Tatizo huyu Kikwete amekuwa legelege mno! Ingekuwa enzi za Mwalimu "hawa wote" wangeitwa Magogoni na baadaye kuwekwa 'kizuizuni' Kigamboni. Muulizeni Aboud Jumbe Mwinyi. Kama ZNZ ni nchi Rais gani angekubali kufanywa hivyo?
Pinda aliwaambia bila kumung'unya maneno ZNZ sio nchi, Mahakama kuu ilishasema ZNZ sio nchi. Kikwete legelege akarikoroga eti ZNZ ni nchi ndani ya mipaka JMT na ZNZ sio nchi nje ya mipaka JMT.
BLW limeondoa suala la mafuta na gasi asilia kwenye mambo ya Muungano. Khatibu akawaambia hicho wanachofanya BLW ni utoto, chombo chenye mamlaka ya kuliondoa hilo suala ni Bunge la JMT. Kikwete anaona haya yote lakini anayanyamazia. Matokea yake ZNZ wamefanya mabadiliko haramu kwenye katiba yao, yanayokinzana na katiba ya JMT ambayo ndiyo mama.
Historia inatufundisha kwamba hakuna nchi yoyote dunia iliyotoakipande cha ardhi yake in a siliver plate, Tangia East Timor, Sudan ya Kasikazini, mpaka leo N. Ireand, Taiwan wanapigania, Nchi zilizokuwa Jamhuri za Yugoslavia, Russia etc.
Kama wanzazibari wanataka kuirudisha nchi yao kutoka Tangayika, Jussa na wenzake waende msituni waone kilichomnyoa kanga manyoa. Au wamesahau yaliyompata Nduli Idd Amin Dada.
SMZ ni sawa serikali za Kijiji, wilaya, mkoa kama ilivyo huku Tanzania bara, tofauti ni kwamba wao wanaye ceremonial president. Rais gani wa nchi ambaye hata akienda Burundi hawezi kupigiwa mizinga 21? Sasa huyu ana tofauti gani na Rais wa TFF? Tuwaambie ukweli hawa wazanzibari ili wafahamu status quo yao, mambo ya kulembalemba ya JK hayana nafasi kwenye masuala ya kisheria.