Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 56,914
- 30,975
Kampuni ya ndege ya Precision Air kuongeza safari za ndege zake
19 May 2008
By ITV Habari
Kampuni ya ndege ya Precision Air imesema itaongeza safari za ndege zake kutokana kuwepo kwa ndege mpya aina ya Boing 737 Dashj 300 iliyokodishwa kutoka nchini Ireland na kuanza kutoa huduma zake hapa nchini.
Meneja ubora na usafiri kutoka shirika hilo Bw. Allen Sharra amesema kwa sasa ushindani katika sekta ya usafiri wa anga umekuwa mkubwa, na kinachotakiwa ni kutoa huduma bora kwa wateja na kuhakikisha wanajipanga vema kukabiliana na ushindani.
Kwa sasa shirika hilo lina jumla ya ndege 9 zinazotoa huduma katika mikoa mbalimbali hapa nchini, na kuongeza kuwa ujio wa ndege hiyo utaongeza safari za shirika hilo katika nchi za Rwanda, Angola, Lubumbash, na Johannesburg.
*
19 May 2008
By ITV Habari
Kampuni ya ndege ya Precision Air imesema itaongeza safari za ndege zake kutokana kuwepo kwa ndege mpya aina ya Boing 737 Dashj 300 iliyokodishwa kutoka nchini Ireland na kuanza kutoa huduma zake hapa nchini.
Meneja ubora na usafiri kutoka shirika hilo Bw. Allen Sharra amesema kwa sasa ushindani katika sekta ya usafiri wa anga umekuwa mkubwa, na kinachotakiwa ni kutoa huduma bora kwa wateja na kuhakikisha wanajipanga vema kukabiliana na ushindani.
Kwa sasa shirika hilo lina jumla ya ndege 9 zinazotoa huduma katika mikoa mbalimbali hapa nchini, na kuongeza kuwa ujio wa ndege hiyo utaongeza safari za shirika hilo katika nchi za Rwanda, Angola, Lubumbash, na Johannesburg.
*