Press conference: Lowassa apelekewa ujumbe mzito

Press conference: Lowassa apelekewa ujumbe mzito

Lowasa alihusika na ufisadi ujenzi wa jengo la ukumbi wa mikutano AICC?! Haya si yalijengwa Lowasa akiwa labda primary school? CCM msiruhusu wajinga kama huyu hoza kuvuruga watu. Lowasa atuhumiwe kwa haki si uzandiki kama huu.
Mimi sioni tatizo hata kama Lowassa ni fisadi; atupatie orodha ya wanachama wenzie ambao sio mafisadi kwanza
 
Aa Sisihuku Tunachekea Pembeni, Tunasubili Mumpitishe Huyo Lowasa, Alafu Tuchukue Nchi Mapemaa.
 
Tunasubiri huyu naye pia akemewe na kupewa adhabu stahiki, maana anafanya kampeni kabla ya muda. Lowassa amefungiwa hawezi kajibu na hivyo huyu kijana kupewa fursa ya namna hii bila kukaripiwa ni kumwonea Lowassa au mtu mwingine yoyote. Pia ni utovu wa nidhamu kumhusisha mtu na mabaya ambayo huna hakika nayo na hasa mtu anayekuzidi umri!
 
Starring: Francis Heri Hoza
Directed by: Paul Makonda
Produced by: Nape Nnauye
Membe & Co. Productions © 2015
 
Mimi sioni tatizo hata kama Lowassa ni fisadi; atupatie orodha ya wanachama wenzie ambao sio mafisadi kwanza
Wanachama wengine kuwa mafisadi haimpi haki Lowasa naye kuwa fisadi, labda kama nia yako ni kutuaminisha kwamba kweli ccm ni chama cha mafisadi.
 
Wanachama wengine kuwa mafisadi haimpi haki Lowasa naye kuwa fisadi, labda kama nia yako ni kutuaminisha kwamba kweli ccm ni chama cha mafisadi.

Tunamtaka huyo ambaye sio fisadi ili tujipange kumpa kura ya uraisi; afadhali fisadi atakayechapa kazi kuliko fisadi atakayekaa ikulu akichapa usingizi kusubiri migao
 
Hii nyumba ya jirani kwa huu moto unaowaka, mpaka ifike mwezi wa nane itakuwa imebaki majivu.
 
Nashangaa chama kikongwe kama ccm kuruhusu kila anayejiona ana mapenzi na chama kutoa ushuzi hadharani. Haya hayakisaidii chama bali inaonyesha upeo mdogo wa viongozi wake. Kama mkuu wa wilaya alipandishwa cheo - wakati EL alimwona hafai - hayo ni matakwa ya JK na hatujui alitumia vigezo gani. Ndiyo maana hatusongi mbele
 
WATANZANIA WANATAKIWA KUMPUUZA EDWARD LOWASSA

attachment.php


...................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Mwisho upo msemo usemo MAMBO HAYAENDI VIBAYA KWA SABABU WATU WABAYA WANAYAFANYA LA HASHA ILA NI KWA SABABU WATU WAZURI WAMEKAA KIMYA...Kwa niaba ya watu wazuri wote wanaoitakia mema nchii hii Nimeamua kuvunja ukimya dhiidi ya watu wabaya wanaotaka kulipeleka taifa hili sehemu mbaya

Asanteni kwa,kunisikiliza
Nawatakia kazi njema.

Comrade Francis Heri Hoza Mjumbe kamati ya utekelezaji ya balaza la UVCCM mkoa wa morogoro Na Mwenyekiti mstaafu wa shirikisho la ELimu ya juu la wanachama wa CCM Mkoa wa morogoro.

Kweli kabisa watu wazuri tukikaa kimya watu wabaya kama wewe mtaihodhi nchi hii na kujipa HATIMILIKI huku tunawaangalia mkiendelea KUUPEPETA!
KWA KIFUPI MZEE, NENDA KAWAAMBIE WANAFIKI WENZIO KUWA HAYA YA LOWASSA SI MAIGIZO NA MNACHOFANYA NI KUJARIBU KUZUIA MAFURIKO KWA MIKONO! POLENI SANA!
 
Tunamtaka huyo ambaye sio fisadi ili tujipange kumpa kura ya uraisi; afadhali fisadi atakayechapa kazi kuliko fisadi atakayekaa ikulu akichapa usingizi kusubiri migao
Unataka kumpeleka Ikulu ndiko akachapie kazi yake ya ufisadi?! Nilifikiri sehemu stahiki ya fisadi yeyote ni jela!
 
viongozi wa chama kuendelea kumsema mh.EL ni kuvunja kanuni na maadili ya chama.
Kumchonganisha kiongozi aliyeambiwa muda bado kwa watu ni sawa na kuzidi kumpatia umaarufu maradufu.
Kiongozi yeyote ndani ya CCM anayemchokonoa Mh.EL katika kipindi hiki ambacho chama kimepiga marufuku ya kampeni na kujinadi,hakika atakuwa asiye na akili timamu.
Sawa kusemana,lakini walau kwa kutumia akili na si kwa hotuba ndefu isiyokuwa na maana yeyote.
Si vyema na wala si lazima kuita watu na kuanza kumsema senior wako kwa mwamvuli wa UV-CCM.
Sidhani kama hiyo press comference ilikuwa kwenye schedule ya chama.
 
Lowasa alihusika na ufisadi ujenzi wa jengo la ukumbi wa mikutano AICC?! Haya si yalijengwa Lowasa akiwa labda primary school? CCM msiruhusu wajinga kama huyu hoza kuvuruga watu. Lowasa atuhumiwe kwa haki si uzandiki kama huu.

Hayo majengo yalijengwa 1974, na shirika la kitaliani Condote, lowasa alifanya kazi AICC na kuna habari zilivuma alihusika na uvujaji Mali akiwaangalia kiongozi AICC, hata inasemekana yeye na wenzake walimyanganya shamba la njiru na kijege aliyekuwa mmiliki na wakagawana na kuwauzia watu plots na mashirika. Anahusika na shirika la TICS la maconteiners bandarini ambalo linamolikiwa na rafiki zake Rustim
 
Kila mtu anahaki ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi katika nchi hii, mradi anatimiza masharti ya nafasi husika kama Katiba ya nchi inavyotaka.
 
NI YUPI ALIE MSAFI NDANI YA CCM MPAKA NDG LOWASA AONEKANE NDIYE MCHAFU KUWAZIDI WOTE/ jr
 
Lowassa ni fisadi Kwa mujibu wa kauli zenu mbona mnashindwa kumshgulikia MNA dola kila kitu. Mnacholinda hapa no ufisadi uliyofanyika miaka kumi mnaungana bila kujua kilicho waunganisha. CCM without Lowassa rest in peace.
 
Mbona mnahangaika sana???????? Mtatuaminisha sasa na sisi kuwa huyu jamaa anafaa
 
Back
Top Bottom