Prof. Lipumba: Rais Samia Kadanganywa na Kikosi kazi cha Demokrasia, hatukukubaliana vile

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ameoneshwa kusikitishwa na baadhi ya masuala yaliyowasilishwa na Kikosi Kazi cha kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa Nchini kinachoongozwa na Mwenyekiti Prof. Rwekaza Mukandala kwa kueleza kuwa baadhi ya masuala hayo yaliyowasilishwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan na kupitia kwake kwa Umma si miongoni mwa yale waliyokubaliana kwenye mkutano wa Baraza la vyama vya siasa uliofanyika Jijini Dodoma

Akizungumza na Wanahabari kwenye makao makuu ya Ofisi za Chama hicho Jijini Dar Es Salaam Prof.Lipumba amefafanua kuwa kwenye Mkutano huo ambao ndio uliopelekea kuundwa kwa Kikosi Kazi hicho hakutokea Mjumbe yeyote aliyependekeza kuwa mchakato wa Katiba mpya ufanyike baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, hivyo ameeleza kuwa ameshangazwa kusikia Prof.Mukandala na Kikosi cahe wanawasilisha jambo ambalo ni kinyume na makubaliano ya Wajumbe wa Mkutano huo

Mwenyekiti huyo wa CUF amewataka Wajumbe wa Kikosi Kazi hicho kufanya kazi wanayopaswa kufanywa badala ya kuanza kugeuka na kufikiri wanamtumikia Rais au Serikali
IMG-20220328-WA0026.jpg
IMG-20220328-WA0027.jpg
IMG-20220328-WA0028.jpg
IMG-20220328-WA0025.jpg
IMG-20220328-WA0029.jpg
IMG-20220328-WA0023.jpg
 
Kitu kikubwa ni kuwa wanasiasa wanakula kila mema tunaoumia nini sisi wananchi wao hata hawajali
 
Mzee wa kupepesa ulimi kama Nyoka mbele ya yai viza...

Huyu nae ni mtu wa hovyo sana mbele ya pesa... amejaa tamaa isiyomithilika hapo mate yanamtoka kwa miposho wanayolamba akina Zitto si kingine.

Hopeless!!
 
Huyo ni propesa. Mvuto umekwisha. Ruzuku imemwishia. Sasa apige tu kelele. Labda mwendazake na siro watamsaidia.
 
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa Prof. Ibrahim Haruna Lipumba ameoneshwa kusikitishwa na baadhi ya masuala yaliyowasilishwa na Kikosi Kazi cha kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia...
Huyu huwa ni kigeugeu, inawezekana amehofia kupigwa chamani kwake baada ya kupeleka mapendekezo yasiyo na tija
 
Amesikika Profesa Lipumba mjumbe aliyehudhuria mkutano wa TCD Dodoma kikamilifu.

IMG_20220328_181039_990.jpg


Hajui kabisa wazo hili la katiba mpya baada ya 2025 liliasisiwa wapi.

Ni wazi kuwa Profesa Mukandala, Zitto na wenzake wameamua kutucheza shere.

Watu hawa hawapaswi kuendekezwa kwani nchi hii si yao peke yao.

Kwanini isiwe kuwa wamedhamiria kupenyeza maslahi yao binafsi kwenye suala hili?

Watu hawa wanaaminika vipi tena kutokea hapa?
 
Back
Top Bottom