Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Sitegemei wale wa TLP na UDP (Mrema na Cheyo) nao wakatae "posho za vikao"..
 
Wabunge wa chama cha NCCR mageuzi wamesema wameandika barua kumtaka spika azielekeze posho zao kwenye mfuko wa maendeleo Kigoma. Wamesema watampatia spika barua hiyo kesho. Source: Taarifa ya Habari Channel Ten, Saa moja jioni, 12/06/2011.
ni kweli hata mimi nimeona na ka Spika ana akili timamu inabidi awakubalie badala ya kuleta siasa ka alivomfanyia Zitto! Wakati umefika,hakuna jinsi na inabidi akubali vinginevo hataeleweka kwa wenye nchi.
 
Nccr wanapenda sana kufuata mkumbo. Walikuwa wapi kuanza? Walisubiri mpka zito aanze ndo wafuatie?
 
Nccr wanapenda sana kufuata mkumbo. Walikuwa wapi kuanza? Walisubiri mpka zito aanze ndo wafuatie?

Hizi ni siasa za Kigoma typical, wanajua kuwa 2015 wataulizwa mwenzenu Zitto alielekeza posho zake kwa ajili ya maendeleo ya Kigoma kwa nini ninyi hamkufanya hivyo?. Na kama Peter Serukamba naye angekuwa hana ngao ya kulindwa na Chakachua nae angetangaza the same. Tukiwa na uchaguzi huru na haki nchi itaendelea, CCM kiburi chao kinatokana na kushindishwa na wakurugenzi wa uchaguzi na si wananchi, hivyo hutasikia hata mmoja akiunga mkono hoja hii ya wananchi.
 
lakini kudos ni kwa cdm ambaye nimuanzilishi kama vip kudos zitto..
CDM bado wanakula posho,mpaka za halmashauri Arusha wasikomtambua meya,na katibu mkuu wao anaishi kwa posho....don't even go there!
 
Wabunge wa kweli wataonekana baada ya posho kufutwa. Leo kuna posho, bado kuna wabunge kibao wanakacha vikao vya bunge,sembuse kusipokuwa na posho.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kupitia Naibu mkuu wa kambi ya upinzani Mh Zitto Kabwe wameonyesha uvumbuzi, ujasiri, uzalendo na uchungu wa matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazodidimiza maendeleo ya nchi. Tatizo linakuja kwa jamaa wa magamba watakuwa na uzalendo wa kuiunga mkono hoja ipitishwe au watakataa kwa sababu wao ndio wengi kama itapigwa kura ya kuiondoa hiyo posho. Yetu macho.Kuna fununu eti posho ikiondolewa wabunge wengi hawatahudhuria vikao, naomba msaada wenu mnaojua kanuni na sheria zinazotumika kuendesha vikao vya bunge.

1. Je, ni HIARI au ni LAZIMA kwa Mbunge kuingia kwenye vikao vya bunge vinavyoendeshwa kwa kodi zetu wamachinga, wakimbizwa na mgambo wa jiji, wakulima wa jembe la mkono tunaotegemea kudra za Mwenyezi Mungu kuleta mvua ili tuvune, wafanyakazi wanaonyanyaswa na kufanya kazi mazingira mabovu ambao mshahara wetu haufikii hata posho moja ya mbunge.?

2. Je, kuna adhabu yoyote anayopewa mbunge asipohudhuria kikao?

NAOMBA KUWAKILISHA
 
Kinachoweza kuwakwamisha wabunge wasiende Dodoma ni kukosa posho ya kujikimu (hii haijapingwa). Wakishalipwa hii, wana haja gani kulipwa nyingine ya vikao, wakati ndiyo kazi waliyokwenda kufanya? Maoni yangu, hakuna haja ya kuilipa, bali uwekwe utaratibu wa kuwabana wasipohudhuria vikao. Kwa sasa kanuni inawabana wasipohudhuria mikutano mitatu mfululizo. Hivyo mbunge anaweza asihudhurie bunge zina la bajeti, pia akakacha la novemba asifanywe kitu. Hapa kuna tatizo.
 
wajibu wa mbunge ni kuhudhuria vikao kuwakilisha wananchi na analipwa mshahara na si posho.kuhudhuria ni wajibu wake kama mfanyakazi wa kawaida,vinginevyo awajibishwe.
 
Kinachoweza kuwakwamisha wabunge wasiende Dodoma ni kukosa posho ya kujikimu (hii haijapingwa). Wakishalipwa hii, wana haja gani kulipwa nyingine ya vikao, wakati ndiyo kazi waliyokwenda kufanya? Maoni yangu, hakuna haja ya kuilipa, bali uwekwe utaratibu wa kuwabana wasipohudhuria vikao. Kwa sasa kanuni inawabana wasipohudhuria mikutano mitatu mfululizo. Hivyo mbunge anaweza asihudhurie bunge zina la bajeti, pia akakacha la novemba asifanywe kitu. Hapa kuna tatizo.
kwa mujibu wa kanuni hizo hapo kuna tatizo kubwa ambalo linatakiwa zirekebishwe haraka maana zinatoa loop holes nyingi sana kwa wabunge kutohudhuria vikao. vikao vitatu ni vingi sana,hakuna dharura ya namna hiyo hata ktk idara zingine za serikali unless kuwepo na justifications kwa cases very special like illness etc na sio kukacha bila sababu,kwa nini wabunge wapewe upendeleo as if wao ni tofauti na wafanyakazi wengine? na kwa kukosa kuhudhuria vikao hivyo vitatu mfululizo,uwakilishi wa wale waliomchagua upoje? pia,kanuni zinaelekeza adhabu gani kwa atakae acha kuhudhuria vikao hivyo?
 
Kuna mkakati wa Wabunge wa CCM kuandaa mandamano hadi kwa Mkuu wao raisi Jk kupinga kitendo cha wabunge wa CHADEMA na NCCR kutaka posho zifutwe. Inadaiwa kitendo cha posho kufutwa kitawaasili sana katika mikakati yao kurudi bungeni mwakani. Kwani wamekuwa wakitumia sehemu ya posho hizo kuandaa Kanga, Vitenge, Pilau, Mashindano ya kombe la mbunge na mengineyo.
Maandalizi yote kwa ajili ya Maandamano hayo inadaiwa yamekamilika na ratiba inaweza kutangazwa mda wowote kuanzia sasa.
 
Kuna mkakati wa Wabunge wa CCM kuandaa mandamano hadi kwa Mkuu wao raisi Jk kupinga kitendo cha wabunge wa CHADEMA na NCCR kutaka posho zifutwe. Inadaiwa kitendo cha posho kufutwa kitawaasili sana katika mikakati yao kurudi bungeni mwakani. Kwani wamekuwa wakitumia sehemu ya posho hizo kuandaa Kanga, Vitenge, Pilau, Mashindano ya kombe la mbunge na mengineyo.
Maandalizi yote kwa ajili ya Maandamano hayo inadaiwa yamekamilika na ratiba inaweza kutangazwa mda wowote kuanzia sasa.
Nasuburi kuona kama Mbunge menye pua kubwa kuliko wote bungeni naye ataandamana.
 
Kuna mkakati wa Wabunge wa CCM kuandaa mandamano hadi kwa Mkuu wao raisi Jk kupinga kitendo cha wabunge wa CHADEMA na NCCR kutaka posho zifutwe. Inadaiwa kitendo cha posho kufutwa kitawaasili sana katika mikakati yao kurudi bungeni mwakani. Kwani wamekuwa wakitumia sehemu ya posho hizo kuandaa Kanga, Vitenge, Pilau, Mashindano ya kombe la mbunge na mengineyo.
Maandalizi yote kwa ajili ya Maandamano hayo inadaiwa yamekamilika na ratiba inaweza kutangazwa mda wowote kuanzia sasa.
Haaa! Kumbe uchaguzi Mkuu utafanyika mwakani? Au ni mimi tu sijakuelewa Mkuu? Any acha waandamane wengine hawajawahi fanya zoezi la kutembea hata nusu kilometa. Polisi wasitoe ulinzi ili tuwatimulie vumbi mitaani. Wezi wakubwa badala ya kuandamana kudai maisha bora kwa wananchi wanalilia wizi kupitia posho. Kila siku nimekuwa nikiamini kuwa Mwana CCM ni lazima akili zifyatuke
 
Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png



Join Date : 12th June 2011
Posts : 11
Thanks0Thanked 1 Time in 1 Post

Rep Power : 0
 
1: Mwakani 2012 hakuna uchaguzi wa wabunge. 2:Huu ni utani tu.
 
mkuu acha waandamane kwani wamekanyagwa mkia. wabunge wa magamba kinachowapeleka bungeni ni posho tu na si lingine asiyejua nani? kwa hiyo wala hatushangai tunawasubiri na maandamano yao.
 
Back
Top Bottom