Naomba niweke wazi mipaka na nchi yetu kama ilivyoainishwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977.
1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.
1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
Na kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibari ya Mwaka 1984 kama ilivyorekebishwa mwaka 2009:
1. "Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la Visiwa
vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka na bahari
yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar"
Kwa tafsiri ya kisheria ni kuwa eneo la Zanzibar ni kama lile lililokuwepo kabla ya kuungana (1964), yaani maili 12 za majini kutoka ufukweni mwake. Na kwamba haina haki ya bahari kuu
na eneo la EEZ maili 200 kutoka ufukweni, kwani mataifa yanayopakana na bahari yameipata mwaka 1982 wakati Makubaliano ya Sheria za Bahari yalipofikiwa.
Ni vizuri watu kama wakina Jussa wafikirie vizuri kabla ya kuzungumza masuala kama hayo. Ni lazima ikumbukwe kuwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa Zanzibar si nchi kwani nchi hiyo hii ndani ya JMT ambaye ni mwananchama wa Umoja wa Mataifa na mwenye haki ya kuomba haki na upendeleo wa Makubaliano ya Sheria za Bahari ya Mwaka 1982.