Prof Haroub Othman na Shivji ni wachochezi?

so the question is, if the arusha declaration didn't promise to do away with our poverty why did we adopt it as our economic, social and political compass? from the early beginning.

Wasn't poverty one of our enemies?- so if we had exhausted all those decades to implement azimio la arusha only to be told by our "muasisi" that it didn't mean to do away with poverty then why did we waste our time with it in the first place?.

Hope, hope, hope,hope- people dont eat hope, dont wear hope, dont sleep in hope, hope will always be there even when you are rich, you will still hope for more!

People want tangible results.
Now i think, if azimio didn't mean to do away with poverty then it was wise to do away with it/modify it , and thus congratulations to president mwinyi.

Mkuu, umelisoma lakini vizuri Azimio La Arusha? Nina nakala soft hapa, I can send you. Na je, umeelewa mantiki nzima ya Mwalimu hapo? Na nani dunia hii anaweza kusema anaweza kumaliza tatizo la poverty? hata Mwalimu, from the outset, didn't promise to do so; alichotupa ni self determination, na kuondokana na minyororo ya unfair global capitalist system, ambayo yeye hakuichukia per se, bali alipigania fair participation;

Mwaka 1970 Mwalimu alitamka haya:

******
"We say man was created in the image of GOD. I refuse to imagine GOD who is poor, ignorant, superstitious, fearful, oppressed, and wretched – which is the lot of the majority of those HE created in his own image. MEN are creators of themselves and their conditions, but under present conditions WE are creatures, not of GOD, but of our fellow MEN.
JKN, 1970
*******

Vinginevyo, Mwalimu hakuchukia Ubepari Per Se, bali unfairness that was inherent in Ubepari. Hata kwenye kitabu chake cha TANU na RAIA, in 1962 (p.8), even before Azimio La Arusha Lililokuja kuzaa UJAMAA, Mwalimu anasema:

"Kwahiyo, ikiwa serikali ya TANU itachukua hatua za kuzuia tofauti iliyopo sasa kati ya watu wa juu na watu wa chini, sina shaka watu wote walio juu hawatapenda. Hata mimi ninayeandika maneno haya, sitapenda; kwani hata mimi napenda kuwa Tajiri! Lakini kitakachotuwezesha kujenga nchi safi siyo tamaa yangu mimi kuwa tajiri, bali ni vitendo ambavyo, ingawa tunajua kuwa vitaudhi wachache, tunayo hakika kuwa ni vya manufaa kwa ndugu zetu walio wengi".

Gamba La Nyoka, no offense, na nina heshimu haki yako kutoa mawazo unavyopenda, lakini niwe mkweli - sijaamini macho yangu niliposoma WEWE kutoa pongezi kwa Mwinyi (na hata ingekuwa Mkapa au Kikwete) kwa madhara ya soko huria yaliyopo sasa, wakati inajulikana wazi kwamba nchi imechukuliwa mateka na IMF na WordBank since 1986. Viongozi baada ya Nyerere wanafanywa na WorldBank na IMF kuwa "viongozi watekelezaji" (au tuseme managers), hawana mamlaka tena kimaamuzi juu ya ndugu zetu vijijini ambao ndio wanatuweka mjini kwa vyakula, na pia wanatupatia fedha za kigeni kutanua na magari ya kifahari kama waheshimiwa kutokana na kilimo cha cha kifukara, ambacho watawala wetu, zaidi ya kuchuma, hawana muda nacho tena kama wakati wa Mwalimu. Ni audience hiyo ambayo Mwalimu hapo juu kwenye my original post ndio ana wa address, kitu ambacho wengine wanaweza kuona Mwalimu ni Mchochezi.

Vinginevyo Gamba La Nyoka, ni muhimu utambue kwamba, hata kama Rais baada ya Nyerere in 1985 angekuwa anaitwa ni Peter, Khadija, Said, au Stella, Rais huyo angeitwa "RUKSA".

Watu wanamkejeli Mwalimu ambae juhudi zake zililenga kitu kimoja tu: To give our country a self determination baada ya kupotezea muda na direction na wakoloni. Hilo ndilo lilimpa heshima kubwa duniani, kiasi cha kuombwa na nchi zote za kusini chini ya Waziri Mkuu wa Zamani wa Malaysia, kutoa mwongozo kama Mwenyekiti (aliefeli na Ujamaa), jinsi gani nchi maskini zinaweza kujikomboa; Sote tunajua mafanikio ya South Commission yalikuwa nini.

With all due respect that I have for Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Je, ni nani/nchi gani/taasisi gani ilimfuata/imemfuata kwenda ku replicate mafanikio ya soko huria Tanzania, katika nchi nyingine za Africa, Latin America, Asia? Unatambua kwamba wakati wa mwinyi, in early 1990s Tanzania ilikuwa nchi ya tatu kwa umaskini duniani – mbele tu ya Somalia na Afghanistan? Unakumbuka hali ilivyokuwa tete? Nina imani hautakuja na jibu kwamba ni kwasababu Mwinyi alipokea nchi ikiwa tete toka kwa Nyerere. Iwapo utasema hayo, Je hicho ndio kipimo cha uongozi ambao unapelekea wewe binafsi kumpa pongezi?

Kwa mtu makini, kusingizia failure za Rais aliyepita kwamba ndio kikwazo kwa rais aliyepo ni kukubali failure, hakuna lingine. Hata wenzetu Marekani, moja ya sababu kubwa zilizomsaidia Obama kushinda uchaguzi mwaka 2008 ilikuwa ni matatizo ya kiuchumi aliyoyaacha Rais aliyemtangulia – yani, BUSH. Lakini katika mbio za uchaguzi mwingine- miaka mine tu baadae (2012), Obama ana kazi ya ziada kushinda tena uchaguzi 2012, lakini tunaona kwamba, sio yeye, wala washauri wake wanaotumia utawala wa Bush kama kisingizio, na wakithubutu tu, game is over, kwani wananchi waelewa (tofauti na wengi wetu Tanzania ambao sio waelewa) watamhoji Obama: Ulitueleza matatizo ya Bush, tukaelewa na kukuamini ili uyatatue, Je umeshindwa tumpe nafasi mtu mwingine?

Gamba La Nyoka, Uchaguzi mkuu wa Marekani 2012, wananchi hawatampigia Kura Obama kwa sababu ya Bush, watampigia kura Obama kwa sababu ya Obama.

Kwa hoja zenu hizi juu ya Mwalimu, sitashangaa hata uchaguzi wa Tanzania miaka 50 ijayo/mwaka 2065, wapo watanzania wengi watakaowakataa wagombea fulani kwa sababu ya Mwalimu Nyerere, sio Kwa sababu ya uwezo na sifa za wagombea.

Mwisho naomba niongezee tu kwamba – na on this one, I am not addressing you as Gamba La Nyoka, bali ni kwa vijana wote, kwani limenijia akilini sasahivi. Vijana wenzangu, viongozi hawa wanaotutuma kuwafagilia au kuwapigia debe, baada ya miaka 15-20 watakuwa wamestaafu wanakula pensheni zao; Wewe utakuwa wapi kijana mwenzangu? Chungeni sana msije mkachagua the wrong side of history sasahivi. Otherwise, utaweka uso wako wapi, na utaishi vipi katika jamii wakati umri wako ndio kwanza utakuwa pengine unakaribia miaka 50 tu, mbichi kabisa, wakati hao mnaowafagilia watakuwa HAI au HOI, kama wastaafu. Ni dhahiri kabisa kwamba, mkiwafuata kwa msaada, ushauri, miaka hiyo, wataambia "Mimi Mstaafu Bwana"

Tafakari.
 
Mchambuzi,

..nadhani tunatakiwa tuwe na a mixed ISS na EPS industrialization program.

..pia naona tatizo lililopo ni serikali kuwa na priorities nyingi kupita kiasi.

Tutaweza lakini kwa bajeti inayotegemea wahisani na direction za WorldBank na IMF? sijasoma sehemu yoyote katika mipango yao kuwa na mikakati ya kusaidia nchi yetu iingie katika mapinduzi ya viwanda, zaidi ya wao kugusia gusia tu on viwanda hapa na pale;
 
With all respect to Alhaj Ally Hassan Mwinyi the architecture of Zanzibar declaration. What we see today is the result of that decleration; I don`t believe that Alhaj Mwinyi had time to read the contents neither he knew intention of peoples around him; but in comparison Arusha declaration was meant to secure and protect national wealth; of course it did not take poverty away neither did not create massive wealths through corruptions and misuse of public funds; more to that Arusha declaration was meant to us - peoples; what did we get out of Zanzibar declaration? Zanzibar declaration was meant for CCM top brands and their inner cronies; Alhaj Mwinyi can not stands in front of Tanzanians and defend Zanzibar declaration;it was a slap on his face!

Chama
Gongo la Mboto DSM

Very well said.
 
Watanzania bwana, ujue Nyerere aliwanyima elimu watu kwa wingi, akawajengea mazingira ya kuwa na hali moja ya maisha(umaskini) ili iwe rahisi kwake kuwatawala kwa kuwa mtu akiwa maskini na hana elimu atahoji au kupinga kipi, hii ndo sababu yeye Nyerere anaonekana kama Nabii Fulani vile, yapo matatizo mengi ya kiuchumi na kisiasa tunayoyashuhudia leo chanzo chake ni Nyerere ila watanzania wengi hawalielewi hili, Mkarage baho!

nadhani hata wewe hauna elimu juu ya ukweli wa mwalimu na elimu, ila sina uhakika kama ukosefu wa elimu hiyo ni kutokana na makosa ya mwalimu;
 
Gamba la Nyoka,

Naona hawa jama zetu wamekuacha na maswali mengi kutokana na mfumo wa Nyerere lakini nakuomba jaribu kuzama deep zaidi ya kufikiria juu juu..

What Azimio la Arusha means ni ku set malengo na sio necessary Azimio hilo ndio liwe nyenzo ya kufikia unakotaka kwenda hapana ila ni dira ya kuondoka ktk hali uliyopo ili kufikia malengo fulani. Sasa watu wanapochukulia kwamba Azimo la Arusha ndilo lilikuwa na malengo ya kuondoa umaskini hivyo tubadilishe itikadi hiyo ndipo wanahoji mbona hatujaondoka ktk umaskini?. Kama kuna sababu leo ambazo zimetufanya bado tupo ktk umaskini basi hazihusiani na Ubepari kama ambavyo Ujamaa haukuhusika..ila tuzifikirie hizo sababu zenyewe..


Pili, swala la equality nadhani wametoa mfano wa mkono wenye vidole vitano, vyote havifanani wala havilingani lakini vyote ni muhimu ktk matumizi ya mkono na huwezi kusema kidole fulani kinahitaji kutazamwa zaidi ya kingine na ushirikiano wa vidole hivi kwa pamoja kunaifanya kazi ya mkono kuwa rahisi. Hivyo unapotazama equality sio kwa marefu na mafupi ya vidole ama kazi ya Azimio la Arusha ilikuwa kunyoosha vidole vyote viwe sawa...(kama wanavyofikiria wapinzani) isipokuwa kujali na kutukuza nafasi ya kila mwananchi kushiriki ktk ujenzi wa Taifa..

Leo hii Wakulima na Wafanyakazi wanadhalilishwa hata wakiomba mishahara zaidi kutokana na kupanda kwa maisha wanapigwa chini wakati mbunge yuko tayari kuongeza POSHO na sio mshahara wake kwa sababu zile zile za kukabiri maisha.. Sasa mbunge ndiye anayekabiri maisha ya wananchi na sii jukumu la kila mwananchi maana ndizo sababu walizozitoa kwamba wao ndio wanao deal na wananchi kila siku.
 
Watawala wanalipinga azimio la Arusha kwa sababu moja tu - Leadership code ambayo ilizuia wizi na ufisadi, hakuna jingine, vinginevyo watawala care less kuhusu uwepo au kutokuwepo kwa mashirika ya umma, viwanda, hali ya Kilimo, wao hawajali, come what may, azimio la zanzibar linawaruhuru to enjoy kwa kuwa na mshahara zaidi ya mmoja, kuwa na hisa katika publicly traded companies, kuwa na nyumba za kupanga, etc;

Mimi nina uhakika, wananchi wakipatiwa nakala ya azimio la arusha au wachapishiwe kwenye gazeti, wale waliokuwa wanamkejeli kutokana na influence ya watawala, na wapiga debe wao, watajutia sana kupoteza muda mwingi kumponda Mwalimu huko vijiweni;

Azimio la Arusha lilikuwa lao (wananchi, right?) Azimio la Zanzibar ni la nani?
 
Pathetic nyerere "man was created by image of god!"

Ndio maana hako ka-azimio hakana maana aise??

Huyo god anayefanana naye ni wake peke yake .. "Mwenyezi Mungu wetu hafanani wala hafananishiwi na chocote katika viumbe vyake far from that"
 
Pathetic nyerere "man was created by image of god!"

Ndio maana hako ka-azimio hakana maana aise??

Huyo god anayefanana naye ni wake peke yake .. "Mwenyezi Mungu wetu hafanani wala hafananishiwi na chocote katika viumbe vyake far from that"

Karibu sana kwenye mjadala TOPICAL, za siku nyingi? Misimamo yako na mwalimu ni ya kidini sana, kama mwenzako Barubaru, Faiza, NasDaz, hamna jingine; ndio maana kwa muda sasa, hii thread mmebakia kama observers tu kwani mmegundua kwamba kutubandikia picha za majengo marefu ya vioo mjini, pantoni jipya, bidhaa tele mlimani city na Quality Plaza, UDOM, mmegundua hapa si mahala pake;

Hata siku moja hamji na hoja zenye mashiko katika harakati zenu mlizotumwa kumweka Mwalimu,BABA WA TAIFA, abakie kama Kinjeketile, Kiongozi wa MajiMaji, katika historia ya nchi yetu; na ndio maana neno kama GOD linapojitokeza, hapo ndio inakuwa your gold rush;

Karibu sana kwenye mjadala, bila ya kuvunjiana heshima za imani zetu; tujadili hoja iliyopo mbele yetu sote kwa maslahi yetu sote; karibu sana;
 
Pathetic nyerere "man was created by image of god!"

Ndio maana hako ka-azimio hakana maana aise??

Huyo god anayefanana naye ni wake peke yake .. "Mwenyezi Mungu wetu hafanani wala hafananishiwi na chocote katika viumbe vyake far from that"
Mkuu wangu usituharibie mjadala tafadhali..... Ebu nikuulize wewe sifa za mwenyezi Mungu ni zipi? majina 99 kwa uchache wa sifa hizi - wewe binadamu huna? na kwa nini iwe wewe na sio viumbe wengine... Mkuu usijaribu kuipinga Injili pasipo kuelewa maana achana na tafsiri za watu ila jaribu kuilewa Injil ilikuwa na maana gani kulingana na Kuran..
Turudi kwenye mada yetu tafadhali..
 
Karibu sana kwenye mjadala TOPICAL, za siku nyingi? Misimamo yako na mwalimu ni ya kidini sana, kama mwenzako Barubaru, Faiza, NasDaz, hamna jingine; ndio maana kwa muda sasa, hii thread mmebakia kama observers tu kwani mmegundua kwamba kutubandikia picha za majengo marefu ya vioo mjini, pantoni jipya, bidhaa tele mlimani city na Quality Plaza, UDOM, mmegundua hapa si mahala pake;

Hata siku moja hamji na hoja zenye mashiko katika harakati zenu mlizotumwa kumweka Mwalimu,BABA WA TAIFA, abakie kama Kinjeketile, Kiongozi wa MajiMaji, katika historia ya nchi yetu; na ndio maana neno kama GOD linapojitokeza, hapo ndio inakuwa your gold rush;

Karibu sana kwenye mjadala, bila ya kuvunjiana heshima za imani zetu; tujadili hoja iliyopo mbele yetu sote kwa maslahi yetu sote; karibu sana;

Ha ha ha! na wewe unayemtetea unafanya hivyo kwasababu za kidini au sivyo?? watu bana!

Mimi nilishakwambia mara nyingi kwamba tatizo la nyerere alikuwa MBOVU period

kwangu mimi ujamaa, ubepari (sera yeyote) siyo tatizo, tatizo ni nani anayesimamia hiyo sera???

kwa hiyo nyerere tungepata faida kama angekuwa kiongozi mzuri hata kwenye ujamaa period..

Mimi mzima aisee, kwangu mimi watoto wangu na ukoo wangu nyerere siyo baba eat it..
 
Katika sheria za marekebisho ya katiba iliyosainiwa na Rais, kuna kifungu cha 21 kinachozuia mtu yeyote kujadili au kutoa elimu kwa wananchi juu ya sheria ya mabadiliko ya katiba, kifungu hiki kiliingizwa siku ileile wabunge walipokuwa wanaipitishwa kwani awali hiki kifungu hakikuwepo, kinyume na hapo huyo mtu atakayevunja hiyo sheria atafungwa miaka mitatu hadi saba na kulipa faini ya kuanzia milioni 5 hadi 15, hii ina maana ya kuwa hairuhusu mwananchi kujadili sheria ya mabadiliko yoyote ya katiba tofauti na kamati itakayoundwa tu na rais ndo yenye mamlaka ya kujadili.

Leo katika mjadala wa kipima joto kilichokuwa kinaendeshwa na mtangazaji Leynfredy Masako kupitia ITV,(SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA), wageni waliokuwepo ni Prof. Shivji, Mbunge wa Ubungo Mnyika na mjumbe wa UDP Ndg Isack Cheyo, cha ajabu kilichoonyeshwa na wahusika wote wanne ni kuwa na hofu kwa kufunguliwa mashitaka kwa kuamua kujadili kitu ambacho kilitungiwa sheria kuwa akisha saini rais hairuhusiwi mtu yeyote yule kuujadili tena , tofauti na hapo ni faini iliyoorozeshwa ndani ya sheria,

Je, serikali itawafungulia mashitaka kwa kuvunja sheria??????
 
Wakiwashtaki, ndio ukweli utadhihirika kuwa sheria hiyo ni dhalimu na inazuia uhuru amabao unatambuliwa na katiba ya 1977 ya JMT,Maana kuna baadhi ya wtu wanadhani ni sheria nzuri tu tusubiri tuone
 
Napenda sana kesi mbuzi ngoja niitafute hii kesi, ktk sherehe hizi za mwisho wa mwaka nitashiriki vema kujadili mabadiliko ya katiba mpya ktk kikao hapa bomani kwangu na pia nitahakikisha kila ninayekutana naye kuanzia sasa nitamkumbusha kuwa katiba mpya sio muarobaini wa matatizo yetu kwa sababu mabadiliko haya tunayayafanya ktk katiba mpya hii ni mabadiliko ya front cover tu, coz intention ya mkoloni bado itabaki ktk katiba yetu kwa kuendekeza wahuni kama werema na Kombani na kuwatusi wasomi wetu kina Shivji.

Naitaka hii kesi kwa kweli, nitaitafuta hii kesi kwa kujadili mabadiliko ya katiba mpaka kwenye daladala alafu nimulikwe na wale usalama wao wa taifa ili niburuzwe mahakamani na mwishowe tutakutana mboni kwa mboni na muendesha mashtaka hapo kizimbani kwetu alafu baada ya kumshinda kesi tutapasuana medulla kama kawida.
 
Back
Top Bottom