Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Tatizo la msingi ni kwamba baadhi ya viongozi wa Zanzibar wamepoteza uwezo wa kuongoza. Hakuna viongozi ambao wana ujasiri wa kusimama dhidi ya watu kama kina Jussa na kuwaambia ukweli; hakuna viongozi Zanzibar wenye uwezo wa kusema na kutetea hoja zao au kupendekeza hoja tofauti na za kina Jussa. Huko kwenye BLW hakuna viongozi wenye ujasiri wa kusimama na kusema hapana!

Wazanzibari wanalazimishwa kuwa na fikra za aina moja na kuwa wasioneshe tofauti yoyote ya mawazo; huu ndio mwanzo wa ule udikteta wenyewe. Wachache ambao wanaweza kuwa ni pro-union wanaogopa kusimama na kuwapinga hawa separasists kama kina Jussa. Hawawezi kwa sababu wamekubali kuingia katika political pandering kwamba kila mmoja akitaka kuonekana ni kiongozi mzuri basi lazima awe against the union, deparaging watu wa bara, kebehi ya Nyerere n.k Matokeo yake watu wenye ujasiri wamekosekana na muungano wao unatokana na chuki sasa.

Hawa Wazanzibar ndugu zetu umoja wao uko kwa sababu wanaonekana kuchukia Muungano na kuichukia Tanzania bara; wanaamini kuwa ni Tanganyika ndio tatizo lao wakati kwa kila kipimo wako wanajiamulia mambo yao mengi wao wenyewe. Wanajiaminisha kuwa wao ni nchi na ina mambo yake na wanataka wawe nchi wakiwa bado kwenye muungano! Bahati mbaya ukweli wameambiwa mara nyingi lakini hawataki kuamini - Zanzibar siyo nchi mahali popote pale isipokuwa kwa Zanzibar yenyewe.

KUna nchi nchi moja tu nayo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Ibara ya 1) ya Katiba Ya Muungano. Na Katiba hiyo inasema wazi kuwa eneo la JMT ni eneo lote la Tanzania Bara na Eneo lote la Tanzania Visiwani na bahari yake! Wazanzibari hawaamini kuwa wao siyo nchi! Wakati umefika tuanze kuwahakikishia ndugu zetu kuwa wao ni sehemu ya Muungano na ni wananchi wa Tanzania. Kama kweli wanaona muungano hauwafahi au ni tatizo wajitokeze tu na kudai kuwa wanataka kutoka nje ya Muungano.

Lakini wafanye hivi kwa kujiuzulu kwanza nafasi zao kwenye Muungano ili wapiganie kujitenga kwa Zanzibar! Haiwezekani upande mmoja wanafurahia matunda ya Muungano wakati huo huo hawautaki!


Mwanakijiji,

Ni vizuri kabla kuandika lolote ni vizuri usome katiba zote mbili ili kujiridhisha na kuweka hoja iliyo na mashiko. Na hata unaposoma Katiba moja basi isome vizuri sana na kuona Mamlaka ya rais wa Znz na serikali yake. Kumbuka kuwa kuna ibara maalum inayotambua na kutambulisha uwepo wa Rais wa Znz na Serikali yake. Lakin vile Katiba ya muungano imebainisha kwa ibara maalum uwepo wa Baraza la wawakilishi Znz na shughuli zake.

Nakushauri zisome ibara hizo kisha lete hoja zake. Kwani kuleta hoja kwa kusoma ibara nusu nusu hakuleti maana kwa wanaokusoma na kuleta mtafaruku na kwa watu makini watakuona kama mchochezi.

Lakin vile vile ukisoma Ibara ya kwanza ya katiba ya Znz imejibainisha wazi kueleza eneo la miliki ya Znz na limebainishwa wazi hapo.
Na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibari ya Mwaka 1984 kama ilivyorekebishwa mwaka 2009:

1. "Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa
vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari
yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar"



Vile vile kumbuka Znz sio wanafiki kwani hata rasimu ya katiba ya Muungano iliyopelekwa kule na Bunge la Muungano ilichanwa hadharani bila kificho kitu ambacho Tanganyika hawakuthubutu kukifanya ila walibaki kughumia tu.

lakin pia wa Znz wapo huru kuujadili muungano kwa mapana yake kuliko Znz. Naweza kusema kuwa mwenye uthubutu wa kusema Muungano ndani ya Bunge ni Tundu Lissu tu wengine woooote wanafiki na waoga wa kuujadili.

Ni vizuri ufikie pahala kuona Bara kuwa kuna ombwe kubwa sana la uongozi sababu kubwa ni kuogopana na unafiki wa baadhi ya watu hususan viongozi. Zanzibar ipo huru.

nafikiri mawazo yako uliyotoa umetoa kwa mfano wa Bara na kuinasibisha Znz kimakosa ima kwa kukusudia ili kuhalalisha mada yako.

Labda nikuulize suala lililopo mezani wewe unalitazamaje? pitia katiba zote kujua mipaka ya kila wizara husika kabla kuleta hoja.
 
Kilichowafikisha hapa viongozi wa Zanzibar ni chaguzi na matokeo ya kijinga. Sasa hivi wanachukua madaraka kwa ridhaa ya Maalim Seif na Jussa. Hili nalo lina mizizi yake huku bara. CCM bara imekuwa ikiwapelekea Wazanzibar wagombea ambao sio chaguo lao.
Kinachonishangaza zaidi ni vijana kama Jussa kuidharau katiba ya JMT kwa makusudi kabisa. Mipaka ya Tanzania ni suala la katiba ya JMT. Mama Tibaijuka hashughulikii ARDHI kwenye suala hili. Anashughulikia mipaka.

Nakuomba kabla kuandika lolote naomba nikuulize.

Je unajuwa mipaka ya kazi ya Waziri wa Ardhi na maendeleo ya makazi wa muungano Prof Tibaijuka? Pitia kwenye katiba ya muungano limebainishwa hilo na utujuze.

 
Barubaru, Katiba ya Zanzibar ipo kwa sababu Katiba ya Muungano imesema "kutakuwa na Katiba ya Zanzibar". Katiba ya Zanzibar haipo nje ya Katiba Ya Muungano. Kati ya Katiba hizo mbili linalotenguka ni lile linalopingana na Katiba ya Muungano linatenguka. Katiba ya Muungano ikipingana na ya Zanzibar, ya muungano haitenguki ni ya Zanzibar ndio inatenguka. Binafsi hata nikiona Katiba ya Zanzibar inasema "Zanzibar ni nchi" kwangu haina maana yoyote kwa sababu Katiba ya Muungano inasema "Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano!"! Hakuna nchi mbili ipo nchi moja!
 
Jamani kwanini wazenj wasipewe nafasi waende zao maana nw kila siku tunawajadili wao.
 
Jamani mamlaka ya Zanzibar kieneo yanaisha wapi? Yainaisha chumbe au zaidi ya chumbe. Will someone kindly tell /define territorial boundaries within which zanzibar enjoys territorial autonomy
Suala la MIPAKA ni suala la KATIBA ya JMT. Walichokifanya Zanzibar kwenye katiba yao ni uhuni mtupu. Ni ubatili kwa mujibu wa katiba ya JMT. Rais wetu hataki kuwaambia hili. Atawaudhi. Baraza la Wawakilishi halina mamlaka yoyote juu ya haya wanayoyajadili. Wanaoweza kufanya hivi ni WABUNGE wao ndani ya BUNGE la JMT ambako BLW lina uwakilishi wa Wabunge watano mbali na wale wa majimbo. Kwa nini Jussa anaachiwa kutamba na kupotosha mambo mengi kiasi hiki kwangu ni kitendawili.
 
Kumbuka kuwa hata Tanganyika haiwezi kufikisha jambo lolote Un kwa sababu haitambuliki kisharia. Na unaposema Tanzania maana yake ni Tanganyika na Zanzibar.

Tunachohoji vipi Tibaijuka waziri wa Ardhi wa Tanganyika apeleke maombi UN kwa niaba ya Tanzania pasi na kuhusisha Znz huusan watunga sharia wa nchi hizo mbili huru zilizoungana kimkataba?

CUF na BLW wameliona hilo japo Chadema wanalipinga kiaina. Kwani hilo sio tatizo kwenu kwani nia yenu ni kuidhulumu Znz na kukuza tanganyika. Znz wameliona hilo na mpaka kieleweke.

lazima mjue Zanzibar ni nchi kamili yenye mamlaka kamili kwa mujibu wa sharia za Znz. Na Muungano wanalijua hilo.



kwenye red sasa nimeelewa tatizo lipo wapi!! na chanzo cha yote ni ccm, utamwitaje waziri asiye wa muungano(yaani wa tanganyika ambayo haipo) waziri wa jamhuri ya muungano wa tanzania (ambae hata UN ndie wanamtambua kimataifa alafu nyumbani hatambuliki). ndio maana chadema tena hata zitto alipendekeza kuwa na aina tofauti ya muungano na hii tuliyonayo maana inajikanganya. maana tibaijuka unapomuita waziri wa ardhi tanganyika wakati tanganyika haipo na wakati huo huo yeye ni waziri wa JMT huu ni mkanganyiko mkubwa sana na source yake ni hawa ccm

angalia hata ya shein sijui makamu wa rais na marais zanzibar watatu ni vurugu isiyokuwa na tija. Tuamke mchakato huu wa katiba tubadili muundo wa muungano.

mwarabu wa oman simamia na akina jusa wako na hilo waliita baraza la wawakilishi simamanieni kidete tuwe na muungano unaoeleweka na si kusimamia sijui tibaijuka ajiuzuru.
 
Kuongezeka kwa eneo la bahari ni kwa manufaa ya wote Tanzania bara na Tanzania visiwani hakuna swala la Zanzibar na Tanganyika sababu ukileta maswala ya kufaidika? masai wa njiro anafaidika vipi na hilo swala kama unataka faida ya moja kwa moaja! Nyerere alisema ukianza kula nyama ya mtu hutoacha kamwe ndio kitu kinachowasumbua ndugu zetu wa zanzibar. Na siku ile alikuwa anawalenga wazanzibar moja kwa moja.
 
Nakuomba kabla kuandika lolote naomba nikuulize.

Je unajuwa mipaka ya kazi ya Waziri wa Ardhi na maendeleo ya makazi wa muungano Prof Tibaijuka? Pitia kwenye katiba ya muungano limebainishwa hilo na utujuze.

Barubaru ili usiendelee kujichanganya na kuchanganya watu kama anavyofanya mpwao Jussa kila mara anza na KATIBA ya JMT halafu kasome hiyo nyingine. Mnataka kulitumia vibaya BLW. Mambo yanayogusa JMT yana katiba moja tu. Hili la mipaka ni mojawapo.
 
Tatizo la msingi ni kwamba baadhi ya viongozi wa Zanzibar wamepoteza uwezo wa kuongoza. Hakuna viongozi ambao wana ujasiri wa kusimama dhidi ya watu kama kina Jussa na kuwaambia ukweli; hakuna viongozi Zanzibar wenye uwezo wa kusema na kutetea hoja zao au kupendekeza hoja tofauti na za kina Jussa. Huko kwenye BLW hakuna viongozi wenye ujasiri wa kusimama na kusema hapana!


Nadhani upendo wetu na muungano unatufanya tutumie mizani tofauti tunapowasikia wale wapinga muungano. Nadhani umevuka mipaka kuonyesha uongezi mzuri ama madhubuti ni wale tu watakoweza kukubali muungano. Si dhani kama hicho ndio kigezo cha msingi kusema huyu ndio kiongozi jasiri ama ana uwezo. Hapa, penzi lako na muungano limekugubika. Kwanini inakuwa kwetu vigumu kukubali labda wengi zanzibar, hawapendi muungano jinsi ulivyo? Kwanini, tunataka kutafuta sauti zile zinazounga muungano?

Wazanzibari wanalazimishwa kuwa na fikra za aina moja na kuwa wasioneshe tofauti yoyote ya mawazo; huu ndio mwanzo wa ule udikteta wenyewe. Wachache ambao wanaweza kuwa ni pro-union wanaogopa kusimama na kuwapinga hawa separasists kama kina Jussa. Hawawezi kwa sababu wamekubali kuingia katika political pandering kwamba kila mmoja akitaka kuonekana ni kiongozi mzuri basi lazima awe against the union, deparaging watu wa bara, kebehi ya Nyerere n.k Matokeo yake watu wenye ujasiri wamekosekana na muungano wao unatokana na chuki sasa.


Kwanini sauti za kupinga tu ndio zisikike? Kwa maelezo yako, unadhani kwa kuwa ndio kimekuwa kigezo cha uongozi bora. Kwa maneno mingine, mtu anayepinga muungano ndio anakubalika kwa wananchi wa zanzibar? Kama ndivyo, tunataka kuwaambia wazanzibar kigezo hicho sio sahihi?

Lakini jambo unaloliibua ni zuri sana, kwamba, je dalili zipi zinazoonyesha wapo wanautaka muungano na kwanini hawajitokezi?

Hawa Wazanzibar ndugu zetu umoja wao uko kwa sababu wanaonekana kuchukia Muungano na kuichukia Tanzania bara; wanaamini kuwa ni Tanganyika ndio tatizo lao wakati kwa kila kipimo wako wanajiamulia mambo yao mengi wao wenyewe. Wanajiaminisha kuwa wao ni nchi na ina mambo yake na wanataka wawe nchi wakiwa bado kwenye muungano! Bahati mbaya ukweli wameambiwa mara nyingi lakini hawataki kuamini - Zanzibar siyo nchi mahali popote pale isipokuwa kwa Zanzibar yenyewe.

Labda ndio muungano wetu ulivyo - unajionyesha katika ukinzani.

Lakini tunatatizo la msingi hapa, kama zanzibar sio nchi yenyewe ni kitu gani sasa? tunasema ni sehemu ya muungano! ndio kitu gani - tanga mkoa? mwanza mkoa! zanzibar ni kitu gani?
 
Watu hawataki kuamini kuwa Zanzibar siyo nchi; nadhani huu ni ujumbe ambao inabidi tuurudie ili ueleweke. Zanzibar iliacha kuwa nchi ilipoungana na Tanganyika kuunda TAnzania. Ilichoachiwa ni kuwa na serikali yake ambayo ni sawa na serikali ya State of Michigan au New York! True, watu wa New York wanajiita New Yorkers, wana GAvana wao, polisi wao, sheria zao bunge lao n.k lakini ni state only ndani ya US nje ya US tunajua kuna nchi moja tu inaitwa United States of America. Na ni Federal Gvt inayohusika na mipaka ya maji. Mamlaka ya karibu states zote yanaishia pale ardhi inapogusa maji na mamlaka ya federal yanaanzia pale pale!
 
Watu hawataki kuamini kuwa Zanzibar siyo nchi; nadhani huu ni ujumbe ambao inabidi tuurudie ili ueleweke. Zanzibar iliacha kuwa nchi ilipoungana na Tanganyika kuunda TAnzania. Ilichoachiwa ni kuwa na serikali yake ambayo ni sawa na serikali ya State of Michigan au New York! True, watu wa New York wanajiita New Yorkers, wana GAvana wao, polisi wao, sheria zao bunge lao n.k lakini ni state only ndani ya US nje ya US tunajua kuna nchi moja tu inaitwa United States of America. Na ni Federal Gvt inayohusika na mipaka ya maji. Mamlaka ya karibu states zote yanaishia pale ardhi inapogusa maji na mamlaka ya federal yanaanzia pale pale!

kama zanzibar sio nchi, tuitaje sasa? Ka mkoa? wilaya? Kijiji? kitongoji? ama?
 
Naamini Baraza la Wawakilishi ni baraza la watu wazima, watu makini na waliopo kwa mujibu wa Katiba yetu ya JMT. Waangalie na kupima yafuatayo:
-Walishajadili na kupitisha azimio zito juu ya mafuta. Nini kimefanyika?
-Walishajadili na kupitisha mabadiliko ya KATIBA ya Zanzibar. Wakachora na mipaka. Zanzibar ikawa "NCHI". Hali ikoje ndani ya katiba ya JMT?
-Katiba ya JMT bado inamtambua Waziri Kiongozi sio hawa makamu wawili bandia wa Rais wa Zanzibar. Barubaru na Jussa mnasemaje?
-Sasa mnalianzisha hili la mipaka ya bahari. Mtafika nalo wapi?
 
Ndugu barubaru,
100% it's none of ur shit business! umekuwa ukijiita kuwa ni raia wa oman, sasa mambo ya Tanzania yanakuhusu nini wewe? we don't need any of ur garbage opinion, we know exactly that shallow minded like you,jussa and the like r trying to instigate something and you always seem to be against the prosperity of our nation, what an advice can a cockroach give to a butterfly!? feed on filthy shit!? NO HELL NO, a butterfly feeds on succulent flowers! it should stick firmly in ur pale mind now and forever that TZ issues are none of oman issues!
Hapo kwenye red, waziri ameomba kuongeza mipaka ya bahari na si ardhi, huko kwenu oman sijui mnatofautishaje kati ya ardhi na bahari!? na kama katiba inasema ni suala ardhi(zanzibar) tu kuwa si la muungano bila kutaja bahari basi hapo ujue waziri ametumia loophole na hivyo hana makosa!
Nakutakia siku njema barubaru bin waruwaru!

Hivi wewe ulikuwa hujui kuwa zanzibar bado iko mikononi mwa Oman? Kweli umelala wewe. Hizi kelele zoote ni kutaka kuvunja muungano ili warudi kwa mfalme wa Oman. Wakivunja muungano basi ujue miaka kumi mbele Tanganyika inakwenda Zanzibar kuomba msaada.
 
kama unalijua Je unajuwa mamlaka na madaraka yao ikiwemo pamoja na mipaka ya madaraka na mamlaka yao? Tueleze basi sio tu kusema unajua kumbe wahitahi darsa.

Asiyetambua mamlaka ya Rais wa Muungano ni Padre Slaa
alikataa matokeo na kumkwepa Kikwete mpaka juzi alipokimbilia chai pale ikulu kwa aibu kubwa na fedheha.

Lakin pia elewa mimi nasimamia Katiba ya Muungano wenu ambao Padre anaukana na Katiba ile ya Znz na ndipo hoja zangu zinaposimama.

Wewe tunajuwa unaabudu wazungu na sababu zinajulikana sio siri. Kumbuka kwetu wazungu tunawadharau na kuwatuma kama vibarua tu japo kwako ni mabwana.



Maada umeanzisha mwenyewe sasa unataka kuikimbia kijanja kwa kuanzisha mijadala tofauti na mada.Asiyejua maana haambiwi maana .
 
Barubaru, Katiba ya Zanzibar ipo kwa sababu Katiba ya Muungano imesema "kutakuwa na Katiba ya Zanzibar". Katiba ya Zanzibar haipo nje ya Katiba Ya Muungano. Kati ya Katiba hizo mbili linalotenguka ni lile linalopingana na Katiba ya Muungano linatenguka. Katiba ya Muungano ikipingana na ya Zanzibar, ya muungano haitenguki ni ya Zanzibar ndio inatenguka. Binafsi hata nikiona Katiba ya Zanzibar inasema "Zanzibar ni nchi" kwangu haina maana yoyote kwa sababu Katiba ya Muungano inasema "Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano!"! Hakuna nchi mbili ipo nchi moja!


Watu hawataki kuamini kuwa Zanzibar siyo nchi; nadhani huu ni ujumbe ambao inabidi tuurudie ili ueleweke. Zanzibar iliacha kuwa nchi ilipoungana na Tanganyika kuunda TAnzania. Ilichoachiwa ni kuwa na serikali yake ambayo ni sawa na serikali ya State of Michigan au New York! True, watu wa New York wanajiita New Yorkers, wana GAvana wao, polisi wao, sheria zao bunge lao n.k lakini ni state only ndani ya US nje ya US tunajua kuna nchi moja tu inaitwa United States of America. Na ni Federal Gvt inayohusika na mipaka ya maji. Mamlaka ya karibu states zote yanaishia pale ardhi inapogusa maji na mamlaka ya federal yanaanzia pale pale!


Ami Barubaru hebu muonee huruma huyu mzee,toka jana amededicate muda wake wote kukupa darsa ili na wewe ukawafundishe wenzako huko ni wapi mnakosea lakini umekataa kujifunza kwa makusudi sheikh,elimu tumeambiwa tuitafute popote hata kama ni uchina tufike kuelimika sasa ami unaipata hapo hapo ukiwa umekaa tena bure bado unachagua kubaki maamuma,kumbe ilmu ni sunna ami na sunna ni kitu chochote alichofanya mtume mohammad SAW,iqra bwana tusonge mbele na mengine achana na wanasiasa,we unaamini kweli maalim seif alikua hajui kinachoendelea kweli ilhali na waziri wake kamtoa kusafiri akitumia pesa za walipa kodi,unadhani alitoroka kazini kwenda UN bila bosi maalim seif kujua sheikh?haifai hivyo.
 
Barubaru ili usiendelee kujichanganya na kuchanganya watu kama anavyofanya mpwao Jussa kila mara anza na KATIBA ya JMT halafu kasome hiyo nyingine. Mnataka kulitumia vibaya BLW. Mambo yanayogusa JMT yana katiba moja tu. Hili la mipaka ni mojawapo.

Ndio maana nikakwambia usome katiba kabla kuleta hoja zako.

Kumbuka kuwa katika mkataba wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar suala la ardhi na makaazi halipo. Kwa maana nyingine suala hilo lipo nje ya Muungano na hili ndilo linalopelekea kuwe na waziri Znz wa Ardhi na makaazi ambaye ni Mh Ali Juma Shamuhuna na Waziri wa Ardhi wa makazi wa Muungano ni Prof Tibaijuka.

Sasa ni vizuri urejee kwenye katiba ya Muungano uone mipaka yao ya kazi.

Kwa kukusaidia kidogo imebainishwa wazi kutoka katika katiba ya muungano imesema hivi. Kuwa atashughulikia mambo yate ya Tanganyika (katiba wamesema Tz Bara) na yale yasiyokuwa ya muungano . Na wa Znz atashughulikia mambo yote ya Zanzibar.

Je wajua kuwa Znz ni nchi. Soma katiba ya Znz inayonena hivi.

Na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibari ya Mwaka 1984 kama ilivyorekebishwa mwaka 2009:
ibara ya 3 na 4
1. "Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa
vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari
yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar"


 
Watu hawataki kuamini kuwa Zanzibar siyo nchi; nadhani huu ni ujumbe ambao inabidi tuurudie ili ueleweke. Zanzibar iliacha kuwa nchi ilipoungana na Tanganyika kuunda TAnzania. Ilichoachiwa ni kuwa na serikali yake ambayo ni sawa na serikali ya State of Michigan au New York! True, watu wa New York wanajiita New Yorkers, wana GAvana wao, polisi wao, sheria zao bunge lao n.k lakini ni state only ndani ya US nje ya US tunajua kuna nchi moja tu inaitwa United States of America. Na ni Federal Gvt inayohusika na mipaka ya maji. Mamlaka ya karibu states zote yanaishia pale ardhi inapogusa maji na mamlaka ya federal yanaanzia pale pale!
Mwanakijiji,
Hili Waziri Mkuu wetu aliwahi kuulizwa na Mh Hamad ndani ya Bunge la JMT. Akalijibu vizuri KIKATIBA. Siku chache baadae Rais wetu alinukuliwa akilijibu hovyohovyo tu kuwa Zanzibar ni nchi ndani ya Muungano. Jibu hili likawapa kiburi hawa jamaa wakaenda kufanya marekebisho batili kwenye katiba yao. Wamezaliwa akina Jussa sasa. Ipo siku tutamtaka JMK aseme kama anailinda na kuitetea KATIBA alioapa kufanya hivo.
 
Hilo aliwezekani hata kidogo. Kwani Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na sio KIKATIBA. Kuna mambo apo nje ya mkataba wa Muungano likiwemo hili la ardhi na makazi.

Sasa unapozungumzia maslahi ya eneo la milki ya arrdhi ni lazima uziusishe pande zote mbili kwani hili si suala la muungano. Alichofanya Tibaijuka ni ubabe kitu ambacho hakikubaliki. Ni mawili tu yanatakiwa hapo ima a withdraw hayo maombi na kuanza mchakato mpya kama nchi zote mbili zitakubaliana au kuanisha kila nchi itanufaika vipi in terms of eneo hilo.

kama OIC ilizimwa na Muungano kwanini na hili lisizimwe.

Tibaijuka amechamke lazima ajiuzuru tu hakuna mjadala.


kwa ccm kuifanya zenji mkoa inawezekana maana kama watu wanaweza kuuza viti vyao vya urais walivyoshinda wanashindwaje kupewa hela wakae kimya.
 
Mwanakijiji,
Hili Waziri Mkuu wetu aliwahi kuulizwa na Mh Hamad ndani ya Bunge la JMT. Akalijibu vizuri KIKATIBA. Siku chache baadae Rais wetu alinukuliwa akilijibu hovyohovyo tu kuwa Zanzibar ni nchi ndani ya Muungano. Jibu hili likawapa kiburi hawa jamaa wakaenda kufanya marekebisho batili kwenye katiba yao. Wamezaliwa akina Jussa sasa. Ipo siku tutamtaka JMK aseme kama anailinda na kuitetea KATIBA alioapa kufanya hivo.

Jamani, jamani - kwahiyo usemalo wewe zanzibar sio nchi? Ni kitu gani sasa - tafadhali naomba jina lake tu - kamkoa, kijiji, kitongoji? Maana kama tunauwezo wa kusema sio nchi basi tuwe na uwezo wa kusema inaitwaje?
 
natamani ningekuwa rais ningeifanya zenj mkoa na hao vimbelembele kama jusa ningewarudisha kwao uaharabuni, hawa ndio wanaotududisha nyuima. Tanahitaji raisi mbabe ndio tuendelee. La sivyo hatutafika mahali. Huyu jussa ni ni mtu hatari na si mzalendo kabisa ni mamluki

If this is the right time to wage war in the land of peace, it's the time. Everyone was ready and now Tanzania will fall apart.
 
Back
Top Bottom