;
Taa yake haizimiki usiku.
19Hutia mikono yake katika kusokota;
Na mikono yake huishika pia.
20Huwakunjulia maskini mikono yake;
Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.
21Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake;
Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.
22Hujifanyia mazulia ya urembo;
Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.
23 Mume wake hujulikana malangoni;
Aketipo pamoja na wazee wa nchi.
24Hufanya nguo za kitani na kuziuza;
Huwapa wafanya biashara mishipi.
25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake;
Anaucheka wakati ujao.
26Hufumbua kinywa chake kwa hekima,
Na sheria ya wema iko katika ulimi wake.
27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake;
Wala hali chakula cha uvivu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom