Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 34,063
- 79,427
Hamjambo!
Katika vita ya mtandaoni, hasa vita maneno. Kuna kanuni zake.
Unapotupiana maneno na mtu kama unakombora kubwa kuliko haupaswi kulichelewesha sana kama vile katika vita vya silaha mfano Nyukilia ambazo hutolewa kidogo kidogo na kutokea yenye uwezo mdogo kufuatia yenye uwezo Mkubwa
Vita ya maneno ili ushinde lazima uangalie tension, shauku, hamu kubwa ya watazamaji, vita ya maneno watazamaji hutaka kusikia kombora kubwa kuliko hasa likitolewa dakika za mapema kabisa ili kumaliza kazi.
Vita ya maneno hasimu huwa na hofu ya kusemwa zile tabia zake mbaya za siri, usipomsema katika dakika za mwanzo, ukasema mambo ya kawaida. Tayari unampa mazingira ya kuzoea hofu na kisaikolojia ukishazoea hofu ya kile unachotarajia inapunguza uzito wa kombora lenyewe hata likitupwa.
Ikiwa unamchelewesha mtu katika vita ya Maneno jitahidi uwe na taarifa kubwa ya kutisha ambayo yeye(hasimu wako) anajua taarifa hiyo hauna. So inakuwa suprise sio tuu kwa Mashabiki bali hata kwa adui. Na hilo linakuwa pigo moja takatifu ambalo lazima liitwe Knock out.
Sasa Polepole press ya kwanza watu walijua atatuma vyuma vya uhakika, kisha awamu ya pili kutuma ushahidi, yeye watu wanamsubiri wakijua atakuwa na jambo zito. Akaboronga.
Watu wakasema huenda anavuta kasi, kapanga shambulizi la Pili, akaboronga.
Mpaka hasimu zake wamemdharau.
Alafu mbaya zaidi mlengwa Mkuu ambaye ni Rais yupo Kimya.
Na hili nilishaeleza kuhusu mpambano unavyokuwa.
Rais hawezi kujibu shambulizi lililopoa. Na nilimwambia kuwa ukimya wa Rais kwake auhesabu kama ishara ya hatari.
Kikawaida mtu ambaye unajua siri zake ukianzisha vita naye. Kama atakupiga shambulizi lililopoa huwezi mjibu kwani unajua hajamaliza risasi zake. Kwamba kuna risasi anayoitegemea.
Ni tofauti na Gwajima Vs Makonda. Gwajima alipokuwa katika vita vya Maneno na Makonda, Gwajima alianzia moja kwa moja kwenye kiini. Kisha akaacha ngoma imehang huku ushahidi ukiwa unafuata kwa shambulizi alilofanya.
Gwajima Vs Serikali ambao ni kivuli cha watekaji kwa Mujibu wake.
Shambulizi lake alianzia juu na hakuwa na risasi nyingine. Vita ilianza kwa tensioni kubwa.
Rais alimjibu kwa sababu alijua Gwajima amemaliza risasi zake na hana tegemeo jingine tena. Hana kipya atakachoongea.
Polepole yeye katoa shambulio lililopoa Sana. Madhara yake sio makubwa.
Hata kuzima mitandao ni hofu tuu.
Lakini ni kiashiria kuwa Polepole anataarifa nyingi na nyeti sana.
Polepole angerusha mawe mazito hata vipande nusu ambavyo vitamfanya awaabishe adui zake na awapagawishe. Kisha hatua inayofuata aseme anakuja na ushahidi ambao utawashangaza, na aseme atauweke hadharani na kila mtu atauona.
Huku akisema amebakisha vyuma vingine ambavyo vitaitetemesha nchi.
Ukishatoa madai ya kumdhalilisha hasimu wako utakuwa upo nusu ya ushindi. Kuthibitisha utakuwa umemaliza kazi.
Kadiri Polepole anavyochelewa ndivyo mashambulizi yake yanakosa nguvu.
Yaani leo hata aje aseme kitu gani hakitakuwa na nguvu ya maana kama angeshambulia mwanzoni.
Tayari watu wameshazoea, watu wameshapredict, hasimu kashazoea tension jambo ambalo kwenye vita ya maneno sio zuri.
Soma >> GE2025 - Polepole: Kuongea na watanzania Agost 6, saa 2:00 kuhusu mustakabali wa taifa
Polepole hata zile trick za majigambo na mikwala ya kusema yeye yupo tayari kufa lakini lazima hasimu wake alale nao mbele hatilii mikazo katika laini hizo.
Yupo katika vita kubwa lakini anapambana kwa namna laini sana. Jambo ambalo unagundua kuna kitu hakipo sawasawa.
Anyway! Sisi tupo!
Na tutakuwepo!
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Katika vita ya mtandaoni, hasa vita maneno. Kuna kanuni zake.
Unapotupiana maneno na mtu kama unakombora kubwa kuliko haupaswi kulichelewesha sana kama vile katika vita vya silaha mfano Nyukilia ambazo hutolewa kidogo kidogo na kutokea yenye uwezo mdogo kufuatia yenye uwezo Mkubwa
Vita ya maneno ili ushinde lazima uangalie tension, shauku, hamu kubwa ya watazamaji, vita ya maneno watazamaji hutaka kusikia kombora kubwa kuliko hasa likitolewa dakika za mapema kabisa ili kumaliza kazi.
Vita ya maneno hasimu huwa na hofu ya kusemwa zile tabia zake mbaya za siri, usipomsema katika dakika za mwanzo, ukasema mambo ya kawaida. Tayari unampa mazingira ya kuzoea hofu na kisaikolojia ukishazoea hofu ya kile unachotarajia inapunguza uzito wa kombora lenyewe hata likitupwa.
Ikiwa unamchelewesha mtu katika vita ya Maneno jitahidi uwe na taarifa kubwa ya kutisha ambayo yeye(hasimu wako) anajua taarifa hiyo hauna. So inakuwa suprise sio tuu kwa Mashabiki bali hata kwa adui. Na hilo linakuwa pigo moja takatifu ambalo lazima liitwe Knock out.
Sasa Polepole press ya kwanza watu walijua atatuma vyuma vya uhakika, kisha awamu ya pili kutuma ushahidi, yeye watu wanamsubiri wakijua atakuwa na jambo zito. Akaboronga.
Watu wakasema huenda anavuta kasi, kapanga shambulizi la Pili, akaboronga.
Mpaka hasimu zake wamemdharau.
Alafu mbaya zaidi mlengwa Mkuu ambaye ni Rais yupo Kimya.
Na hili nilishaeleza kuhusu mpambano unavyokuwa.
Rais hawezi kujibu shambulizi lililopoa. Na nilimwambia kuwa ukimya wa Rais kwake auhesabu kama ishara ya hatari.
Kikawaida mtu ambaye unajua siri zake ukianzisha vita naye. Kama atakupiga shambulizi lililopoa huwezi mjibu kwani unajua hajamaliza risasi zake. Kwamba kuna risasi anayoitegemea.
Ni tofauti na Gwajima Vs Makonda. Gwajima alipokuwa katika vita vya Maneno na Makonda, Gwajima alianzia moja kwa moja kwenye kiini. Kisha akaacha ngoma imehang huku ushahidi ukiwa unafuata kwa shambulizi alilofanya.
Gwajima Vs Serikali ambao ni kivuli cha watekaji kwa Mujibu wake.
Shambulizi lake alianzia juu na hakuwa na risasi nyingine. Vita ilianza kwa tensioni kubwa.
Rais alimjibu kwa sababu alijua Gwajima amemaliza risasi zake na hana tegemeo jingine tena. Hana kipya atakachoongea.
Polepole yeye katoa shambulio lililopoa Sana. Madhara yake sio makubwa.
Hata kuzima mitandao ni hofu tuu.
Lakini ni kiashiria kuwa Polepole anataarifa nyingi na nyeti sana.
Polepole angerusha mawe mazito hata vipande nusu ambavyo vitamfanya awaabishe adui zake na awapagawishe. Kisha hatua inayofuata aseme anakuja na ushahidi ambao utawashangaza, na aseme atauweke hadharani na kila mtu atauona.
Huku akisema amebakisha vyuma vingine ambavyo vitaitetemesha nchi.
Ukishatoa madai ya kumdhalilisha hasimu wako utakuwa upo nusu ya ushindi. Kuthibitisha utakuwa umemaliza kazi.
Kadiri Polepole anavyochelewa ndivyo mashambulizi yake yanakosa nguvu.
Yaani leo hata aje aseme kitu gani hakitakuwa na nguvu ya maana kama angeshambulia mwanzoni.
Tayari watu wameshazoea, watu wameshapredict, hasimu kashazoea tension jambo ambalo kwenye vita ya maneno sio zuri.
Soma >> GE2025 - Polepole: Kuongea na watanzania Agost 6, saa 2:00 kuhusu mustakabali wa taifa
Polepole hata zile trick za majigambo na mikwala ya kusema yeye yupo tayari kufa lakini lazima hasimu wake alale nao mbele hatilii mikazo katika laini hizo.
Yupo katika vita kubwa lakini anapambana kwa namna laini sana. Jambo ambalo unagundua kuna kitu hakipo sawasawa.
Anyway! Sisi tupo!
Na tutakuwepo!
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam