Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Ndugu yangu siku zote huwezi kujuwa umuhimu wa kitu mpaka kikutoke?

Kumbuka Znz na Tanganyika zote ni nchi huru kabisa, nje ya muungano kila nchi itaangalia namna ya kuweza kujiendesha. Kupata taabu au kudorora uchumi wa nchi yoyote inategemea na mipango, mikakati na vipaumbele katika masuala a maendeleo na kukuza uchumi.

Kwa mimi kama mchumi kitaaluma nasema nchi hizo zinategemeana kiuchumi kwa namna moja au nyingine. Lakin ukienda mbaali zaidi utaona Znz wanadhulumiwa kidogo kutokana na population. Znz wapo 1.4 Milioni na Tanganyika 40 Milioni.

Onyesha jinsi wanavyodhulumiwa...!
 
Tibaijuka amshangaa Jussa kupinga mradi wa kiuchumi

Aziza Masoud


WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameshangazwa na kauli iliyotolewa na Mwakilishi wa Mji Mkongwe, Ismail Jussa (CUF), kuhusu mradi wa kuongeza eneo la ziada nje ya ukanda wa uchumi baharini.Akizungumza Dar es Salaam jana, Profesa Tibaijuka alisema haoni sababu ya kugombana wakati ombi hilo liliwasilishwa kama Serikali ya Jamhuri ya Muungano na wakati wa mchakato wa kuandaa, wananchi wa Zanzibar walishirikishwa.

Profesa Tibaijuka alitoa kauli hiyo baada ya Jussa kusema mbele ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kwamba, ongezeko hilo halihusu Serikali ya Jamhuri, bali Serikali ya Tanzania Bara na kitendo kilichofanyika kinaonekana kuhujumu eneo la bahari ya Zanzibar."Sioni sababu ya kugombania fito wakati nyumba tunayoijenga ni moja, siku zote tukipima mipaka huwa tunapima kati ya Jamhuri ya Muungano na nchi husika, hakuna siku tuliyopima mipaka ya Tanzania Bara wala visiwani peke yake kwenye suala hili," alisema Profesa Tibaijuka.

Alisema ni muhimu watu kujua suala la ongezeko ukanda wa uchumi katika eneo la bahari, kwani ni suala nyeti na litakuwa jambo la kusikitisha kama wataanza kuvutana wenyewe kabla halijamalizika.
"Hivi inakuingia akilini, mimi niliyepewa kazi ya uwaziri na Rais niende Marekani kudai ardhi bila watu kujua, ni suala la kusikitisha siwezi kukurupuka kwenda kudai eneo la nchi bila ruhusa ya viongozi, watu wanadai nijiuzulu nitakuwa wa kwanza kuondoka madarakani kama nikijua kosa nililolitenda," alisema.
Alisema madai ya Jussa kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) haikushirikishwa katika mchakato huo, hayaendani na yaliyojiri kutokana na wajumbe na viongozi wa SMZ kushiriki na kufanya kazi kwa bidii katika mchakato wa kudai eneo hilo. Mwisho.

Makosa yako ni haya.

1. Wewe wizara yako sio miongoni mwa mambo ya Muungano. Kwanini uliwasilisha wewe na sio waziri wa mambo ya nje?

2. Kwanini usihakikishe kuwa BLW lina taarifa za ongezeko hilo?

3. Je unaweza kuwaeleza wananchi kuwa umeomba eneo gani liongezwe (weka ramani) na sio kusema ukubwa tu (tuone uhalali wake)

4.Je hukuona wewe kuwasilisha kitu cha muungano kimataifa ni kuvunja sheria na katiba za Muungano? Wizara yako si wizara ya Muungano.

Je unajuwa kuwa mumeungana Kimkataba na sio kikatiba na Tz ni muungano wa nchi mbili huru tanganyika na Znz.
 
Zanzibar ni nchi ndani na si nchi nje - Jakaya Kikwete
 
Onyesha jinsi wanavyodhulumiwa...!

Anzisha uzi maalum kuhusu hilo na nitaweka Darsa hapo. Kwani nina data kamili kuhusu uchumi wenu kiundani zaidi na naujuwa vilivyo na nimeufanyia kazi kwa zaidi ya miaka sabaa nikiwa wizara ya fedha na mipango kwenye muungano.

 
Anzisha uzi maalum kuhusu hilo na nitaweka Darsa hapo. Kwani nina data kamili kuhusu uchumi wenu kiundani zaidi na naujuwa vilivyo na nimeufanyia kazi kwa zaidi ya miaka sabaa nikiwa wizara ya fedha na mipango kwenye muungano.
Sasa Jussa unaendelea kulalamika nini wakati Tibaijuka ameshakujibu?
 
Kumbuka kuwa ninaposema ving'ora ninamaanisha msafara.

Na msafara wowote kisheria ni ule unao ongozwa Polisi. Ambao kwa Tanganyika ni watu watatu tu ki protocal wanapata hiyo nao ni waziri mkuu, Rais na Makamo wa Rais wa Muungano. Na maalim Seif na Balozi Iddi wanapewa sawa nao pasi na kumsahau Rais wa Znz. wakiwa tanganyika.

je unasemaje hapo? je hawatambuliwi? kama hawatambuliwi kwanini wapewe status ya juu namna hiyo kwene mapokezi na misafara yao?
Pitia sheria vizuri utambue msafara ni nini?

Hata Raila Odinga akija Tanganyika anapewa heshima ya kuongozwa kwa ving'ora japo katiba yetu ya JMT haimtambui, same to Sharifu na Seif
 
Makosa yako ni haya.

1. Wewe wizara yako sio miongoni mwa mambo ya Muungano. Kwanini uliwasilisha wewe na sio waziri wa mambo ya nje?

2. Kwanini usihakikishe kuwa BLW lina taarifa za ongezeko hilo?

3. Je unaweza kuwaeleza wananchi kuwa umeomba eneo gani liongezwe (weka ramani) na sio kusema ukubwa tu (tuone uhalali wake)

4.Je hukuona wewe kuwasilisha kitu cha muungano kimataifa ni kuvunja sheria na katiba za Muungano? Wizara yako si wizara ya Muungano.

Je unajuwa kuwa mumeungana Kimkataba na sio kikatiba na Tz ni muungano wa nchi mbili huru tanganyika na Znz.

Ufafanuzi wa Waziri Tibaijuka umetufumbua macho na sasa tumeelewa kwamba mchakato huo mkubwa na muhimu uliendeshwa na kamati mbalimbali zilizoundwa tangu mwaka 2007, ikiwamo kamati ya makatibu wakuu iliyoongozwa na Katibu Mkuu katika Wizara ya Maji, Nishati, Ujenzi na Makazi Zanzibar, Mwalimu Mwalimu na kwamba aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji Ramani, Haji Adam Haji ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi. Sasa tumejua pia kwamba Pandu Makame kutoka katika Ofisi ya Makamu wa Rais ndiye aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa Kamati ya Utekelezaji.

Tumefarijika kusikia kutoka kwa waziri huyo kuwa, zoezi la kupima alama za sehemu ya bahari inayoombwa lililofanyika Januari mwaka jana, masheha wa Kiuyu, Maziwa Ng'ombe, Kojani na Vitongoji walioko katika Kisiwa cha Pemba walishirikishwa, huku wenzao wa Makunduchi katika kisiwa cha Unguja pia wakishirikishwa. Hata wakati wa kuwakilisha andiko hilo huko UN ujumbe wa nchi yetu uliwahusisha viongozi wa pande mbili za Muungano, akiwamo Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Ayoub Mohamed Mahamoud.
 
Kuna baadhi ya wazanzibari wana agenda yao. Makabrasha yaliyowasilishwa UN yako public (online) kwa nini msiende huko mkayasoma na ramani zimewekwa huko. Eneo linaloombwa ni hili linaloonekana kwenye ramani hii. Ramani hii ni Official (imenyofolewa kutoka kwenye executive summary ya submission iliyopelekwa UN)
ExtendedContinentalShelf_TZ.jpg
 
Kuna baadhi ya wazanzibari wana agenda yao. Makabrasha yaliyowasilishwa UN yako public (online) kwa nini msiende huko mkayasoma na ramani zimewekwa huko. Eneo linaloombwa ni hili linaloonekana kwenye ramani hii. Ramani hii ni Official (imenyofolewa kutoka kwenye executive summary ya submission iliyopelekwa UN)

Hawa jamaa kwa 'kilomolomo'...!
 
Ufafanuzi wa Waziri Tibaijuka umetufumbua macho na sasa tumeelewa kwamba mchakato huo mkubwa na muhimu uliendeshwa na kamati mbalimbali zilizoundwa tangu mwaka 2007, ikiwamo kamati ya makatibu wakuu iliyoongozwa na Katibu Mkuu katika Wizara ya Maji, Nishati, Ujenzi na Makazi Zanzibar, Mwalimu Mwalimu na kwamba aliyekuwa Mkurugenzi wa Upimaji Ramani, Haji Adam Haji ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi. Sasa tumejua pia kwamba Pandu Makame kutoka katika Ofisi ya Makamu wa Rais ndiye aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti mwenza wa Kamati ya Utekelezaji.

Tumefarijika kusikia kutoka kwa waziri huyo kuwa, zoezi la kupima alama za sehemu ya bahari inayoombwa lililofanyika Januari mwaka jana, masheha wa Kiuyu, Maziwa Ng'ombe, Kojani na Vitongoji walioko katika Kisiwa cha Pemba walishirikishwa, huku wenzao wa Makunduchi katika kisiwa cha Unguja pia wakishirikishwa. Hata wakati wa kuwakilisha andiko hilo huko UN ujumbe wa nchi yetu uliwahusisha viongozi wa pande mbili za Muungano, akiwamo Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Ayoub Mohamed Mahamoud.

Suala dogo tu hapa.

Kwanini Prof Tibaijuka alichukua madaraka a kuwasilisha suala hili UN wakati anajuwa fika kwa mujibu wa katiba ya muungano yeye hana mamlaka ya kuwasilisha kitu cha muungano? Jukumu hilo alipaswa kuwasilisha membe ambaye ni waziri wa mambo ya nje na wizara yake ni ya muungano?

Kama walihusisha masheha , kwanini wasishirikishe BLW pia kama walivyofanya wao walishirikisha Bunge la muungano?

Kifupi amevunja sharia na laazima ajiuzuru tu hakuna jinsi.

 
Hata Raila Odinga akija Tanganyika anapewa heshima ya kuongozwa kwa ving'ora japo katiba yetu ya JMT haimtambui, same to Sharifu na Seif

Kwani Raila Odinga ni mtanzania?
 
WC,,
Suala la ardhwi sio suala la kisiasa hilo ni rasilimali ya nchi hoyo. Ndio maana unasikia watu wanapigana na kuuwana kutokana na kugombea ardhi..

Labda nikuulize Je unajuwa kwanini suala la ardhi halimo katika hati ya makubaliano ya Muungano?
Kila nchi ina waziri wake wa Ardhi.

Kama suala hilo ni genuine halina shaka wala hila zozote kwanini lisiwasilishwe na Waziri wa mambo ya Nje na mawaziri wote wa ardhi wa nchi zote mbili kuwa wasindikizaji tu?

Kwani masuala ya mambo ya nje ni moja katika makubaliano katika hati ya muungano.

Kwanini asiwasilishe Membe au naibu wake Mahadhi Maalim. Tibaijuka amewasilisha kama nani?
Tatizo sasa ni Tibaijuka kuwasilisha badala ya Membe? Mbona unahamisha magoli kila mara? Bila shaka unafahamu uzoefu wa Mama Tibaijuka kwenye corridors za UN. Bila shaka unakumbuka pia kuwa amekuwa Mkurugenzi wa Habitat na hivyo masuala ya ardhi hayampigi chenga.
Suala hili sio la ardhi pekee. Liangalie kwa upana wake. Angalia pia walioshiriki kuliandaa ni watumishi wa wizara zipi za Zanzibar na wale wa Muungano. Unachosahau au haukijui ni kuwa wizara zote za serikali ya JMT ni wizara za Muungano na ndio maana unaweza ukamkuta Mzanzibar anateuliwa kuwa waziri au naibu. Hili limetokea mara kadhaa tangu enzi za Mwalimu. Unakumbuka mtu mwenye asili ya Oman kama wewe ambaye ni Mzanzibar asiyependwa na Wazanzibar amewahi kuwa Waziri Mkuu wa Nchi hii?
 
Suala dogo tu hapa.

Kwanini Prof Tibaijuka alichukua madaraka a kuwasilisha suala hili UN wakati anajuwa fika kwa mujibu wa katiba ya muungano yeye hana mamlaka ya kuwasilisha kitu cha muungano? Jukumu hilo alipaswa kuwasilisha membe ambaye ni waziri wa mambo ya nje na wizara yake ni ya muungano?

Kama walihusisha masheha , kwanini wasishirikishe BLW pia kama walivyofanya wao walishirikisha Bunge la muungano?

Kifupi amevunja sharia na laazima ajiuzuru tu hakuna jinsi.

Barubaru unashangaza kidogo. Bunge la Muungano halina Wazanzibari? BLW haliwakilishwi kwenye Bunge la Muungano? Ilikuwa ni kazi ya Mama Tibaijuka kulijulisha BLW? Nitakuelewa kama kelele hizi za kijinga zikiishia kwa Shamhuna ambaye alijua kila hatua ya mchakato huu. BLW ni chombo cha Muungano?
 
Barubaru unashangaza kidogo. Bunge la Muungano halina Wazanzibari? BLW haliwakilishwi kwenye Bunge la Muungano? Ilikuwa ni kazi ya Mama Tibaijuka kulijulisha BLW? Nitakuelewa kama kelele hizi za kijinga zikiishia kwa Shamhuna ambaye alijua kila hatua ya mchakato huu. BLW ni chombo cha Muungano?


WC,

Nafikiri kabla ya kuleta suala hili ni vizuri ujue Bunge la muungano ni nini na nini mipaka yake ya kazi. Suala hilo lipo kwenye katiba au hata tovuti ya Bunge. Lakin pia soma kazi za BLW na mipaka yake ya kazi kama ilivyo ainishwa katika katiba ya Muungano na ile ya Zanzibar.

Kisha tuendelee na mujadala. Kwani si vizuri kutafuniwa kila kitu ni lazima usome ili ujuwe kabla ku argue au kuuliza suala.
 
Tatizo sasa ni Tibaijuka kuwasilisha badala ya Membe? Mbona unahamisha magoli kila mara? Bila shaka unafahamu uzoefu wa Mama Tibaijuka kwenye corridors za UN. Bila shaka unakumbuka pia kuwa amekuwa Mkurugenzi wa Habitat na hivyo masuala ya ardhi hayampigi chenga.
Suala hili sio la ardhi pekee. Liangalie kwa upana wake. Angalia pia walioshiriki kuliandaa ni watumishi wa wizara zipi za Zanzibar na wale wa Muungano. Unachosahau au haukijui ni kuwa wizara zote za serikali ya JMT ni wizara za Muungano na ndio maana unaweza ukamkuta Mzanzibar anateuliwa kuwa waziri au naibu. Hili limetokea mara kadhaa tangu enzi za Mwalimu. Unakumbuka mtu mwenye asili ya Oman kama wewe ambaye ni Mzanzibar asiyependwa na Wazanzibar amewahi kuwa Waziri Mkuu wa Nchi hii?

Suala sio Uzoefu kama ni mzoefu basi angechaguliwa kuwa waziri wa Muungano katika masuala haya ya mambo ya nje na masuala ya kimataifa.

Suala hapa tunasimamia sheria. Yeye kwa mamlaka aliyopewa ya waziri wa ardhi na makaazi hana mandate yoyote kule Znz kwa mujibu wa Katiba ya muungano. Wizara ya Ardhi sio miongoni mwa wizara ya muungano kama zilivyo wizara za nje, mambo ya ndani au muungano.

masuala yote a mahusiano ya mambo ya nje ni suala la wizara ya mambo ya nje. sasa suala yeye aliwakilisha kama nani? Je hakujuwa kuwa kuwasilisha suala la muungano kwa yeye kuwa ni kosa kisheria na kuvunja katiba ya muungano na ile ya Znz?

Kwanini asijiuzuru hapo kwa kuvunja sharia?

 
Ukiangalia katika masuala mbalimbali, picha tunayoipata ni kuwa wengi wa Wazanzibari ni Wabinafsi na Wachoyo. Hii hofu ya kufikiria kuwa eneo litakaloongezwa litakuwa la Tanganyika, na Wazanzibari watanyang'anywa eneo lao inatokana na nini? Hivi tangu mwungano huu uanzishwe ni kitu gani Wazanzibari wamenyang'anywa na Tanganyika? Hivi katika mambo haya ambayo tunayowafadhili Wazanzibari, Wazanzibari wanaweza kuwafanyia Watanganyika?

Wengi wao wamesomeshwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam bure, kwa kulipiwa na serikali ya Tanzania (Tanganyika); kwa muda mrefu wamepewa umeme bure; wabunge wao licha ya kuwakilisha watu wachache sana wanapewa haki zote sawa na wabunge wa bara ambao wanawakilisha maelfu ya watu ambao wanachangia bajeti ya mwungano karibu kwa 100%, Wazanzibari wamewahi kupewa uwaziri kuongoza wizara za serikali ya Tanzania zisizo za mwungano, Wazanzibari wanamiliki mashamba Tanzania bara, n.k. Hawa watu hawana hata shukrani, na upole wa Tanganyika unawafanya wadeke sana. Sidhani kama Tanganyika ina haja hata na bakuli moja ya maji ya bahari ya Zanzibar. Tanganyika ina Pwani ya bahari toka Tanga hadi Mtwara, ina maziwa: Ziwa Nyasa lenye dhoruba kubwa kuliko maziwa yote Duniani, ina Ziwa Tanganyika lenye kina kirefu kuliko yote, ina Ziwa Victoria ambalo ni kubwa kuliko yote; yapo na mengine kama Eyasi, Manyara n.k. Tanganyika ina mito mikubwa na mirefu inayotiririsha maji usiku na mchana, masika na kiangazi, halafu iende ikaipokonye Zanzibar bahari yake kwa lengo gani? Tangayika ina uwezo wa kuwachukua Wazanzibari wote na kuwapa wilaya moja ya Tanganyika, wakaishi kwa nafasi, na ardhi nyingine ikabakia. Wazanzibari, sisi tunawaona ninyi kuwa ni ndugu zetu, tuna-sacrifice mambo mengi kwaajili ya upendo wetu kwenu lakini hamna shukrani. Kuna siku tutawachoka, tutawaachia na ndipo mtajua thamani ya kile ambacho mmekuwa mkikichezea kwa miaka mingi.

suala la kujiuliza
Kama kweli Tanganyika ina utajili wote huo, Mbona masikini?

 
Kuna baadhi ya wazanzibari wana agenda yao. Makabrasha yaliyowasilishwa UN yako public (online) kwa nini msiende huko mkayasoma na ramani zimewekwa huko. Eneo linaloombwa ni hili linaloonekana kwenye ramani hii. Ramani hii ni Official (imenyofolewa kutoka kwenye executive summary ya submission iliyopelekwa UN)
Someni jamani! kwanini kulalamika tu!?
 
Barubaru,
Acha kukwepa. Jibu hoja zangu kwenye hizo post mbili. Acha kunikimbizia kungine. SAS amewahi kuwa Waziri Mkuu wa nchi hii huku Zanzibar ikiwa na Waziri Kiongozi wake. Ni sheria ilivunjwa? Ni ipi hiyo? Mama Tibaijuka kavunja sheria gani? Hakutumwa na Rais wa JMT?
 
Suala sio Uzoefu kama ni mzoefu basi angechaguliwa kuwa waziri wa Muungano katika masuala haya ya mambo ya nje na masuala ya kimataifa.

Suala hapa tunasimamia sheria. Yeye kwa mamlaka aliyopewa ya waziri wa ardhi na makaazi hana mandate yoyote kule Znz kwa mujibu wa Katiba ya muungano. Wizara ya Ardhi sio miongoni mwa wizara ya muungano kama zilivyo wizara za nje, mambo ya ndani au muungano.

masuala yote a mahusiano ya mambo ya nje ni suala la wizara ya mambo ya nje. sasa suala yeye aliwakilisha kama nani? Je hakujuwa kuwa kuwasilisha suala la muungano kwa yeye kuwa ni kosa kisheria na kuvunja katiba ya muungano na ile ya Znz?

Kwanini asijiuzuru hapo kwa kuvunja sharia?

Mkuu kichwa chako kina matatizo gani au ni chuki tu? Umeshaambiwa ule ujumbe uliokwenda UN uliwakilishwa na viongozi wa pande mbiii za Muungano. Mbona unahangaika na mama wa watu aliyeanza uwaziri mwishoni mwa 2010 wakati mchakato huo ulikuwa umeshaanza kwa miaka kadhaa!! Hawa viongozi waliowakilisha Zanzibar kwenye huo ujumbe uliokwenda UN pamoja na wazanzibari wote walioshiriki huo mchakato tangu 2007 nao wawajibike?
 
Back
Top Bottom