Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Bado sijamwona swahiba wa MS, Faiza Foxy sijui nae ataendeleza utaifa unaoanza kumwingia MS au ataendelea kushikilia magamba yake yasidondoke.
 
Wewe ni limbukeni mkubwa naona we na shozi mmetumwa na NAPE,Upeo wenu ni finyu,mnawaza kwa kutumia makamasi,hamna uzalendo wa nchi hii,haya waslimieni Masaki na mmwambie yule mdogo anayesoma MAREKANI kwa WIZI ZA wa kodi za maskini wa TANZANIA,arudi kuja kuwasalimu.
 
Cdm kazeni uzi,pasijetokea mgawanyiko!Wananchi tuko nyuma yenu!we are supporting you all!Keep on going
 
me naungana na ww kaka huyu zitto ni mnafiki wa cdm mbona kuna pesa gari na kiwanja cha ufukweni alihongwa na thithiem ameshindwa kusema vipelekwe jimboni?wajinga wenzie wa cdm ndo ataendelea kuwa fitini lkn sisi wengine tunaojua data zake tunamwangalia.in short anatafuta umaarufu kupitia hizo posho km kawaida yake.
Sasa si alihogwa na mijinga ulitaka afanyeje!
CCM mmekwisha kabisa!
ZITTO WE ENDELEA TU NA MOVE YAKO! ACHANA NA HAWA MAFISADI WA MAGAMBA
 
Wanasiasa wanawageuza wananchi kuwa wajinga, na bahati mbaya tunaponzwa na ushabiki wa vyama. Akishasema kiongozi wangu wa chama ni sahihi hakuna kuquestion.

Ukisoma Habari Leo, ya leo Mbowe anasema Shangingi lake (V8) hawezi kuacha kulitumia sababu tayari kashapewa, anasahau katibu wake (Dr.Slaa) alivomshambulia W/Mkuu kuwa anatumia gari la kifahari.
Na kwa nini ruzuku za vyama zisivutwe, wanachama ndio wachangie vyama vyao? Tunapoteza pesa nyingi kwa vyama ambavyo mi naona wengi ni kunufaisha viongozi wa vyama vya siasa. Hili hawataki kabisa.
Ukiangalia kwa undani unaona kuwa hatujawa na viongozi wenye nia ya dhati. Wengi ni makelele ya kutafuta umaarufu na kuchumia matumbo yao.
Let us be realistic,Wanachama wengi ikija kwenye kuchangia vyama vyao wanakuwa wagumu.Kapite mapato na matumizi ya chadema wakati wa uchaguzi uangalie ni kiasi gani wanachi walichangia pamoja na kufanya kampeni kubwa ya kuwaamasisha wananchi kuchangia.

Mapato makubwa yanatokana na wafanyabiashara wakubwa na asilimia kubwa wanajua pesa zao zitarudi kwa namna moja au nyingine kupia misaada yao.Wengi wetu sisi wachangiaji wadago wadogo ikija kwenye swala la kuchangia, we are talking the talk not walking the walk.
 
Shosi, naona na wewe ni mbunge au umetumwa na mbunge. Kupunguza posho maanake nn? CDM wameshatoa msimamo kuwa posho hawazitaki, zielekezwe kwingine, kwa huli wameshatimiza wajib wao tuliowatuma bungeni. Maamuzi magumu kama haya yanauma sana ingawa ya manufaa kwa uma wa waTZ. Wewe na Nkulo mna mawazo yanayofanana. HUU Ni Mwiba mkali kwa CCM
 
Inatakiwa siku hiyo kupiga kura ya ndio au hapana,siyo ile kura ya siri,ili tuweze kuwaona na kuwajua wabunge wetu wanaotokwa mate pamoja na udenda wa posho.
 
Watanzania tumekuwa watu wa ajabu sana. Namshangaa mtoa mada anamwita Zitto mnafiki. Ningekuona wa maana kama ungempongeza kwanza then ungeshauri njia bora za matumizi ya hizi pesa, sio kumkejeli. Lazima tukubali kwamba this is a step in the right direction. Inaonekana kwako unaona ni sawa tu, tena kuna wabunge wengine useless hata michango huwa hawatoi, kazi wanayofanya ni kula posho tu.
KDI ni ya nani? Nani mwanzilishi wa KDI?
 
"Kwa mfano, mimi ni mjumbe wa Kamati ya Uongozi (ya Bunge), nasaini 'sitting allowance' katika kikao cha Bunge, nikiitwa katika kikao cha kamati ya uongozi nasaini tena sitting allowance na hata kama kutakuwa na kikao kingine jioni naweza kulipwa, sasa kama huo siyo wizi ni nini?"

Alisema pamoja na kwamba wabunge wa Chadema akiwamo yeye wanachukua posho hizo, kamwe hawataacha kusema kwani tatizo si wao kuchukua, bali sera inayoruhusu ufujaji huo wa mali ya umma.

Maneno ya rangi nyekundu hapo juu yamesemwa na Chairman Mbowe.
Huyu Mangi hayuko serious. Anaping posho huku anadai yeye na wenzake wataendelea kuichukua.
Bunge letu ni la kupewa pole kwa kuwa na Kiongozi wa Upinzani kama Mbowe....what a disgrace to Tz!
Kama mmegundua kuwa mnaibia Watz si muache kuendelea kuchukua kama Zitto?
ACHENI UNAFIKI.
 
Inabidi tuanzie mahala: kuokoa pesa za walipa kodi na kupunguza kasi ya watu kukimbilia siasa badala ya taaluma zao. Posho za wabunge zifutwe.
 
asipo saini unajua zitaenda wapi ! kama bado suala hilo halijapatiwa ufumbuzi na kusitishwa kisheria akiziacha zitaenda kwa magamba kumshughulikia yeye mwenyewe, hivyo kuzichukuwa ni lazima ila azielekeze kwa watu walio mchagua, azikusanye wee zikiwa nyingi awapelekee jimboni kwake kuongeza nguvu katika shughuli za maendeleo.
 
"kwa mfano, mimi ni mjumbe wa kamati ya uongozi (ya bunge), nasaini 'sitting allowance' katika kikao cha bunge, nikiitwa katika kikao cha kamati ya uongozi nasaini tena sitting allowance na hata kama kutakuwa na kikao kingine jioni naweza kulipwa, sasa kama huo siyo wizi ni nini?"

alisema pamoja na kwamba wabunge wa chadema akiwamo yeye wanachukua posho hizo, kamwe hawataacha kusema kwani tatizo si wao kuchukua, bali sera inayoruhusu ufujaji huo wa mali ya umma.

maneno ya rangi nyekundu hapo juu yamesemwa na chairman mbowe.
Huyu mangi hayuko serious. Anaping posho huku anadai yeye na wenzake wataendelea kuichukua.
Bunge letu ni la kupewa pole kwa kuwa na kiongozi wa upinzani kama mbowe....what a disgrace to tz!
Kama mmegundua kuwa mnaibia watz si muache kuendelea kuchukua kama zitto?
Acheni unafiki.
nashawishika unafikiria kwa kutumia makalio badala ya ubongo.
 
KDI ni ya nani? Nani mwanzilishi wa KDI?

Nina mashaka na uelewa wa mtoa mada hasa baada ya kuuliza hili swali. Kabla hujashutumu ni bora ukafanya uchunguzi na uje na taarifa kamili kuwa KDI ilianzishwa lini, nani aliianzisha na inashughulika na nini kuliko kuja kumwaga porojo hapa Jamvini, Hapa tunaondoa kabisa dhana ya Great thinker kwa mtindo huu, Wanajamii kabla hujapost kitu ni bora ufanye uchunguzi na uje na Uzi kamili, Inashangaza mtoa habari yeye baada ya kuuuelewesha uma na yeye anakuwa miongoni mwa wauliza maswali kwa habari/makala aliyoileta. Next time usipost kitu kama hujafanya uchunguzi sababu nitaku-:brick:
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Hii hoja sio ya FAM na ZZK, ni hoja ya watanzania wote wenye kupenda nchi yao. Tulifanyie kazi.
 
Sitegemei Hamad azungumze tofauti na alivyosema kwa kuwa hiyo ilikuwa ni hoja ya Chadema. Na hapo mjue huyu bwana kafika mwisho wake wa maisha ya kisiasa. Unaona hata uongozi wa wabunge wa cuf chama chake kimemuengua. Hana jipya.
 
Kwani mwizi akikiri kosa katika famili, anaambiwa ni mnafiki au assibe tena. Watu wangine tumekosa uzalendo kabisa kiasi cha kua vipofu. Walimu watu wanaolipwa 200,000 wanapata teaching allowance kwa kufundisha kwanye mazingira magumu. Zile seat za bunge letu ni too comfotable to get an allowance. Wako wafanyakazi wanaofanya kazi za hatari sana na hawapewi allowance. Trilioni moja, hela ya kujikimu, mshahara millioni 12. yote hayo unamwambia nini mkulima wa Tanzania. Eti unafiki. Rafiki!

Ahsante sana FS. Trillioni moja ni pesa nyingi sana ambayo inaweza kumaliza au kuyapunguza baadhi ya matatizo katika nchi yetu kama vile kuhakikisha Wajawazito wanakuwa na vyumba vikubwa badala ya kuendelea kubanana katika vyumba vidogo na pia kuhakisha kwamba hakuna mja mzito nchini atakayelala chini tena au kushare kitanda na wajawazito hadi saba! Zinaweza kuhakikisha wanafunzi wetu hawakalii matofali tena au kukaa chini na pia kusomea katika vyumba visivyokuwa na hadhi ya kuitwa madarasa.

Kuongeza vyoo mashuleni au kujenga vipya katika mashule yasiyo na vyoo. Kuongeza mishahara/marupurupu ya walimu/madaktari/manesi ili waweze kusaidiwa katika kukidhi kupanda sana kwa gharama za maisha.

Wengine chochote kile kitakachosemwa na kiongozi wa CHADEMA hata kama kimejaa busara na hekima za hali ya juu katika kuboresha au kuongeza tija ndani ya nchi yetu bado watakiona ni kibaya tu tena kimejaa unafiki, lakini cha kutia moyo ni kwamba Watanzania wengi wameanza kufungua macho.
 
Hii nimeipenda maana sasa inawapiga wabunge wa magamba kwenye ankle watashindwa kutembea.
Nafikiri ili kuwamaliza, CDM iwarecord wabunge wa magamba watakao kuwa wanapinga hoja hiyo kisha baada ya bunge ni kupita majimboni kwao kumalizia mchezo.

Huu ni mtego makini bunge hili hawatapigiana makofi tena!

Hongera chadema kwa maujanja yenu!
 
Back
Top Bottom