Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,104
- 43,357
Kwani tatizo la Watanzania ni Lowassa?
Mkuu wengi Tu wameshatangaza nia, akiwemo yule wa kimya kimya lakini CCM (Vuvuzela & company) wanahangaika Na EL ambaye bado hajatangaza even though nia ipo. Mtachokaaaaaaambona waliojitangaza kutaka urais wapo ila kla cku anatajwa huyu lowasa! naanza kuamin kuwa huyu jamaa ana power
Nashangaa chama kikongwe kama ccm kuruhusu kila anayejiona ana mapenzi na chama kutoa ushuzi hadharani. Haya hayakisaidii chama bali inaonyesha upeo mdogo wa viongozi wake. Kama mkuu wa wilaya alipandishwa cheo - wakati EL alimwona hafai - hayo ni matakwa ya JK na hatujui alitumia vigezo gani. Ndiyo maana hatusongi mbele
Kweli kabisa watu wazuri tukikaa kimya watu wabaya kama wewe mtaihodhi nchi hii na kujipa HATIMILIKI huku tunawaangalia mkiendelea KUUPEPETA!
KWA KIFUPI MZEE, NENDA KAWAAMBIE WANAFIKI WENZIO KUWA HAYA YA LOWASSA SI MAIGIZO NA MNACHOFANYA NI KUJARIBU KUZUIA MAFURIKO KWA MIKONO! POLENI SANA!
viongozi wa chama kuendelea kumsema mh.EL ni kuvunja kanuni na maadili ya chama.
Kumchonganisha kiongozi aliyeambiwa muda bado kwa watu ni sawa na kuzidi kumpatia umaarufu maradufu.
Kiongozi yeyote ndani ya CCM anayemchokonoa Mh.EL katika kipindi hiki ambacho chama kimepiga marufuku ya kampeni na kujinadi,hakika atakuwa asiye na akili timamu.
Sawa kusemana,lakini walau kwa kutumia akili na si kwa hotuba ndefu isiyokuwa na maana yeyote.
Si vyema na wala si lazima kuita watu na kuanza kumsema senior wako kwa mwamvuli wa UV-CCM.
Sidhani kama hiyo press comference ilikuwa kwenye schedule ya chama.
Lowassa ni fisadi Kwa mujibu wa kauli zenu mbona mnashindwa kumshgulikia MNA dola kila kitu. Mnacholinda hapa no ufisadi uliyofanyika miaka kumi mnaungana bila kujua kilicho waunganisha. CCM without Lowassa rest in peace.
watanzania wanatakiwa kumpuuza edward lowassa
.
Hivi vitoto vya mitaani vikishamtukana EL, vinazawadiwa ukuu wa wilaya. hivi ni nani mwenye mmlaka na kugawa hivi vyeo visivyosomewa? nahisi huyo ndie mfadhili wa kila mbaya wa EL na kwa maana hiyo yeye ndio mbaya kiongozi.
.
Kama mlijua yote hayo ilikuwaje bado ni mbunge, mwenyekiti wa kamati nyeti bungeni, na hata nafasi zote alizozishika baada ya kula hela za AICC? Japo mimi najua AICC ilijengwa wakati wa EAST AFRICA COMMUNITY Lowasa akiwa bado kijana na alikuwa umoja wa bijana na TANU. Lowasa amekuwa mkurugenzi na sio msamizi wa ujenzi wa jengo la AICC.
Kwa vile alitoka hapo na kuwa waziri hadi waziri mkuu huo unaoongea ni upuuzi ma unastahili kupuuzwa.
Issue ya afya ni siri ya mtu na daktari wake tupe ukweli na sio kuropoka. Mrema alipoambiwa anaumwa aliweka vyeti wazi wewe weka vya Lowasa. Mbona JK alianguka majukwaani wakati wa kampeni lakini hadi sasa ni raisi?? Mkikosa cha kuongea muwe mnakaa kimya. Watanzania mnao onhea nao sio wale wa 1954, hilo mlijue kabisa.
Naomba niweke angalizo hapa mimi sio mwana Ccm na wala sijawahi kuwa mwana Ccm na sitokaa niwe mwana Ccm kutokana na unafiki wenu, ila imenilazimu kuandika haya kupinga huu ujinga wa kitoto mnaoanza kuwaletea watu wenye akili.
Mungu alishakataza ufisadi katika Ardhi. Iweje Mungu huyo huyo amteua fisadi kuwa Rais wa nchi?
Mkuu Kama ni hivyo mbona huu mtambo wa kuzalisha mafisadi -ccm hatujauteketeza toka kwenye USO wa duniaMungu alishakataza ufisadi katika Ardhi. Iweje Mungu huyo huyo amteua fisadi kuwa Rais wa nchi?