Hivi hapa tatizo ni kushindwa kuelewa Lugha au mna tatizo gani nyie wandugu? Wapi mtoa mada alikopotosha, Je Wajerumani hawakuweka Base yao katika eneo la Lugalo walipotaka kumshambulia Mkwawa katika hiyo miaka ya 1891 na Wajerumani kupata kipigo kikali? Ni wapi mtoa mada alikosema kitu tofauti?
Hebu someni tena alichoandika Mtoa mada, na kisha angalieni "references" zilizowekwa humu na
Punjab Singh,
Ritz, na
FaizaFoxy ili mjue kuwa ima ni weupe wa historia au mna uwezo mdogo wa kuelewa na kutafsir kilichoandikwa. Na huenda ndio ikawa sababu, pamoja na kujinasibu kwenu kuwa mmesoma, lakini mmekuwa vinara wa kuiingiza nchi katika "mikataba ya Giza"; kumbe mna upeo mdogo kutafsiri maandishi.
Gautama,
Kila siku akitufunza Maalim wetu
Sheikh Haruna akisema,"Ingia kwenye
mnakasha kwa nia ya kujifunza kutoka kwa mwenzako.''
Umetumia neno, "upuuzi."
Ikiwa ile taarifa wewe huna ilikuwa kumuomba mwenzako kwa adabu na
uungwana akufahamishe rejea.
Mkwawa alikuwa akipata silaha za kupigana na Wajerumani kutoka
kwa Waarabu.
Mkwawa alikuwa akiandika kwa herufi za Kiarabu na jina lake la Kiislam
ni
Abdullah na alikuwa na nduguye ambae alikuwa jemedari katikajeshi
lake jina lake lilikuwa
Yusuf.
Unajua kumekuwa na hofu kubwa sana ya historia ya Uislam kiasi kwa
miaka mingi imefanyika juhudi za makusudi kufuta historia hii.
Songea Mbano Chifu wa Wangoni aliyepambana na Wajerumani
katika Maji Maji jina lake khasa ni
Ali Songea Mbano.
Huyo alinyongwa na wenzake karibu 60 wote Waislam.
Lakini jina la "
Ali" alilopewa na baba yake halitajwi.
Kaburi lake lipo kwenye kumbukumbu ya Maji Maji Mahenge,
Songea atakae afike pale akaone khiyana iliyofanywa kubadilisha
historia hii.
Atakae anaweza kwenda Kalenga atakuta kila kitu pale kuhusu
Mkwawa hadi hizo barua alizokuwa akiandikiana na Waarabu.
Naogopa kusema kuwa katika ujana wetu nikifahamiana vyema na
marehemu
Chief Abdul Mkwawa, kitukuu cha
Mtwa Mkwawa.
Baba yangu pia akijuana na
Abdallah Ross mtoto wa dada yake
Chief Adam Sapi Mkwawa.
Huyu
Abdallah Ross baba yake alikuwa Muingereza.
Nafahamiana vyema tu na mtoto wa
Abdallah Ross ni umri wangu.
Katika mazungumzo ya kawaida sana kati ya wazee wetu hawa mimi
nikiwa mdogo niliokota mengi ambayo leo nikikumbuka nashangaa sana.
Mengine ndiyo haya nayaleta hapa majlis.
Hebu soma hapa chini:
"How many see today in the national museums in East Africa of
names of Omani liberators like
Muhammad bin Khalfan Al-Barwani,
popularly known as "Rumaliza" who put a bullet through a hole killing
a Germany soldier in Tanganyika who was wiping out Hehes?
Or
Bushir bin Salim Al-Harthi who was arrested and hanged in
Pangani because of the war he had unleashed against Germans in
order to drive them from Tanganyika?"
(Kwa kuwa hii ni kutoka kazi ya ambayo niafanyia tafasiri na
haijachapwa sitakupa citation).
Mjadala si ugomvi.
Jadili tu kwa utaratibu ili wasikizaji waone raha kila wakiona post
yako wajikwae kwa kuikimbilia kuisoma.
Ukitaka habari zaidi za
Mkwawa na Waarabu msome
Ali Muhsin
Barwani "Conflict and Harmony in Zanzibar."
Mimi nimekutana na kitukuu cha
Rumaliza, Sheikh Mohamed Said,
Dubai mwaka wa 1991.
Anazo habari nyingi za babu yake mkuu,
Rumaliza na tulizungumza
mengi.
https://www.jamiiforums.com/#_ednref1