Profesa kijana apewa Ubalozi

Profesa kijana apewa Ubalozi

Kuna dogo mmoja wa Francis Mponjoli Kifukwe alichukua Ph.D akiwa na miaka 26 kama sijakosea.

Sasa kama miaka 43 ni mtoto, huyo wa 26 aitwe vipi?
huyo ni Phd sio u professor lakini, mada ilikuwa ni proffesor mwenye umri mdogo
 
Acha ushamba. Prof ni cheo cha chuoni kama jenerali alivyo jeshini. Kama unataka uprofesa, nenda kafundishe chuoni na ufanye tafiti. Kama unataka ujenerali, ingia jeshini. Haina maana kuwa sisi ambao tuko sekta nyingine na kwa hiyo siyo maprofesa ama majenerali, akili zetu siyo nzuri kama za maprofesa ama majenerali.
Phd na huyu ni Prof: kuweni wapole sana.
 
Haitwi Francis kifukwe anaitwa Gwamaka kifukwe

Francis kifukwe alikuwa Rais wa Yanga
Nimeandika kuna mtoto mmoja wa Francis Kifukwe.

Gwamaka Kifukwe ni mtoto wa Francis Kifukwe. Get it?

Rudia kusoma. Gwamaka nimeweka mpaka link ya article inayoongelea habari zake hapo juu.
 
Alichukua masomo ya Ph.D.

Alikuwa na uamuzi wa kutochukua masomo ya Ph.D na kuishia na Masters degree.

Ukiwa umezoea kukaa kwenye kwapa la dunia ambako Ph.D inaonekana kitu cha ajabu ndiyo unaweza kushangaa habari za mtu "kuchukua Ph.D".
Kwapa la dunia sijui ndo hili nililoelewa
 
Dr
Dr Gwamaka Francis Kifukwe
Actually ni Gwamaka Robert Kifukwe.

Kimagharibi mtu ana middle name yake mwenyewe, middle name si first name ya baba.

As in..

John Fitzgeral Kennedy.

Robert Francis Kennedy.

Charles Makongoro Nyerere.

Andrew Burito Nyerere.

Anna Watiku Nyerere.

Anselm Magige Nyerere.

John Guido Nyerere.

Godfrey Madaraka Nyerere.

Rosemary Huria Nyerere.

Pauleta Nyabanane Nyerere.
 
Hatimaye Chuo chetu cha UDSM kimepata kuwa na professor mtoto kuliko wote, amepata ubalozi.
huyu professor ni kijana mdogo sana na ana akili za ziada.

Magufuli anajua kutafuta vichwa, pongezi raisi wetu MAGUFULI

View attachment 1212578
View attachment 1212579
Huyu ni kijana mkuu,sio mtoto.Na very soon atauacha huo ujana.Let's be serious jamani,huwezi kupata Professor mtoto.
 
Kupata PhD mapema hakumfanyi mtu kuwa special. Ni uamzi tu wa mtu kuamua lini aende akasome PhD. Kunaweza kuwa na vitu vingine kama vile bahati ya kupata udhamini... Wengine wanaamua kutafuta pesa kwanza na kusoma baadae. Haina maana kuwa ni wajinga.
Wapi tumezungumzia msio na phd?

Punguza kujistukia
 
ukisomea Tanzania, kwenye shule za "wanyonge" u profesa utapata at age of 45, tena hapo usiwe na sapu hata moja.
dr Masumbuko lamwai ana miaka 57 na bado hajapata u prof hata kuwa associates, though najua jiwe atapewa soon, kisiasa lakini

Dr. Bashiru kasota sana Udsm kwa kigezo cha Umri tu muda mrefu
 
Nimeangalia orodha na kugundua waliofanikiwa ni waliochukulia vyuo vya nje; humu ndani ni uozo mtupu, utasumbuliwa hadi utamani kurudi kulima!


Kweli kabisa

Bongo mtu kapata phd ana miaka 57 halafu Wewe akupe na Miaka 28??

Kwenye Research tu ya Masters watu wanakoma yaana anaweza akakuahirishia Masters yako kwa kuwa tu font size uliyotumia sio ile anayoitaka yeye
 
Kwapa la dunia sijui ndo hili nililoelewa
Unaweza kuwa profesa bila Ph.D, kwa mfano Marekani profesa ni mtu anayefundisha Chuo Kikuu, hata ukiwa na Masters degree lakini unafundisha chuo kikuuu ni profesa.

Kwenye mifumo mingine kama Tanzania, Uprofesa ni ngazi, unaweza kuwa na Ph.D lakini ukawa hujafika ngazi ya uprofesa, ukawa "Senior Lecturer" or something like that lakini si Profesa.

Nchi kama Ufaransa Le Professeur ni mwalimu tu, hata wa sekondari.
 
Definition ya Professor nayo ni muhimu kuzingatiwa. Tanzania Professor ni cheo cha academia unachopata baada ya kuibuka through the ranks, upate Ph.D, ufundishe miaka kadhaa etc. Kuna kupitia kuwa Associate Professor kwanza kabla ya kuwa full Professor.

Ushawahi kuisoma prospectus yoyote ya UDSM hususan za miaka ya 80 au 90?

Hususan kuhusu orodha ya academic staff ambayo ilikuwa inachapishwa mwishoni mwa kitabu hicho?

Orodha hiyo ilikuwa ni ya majina ya walimu pamoja na sifa zao za kitaaluma [academic qualifications].

Kama utakuwa umewahi kuisoma basi utajua kuwa, kwa kipindi hicho [sina hakika kwa sasa, huenda mambo yamebadilika], ilikuwa inawezekana mtu kuwa professor au associate professor bila hata ya kuwa na PhD.

Wawili wanaokuja kwenye kumbukumbu zangu [sikumbuki mahsusi ni prospectus za miaka ipi] ni Prof. Ernest Wamba Dia Wamba na Prof. Mgongo Fimbo.

Sikuwahi kuona PhD. mbele ya majina yao.

Labda mkuu Companero kwenye maktaba yake anaweza kutusaidia ikitokea ana hizo prospectus za miaka hiyo niliyoitaja.
 
Unamaanisha GWAMAKA NJOBELO wa MZUMBE?
Kweli kuna huyo kijana wa Mponjoli Kifukwe anaitwa GWAMAKA kama sijakosea ni kichwa sana , mara ya kwanza kumsikia alikuwa hapo UONGOZI INSTITUTE akiminterview Kaguta Museveni;sasa sijui kama bado yupo hapo au amehama!!! Ni vijana wenye vision kama huyu ndio watakaoikomboa Tanzania.
 
Back
Top Bottom