NI VICHEKESHO,
WANAOMSHAMBULIA LOWASA RUKSA!!
WANAOTOA MAONI YAO KWAMBA LOWASA ANAFAA, HAPA TUNA AMBIWA LOWASA ANAFANYA KAMPENI!
Hii ina tofauti gani na unampiga mtu huku umemfunga mikono asijibu wala kujitetea?
The much I know Huyu bwana hajatangaza kugombea urais.
Basi kama ni ruksa watu kutoa maoni yao kwa mtu asiyefaa kugombea basi na iwe ruksa na watu kushauri au kwenda kumsihi mtu atangaze nia.
Mti wenye matunda mazuri ndio hupigwa mawe na wenye akili zetu tumesha realize kwamba Lowasa anafaa.
Hili kwa kweli lazima tulipigie kelele.
Sio haki kabisa.
Huu ni uonevu mkubwa na unafanywa makusudi ili ajibu halafua waanzishe malumbano yasiyo na tija.
Mfano tu Juzi prof. Muhongo na Januari tumeambiwa wamepewa tuzo ya wanasiasa wenye mafanikio ,hili ni jambo zuri mtu akisifiwa lakini hata hivyo sijamsikia hatujamsikia Membe na Nape wakitoa tamko la kupinga na kusema kuwa hiyo tuzo ilipangwa.
Lowasa akiambiwa kuwa anaongoza kwenye tafiti inakua ni jazba na vitisho kwa wale walioandaa tafiti hizo.
Ni kweli kabisa kama kusema kuwa mtu anafaa kugombea urais ni kampeni basi hata kusema kuwa hafai nayo ni kampeni pia mana zote zina zungumzia uchaguzi.
Kama tunaambiwa watu wanatumwa kumshawushi agombee basi tuambiwe pia hawa wengine nao wametumwa kwani ikulu sio mali ya kikundi cha watu hata waamue eti fulani yeye hafai hata kuchukua form ili tuasiingie wakati amekua mpaka waziri mkuu.
Mfano uko wazi wakati serikali na viongozi wa CCM imesema wananchi wapigie kura ya NDIO kwemye katiba pendekezwa ,lakini jumuia ya maaskofu wa kikristo waliposema ipigiwe kura ya HAPANA ilionekana kwamba ni kuwashinikiza wananchi na nikinyume na demokrasia na ilileta mzozo mkubwa.
Kwenye siasa kupinga na kukubali vyote ni kampeni.
Kwa hiyo wanaopita kumpiga kampeni kuwa Lowasa hafai nao wakemewe vinginevyo na wale wanaosema anafaa waachwe .
Hiki lisipopigiwa kelele litaendeleza hizi siasa za chuki na visasi ndani ya CCM.
Utumishi na uongozi wa umma hautakiwi ufanyike kwa chuki na makundi kwani hakuna anayeweza kusema atatawala kwa katiba yake tofauti na katiba na sheria za nchi.