Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Sitegemei Hamad azungumze tofauti na alivyosema kwa kuwa hiyo ilikuwa ni hoja ya Chadema. Na hapo mjue huyu bwana kafika mwisho wake wa maisha ya kisiasa. Unaona hata uongozi wa wabunge wa cuf chama chake kimemuengua. Hana jipya.

Sio hivyo tu huko zanzibar kuna wabunge wengine kwanza ni kama madiwani wa Tanzania bara. Kuna majimbo mbunge jumla ya idaidi waiga kura jimboni ni i kichekesho .Mpaka unajiuliza serikali ilikuwa na ulazima gani wa kugawanya majimbo mengi hivyo.

Na bado wananchi tutadai hata idadi ya wabuge na majimbo ipungue maana inaonekana mengi yanaanzishwa kwa sabbau ya kisiasa.
 
mkuu in the model world you head should be multi-task hata simu siku hizi ni multi-task hacha uvivu
yeah?! Multi. Thas y as a nation we fail to set priorities. Start with mkukuta then kilimo kwanza, mafisadi, then fuel, prices, inflation, infrastructure, health, education, water, then samunge, RACHEL, magamba, bajet, posho, u name it. Miluzi mingi humpoteza mbwa
 
Sio hivyo tu huko zanzibar kuna wabunge wengine kwanza ni kama madiwani wa Tanzania bara. Kuna majimbo mbunge jumla ya idaidi waiga kura jimboni ni i kichekesho .Mpaka unajiuliza serikali ilikuwa na ulazima gani wa kugawanya majimbo mengi hivyo.
We ngoja Katiba mpya ije, wabunge-madiwani wa Zanzibar tunawachinjilia baharini. Na Muungano wenyewe tunauvunja.
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Haya maposho yakiondoka itakuwa na faida kubwa sana katika uchumi wa tz kwa kuwa itaögeza investment multipler. Wabunge wasiongope waunge mkono hoja hii ya cdm kwa sababu rate ya wasomi wanaohitimu haiendani na level ya maendeleo yasije yakatokea ya libya na misri. Nimawazo 2
 
Mohamed Shossi said:
Wanasiasa siku zote huwa wanawafanya wananchi kuwa ni wajinga na hawana uwezo wa kufikiri. Haijalishi mwanasiasa anatokea chama gani au jimbo gani wote hutegemea umbumbumbu wetu kuwa ni mtaji wao.Si tumewasikia wakipinga posho za vikao vya bunge?wengine wamefika mbali hata kuandika barua kusema hawataki posho na wameelekeza kuwa posho zisiingie mfuko wa "shati" bali ziingizwe moja kwa moja kwenye mfuko wa "koti" kimantiki wanasema hawataki posho dhumuni likiwa kubana matumizi ya serikali sasa unapoikataa na kuelekeza ile ile posho upewe lakini kwa kutumia utaratibu mwingine ni usanii na kiini macho!

Nashangaa watu wameshindwa kuelewa hili na kulisifia! Sijui ni upovu au ni umbumbumbu wetu ndio unaotufanya tuwe hatuoni! au sijui ni "ukipenda chongo"?Tumeshuhudia posho zao wanazopeana tena huku wakikataa zisikatwe kodi ambayo itasaidia kuongeza makusanyo ya serikali. Kwa akili ya kawaida na mwenye uwezo wa kufikiri hawa wanaopiga kelel kuhusu posho tuwaulize wao wakiwa nje ya makao makuu kwa ajili ya shughuli za chama kama zile zilizozoeleka za "maandamano ya nguvu za umma" wanalipana posho kiasi gani? nusu ya hizo wanazogomea au zimezidi? au hawalipani kitu kwa kukwa wapo kwenye kazi walizopewa na chama? Kama wanalipana basi wanatafuna pia mapato yanayotokana na mlipa kodi kwani wanatumia ruzuku wanayopewa ambayo inatokana na kodi zetu!

My take:Kwa kuonyesha nia njema haitakuwa vibaya vyamka vya siasa vikaomba kupunguziwa ruzuku ili pesa nyingine zitakazobaki zikaelekezwa kwenye kufidia bajeti kuu. Najua hili litakuwa gumu sana lakini madhalan chama kina pokea 100 kikipokea 50 n a hamsini ikaelekezwa kwenye maendeleo si jambo baya na hii iapply kwa vyama vyote pamoja na chama tawala.

Shossi,

..kwa upande wangu nadhani hili ni wazo ambalo bado ni changa na linapaswa kufanyiwa kazi kwa minajili ya kuliboresha.

..hakuna haja ya kuanza kuitana majina kama huyu MNAFIKI, ua huyu vile ktk kujadili suala sensitive kama hili.

..kwa mtizamo wangu, alicho-suggest Zitto ni kitu kizuri, isipokuwa tunatakiwa tutafute njia za kuziba mianya ya ubadhirifu inayoweza kujitokeza huko mbeleni.

..nasikitishwa sana na kauli na msimamo wa serikali kupitia waziri wa fedha Mustapha Mkulo. yeye ameonyesha nia ya kuwagawa wabunge na kuwakomoa waliotoa hoja hii kwa kutumia suala hili la posho.

..KINACHOPASWA KUFANYIKA NI WABUNGE KUTAFUTA NAMNA YA KUBANA MATUMIZI NA KUZIELEKEZA PESA ZITAKAZOOKOLEWA KWENYE MIRADI YA MAENDELEO NA HUDUMA ZA KIJAMII.
 
Kama Sheria zitaruhusu basi wabunge wa ccm washtakiwe kwa kuhujumu uchumi, pamoja na bajeti je makadiria na matumizi ya Bunge yanajukikana?
 
dah! "we love our country but our country don't lv us" watawala wetu wametumia elimu tulizowasomesha kwa kodi zetu kutusaliti kwa nguvu zote. wabunge wanakomalia posho kuliko maslahi ya taifa letu watz, hawana uzalendo hata kidogo isipokuwa wana matumbo? saa inakuja watawala wote mkae chonjo, kwa kuwa hamjui saa wala wakati ambao nguvu ya UMMA itakapokuja kwenu, kwani itakuwa ni kilio na kusaga meno, nyie endeleeni kujimwagia Petrol na kuogea mafuta ya taa karibu na moto tu.Mungu ibariki TZ, MUNGU ibariki CDM.​
 
Mimi ninachoshindwa kujua hapa ni kuhusu hawa wabunge. Mwajiri wao ni nani na anawalipa mshahara wa mwezi kwa kazi ipi.
Mimi nafikiri wabunge ni kama madiwani ambao wanaisimamia serikali, hivyo wanatakiwa kulipwa posho tu wanapohudhuria vikao.
Kinyume chake wamajiwekea mishahara minono, posho za kugusa tu, mashangingi nk. na kuwaacha mbali watumishi wa umma na binafsi ambao ndo wanastahili kulipwa mshahara wa mwezi.
Na wanachofanya kubana matumizi ya serikali kwa kupunguza au kuondoa posho na safari za ndani na nje kwa maafisa wake ni uonevu kwani wanawazidi maslahi kwa kiasi kikubwa sana. Mfano, mshahara wa mtumishi wa serikali 150,000/=, mbunge 7,000,000/=. Hapo kuna usawa kweli. Nafikiri hao wabunge wanaolilia posho za elfu 70 zitolewe wangekuja na hoja ya kufuta mishahara ya wabunge kwani si wafanyakazi, na badala yake walipwe posho za kuhudhuria vikao tu.
Nawasilisha.
 
hili swala ambalo ameliibua mbunge wa chadema mh.zitto kabwe kuhusu matumizi ya posho serikalini nakubaliana naye 100% kabsa haiwezakani mwalimu mwenye mshahara laki na nusu atoe fedha ake katka mshahara wake anunue chai na chakula akiwa shuleni anafundisha wakati wabunge na wengine maofisini wasio kuwa na majukumu mazito wanapewa posho za chakula hadi za kusinzia kazini na mishahara yao ni mamilioni uwoni tunategeneza gap la alienacho aendelee kuongezewa wakati asionacho anyanganywe ckubaliani nalo psodho futilia mbali nipeni mawazo yenu mwanaharakati mwenye kusubiri kufa
Umenena vyema ndugu, juzi nimefika hospitali kijijini Mbulu daktari anaona wagonjwa foleni nje nimekaa tangu saa 4 na sikumwona anatoka, imefika saa 8 akaja nesi mbio kumwita wanadharura wodini, akatoka akisema hata chai sijanywa, akampa yule nesi 500 amletee soda kibandani huku yeye akitimua mbio kuelekea wodini. Nadhani na hawa wanatakiwa angalau chai na chakula na sio wabunge kulipwa posho. Naunga mkono hoja.
 
Slaa mwenyewe alijifanya kupigia kelele mshahara wa wabunge upunguzwe, alipo pata ukatibu mkuu akawalazimisha CHAKushindwa wamlipe kama mbunge, na kwanza kupinga hii hoja yako atakuwa Slaa. Na anae bishia hili basi huyo ni mwenda wazimu kabisa, abishe tu ili tumjue sasa

Kwa maoni yangu suala la kupunguza au kuondoa posho za sitting kwa upande wa wabunge tunapaswa kulitizama kwa makini bila kuweka ushabiki wa kisiasa mbele na bila kujali nani kalianzisha. Tunapaswa kuangalia mantiki ya hoja yenyewe bila kujali nani ameitoa. Kama DR SLAA anaendelea kupokea posho naye atakuwa muathirika wa mabadiliko haya kama yatafanyika.

Mimi kwa upande wangu naona hoja hii ina mantiki. Kuhudhuria vikao vya bungo ndie kazi ya msingi ya wabunge. Wabunge wanalipwa mishahara mizuri tu na wanapewa posho za kujikimu (perdium) wanapokuwa nje ya majimbo yao. Wanapopokea tena sitting alowances tena kwa kiwango kikubwa kuliko perdium katika nchi masikini kama Tanzania kwa kweli inaleta mushikeli. Mimi naona kwa hili CHADEMA wameongea hoja ya msingi na yenye manufaa ambayo wabunge hawapaswi kuipuuza wala kuipa majibu ya juu juu. Haitoshi tu kusema kwamba mbona wabunge wa Chadema wanapokea au asiyetaka asieache bali wabunge pamoja na serikali wanatakiwa wajenge hoja juu ya umhimu na uhalali wa posho hiyo kwa wabunge kama wanaona bado kuna umhimu wa kuwepo.
 
hii posho ni kubwa sana na ndo inachangia kuwa na wabunge ambao hawako kimaslai ya taifa
 
Jamani sitting allowance zimezidi, ndo maana maofisini wamebaki walalahoi. Wakuu wako kwenye warsha, seminar, vikao, hafla....Posho, posho, poshooooooo, aaagrrr. Utendaji unapunguaaa, ubunifu unadorora, ufanisi mashakani! Tunaenda wapi? :smash:
 
Wabunge wa chama cha NCCR mageuzi wamesema wameandika barua kumtaka spika azielekeze posho zao kwenye mfuko wa maendeleo Kigoma. Wamesema watampatia spika barua hiyo kesho. Source: Taarifa ya Habari Channel Ten, Saa moja jioni, 12/06/2011.
 
This is now good. Ila nawapongeza sana CDM kwa kuwa author wa mabadiliko mengi ,bravo!!!!!!!!. CCM what are you waiting for? au mnaona noma kuyarudia matapishi yenu. Hapa ni mtego na ni jaribu pale unamtupia fisi(CCM) mfupa halafu unamwambia aukatae wakati ndo alioufuata. Tunawakodolea macho tuone kama ninyi ni wanaume kweli acheni posho!!!!!!!!!!!!!!!!

Tamaa ya CCM haitawaacha kuziachilia posho walafi wakubwa hawa
 
Safi wabunge wa NCCR, hii ndiyo inaitwa uongozi wa kambi ya upinzani, kuonesha njia ambayo kila mpenda mabadiliko anaona inafaa. Hongea CDM kwa kuonesha njia.
 
Kudos NCCR,siyo CCM,CDM,CUF,UDP....wengi wezi tu.
 
Back
Top Bottom