Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Kumbuka kuwa kwa biashara alizokuwa wanafanya wazee wangu basi kodi yake ingetosha kusomesha watoto zaidi ya wanane hadi Chuo kikuu lakin sie tumesoma watatu tu. Na watano wengine tumechangia kwa jamii nyingine kama wewe wenye dhana ya kuwa kuna cha bure duniyani.

Turejee kwenye Mada.

Je Znz itanufaikaje na hicho kilichooombwa na Prof Tibaijuka?

Kama hakuna namna kwanini BLW wasihusike katika kadhia hii nzima?

Kwa kuwa ni msomi tena wa ngazi zote tatu sidhani kama hauelewi kodi ni nini na zinalipwa kwa sababu gani. Wapo Watanzania wengi tu ambao wazazi wao walilipa kodi kama hao wazee wako lakini wewe ukachukua nafasi yao. Ukasoma wewe chuo kikuu huku ukijifanya Mtanzania!
Zanzibar ni sehemu ya Tanzania. Kunufaika ni lazima kama ambavyo imenufaika na mengine mengi tangu mwaka 1964 likiwemo la wewe kusoma chuo kikuu cha Dar bure!
BLW litaarifiwa tu muda ukifika. Mambo bado yako ngazi ya serikali. Mbona unasahau kuwa kuna WABUNGE wa Zanzibar kwenye Bunge la JMT? Au wenye akili na uchungu kwa "nchi" yao ni wajumbe wa BLW tu?
 
Nianze tu kwa kusema Zanzibar kuna matatizo Mengi umeme unakatika kila siku Jusa yuko kimya,elimu mbovu yuko kimya,wazanzibar wanazidi kuteseka yeye analeta siasa.
Ulichoongea Jusa ni upumbavu maana Tanganyika ina eneo la Bahari toka TANGA mpaka LINDI unaweza kadiria ni kilometa ngapi hizo?kwanza unajua ni upande gani wanataka kuongeza,kama wanataka kuongeza upande wa Pwani zanzibar wawahusishe ya nini?kwanza kwa upande wa zanzibar hawawezi kuongeza maana ukitoka pemba unafika mombasa.
Hata kama wataongeza upande wenu ulitakiwa kukaa na viongozi wa serikali kujua mustakabathi wa hayo sio kupiga kelele kwa kitu ambacho kitafanyika miaka 20 au 30 ijayo.PEMBA ,MTWARA KUNA MAFUTA HAYAJACHIMBWA NDIO HAYO YA KATIKATI YA BAHARI YATACHIMBWA.
WASAIDIE WAZANZIBAR KUPATA ELIMU BORA,UMEME BORA,AFYA BORA ,BADO WANAKUNYWA MAJI MACHAFU,WANALALA PA CHAFU ALAFU UNAFANYA SIASA UNABOA SANA.
 
Hilo aliwezekani hata kidogo. Kwani Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na sio KIKATIBA. Kuna mambo apo nje ya mkataba wa Muungano likiwemo hili la ardhi na makazi.

Sasa unapozungumzia maslahi ya eneo la milki ya arrdhi ni lazima uziusishe pande zote mbili kwani hili si suala la muungano. Alichofanya Tibaijuka ni ubabe kitu ambacho hakikubaliki. Ni mawili tu yanatakiwa hapo ima a withdraw hayo maombi na kuanza mchakato mpya kama nchi zote mbili zitakubaliana au kuanisha kila nchi itanufaika vipi in terms of eneo hilo.

kama OIC ilizimwa na Muungano kwanini na hili lisizimwe.

Tibaijuka amechamke lazima ajiuzuru tu hakuna mjadala.


Zanzibar siyo nchi, wala haina uwezo wa kwenda UN kuongeza au kupunguza hata square centimetre moja ya eneo la Tanzania. Zanzibar siyo mwanachama wa Umoja wa Mataifa na haina kiti Umoja wa Mataifa. Masuala ya ardhi siyo ya mwungano lakini kimataifa Zanzibar haina eneo katika ramani ya Dunia, isipokuwa Jamhuri ya Mwungano wa Tanzania.

Wazanzibari kila siku wanaota mafuta, mafuta ambayo mpaka leo hii hayajathibitika mahali popote huko visiwani. Viongozi wote wa Zanzibar walihusishwa katika mijadala yote ya awali. Hakuna busara, sheria wala kanuni yeyote iliyovunjwa na Prof. Tibaijuka. Hawezi kujiuzuru na wala hatajiuzuru, na wala ombi la kuongeza eneo la bahari ya Tanzania halitaondolewa. Tanganyika ni nchi kubwa haina haja na eneo lolote la Zanzibar, katika eneo litakaloongezwa, kama limeongezwa kutoka Zanzibar litakuwa chini ya milki ya Zanzibar, na lile litakaloongezwa kutoka Tanganyika, litakuwa chini ya milki ya Tanganyika.

Wazanzibari wafute ndoto za kila siku za Zanzibar ni nchi, nenda katika kumbukumbu zote za kimataifa, hakuna nchi inayoitwa Zanzibar. Nchi ya Zanzibar imo vichwani mwa Wazanzibari wachache but practically does not exist.

Wazanzibari msijenge mbegu ya chuki, watoto na wajukuu zenu, siku za mbeleni watashindwa kwenda kuhifadhiwa Tanganyika. Baadhi ya tafiti za kitaalam haziioni Zanzibar baada ya miaka 50 kwenye uso wa Dunia, itakuwa imepotelea baharini kutokana na mabadiliko ya Tabia nchi. Kwa hii chuki mnayojenga, mtaenda wapi? Au mtaishi ndani ya hiyo bahari mnayoipigia kelele?
 
Unachosema ni sahihi kabisa. Lakin kitendo cha upande mmoja wa muungano kujichukulia madaraka ya kuusemea upande mwingine wa muungano pasi na kuwajuza na kuwashirikisha hilo ni kosa lisilo sameheka hata kidogo iwe kibinadam au hata kisheria.

Wanachohoji hapo Znz ni kutoshirikishwa katika mchakato mzima hususan BLW kwa jambo kubwa kama hilo la kuomba eneo la bahari la kuongeza.

sasa BLW linauliza Je Znz wanapata kiasi gani katika hilo ongezeko? nini maslah ya Znz hapo katika hilo ongezeko?.


Kikatiba, zanzibar inashirikiswa katika kugawa mipaka ya ndani si ya Jamhuri. Kibinadamu na kihistorial hayo ni masuala mengine kaka - haswa katika hali hii tete ya muungano.
 
Wazanzibari msijenge mbegu ya chuki, watoto na wajukuu zenu, siku za mbeleni watashindwa kwenda kuhifadhiwa Tanganyika. Baadhi ya tafiti za kitaalam haziioni Zanzibar baada ya miaka 50 kwenye uso wa Dunia, itakuwa imepotelea baharini kutokana na mabadiliko ya Tabia nchi. Kwa hii chuki mnayojenga, mtaenda wapi? Au mtaishi ndani ya hiyo bahari mnayoipigia kelele?

vitisho hivi sasa
 
Vile vile kumbuka kuwa JF ni open forum kwa kila mtu kuweza kujiunga bila kutazama uraia, dini, kabila au jinsia kwa mujibu wa rules za JF. Na mimi ukinisoma kiumakini sana nasimamia sheria zenu wenyewe na katiba zenu za Muungano na ile ya Zanzibar.

sasa mimi sina jipya zaidi ya kusaidia kulinda sheria zenu mlizojitungia wenyewe. Na nasimama kwa hilo na kama unaniona natoka nje ya katiba zenu iwe ya Muungano au ile ya Znz au rules za Jf niko tayari kabisa kuhukumiwa.

Hivi unasababu yoyote unayoweza kufikiri japo kwa kufikirika, muungano unafaida?
 
Bunge la Muungano limeshirikishwa na kuwakilishwa na Mbunge wa Mafia.

Kama nilivyokubainishia hapo awali kuwa Suala la Ardhi na makaazi sio suala la muungano. Kwa sababu hiyo iliwapasa kama waliweza kupitisha katika Bunge la Muungano ni lazima vile vile BLW walitakiwa walijadili kwa kina pia na kupata muafaka wake. Kwani waziri wa Ardhi na Makaazi wa Znz ilitakiwa kuwasilisha barzani kama ingepata muswada huo toka Tanganyika.

Kwa kutowashirikisha Znz na BLW ni kosa kubwa sana hususan kwa jambo hilo lisilokuwamo katika mkataba wa muungano wa Tz.

Suala dogo tu, Nini maslahi ya Znz katika hilo.
Je Znz itapata eneo gani katika hili waliloliomba.

Kumbuka kuwa Muungano ni kama Koti, likikuchosha unalivua na kuliacha.. Haya ni maneno ya Rais wa kwanza wa Znz Karume 1


Ukiangalia katika masuala mbalimbali, picha tunayoipata ni kuwa wengi wa Wazanzibari ni Wabinafsi na Wachoyo. Hii hofu ya kufikiria kuwa eneo litakaloongezwa litakuwa la Tanganyika, na Wazanzibari watanyang'anywa eneo lao inatokana na nini? Hivi tangu mwungano huu uanzishwe ni kitu gani Wazanzibari wamenyang'anywa na Tanganyika? Hivi katika mambo haya ambayo tunayowafadhili Wazanzibari, Wazanzibari wanaweza kuwafanyia Watanganyika?

Wengi wao wamesomeshwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam bure, kwa kulipiwa na serikali ya Tanzania (Tanganyika); kwa muda mrefu wamepewa umeme bure; wabunge wao licha ya kuwakilisha watu wachache sana wanapewa haki zote sawa na wabunge wa bara ambao wanawakilisha maelfu ya watu ambao wanachangia bajeti ya mwungano karibu kwa 100%, Wazanzibari wamewahi kupewa uwaziri kuongoza wizara za serikali ya Tanzania zisizo za mwungano, Wazanzibari wanamiliki mashamba Tanzania bara, n.k. Hawa watu hawana hata shukrani, na upole wa Tanganyika unawafanya wadeke sana. Sidhani kama Tanganyika ina haja hata na bakuli moja ya maji ya bahari ya Zanzibar. Tanganyika ina Pwani ya bahari toka Tanga hadi Mtwara, ina maziwa: Ziwa Nyasa lenye dhoruba kubwa kuliko maziwa yote Duniani, ina Ziwa Tanganyika lenye kina kirefu kuliko yote, ina Ziwa Victoria ambalo ni kubwa kuliko yote; yapo na mengine kama Eyasi, Manyara n.k. Tanganyika ina mito mikubwa na mirefu inayotiririsha maji usiku na mchana, masika na kiangazi, halafu iende ikaipokonye Zanzibar bahari yake kwa lengo gani? Tangayika ina uwezo wa kuwachukua Wazanzibari wote na kuwapa wilaya moja ya Tanganyika, wakaishi kwa nafasi, na ardhi nyingine ikabakia. Wazanzibari, sisi tunawaona ninyi kuwa ni ndugu zetu, tuna-sacrifice mambo mengi kwaajili ya upendo wetu kwenu lakini hamna shukrani. Kuna siku tutawachoka, tutawaachia na ndipo mtajua thamani ya kile ambacho mmekuwa mkikichezea kwa miaka mingi.
 
Je wajua kuwa Rais wa Kwanza wa Znz na makamo wa kwanza wa rais wa Muungano , Amani Karume (Karume 1) taarih 16th Feb 1971 alisema alipohojiwa na waandishi wa habari uwanja wa ndege wa Znz akitokea Dar kuhusu Muungano alisema
" Muungano huu ni kama Koti, Likikuchosha unalitoa na kulivua "


Aheri mngelivua hili koti ila wasiwasi wangu ni kuwa huenda ndani ya koti hakuna hata vest.
 
Nadhani wewe unachotaka kuelezea ama kushawishi hapa ni upupu mtupu.Tanzania ni muungano wa Zanzibar na Tanganyika sasa waziri wa Tanzania anapokuwa hana mamlaka Zanzibar kwa sababu Zanzibar ni nchi,hoja yako inakosa mwelekeo.

Huwa najiuliza hivi watu kama ninyi na hao kina Jusa mnasiri gani dhidi ya wananchi! .Mtazamo wangu wananchi wanahitaji huduma bora za jamii na usalama wa maisha yao .Ila wote mnaoleta hizi chokochoko ni waroho wa madaraka, badala ya kuishauri na kuikosoa serikali kuweka uwiano wa matumizi ya rasilimali kwa manufaa ya wananchi,ninyi mpo majukwaani mkidai Zanzibar ni nchi.Mnachokitaka hakitakaa mkipate kwa sababu wengi wenu hamjui mnachohitaji.

Halafu ningewashauri wewe na hao wapiga debe wenzako kina Jusa kipindi hichi cha kubadili katiba ndio muafaka kuweza kuweka mambo sawa kwa yale yote mnayoona ni kikwazo.Ila kutokana na kuwa mna ajenda zenu za siri mnatanguliza matakwa yenu binafsi badala ya matakwa ya wananchi.

Hiyo ardhi /bahari inayoongezwa ni ya Tanganyika ama Tanzania! kwanza hiyo Tanganyika haipo sasa sijui kinachowapandisha majukwaani na kupaza sauti kama vile nyie sio watanzania.Wapemba wanaofanya biashara Kariakoo na kusaidia ndugu zao walioko Zanzibar isingekuwa huu muungano unafikiri mambo yangekuwaje! .Nadhani ni vyema kuleta hoja zenye/zilizofanyiwa utafiti na sio kutoa hoja kutokana na hulka za mrengo wa kivyama.

Tatizo la wachangiaji wengi humu mnatumia muda mwingi kuchangia kuliko kujifunza,nenda kajifunze mambo yaliyo ya muungano na yaliyo nje ya muungano then pitia kwenye comment yako hapo nilipo 'bold' ili ujifunze,labda kwa kukusaidia mawaziri kama maghembe,Tibaijuka,Mkuchika hawana mamlaka yoyote ZNZ,hayo ndo makubaliano ya muungano, Fact kama hiyo haitegemei uhalali wake au maoni yako hiyo ndo hali halisi iwe sahihi au sio sahihi kuna mawaziri hawahusiki na ZNZ even if wanatambulishwa kama mawaziri wa Tanzania jifunze mambo utajua kuacha kuita UPUPU kila usichikijua.
 
Ata vile Zanzibar ni mkoa. Nadhani JK amelegea fulani katika kuitumikia JMT na ndo maana watu wa Z wamejisahau kuwa hiyo si nchi bali ni mkoa. Nadhani kila mkoa wa JMT huwe na tawala kama za Z ili tupeleke maendeleo kwa wananchi. Mf. Serikali ya mkoa wa Z, Serikali ya Mkoa wa Dar, n.k.
UNITED NATION WANAITAMBUA ZANZIBAR NI NCHI HATA KABLA YA JINA LA TANZANIA HALIJAUNDWA
" WAKE UP TANGANYIKANS THIS IS THE ONLY TIME TO FIGHT TO GET BACK OUR TANGANYIKA"

images

Zanzibar ikiwasilishwa katika umoja wa mataifa 1963

KAMA WEWE NI MTANGANYIKA HALISI BASI IJUE HISTORIA YA NCHI YAKO KULIKO KUBERULIWA BERULIWA
TUU NA MAJACUC:focus:


A%20S%20465.gif
THEY ALWAYS PROUD TO BE ZANZIBARIS EVERY WHERE THE GO AROUND THE WORLD
A%20S%20465.gif

 
Hivi kwa nini Jussa analalamikia "Extended Continental Shelf", lakini hajalalamikia "Exclusive Economic Zone" ya sasa hivi. Labda atueleze kwamba EEZ kwa upande wa Tanzania inamilikiwa na nani, ni Zanzibar au Tanzania? na ni nani mwenye haki na matumizi ya EEZ.
 
Hivi Zanzibar inatambuliwa UN kama nchi? Hivi UN waweza pokea ombi toka kwa mwanachama ambaye si nchi akiishtaki nchi? Zanzibar kwenda kupinga UN wataenda kama nani hadi UN wawasikilize? Hivi CUF wanajua wanachoongea? Hivi UN wanafikiri ni Jimbo la Wawi ambako mwana CUF yeyote aweza enda na kusema lolote.CUF hata wakienda UN nobody will listen to them after all CUF is not a UN member.

UNITED NATION WANAITAMBUA ZANZIBAR NI NCHI HATA KABLA YA JINA LA TANZANIA HALIJAUNDWA
" WAKE UP TANGANYIKANS THIS IS THE ONLY TIME TO FIGHT TO GET BACK OUR TANGANYIKA"

images

Zanzibar ikiwasilishwa katika umoja wa mataifa 1963

KAMA WEWE NI MTANGANYIKA HALISI BASI IJUE HISTORIA YA NCHI YAKO KULIKO KUBERULIWA BERULIWA
TUU NA MAJACUC:focus:


A%20S%20465.gif
THEY ALWAYS PROUD TO BE ZANZIBARIS EVERY WHERE THE GO AROUND THE WORLD
A%20S%20465.gif

 
UNITED NATION WANAITAMBUA ZANZIBAR NI NCHI HATA KABLA YA JINA LA TANZANIA HALIJAUNDWA
" WAKE UP TANGANYIKANS THIS IS THE ONLY TIME TO FIGHT TO GET BACK OUR TANGANYIKA"

images

Zanzibar ikiwasilishwa katika umoja wa mataifa 1963

KAMA WEWE NI MTANGANYIKA HALISI BASI IJUE HISTORIA YA NCHI YAKO KULIKO KUBERULIWA BERULIWA
TUU NA MAJACUC:focus:


:A S 465:THEY ALWAYS PROUD TO BE ZANZIBARIS EVERY WHERE THE GO AROUND THE WORLD:A S 465:

Fatal5,

..Tanganyika ilipata uanachama wa UN mwaka 1961 au 1962 baada ya kupata uhuru wetu.

..kuna juhudi kubwa zinafanyika kuwapotosha Wazanzibari kwamba Tanganyika haikupata kuwa mwanachama wa UN.

..Zanzibar nayo ilipata uanachama wa UN mwaka 1963 kama ulivyoonyesha hapo kwenye picha.

..mwaka 1964 tulipoungana, Tanganyika, na Zanzibar, zili-surrender uanachama wao, na kuchukua uanachama mpya kwa jina la Tanzania.

..serikali ya Mapinduzi Zanzibar haitambuliki ndani ya UN, kwa msingi huo waziri wake wa Ardhi hawezi kwenda ktk vikao vya UN na kuwasilisha ombi la kuongeza eneo la mipaka ya Zanzibar.

..Waziri wa ardhi ktk serikali ya muungano naye hana mamlaka juu ya masuala ya ardhi yanayoihusu Zanzibar. Wazanzibari wanaweza kujenga hoja hiyo na wakawa sahihi.

..Ombi hili la kuongezewa mipaka ilipaswa lifanywe na WAZIRI WA MAMBO YA NJE wa serikali ya muungano kwasababu mamlaka yake yanamruhusu kuizungumzia Tanzania visiwani/Zanzibar ktk umoja wa mataifa. Mawaziri wa ardhi wa Tanzania bara na Zanzibar wangeweza kuwepo ktk ujumbe unaoongozwa na Waziri wetu wa mambo ya Nje.

..kwa hali ilipofikia sasa hivi njia muafaka ya kurekebisha tatizo hili dogo ni kusubiri majibu ya UN kuhusu maombi yetu ya kuongezewa mpaka. Baada ya hapo turejee kwenye mipaka ya Tanganyika na Zanzibar kabla ya muungano wa 1964 ili kuweza kujua kila upande utapata eneo kiasi gani.
 
Barubaru,

..kama Wazanzibari wanataka Prof.Anna Tibaijuka ajiuzulu basi wabunge toka Zanzibar wawasilishe hoja hiyo ktk bunge la muungano.

..kuendelea kupiga makelele ktk vikao vya baraza la wawakilishi siyo njia muafaka ya kushinikiza waziri ktk serikali ya muungano kujiuzulu.
 
hawa vichwa ubao nani aliwaambia zanzibar ina haki miliki ya bahari ya hindi! fools at work.
 
Lakini kwanini Hamsomi kabla ya kumshambulia Mama Tibaijuka? huu mpango wa kuomba ardhi zaidi baharini ilikuwa ni mpango toka Mwaka 2007 yeye kautekeleza Mwaka 2012

Na sio Ardhi ya bahari kaskazini Mwa Tanzania ni kusini Mwa Tanzania karibia na Comoro na Madagascar

Kwahiyo Ugomvi ni nani anautaka na kuutafuta?
 
Mamlaka ya JMT ni kamili. Eneo la jamhuri ya Muungano ni eneo zima la bara na visiwani. Hakuna eneo lolote la 'nchi ya Zanzibar' ambalo si eneo la JMT. Kama lipo niambie. Katiba ya ZNZ inaweza kusema lolote lakini ikipingana na ile ya Muungano vipengele vyake ni batili. Zanzibar ni nchi kwa Wazanzibari tu; siyo nchi inayotambulika mahal popote duniani. Kuwa na jeshi, mahakama, na rais (mihimili mitatu ya dola) hakuifanyi ZNZ kuwa nchi vinginevyo miye ningetamba niko "nchi" ya Michigan! Kuongeza eneo la bahari kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar na kwa Tanzania nzima. Wananchi wa ZNZ yawapasa wafurahi na kuunga mkono uamuzi huu wa serikali ya JMT.

Tanganyika na Zanzibar...miaka ya iliyobakia ya Tanzania ni michache sana. Sasa jifunze kutumia jina lenu , sio aibu kama kweli wewe mzalendo.
 
Nianze tu kwa kusema Zanzibar kuna matatizo Mengi umeme unakatika kila siku Jusa yuko kimya,elimu mbovu yuko kimya,wazanzibar wanazidi kuteseka yeye analeta siasa.
Ulichoongea Jusa ni upumbavu maana Tanganyika ina eneo la Bahari toka TANGA mpaka LINDI unaweza kadiria ni kilometa ngapi hizo?kwanza unajua ni upande gani wanataka kuongeza,kama wanataka kuongeza upande wa Pwani zanzibar wawahusishe ya nini?kwanza kwa upande wa zanzibar hawawezi kuongeza maana ukitoka pemba unafika mombasa.
Hata kama wataongeza upande wenu ulitakiwa kukaa na viongozi wa serikali kujua mustakabathi wa hayo sio kupiga kelele kwa kitu ambacho kitafanyika miaka 20 au 30 ijayo.PEMBA ,MTWARA KUNA MAFUTA HAYAJACHIMBWA NDIO HAYO YA KATIKATI YA BAHARI YATACHIMBWA.
WASAIDIE WAZANZIBAR KUPATA ELIMU BORA,UMEME BORA,AFYA BORA ,BADO WANAKUNYWA MAJI MACHAFU,WANALALA PA CHAFU ALAFU UNAFANYA SIASA UNABOA SANA.


Matatizo yote hayo uliyoyataja sababu ni Muungano. Lakini muda sio mrefu ,Muungano utavunjika hapo Zanzibar itaanza kupumua kama nchi nyengine duniani.
Kwenye RED; Hivi Tangayika wanakunywa maji safi ? Hivi kila mtanganyika anapata elimu bora? afya bora ,wanalala pazuri ? naona wewe ndio onaboa sana...
 
Ukiangalia katika masuala mbalimbali, picha tunayoipata ni kuwa wengi wa Wazanzibari ni Wabinafsi na Wachoyo. Hii hofu ya kufikiria kuwa eneo litakaloongezwa litakuwa la Tanganyika, na Wazanzibari watanyang'anywa eneo lao inatokana na nini? Hivi tangu mwungano huu uanzishwe ni kitu gani Wazanzibari wamenyang'anywa na Tanganyika? Hivi katika mambo haya ambayo tunayowafadhili Wazanzibari, Wazanzibari wanaweza kuwafanyia Watanganyika?

Wengi wao wamesomeshwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam bure, kwa kulipiwa na serikali ya Tanzania (Tanganyika); kwa muda mrefu wamepewa umeme bure; wabunge wao licha ya kuwakilisha watu wachache sana wanapewa haki zote sawa na wabunge wa bara ambao wanawakilisha maelfu ya watu ambao wanachangia bajeti ya mwungano karibu kwa 100%, Wazanzibari wamewahi kupewa uwaziri kuongoza wizara za serikali ya Tanzania zisizo za mwungano, Wazanzibari wanamiliki mashamba Tanzania bara, n.k. Hawa watu hawana hata shukrani, na upole wa Tanganyika unawafanya wadeke sana. Sidhani kama Tanganyika ina haja hata na bakuli moja ya maji ya bahari ya Zanzibar. Tanganyika ina Pwani ya bahari toka Tanga hadi Mtwara, ina maziwa: Ziwa Nyasa lenye dhoruba kubwa kuliko maziwa yote Duniani, ina Ziwa Tanganyika lenye kina kirefu kuliko yote, ina Ziwa Victoria ambalo ni kubwa kuliko yote; yapo na mengine kama Eyasi, Manyara n.k. Tanganyika ina mito mikubwa na mirefu inayotiririsha maji usiku na mchana, masika na kiangazi, halafu iende ikaipokonye Zanzibar bahari yake kwa lengo gani? Tangayika ina uwezo wa kuwachukua Wazanzibari wote na kuwapa wilaya moja ya Tanganyika, wakaishi kwa nafasi, na ardhi nyingine ikabakia. Wazanzibari, sisi tunawaona ninyi kuwa ni ndugu zetu, tuna-sacrifice mambo mengi kwaajili ya upendo wetu kwenu lakini hamna shukrani. Kuna siku tutawachoka, tutawaachia na ndipo mtajua thamani ya kile ambacho mmekuwa mkikichezea kwa miaka mingi.

Mnawalipia hizo gharama zote kwanini? mnaupenda sana siyo?

Kama mnawalipia na mnaona ni mzigo si muwambie walipie hizo gharama au muache kulipia?

Ama mnapata faida sana kufanya hivyo? kwanini mnabeba hasara?

siyo bure.
 
Back
Top Bottom