Prof Haroub Othman na Shivji ni wachochezi?

This is ridiculous isn't it?- kwenye Majukwaa tunaambiwa na Waunda Azimio, "usawa", "usawa", then many years later wanatuambia, "si usawa kwa maana vidole havilingani".

You ask me what did I find on my own, I just find that we were duped!, a kind of Animal farm where some animals are more equal than others. this kind of flip flop is destined to fail and this is what happened exactly few years later.

ngoja sasa nikuwekee baadhi ya masharti ya Azimio la arusha then utaona kwamba Azimio la Arusha lilihitaji modification katika kipengele cha Maadili ya Viongozi...................................

Naomba nianze na suala la Azimio La Arusha na Miiko ya Uongozi, then baadae nitakurudia na suala juu ya Azimio la Arusha na Equality/Usawa. Suala la usawa naona kama vile limeanza kuchukua mkondo wa Legal Interpretation Vis-a-Vis Social Interpretation.

Kama nilivyosema awali, historia inatuonyesha wazi kwamba, ni jambo moja tu ndilo linalowakera wakubwa juu ya Azimio la Arusha – na suala hilo halina uhusiano wowote na hisia zao kuhusu jinsi gani Azimio la Arusha linaweza au haliwezi kumsaidia mkulima/maskini (the 70% of the population). Jambo la msingi lililowanyima wakubwa usingizi juu ya Azimio La Arusha, sio jingine bali lile la Maadili ya Uongozi/Leadership Code, hakuna jingine. Je, Gamba la Nyoka, unalipinga hili?

Katika kikao cha CCM-NEC Zanzibar (1992) kilichoua Azimio la Arusha na kuzaa Azimio la Zanzibar, agenda kubwa/iliyo dominate kikao kile ilikuwa Maadili ya Uongozi na jinsi gani ya kutupilia mbalu suala hilo ili wakubwa wafaidi matunda ya soko huria, huku wananchi wakitapa tapa na massive unemployment and mushrooming of informal sector. Kwani, masuala mengine ndani ya Azimio la Arusha walisha yaua kimya kimya siku nyingi sana (tangia 1986), bila hata ya kuwaandaa au kuwapa wananchi elimu ya uraia juu ya mabadiliko yaliyokuwa yanakuja. Na mpaka leo hii, maskini wamebaki wameduwaa, na bado hawajaombwa msamaha. Isitoshe, kikao cha CCM – NEC 1992, kilifanyika wakati consensus among watawala tayari ilikuwa kamba - Ujamaa umeshindwa, kwani tayari walikuwa wanatekeleza sera za Soko Huria since 1986.

Kilichobakia lilikuwa namna ya kuhalalisha Ufisadi, namna ya kuiba mali ya umma kwa urahisi, kwani CCM (kikiwa chama pekee wakati huo), kilikuwa kinapiga marufuku wizi wa mali ya umma. Kwahiyo, RUKSA ya kuachia mabepari wa nje, wakwapue mali ya umma ilikuwa inawanyima watawala wetu raha, sio kwasababu wananchi walikuwa wanateseka, bali kwasababu, kanuni za Chama hazikuwaruhusu watawala na wao wafaidike na soko huria holela. Isitoshe, baba mzazi wa Azimio la Arusha Mwalimu Nyerere, alikuwa hai bado, sasa wangefaidi vipi? Ndipo wakapata njia, na kumzunguka Mwalimu, kwani hata kwenye msiba wa mtoto wa Mwalimu - Azimio La Arusha, kule Zanzibar, Mzazi huyo, hakualikwa ashiriki kuomboleza msiba ule.

Gamba La Nyoka, kama kulikuwa na justification ya kuliua Azimio La Arusha, in the eyes of the poor, kwanini Mwalimu hakushirikishwa?

Naomba maoni yako kwenye hili. Otherwise, mimi binafsi, mtazamo wangu ni kwamba, pengine Mwalimu angeongea yale yale aliyo ongea mwaka 1987 (see my original post), na pengine kupelekea mzee wa watu kuitwa Mchochezi. Gamba LA Nyoka, ni katika miaka hiyo hiyo (in early 1990s), kipindi kilichopeleka ufisadi to the next level, chota chota ya wazi wazi ya rasilimali za UMMA na mabepari wa nje, wakishirikiana na mafisadi wa humu ndani, IN THE NAME OF SOKO HURIA, Tanzania tukafikia kiwango cha kuwa nchi ya tatu kutoka mwisho kwa umaskini by 1993-4, mbele tu ya Somalia na Afghanistan. GDP PER CAPITA yetu ilishuka below $100, from $310 IN 1985. Tumeshalizungumzia ili kwamba Kiongozi (1993-4), Kumlaumu Mwalimu (1985) ni Sawa na Obama (2012) kumlaumu Bush (2008), KITU AMBACHO HATA OBAMA HAWEZI THUBUTU KWANI ITAKUWA KWAHERI FOR HIM!

Kuna makala moja by Irene and Roland Brown that was published in early 1970s, titled "Approach to Rural Mass Poverty", ambayo inatupa picha halisi kuhusu yaliyojiri katika kikao ambacho Azimio La Arusha lilikuwa tabled mbele ya viongozi wa TANU na Serikali Yake. Kifuatacho below ni a proof kwamba lengo kuu la Azimio La Zanzibar halikuwa kuwaokoa wananchi kutoka kwenye Umaskini, bali kuwaokoa viongozi kutoka kwenye Umaskini kwa tiketi halali ya ufisadi. Kwani, unlike before, sasa Azimio la Zanzibar lilitoa RUKSA kwa wao kujilimbikizia, bila mipaka/muongozo/masharti.

According to makala ya Irene and Roland Brown, Viongozi wengi sana wa TANU in 1967, walilipinga Azimio la Arusha Mbele ya Mwalimu kwa hoja zifuatzo: (Irene and Roland Brown, pp 13-14):

["A Politician", they said, "has no security. Today he is a Minister, Tomorrow he is not, today he is an MP, after five years he is not, (or may be not), today he is a regional or area commissioner, tomorrow he is unemployed, today he is chairman of the region, district, or Town and tomorrow someone else may be elected in his or her place. Why does the Arusha Declaration prevent such leaders from providing by other means, for their future?"]

Mwalimu Nyerere Responded as follows:

"Leaders ask this question more than any other and it is the most serious and dangerous question of all. Personal difficulties of the leaders are interest to the people only to the extent that they might be of such a degree that the leader cannot do his work properly. It is this consideration which causes some leaders to be paid while they carry responsibility. Leaders often forget this, and especially do they tend to forget the purposes of leadership in a socialist Tanzania: it is a good thing if the Arusha Declaration and its leadership requirements act as a constant reminder."

Mwalimu Nyerere went on to Ask:

["Which is the politician who sent to the people at election time and asked them to elect him so that he could provide for his future? Which Area or Regional Commissioner or other TANU worker got his job by saying he wanted to improve his personal position and get security for his future? Whenever a person seeks political work, whether it is through election or by appointment, he says he wants the opportunity to serve the people, to guard their interest and further their aspirations. What right has such a person, once he has the appointment he sought on this basis, use his responsibility for his own betterment? This question is absolutely central to the Arusha Declaration and to the whole purpose of TANU and the independent Tanzania."]

Gamba La Nyoka, naomba kwa sasa nikuache na maswali mawili:

Kwanza, Gamba la Nyoka, kwa mtiririko wa hoja zako, ni wazi kwamba iwapo wewe ungekuwa ni mmoja ya viongozi mwaka 1967, ungekuwa na msimamo sawa na hao waheshimiwa hapo juu. Now, let us assume ulikuwa kwenye chumba kile, and you had an opportunity kumjibu Mwalimu kwa hoja, ningependa sana kujua ungemjibu nini Mwalimu. Jibu lako litatusaidia sana to shed more light katika huu mjadala on Azimio La Arusha.

Na pili, Gamba La Nyoka, tuseme unakutana na wakulima katika kijiji kimoja Tanzania, ambao soko huria limewacha hoi bin taaban, suala la soko huria kuwacha 70% ya watanzania HOI sidhani kama lina mjadala; Sasa, katika mjadala wako na wakulima/maskini hawa wa watu, juu ya hali zao ki-uchumi, ki-jamii n.k, mmoja wao anatoa hoja kwamba Azimio La Arusha (1967 – 1992) lilikuwa ni la Wananchi, na Azimio la Zanzibar (1992 – 2011) ni la Watawala, utamjibu nini? Jibu hilo nalo litatusaidia sana to shed more light katika huu mjadala wetu on Azimio la Arusha.
 
Ha ha ha! na wewe unayemtetea unafanya hivyo kwasababu za kidini au sivyo?? watu bana!

Mimi nilishakwambia mara nyingi kwamba tatizo la nyerere alikuwa MBOVU period

kwangu mimi ujamaa, ubepari (sera yeyote) siyo tatizo, tatizo ni nani anayesimamia hiyo sera???

kwa hiyo nyerere tungepata faida kama angekuwa kiongozi mzuri hata kwenye ujamaa period..

Mimi mzima aisee, kwangu mimi watoto wangu na ukoo wangu nyerere siyo baba eat it..

Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa, ni Mbovu ONLY WHEN HE IS COMPARED TO HIMSELF.
 
Gamba la Nyoka,

Mkuu wangu na wewe pia...duh ama kweli wadanganyika sasa hivi wamechoka hadi kufikiria....Kwanza kabisa
Nimewahi kusema huko nyuma usijaribu kutafsiri Azimio la Arusha kisha ukalitoa makosa kwa sababu ya mazingira ya nchi nyingine bali tazama mazingira yako na ndipo utaweza kulielewa..

1. Wakati tunapata Uhuru hadi 1967 tulikuwa na wanataaluma wachache sana na hawa wote tuliwahitaji sana ktk sehemu zao za kazi. Kama tungejaribu kuruhusu hawa viongozi wafanye biashara amna kuwa na kofia mbili kwa ujumla wake wananchi wengi wangekosa huduma zinazotakiwa. Kwa hiyo tulihitaji mchango wao zaidi na kwa bahati nzuri tulifuta Ujinga kwa asilimia kubwa kabisa maradhi kama Ukoma, ndui na malaria yalikuwa karibu na kukomeshwa. Tuliweza jenga miundombinu na viwanda muhimu within 15 yrs ambavyo tumeshindwa kujenga in 27 yrs!

FACT - Baada ya kuacha AZIMIO LA ARUSHA tatizo hilo limejitokeza? - NDIYO, tena hata baada ya kuwa na wataalam wengi hata viongozi wetu wameshindwa kuzihudumia ofisi zao za kazi kwa sababu ya majukumu binafsi (biashara zao)..Kila wizara yetu ya huduma iko nyuma ya utekelezaji wake kwa asilimia zaidi ya 80..

2. Confilct of Interest- Kulingana na mazingira yetu Mbunge ndiye alikuwa waziri, wabunge ndio waliku Ma CEO wa mashiirika ya UMMA na kahdlika kumbuka kwamba nguzo za uchumi zilishikwa na serikali hivyo viongozi wote wa ngazi za juu ktk sehemu hizi walikuwa viongozi wa ndani ya chama pia..Ukiwapa nafasi viongozi hawa kuwa na biashara nje ya kazi zao lazima kutatokea matatizo ya Conflict of interest...Hatukuwa na sokohuria ambalo hawa viongozi wangenunua hisa na kuwa nje ya uatwala wa haya mashirika,

FACT - Je baada ya kuacha Azimio la Arusha imetokea Hivyo.. NDIYO.. Leo hii waziri wa Utalii ana shirika la Utalii kama sii yeye mkewe au mwanaye ana tender zote za wageni zinapitia kwake, aidha waziri au CEO umenunua share ktk mradi wa wizara yake hivyo tender yoyote inayopatikana huisukuma ktk kampuni yake hata kama hawana uwezo.Na hadi leo kuyaweka mashirika yetu katika soko huria inapigwa vita vikali na hawa viongozi kwa sababu they make huge money kwa kununua hisa ktk mashirika binafsi.

Wallstreet ina fail kwa sababu yao. Train kwenda Kigoma linadumaa kwa sababu wana malorry yao, Usafiri Dar umekwama kwa sababu wana Daladala zao yaani list ni kubwa hata huwezi kuiweka ktk ukurasa mmoja.

Hakuna sheria ama Azimio lolote linalosisitiza uchafu ufanyike! uliona wapi Azimio linalosema Ufisadi umekubaliwa bali sheria ndizo hulegezwa hivyo Ufisadi unajitokeza. Kama wakati wa Mkapa, Ujambazi ulikuwa mkubwa sana na hakuna sheria wala Azimio la kuruhusu Ujambazi..Kinachotazamwa ni sababu zipi tulizosababisha Ujambazi kupanda zinapigwa hadi unatokomea.. Katika hili la Ufisadi we are into denial kwa sababu nakumbuka vizuri wakati wa Mkapa wananchi walilia sana na Ujambazi lakini walipuuzwa hadi JK alipoingia madarakani na wakatumia nguvu kubwa sana kuuvunja lakini tatizo ni kwamba ilikuwa ni kampeni ya muda tu..
 
Katika kikao cha CCM-NEC Zanzibar (1992) kilichoua Azimio la Arusha na kuzaa Azimio la Zanzibar, agenda kubwa/iliyo dominate kikao kile ilikuwa Maadili ya Uongozi na jinsi gani ya kutupilia mbalu suala hilo ili wakubwa wafaidi matunda ya soko huria, huku wananchi wakitapa tapa na massive unemployment and mushrooming of informal sector. Kwani, masuala mengine ndani ya Azimio la Arusha walisha yaua kimya kimya siku nyingi sana (tangia 1986), bila hata ya kuwaandaa au kuwapa wananchi elimu ya uraia juu ya mabadiliko yaliyokuwa yanakuja.

Bwana Mchambuzi:
Ukweli ni kwamba Mwalimu Nyerere aliendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM mara tu alipong'atuka mwaka 1985, kwa hiyo notion ya kudai kwamba masuala mengine ya azimio la arusha waliyaua kimya kimya as if Mwalimu hakushiriki fully vikao vya Chama, mwaka 1986 si ya kweli!.

Umeniuliza kwamba ningemjibu vipi Mwalimu kuhusiana na maadili ya viongozi?- infact ningemjibu wazi kwamba, pamoja na kwamba ni kiongozi lakini nina haki ya kutumia ujuzi wangu mwingine kwa malipo halali ya kazi yangu, kisha ningemweleza wazi kwamba sioni mantiki ya mimi kutokuweza kupangisha nyumba yangu niliyoijenga kwa jasho langu mwenyewe, kwani kwa kufanya hivyo sijaiibia serikali!.

ndo maana nimeweka vipengele viwili vilivyofanyiwa mabadirisho na Azimio la Zanzibar najinukuu hapa chini, kisha naomba maoni yako kuhusiana na vipengele hivyo:

kipengele cha 4 kinasema hivi:

ASIWE NA MISHAHARA MIWILI.
Hii ilikuwa inadumaza, inakwaza mtu mwenye uwezo wa kutumikia kazi mbili kwa ufanisi kujiinua, na kutoa mchango mkubwa kwa jamii!, mathalani kuna ubaya gani daktari Bingwa/kiongozi wa idara kuwa daktari na kuwa lecturer na kisha kupokea ujira kwa kazi zake hizo mbili anazofanya?.

Azimio la Zanzibar lilikuja kuondoa discrepancies kama hizi, sasa badala ya watu kuona kwamba ni modification ya msingi kwa sababu Azimio la Arusha siyo Msahafu, wakaona kwamba eti ni kulipinga Azimio Zima, HIYO SI KWELI. bali hayo ni mabadiriko ya msingi ambayo yalibidi yafanywe kutokana na wakati.

kipengele cha Tano cha maadili ya Kiongozi kinasema hivi.
ASIWE NA NYUMBA YA KUPANGISHA
Hii pia ilikuwa ni kikwazo na unnecessary, kama mimi ni mkulima na mfanyakazi nina kipato halali kwa nini nisiweze kuwa na nyumba na nikaipangisha pia?.
Je kama nina nyumba tupu, au nina nyumba ambayo siitumii yote, je siwezi kupangisha vyumba vilivyobaki?.

Bwana Mchambuzi, Msingi mwingine wa Azimio la Arusha lilikuwa ni kwamba njia zote za Uchumi zimilikiwe na Umma kupitia Serikali, sasa mimi sitaki kuingia katika mjadala wa kiitikadi, lakini ni dhahiri Serikali ili "overdo" utekelezaji wa dhana hii, kwa maana hata viwanda vidogo vidogo ilikuwa lazima vimilikiwe na Serikali, Serikali ingeruhusu uwanzishaji wa viwanda binafsi toka awali ili kutimiza lengo la kujitegemea, hata baadhi ya mashamba kama vile mkonge Serikali ilikuwa haina haja ya kuyahodhi( Nyerere alikiri kukosea katika hili).

Sera ya Soko huria aliyoiadapt Mzee Mwinyi siyo mbaya, ubaya unakuja pale aliposhindwa kuweka mechanism ya kumlinda mlaji/mtumiaji kupitia mechanism ya kuangalia bei vis-a-vis kiwango kinachokubalika kwa mfanyabiashara naye apate faida lakini si ya kupitiliza na hatimaye kumuumiza mlaji.

Lakini Kikubwa bwana Mchambuzi, ilikuwaje ikawa Rahisi kubadirisha Vipengele vya Maadili ya Uongozi kimya kimya?- Je haya maadili ya Uongozi yalipata kuwa ndani ya Katiba yetu?, je yalikuwa ni sehemu ya Sheria zetu?- Kama Mwalimu hakuyaweka hayo ndani ya Katiba na Sheria zilizotungwa na Bunge alitegemea nini?.

Narudia kusema, Azimio la Zanzibar halikuua azimio la Arusha bali lililiboresha!- Muda ulikuwa umefika wa kwenda na wakati, mambo ya Viongozi kutokuweza kupangisha Nyumba zao yalikuwa yamepitwa na wakati!, na Azimio la Zanzibar ndilo lilikifanya.
Mwalimu Nyerere mwenyewe katika maandishi yake mengi anasema wazi, yale yenye makosa mnarekebisha, mazuri mnachukua.

Sasa basi bwana Mchambuzi, mambo ya MAAZIMIO tuviachie vyama vya Siasa, mimi Si mwanachama wa Chama Chochote cha Siasa, nitachagua Chama kulingana na wakati na mazingira yangu!, nikiwa middle class naweza kufavor chama fulani, nikiwa tajiri naweza kufavor chama kingine. Cha msingi ni katiba ambayo iko fair kwa raia wote na sheria zinazo level ground kwa raia wote kuishi kwa jasho lao, Mambo ya Azimio la Arusha/ Zanzibar ni mali ya WanaCCM, kwa sababu ilikuwa ni dira yao waiongoze nchi vipi!.

Kama chama kinaona mambo ni ya Msingi basi kiyatungie sheria, au kiyaingize katika katiba kupitia bunge la Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, badala ya kubaki kama Maazimio, kwa maana katika nyakati hizi Chama hakishiki hatamu siyo kama enzi zile!
 
Bwana Mchambuzi:
Ukweli ni kwamba Mwalimu Nyerere aliendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM mara tu alipong'atuka mwaka 1985, kwa hiyo notion ya kudai kwamba masuala mengine ya azimio la arusha waliyaua kimya kimya as if Mwalimu hakushiriki fully vikao vya Chama, mwaka 1986 si ya kweli!.

Umeniuliza kwamba ningemjibu vipi Mwalimu kuhusiana na maadili ya viongozi?- infact ningemjibu wazi kwamba, pamoja na kwamba ni kiongozi lakini nina haki ya kutumia ujuzi wangu mwingine kwa malipo halali ya kazi yangu, kisha ningemweleza wazi kwamba sioni mantiki ya mimi kutokuweza kupangisha nyumba yangu niliyoijenga kwa jasho langu mwenyewe, kwani kwa kufanya hivyo sijaiibia serikali!.

ndo maana nimeweka vipengele viwili vilivyofanyiwa mabadirisho na Azimio la Zanzibar najinukuu hapa chini, kisha naomba maoni yako kuhusiana na vipengele hivyo:



Bwana Mchambuzi, Msingi mwingine wa Azimio la Arusha lilikuwa ni kwamba njia zote za Uchumi zimilikiwe na Umma kupitia Serikali, sasa mimi sitaki kuingia katika mjadala wa kiitikadi, lakini ni dhahiri Serikali ili "overdo" utekelezaji wa dhana hii, kwa maana hata viwanda vidogo vidogo ilikuwa lazima vimilikiwe na Serikali, Serikali ingeruhusu uwanzishaji wa viwanda binafsi toka awali ili kutimiza lengo la kujitegemea, hata baadhi ya mashamba kama vile mkonge Serikali ilikuwa haina haja ya kuyahodhi( Nyerere alikiri kukosea katika hili).

Sera ya Soko huria aliyoiadapt Mzee Mwinyi siyo mbaya, ubaya unakuja pale aliposhindwa kuweka mechanism ya kumlinda mlaji/mtumiaji kupitia mechanism ya kuangalia bei vis-a-vis kiwango kinachokubalika kwa mfanyabiashara naye apate faida lakini si ya kupitiliza na hatimaye kumuumiza mlaji.

Lakini Kikubwa bwana Mchambuzi, ilikuwaje ikawa Rahisi kubadirisha Vipengele vya Maadili ya Uongozi kimya kimya?- Je haya maadili ya Uongozi yalipata kuwa ndani ya Katiba yetu?, je yalikuwa ni sehemu ya Sheria zetu?- Kama Mwalimu hakuyaweka hayo ndani ya Katiba na Sheria zilizotungwa na Bunge alitegemea nini?.

Narudia kusema, Azimio la Zanzibar halikuua azimio la Arusha bali lililiboresha!- Muda ulikuwa umefika wa kwenda na wakati, mambo ya Viongozi kutokuweza kupangisha Nyumba zao yalikuwa yamepitwa na wakati!, na Azimio la Zanzibar ndilo lilikifanya.
Mwalimu Nyerere mwenyewe katika maandishi yake mengi anasema wazi, yale yenye makosa mnarekebisha, mazuri mnachukua.

Sasa basi bwana Mchambuzi, mambo ya MAAZIMIO tuviachie vyama vya Siasa, mimi Si mwanachama wa Chama Chochote cha Siasa, nitachagua Chama kulingana na wakati na mazingira yangu!, nikiwa middle class naweza kufavor chama fulani, nikiwa tajiri naweza kufavor chama kingine. Cha msingi ni katiba ambayo iko fair kwa raia wote na sheria zinazo level ground kwa raia wote kuishi kwa jasho lao, Mambo ya Azimio la Arusha/ Zanzibar ni mali ya WanaCCM, kwa sababu ilikuwa ni dira yao waiongoze nchi vipi!.

Kama chama kinaona mambo ni ya Msingi basi kiyatungie sheria, au kiyaingize katika katiba kupitia bunge la Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, badala ya kubaki kama Maazimio, kwa maana katika nyakati hizi Chama hakishiki hatamu siyo kama enzi zile!
Nani amekwambia hatukuwa na viwanda vidogo vidogo vya watu binafsi?
 
Kiranga, haujaelewa dhumuni la mada yangu; Jasusi na wengine wamenisoma vizuri; Jasusi hapo juu has inferred mtazamo wangu mia kwa mia;
wakati mwingine inabidi tu uvumilie ujinga wa mwenzio. Utadhani mtu hakufundishwa fasihi bwana, loh!
 
Weren't we told that Ujamaa refers to equality?- what equality were we talking about then?

The Arusha Declaration refered to relative equality among the citizenry; the difference in income between wananchi had to be narrowed progressively. siku hizi tofauti ya kipato kati ya walionacho[ matajiri] na wasionacho[masikini] ni astronomical !! Kuna vijana kwa sababu ya kuwa ukoo wa watawala wamekwisha kuwa matajiri wa kutupa hardly mwaka mmoja baada ya kuhitimu masomo wakati wenzao waliokuwa nao na ambao walikuwa na akili kuliko wao darasani bado wanatafuta ajira/hawana kipato!!This is just a hint of how lopsided the income distribution is in this country.
 
Ha ha ha! na wewe unayemtetea unafanya hivyo kwasababu za kidini au sivyo?? watu bana!

Mimi nilishakwambia mara nyingi kwamba tatizo la nyerere alikuwa MBOVU period

kwangu mimi ujamaa, ubepari (sera yeyote) siyo tatizo, tatizo ni nani anayesimamia hiyo sera???

kwa hiyo nyerere tungepata faida kama angekuwa kiongozi mzuri hata kwenye ujamaa period..

Mimi mzima aisee, kwangu mimi watoto wangu na ukoo wangu nyerere siyo baba eat it..

Topical
Upo usipotee; hivi sasa hivi tunafuata sera gani? Kama zipo vipi masimamizi anazisimamia vizuri? Usikonde na Mwalimu Nyerere wewe mwite mjomba wa Taifa inatosha ukiliona hilo gumu mwite hayati au marehemu Mwalimu Nyerere ama vipi usiwe diktekta waachie watoto wakikua wataamua wenyewe.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Mkuu wangu usituharibie mjadala tafadhali..... Ebu nikuulize wewe sifa za mwenyezi Mungu ni zipi? majina 99 kwa uchache wa sifa hizi - wewe binadamu huna? na kwa nini iwe wewe na sio viumbe wengine... Mkuu usijaribu kuipinga Injili pasipo kuelewa maana achana na tafsiri za watu ila jaribu kuilewa Injil ilikuwa na maana gani kulingana na Kuran..
Turudi kwenye mada yetu tafadhali..

Mkandara
Topical mkubali tu; huyo ni active board member Bora Haram (T) Limited

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Gamba La Nyoka, tuseme unakutana na wakulima katika kijiji kimoja Tanzania, ambao soko huria limewacha hoi bin taaban, suala la soko huria kuwacha 70% ya watanzania HOI sidhani kama lina mjadala; Sasa, katika mjadala wako na wakulima/maskini hawa wa watu, juu ya hali zao ki-uchumi, ki-jamii n.k, mmoja wao anatoa hoja kwamba Azimio La Arusha (1967 – 1992) lilikuwa ni la Wananchi, na Azimio la Zanzibar (1992 – 2011) ni la Watawala, utamjibu nini? Jibu hilo nalo litatusaidia sana to shed more light katika huu mjadala wetu on Azimio la Arusha.

Hilo ni swali ambalo haujanipatia majibu bado. Naomba ukipata muda, unirudie na hilo.

Vinginevyo, upo sahihi kwamba mjadala unaoegemea itikadi za vyama hauwezi kuwa na tija. Ninachojaribu jadili lakini ni suala ambalo kwa mtazamo wangu linagusa taifa kwa ujumla, hata kama mwanzilishi wake alikuwa TANU. Nitajitahidi kuepuka mijadala ya kiitikadi, na badala yake kuelekeza nguvu zaidi kwenye masuala yenye maslahi ya taifa. Niwie radhi napoenda kinyume.

Naomba nianze kwa kujibu hoja ifuatayo, halafu nitakurudia kwenye hoja zako nyingine baadae kidogo, bila ya kusahau suala la Equality and the Declaration, kama nilivyoahidi.

Umeniuliza kwamba ningemjibu vipi Mwalimu kuhusiana na maadili ya viongozi?- infact ningemjibu wazi kwamba, pamoja na kwamba ni kiongozi lakini nina haki ya kutumia ujuzi wangu mwingine kwa malipo halali ya kazi yangu, kisha ningemweleza wazi kwamba sioni mantiki ya mimi kutokuweza kupangisha nyumba yangu niliyoijenga kwa jasho langu mwenyewe, kwani kwa kufanya hivyo sijaiibia serikali!.

ndo maana nimeweka vipengele viwili vilivyofanyiwa mabadirisho na Azimio la Zanzibar najinukuu hapa chini, kisha naomba maoni yako kuhusiana na vipengele hivyo...

Hoja yako kwamba mwaka 1967, kama kiongozi wa taifa huru lenye miaka 6 tu, una haki ya kutumia ujuzi wako mwingine mahali popote, popote wapi? katika uchumi upi Gamba La Nyoka? Soko lipi wakati 95% ya nchi ni vijiji/wakulima? au una maanisha bwana shamba binafsi? Unazijua takwimu za uchumi za aliotuachia Mkoloni zilikuwaje Gamba La Nyoka? Social conditions pia?

Sina uhakika kama nitakuw asahihi kutamka kwamba, umejisahau kabisa kwamba taifa lilikuwa ndio kwanza jipya kwa kila hali, hapakuwa na incentives zozote za maana in the economy (tofauti na Kenya kwa mfano), to exploit other opportunities in any meaningful way – mfano, aggregate demand/purchasing power, however we should put it, ni kama haikuwepo;

In 1967, population ilikuwa around 9 million, with 95% (about 8.5 million Tanganyikans) vijijini/wakulima; and only 5% (about 50,000) of the population as urbanites; Mbali ya hilo, kulikuwa na uhaba wa wataalam – engineers, walimu, madaktari, almost an absence of a tax base, thereby mapato ya nchi yakiendelea kutegemea kumkamua wakulima (95%) of the population, kwa mtindo ule ule wa producing what we don't consume (e.g. pamba, mkonge..) and consume what we don't produce (e.g. skuna, kaniki…), a system inherited from mkoloni, only 6 years before, huku watanganyika 8.5 million wakiwa bado na kumbukumbu za ahadi za Mwalimu juu ya nini atawafanyia iwapo watapambana kumwondoa mkoloni - ajira, huduma za kijamii…; hata kama Mwalimu alilemewa na huduma hizi, na mashirika ya umma yasio na ufanisi – there is one thing that he did – Hakuvunja ahadi yake kwa watanganyika ya huduma bure za afya na ajira kwa wengi, suala ambalo hata chama makini kama CHADEMA kimeliona in 2010;

Gamba La Nyoka, naomba usisahau hii takwimu - katika watanganyika takriban milioni tisa (9) in total (1967), watanganyika kama 8,500,000 wapo vijijini/wakulima, only 50,000 ndio wapo mijini, baadhi yao ndio hao viongozi wa TANU ambao wamebahatika to occupy ajira zilizoachwa na mkoloni, majumba ya mkoloni, lakini wakitegemea the rural sector - the 8,500,000 vijijini ndio wawalishe chakula (food crops production), lakini pia vilevile mazao yao ya kilimo ndio yalipatie fedha za kigeni kunulia magari ya kifahari ya watawala, na kuwalipa posho na mishahara watawala;

Gamba la Nyoka, hivi kweli, ukiwa pale mezani na Mwalimu (1967) kumpinga on his Leadership code embedded in the Azimio La Arusha, unakuwa na uelewa wa hali halisi kweli - picha halisi ya Tanganyika in a socio-economic context, in 1967 ipo vipi na kama inaweza accommodate all that; Kwa kweli, in my humble opinion, wale wote wanaoshindwa kuelewa hili hata baada ya kui digest mara kadhaa, hakika wana haki ya kumwona Mwalimu alikuwa na matatizo kimaamuzi in 1967, na kwamba alilipoteza taifa hili, taifa ambalo kiuchumi leo hii halina tofauti na wenzetu walioamua kuingia soko huria 1962 (sio ujamaa kama sisi), moja kwa moja kama Kenya. Human Development Index Kenya puts us on the same league na wao; Hii haitoshi kutuambia kwamba tatizo letu sote waafrika sio Ujama au Ubepari bali ni the unfair integration of our societies into the global capitalist system? Ni vigumu kuelewa kwanini bado kuna watanzania wanaomlaumu Nyerere;

Otherwise, ni dhahiri kwamba kwa wakati ule (1967), hata kama viongozi, wangepewa haki ya kujitafutia riziki zao as you rightly put it Gamba La Nyoka, uchumi and the market for that haukuwepo, sana sana viongozi hao wangeishia tu kuiba mali ya umma. Akina kina Charles Njonjo pale Kenya, walikuwa wanawafanya watawala wetu Tanganyika, wadondokwe na mate kwa kutamani na wao wafaidi MATUNDA YA UHURU kama wenzao Kenya. Gamba la Nyoka, in 1967, matunda ya uhuru is for whom, the 50,000 Tanganyikans? The 8,500,000…?

Mimi nina imani kabisa kwamba hatua ya Mwalimu wa done on justified grounds; Kwani hata mwaka 1962, mwaka mmoja tu baada ya uhuru, aliwaondolea uvivu viongozi wenzake, kwa kuwapa maneno yafuatayo – TANU NA RAIA, 1962:

["Wakoloni walipokuwa hapa walipanga mishahara bila ya kujali uwezo wetu kuilipa mishahara hiyo, na bila kuilinganisha mishahara hiyo na mapato ya watu wetu. Lakini wao ilikuwa ni ada yao kufanya hivyo. Serikali ya wageni haiwezi kujali maisha ya raia. Serikali ya ilikuwa ni serikali ya ubwana na ufahari; na walijitimizia ubwana wao na fahari yao, bila ya kujali uwezo wa watu wetu wa kugharamia ubwana huo na fahari hiyo.

Lakini baadhi yetu tulikuwa hatutambui jambo hilo. Waafrika wengi tulikuwa tumekwisha kusahau kwamba mzigo ule wa ubwana na ufahari ni mzito mno na watu wetu hawawezi kuubeba. Kilichokuwa kikituuma ni kwamba ubwana ule na fahari ile wazungu waligawana wenyewe tu, bila kutugawia na sisi pia; baadhi yetu hatukuwa tunadai uhuru ili uwapunguzie watu wetu mzigo huu wa ubwana na ufahari, bali tama yetu ilikuwa ni kukalia viti vile vya ubwana na ufahari. Tamaa yetu haikuwa kushika vyeo tu, vilivyokuwa vimeshikwa na wazungu hapo zamani, tulitaka na mishahara pia iliyokuwa ikifuatana na vyeo bila kujali kama watu wetu wanaweza kulipa mishahara hiyo, na bila kujali maisha ya watu."]


JKN, Tanu na Raia, 1962.
********

Ntakurudia juu ya hoja zako nyingine.
 
Mchambuzi,
Shukran mkuu wee fimbo yao....Yes, a powerful speech by Nyerere mwaka gani huo 1962... daaaah! Mungu amweke mahala pema peponi yaani aliona mbali sana... leo yanajirudia tu...
 
Mchambuzi,
Shukran mkuu wee fimbo yao....Yes, a powerful speech by Nyerere mwaka gani huo 1962... daaaah! Mungu amweke mahala pema peponi yaani aliona mbali sana... leo yanajirudia tu...

Ni kweli yanajirudia Mkandara, na Kitabu cha TANU NA RAIA ni cha mwaka 1962; Ukitazama, hata suala la posho za wabunge na jinsi gani kina Zitto na wengine wanaliona ni mzigo, ni suala mwalimu alishaona kwamba - UCHUMI WETU ambao ni wa watanzania walio vijijini, hauwezi beba mzigo huo; Mwalimu katika ukurasa wa 6 - 8, katika kitabu hicho analifafanua vizuri sana suala zima la mishahara na posho kwa viongozi wa serikali, kwa hoja zile zile ambazo leo hii wanasiasa wetu katika soko huria wanalijadili;
 
............................
Lakini baadhi yetu tulikuwa hatutambui jambo hilo. Waafrika wengi tulikuwa tumekwisha kusahau kwamba mzigo ule wa ubwana na ufahari ni mzito mno na watu wetu hawawezi kuubeba. Kilichokuwa kikituuma ni kwamba ubwana ule na fahari ile wazungu waligawana wenyewe tu, bila kutugawia na sisi pia; baadhi yetu hatukuwa tunadai uhuru ili uwapunguzie watu wetu mzigo huu wa ubwana na ufahari, bali tama yetu ilikuwa ni kukalia viti vile vya ubwana na ufahari. Tamaa yetu haikuwa kushika vyeo tu, vilivyokuwa vimeshikwa na wazungu hapo zamani, tulitaka na mishahara pia iliyokuwa ikifuatana na vyeo bila kujali kama watu wetu wanaweza kulipa mishahara hiyo, na bila kujali maisha ya watu."]


JKN, Tanu na Raia, 1962.
********

Ntakurudia juu ya hoja zako nyingine.

Ndio maana ubwana fahari huu mapaka sasa mawaziri wanatoka masaki kwenda posta na VX. Wamejiweka hiyo kama standard. Watu hata wakiajribu kuongelea waziri kutumia vitara wanaonekana wanataka kudhalilisha status ya viongozi wetu(Watawala).

Ukidaisi sana haya ma VX mengi mileage nyingi zinaishia kwenye lami tena mjini . Waziri akienda mkoani kikazi anapaa na ndege.

Sasa hakuna hata mmoja anayefikiria kuwa VX inayotumia 140 lt per week ingekuwa ni VITARA angeweza japo kuokoa matumizi ya 50 lt kwa wiki. Sasa kila VX ya waziri na katibu mkuu ingeuwa nia vitara kwa wizara15 kwa mwaka. Pesa nyingi sana ingeokolewa. Laini hawajali na haiwaumi.
May be pato la taifa likiongezeka tutaona mawaziri wa miaka ijayo wanatumia HAMMER. hakuna Uzalendo

Sasa kwa kuwa bunge lilionekana kuanza a kuwa mtetezi wa wananchi na lenyewe likaingizwa kweye mtego na serikali Sasa hivi wabunge wamekuwa watendaji . Wana CDF. Posho na mishahara yao haitakiwi kuzingatia mwaka wa fedha na bajeti kama watumishi wengine. Na wenyewe hawashtuki. Ni sababu hata wabunge wetu wengi na wenyewe wanajiona si watumishi bali VIONGOZI

Ndio huu UBWANA MKUBWA tena wa kibepari watu wanadhani Dewji anaweza kuwa mbunge bora kuliko mkulima au mwalimu fulani wa sekondary. Just bcs ana uwezo wa kuchmoa pesa yake mfukoni. Je hiyo ndiyo kazi ya mbunge.
 
May be pato la taifa likiongezeka tutaona mawaziri wa miaka ijayo wanatumia HAMMER. hakuna Uzalendo

Tuna waheshimiwa tayari wapo huko; sasa inakuwa vigumu kuwaelewa kwenye TV wanapopinga suala la posho, sasa hatujui Fuel Guzzler kama HAMMER litakaa vipi barabarani; unless wao tayari wana bahati ya kuwa na mishahara miwili, nyumba za kupanga, na hisa katika publicly traded companies;
 
Tuna waheshimiwa tayari wapo huko; sasa inakuwa vigumu kuwaelewa kwenye TV wanapopinga suala la posho, sasa hatujui Fuel Guzzler kama HAMMER litakaa vipi barabarani; unless wao tayari wana bahati ya kuwa na mishahara miwili, nyumba za kupanga, na hisa katika publicly traded companies;
Bora afanye hivyo kwa ipato chache lakini sio anatumia STK hammer bila kujishtukia. Tena mwingine unakuta anaitwa waziri wa mazingira.

Mayaor wa London nasikia anatumia baiskeli. Ana lead by example lakini sisi kwetu viongozi wetu wana lead by just by words. Ndio maana tunaweza kumosoa nyerere lakini alijaribu kuishi maisha ya kile alichouwa anatangaza.

UBWANA FAHARI ndio siku moja nimewai kuuliza ni mbunge gani yuo tayari kuonyesha mfano wa kukubali kuchongesha pair moja au mbili ya viatu vyake kwa mafundi wa Tanzania. je huu sio mfano wa ujamaa na ujitegema. Je sio mfano wa kupenda vya nyumbani. Majibu yatakuwa Quality. Lakini wenye majukwaa wansema watanzania tupende bidhaa zetu. Huyo huyo waziri hata asali anayonunua supermaket inatoka UAE. eti soko huria na wala hajali wala hajiuli kwa nini supermarket zetu hakuna asali ya TABORA

David cameron wa UK mwenyewe inawezekana moyoni anapenda kutumia gari ya kijerumani au ya kijapan kuliko ile anayotumia lakini inapsasa kutumia gari ya UK kuonyesha uzalendo. Ndio huu ujamaa na uzalendo viongozi wetu wanakosa
 

Mwl Nyerere was behaving like a substitute player after retirement in 1985. You always see the opportunity of scoring and change the game plan when you are watching it but you get lost when you are actually on the pitch.

It is true that hope was the best weapon to maintain peace and Nyerere knew it, he knew that as more and more Tanzanians get educated and more and more educated Tanzanians lost their hopes after graduating without having employment of their dream, they will start to use their education educating others that there was no hope then, there is no hope now and there will be no hope in the future. The best hope he saw was to change country's leadership to revive the hopeless hopes of Tanzanians. When you in the same party change country presidents to 2, 3, 4 and still there is no hope for the hopeless Tanzanians. People will lose hope for the party, once people lose faith for the party in order to revive their hopes; the only remaining option is to change the party in power.

If CCM is smart enough to know this, it will not force to remain in power to coerce the hopeless Tanzanians. A hopeless individual does not value life or death, and when that happens which is happening now, there will be no fear, and that is where Mwalimu Nyerere player's substitute mind will bear fruit and materialised sooner or later(2015). The best way to preserve hope which is done everywhere in the way is to let people choose whoever they think will recharge the hope minds.

The current CCM moguls should learn that, we should not wait reconciliatory actions after some of them are summoned to The Hague. They should let people choose their leader and not force them a leader using Police and military equipment to oppress the hopeless people. Nyerere's philosophy will be proved right.
 
Gamba La Nyoka, tuseme unakutana na wakulima katika kijiji kimoja Tanzania, ambao soko huria limewacha hoi bin taaban, suala la soko huria kuwacha 70% ya watanzania HOI sidhani kama lina mjadala; Sasa, katika mjadala wako na wakulima/maskini hawa wa watu, juu ya hali zao ki-uchumi, ki-jamii n.k, mmoja wao anatoa hoja kwamba Azimio La Arusha (1967 – 1992) lilikuwa ni la Wananchi, na Azimio la Zanzibar (1992 – 2011) ni la Watawala, utamjibu nini? Jibu hilo nalo litatusaidia sana to shed more light katika huu mjadala wetu on Azimio la Arusha.

Watawala au nitumie neno viongozi nao ni sehemu ya Wananchi, ni sehemu ya Raia, Watawala ni watawala kama sehemu ya mgawanyo wa kazi tu, KUWA KWAO WATAWALA/VIONGOZI HAIWI NI SEHEMU YA KUWAPA PRIVILEDGE ZAIDI KULIKO WANANCHI WENGINE, NA PIA KUWA WAO WATAWALA HAKUWEZI KUWA SABABU YA KUWANYIMA WAO NAFASI YA KUTUMIA NGUVU ZAO, AKILI ZAO, NA MAARIFA YAO KUJIPATIA KIPATO HALALI ILIMRADI HAWATUMII NAFASI ZAO KUJINUFAISHA KINYUME CHA SHERIA.

Bwana Mchambuzi Unasema hivi:
Hoja yako kwamba mwaka 1967, kama kiongozi wa taifa huru lenye miaka 6 tu, una haki ya kutumia ujuzi wako mwingine mahali popote, popote wapi? katika uchumi upi Gamba La Nyoka? Soko lipi wakati 95% ya nchi ni vijiji/wakulima? au una maanisha bwana shamba binafsi? Unazijua takwimu za uchumi za aliotuachia Mkoloni zilikuwaje Gamba La Nyoka? Social conditions pia?

Mimi ninasema kwamba, Kama Azimio lilikuwa ni Jaribio/Experiment tu ya muda fulani, then Swali lako hilo lingekuwa Legitimate, lakini kama Authors wa hilo azimio walitegemea kuwa Azimio ni all time compass for our social, economical and political Compass walipaswa kuangalia je hiyo code of conduct ilikuwa sustainable, 10, 20, 30 years from the point of adoption?- kwa sababu hiyo hoja ya nchi Changa oneday ingekufa, Maana Taifa oneday lisingeitwa Taifa Changa. Sasa je cha kujiuliza bwana Mchambuzi je ni lini basi hayo Masharti ya Viongozi yangelegezwa?, pindi Taifa likishakuwa na Umri Mkubwa au pindi Umasikini katika Taifa ungekuwa umepigwa Vita?.
Kumbe basi, iwapo kigezo kilikuwa ni umasikini wa nchi/Taifa changa ndo ilikuwa Sababu ya kuweka Masharti hayo mimi ninayaita "Makali kupita kiasi", then pindi umasikini au taifa lingekuwa limekua(si changa tena) yangeondoka tu!, it was the matter of time!, HOJA YANGU YA MSINGI HAPA NI KWAMBA, AUTHORS WA MASHARTI YA VIONGOZI HAWAKUYAWEKA MASHARTI HAYO KUAKISI MATOKEO YANAYOWEZA KUTOKANA NA NYAKATI NA POSSIBILITY ZA MABADIRIKO YA KIUCHUMI NA KIJAMII KWA NYAKATI MBALIMBALI MIONGO KADHAA MBELE, KIGEZO CHAO KIKUBWA KILIKUWA NI UCHANGA/UMASIKINI WA TAIFA, JE TAIFA LINGEKUWA SI CHANGA/SI MASIKINI TENA TUNGEFANYAJE?-TUNGEENDELEA KUWAZUIA VIONGOZI KUTOKUWA NA NYUMBA ZA KUPANGA KUJIONGEZEA KIPATO, HATA KAMA NYUMBA WANAZO NA DEMAND IPO ZIKAE TUPU?.

Kwa hivi sasa nchi yetu siyo kwamba si masikini, ni masikini na bado asilimia karibu 80 ya Raia wetu ni wakulima, na kiukweli kabisa Tofauti na miaka ya Uhuru wasomi ni wengi, na raia wanajitahidi kupambana kutengeneza opportunity za kujipatia kipato, ni kwa namna gani basi hayo masharti ya uongozi ya Kutokuwa na Nyumba ya kupangisha yangeweza kufanya kazi katika mazingira ya Sasa ni dhahiri yasingefanya Kazi, watu wana ujuzi zaidi ya mmoja, one part mtu ni Engineer another part ni mwalimu wa Physics kwenye college fulani, One part mtu ni Daktari another part ni lecturer, mtu ana degree ya accounting na pia ana degree Computer Science, kwa nini asiweze kutumia ujuzi wake kujipatia kipato-SASA INAKUWAJE AUTHORS WA MASHARTI YA UONGOZI WALISHINDWA KUFORESEE HIZI POSSIBILITIES?- JE KIZAZI CHA SASA KINGEENDELEA KUTOLERATE HIII DISCREPANCY AU KINGEIMODIFY?.

NDIYO MAANA NINAKUBALIANA NA MZEE MWINYI ALIYESEMA KWAMBA, AZIMIO LA ZANZIBAR HALIKUUA AZIMIO LA ARUSHA BALI LILILENGA KULIOKOA, ILA SEMA TU MABADIRIKO KADHAA YALIYOTOKEA ULIMWENGUNI MIAKA MICHACHE ILIYOFUATA TOKA 1991 (AZIMIO LA ZANZIBAR LILIPOKUWA ADOPTED)MPAKA 1995 ALIPOSTAAFU YALIKUWA INEVITABLE KWA NCHI ZA DUNIA YA TATU TUKIWEMO SISI.

BY THE WAY MPAKA MWAKA 1957 , DAR-ES-SALAAM PEKEE ILIKUWA NA WATU 128,742( SOURCE: THE POLITICAL DEVELOPMENT OF TANGANYIKA, BY J.CLAGGET TAYLOR), KWA HIYO KUDAI KWAMBA MIJI YOTE MIKUBWA ILIKUWA NA JUMLA YA WATU 50,000 NI STATISTICALLY INCORRECT.
 
Imeandikwa na Elias Msuya
Mwananchi


MWENYEKITI wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere Profesa Issa Shivji amekosoa Sheria ya Mchakato wa Kuundwa kwa Katiba mpya iliyosainiwa na Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni na kusema kuwa ni mbovu na haitazaa katiba bora.

Novemba 29 mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete alitia saini Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 huku kukiwa na malumbano makali kutoka asasi za kiraia, vikiwemo vyama vya siasa, kupinga hatua hiyo kwa maelezo kwamba, mchakato huo uliendeshwa kwa mizengwe na Hata hivyo, taarifa ya kusainiwa muswada huo iliyotolewa na Ikulu kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa hatua hiyo ya Rais Kikwete, ilikamilisha safari ya kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Mwaka 2011 baada ya Bunge kupitisha muswada huo uliowasilishwa na Serikali huku ikiweka wazi kuwa Serikali itaendelea kusikiliza maoni na mawazo ya wadau na wananchi mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha sheria hiyo.

"Mheshimiwa Rais Kikwete anatoa wito kwa mwananchi yeyote mwenye maoni ama mawazo ya namna ya kuboresha Sheria hiyo, ajisikie yuko huru kutoa maoni yake na Serikali itasilikiza na kuchukua hatua zipasazo'' ilieleza sehemu ya taarifa hiyo iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu Akizungumza katika kipindi cha Kipima Joto kinachorushwa na kituo cha televisheni ya ITV juzi usiku, Profesa Shivji ambaye ni mmoja wa magwiji wa sheria hapa nchini, alisisitiza kuwa sheria hiyo ni mbovu na kamwe haitazaa katiba bora wanayoitaka wananchi na kuwashauri kwenda kupinga jambo hilo mahakamani.


Akichambua sheria hiyo, Profesa Shivji alikosoa kifungu cha 21 akisema kuwa inashangaza kwani kinazuia hata watu kuikosoa sheria hiyo. "Mimi nasema kuwa sheria hii ni mbovu… Katika sheria hii, kifungu hiki kinanizuia hata kusema, sheria hii ni mbovu'. Mimi sijui kulikuwa na fikra gani kuweka kifungu kama hiki, kitu kimoja tu ni kwenda mahakamani kuipinga." Alisema. 



Akichambua kifungu kimoja baada ya kingine katika sheria hiyo, Profesa Shivji alisema kuwa imewatenga kabisa wananchi katika mchakato mzima wa kuandikwa kwa katiba mpya. "Wananchi wanatakiwa kushirikishwa tangu hatua ya kwanza, kwa mchakato wa Bunge, yaani sisi wenyewe tumeshirikishwa kupitisha sheria hiyo kuhakikisha vyombo vyote vinavyohusika vinafuatwa." Alisema Profesa Shivji.

Akitoa mfano wa Kamati ya Bunge ya Masuala ya Katiba, Profesa Shivji alisema kuwa, haikufanya kazi yake kikamilifu hivyo kuwanyima wananchi fursa ya kutoa maoni. "Tulianza awali lakini hatukukamilisha…hatukuwa na sababu ya kutokukamilisha. Tulipoanza kwenye makongamano yale yaliyofanyika tulipata maoni ya wananchi, baada ya kupata maoni, ndipo mchakato wa kuunda katiba,'' alisema Tume ya Rais ya Katiba Kuhusu Tume ya Rais ya Kuunda Katiba, Profesa Shivji, alisema haipaswi kuwa moja kwa moja chini ya Rais bali pia ishirikishe wananchi.

Alitoa mfano wa tume ya aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Edwin Mtei iliyoshughulikia Marekebisho ya Fedha na Tume ya Rais ya Ardhi lakini akasema, Tume ya Katiba siyo ya rais, Hii siyo Tume ya Rais, ni Tume ya Katiba (Constitutional Commission), inayoundwa chini ya sheria zilizopitishwa na Bunge. Hata tume iliyounda Katiba ya mwaka 1977 iliundwa chini ya Mkataba wa Muungano.

Sheria ile ilitaja wazi kwamba rais akikubaliana na Rais wa Zanzibar, ataunda Tume ya Katiba" alisema. Aliendelea kusisitiza ushirikishwaji wa wananchi katika tume hiyo akisema kuwa rais anapaswa kuzingatia maoni ya wananchi katika uteuzi wa wajumbe wake.

"Mfano taasisi mbalimbali za jamii zetu, taasisi za serikali, vyombo vya habari, vyuo vikuu, wanaweza kupendekeza majina mawili, tunaona kwamba hawa watu wanafaa kuwa wajumbe, halafu rais anateua kupitia hayo. 

Hiyo ndiyo namna ya kuwashirikisha wananchi lakini kwa sheria ya sasa hatujui rais anatumia vigezo gani," alisema.

Bunge la Katiba Kuhusu Bunge la Katiba, alisema idadi ya wajumbe 600 wa Bunge hilo ni kubwa mno ukilinganisha na idadi ya Watanzania 40 milioni, hali ambayo alisema italifanya Bunge hilo kutumia gharama kubwa bila sababu. Alitoa mfano wa Bunge lililounda katiba ya uhuru ya India la mwaka 1947 akisema lilikuwa na wajumbe 250 na wakati huo idadi ya wananchi wakiwa 100 milioni.

Alikosoa pia uwiano wa idadi ya wajumbe hao akisema kuwa kati yao, teluthi mbili, yaani wajumbe 400 watakuwa ni wa CCM. Akasema hali hiyo itawanyima fursa wananchi ambao si wanachama wa vyama vya siasa. Kura ya maoni Kwa mujibu wa Profesa Issa Shivji, japo wananchi watapata nafasi ya kupiga kura ya maoni, bado kuna hatari ya kutopata katiba bora kwani hawakupata nafasi ya kutosha ya kutoa maoni yao. 



"Katiba inaweza kuwa na ibara 500, inawezekana kati ya hizo hupendi ibara mbili tu. sasa ukisema hapana ndiyo umeikataa katiba yote kwasababu hatukufuata vizuri mchakato," alisema na kuongeza; "Hata Hitler aliingia madarakani kwa kura ya maoni". Aliongeza kuwa kuna hatari katiba ikapitishwa na idadi ndogo ya wananchi hasa kutokana na tabia ya wananchi kutopenda kupiga kura.

"Sheria hiyo inasema kuwa asilimia 50 ya waliopiga kura siyo waliojiandikisha. Unaweza kukuta katiba ikapitishwa na asilimia 20 tu ya wananchi".



Mjadala huo pia uliwahusisha Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama cha UDP, Isaac Cheyo ambao pia waliipinga sheria hiyo.

Kwa upande wake Mnyika alieleza sababu ya wabunge wa Chadema kususia mjadala wa katiba na kutoka nje ya ukumbi wa Bunge akisema kuwa walipinga muswada huo kusomwa kwa mara ya pili. Alifafanua pia hatua ya chama hicho kwenda Ikulu kumwona rais akisema kuwa rais ni upande wa pili wa Bunge. Mnyika alisisitiza kuwa Chadema hawatasubiri kwenda mahakamani, ili kupinga sheria hiyo bali watafanya mikutano nchi zima na kueleza ubaya wa sheria hiyo.



"Tutakwenda kwa wananchi tuwaambie ubaya wa sheria hii. Watapiga kura ya hapana, hata kama hatutapata katiba, tutakuwa tumeleta mabadiliko". Naye Cheyo alisema mchakato mzima wa kuandikwa kwa katiba mpya umehodhiwa na rais huku wananchi wakizuiwa kutoa maoni yao.

"Bunge la kutunga katiba ni Bunge la chama kile kile, limekuwa likiaminiwa na chama hicho hicho. Tuangalie ‘composition'(wanaounda) ya Bunge, inachukuwa watu gani, vinginevyo tutakuwa hatuwatendei haki wananchi," alisema Cheyo.

Awali asasi mbalimbali ndani ya jamii zikiongozwa na Jukwaa la Katiba Tanzania, zilieleza kutoridhishwa na hatua zilizochukuliwa na serikali katika kuendesha na kusimamia mchakato mzima wa kupitishwa kwa sheria hiyo.

Wanaharakati walitishia kuitisha maandamano endapo Bunge lingeipitisha sheria hiyo huku Chama Wanasheria Tanzania, kikitishia kufikisha suala hilo mahakamani. Hata hivyo tangu Rais Kikwete aliposaini sheria hiyo, amekuwa akikutana na makundi mbalimbali, wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa na kupokea maoni ya kuhusu kutungwa kwa katiba mpya.
 
Back
Top Bottom